JK ammwagia sifa Lowassa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,268
33,040
Monduli%281%29.jpg

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa, kwa wapiga kura wa jimbo hilo wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo jana.



Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amemsifu Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kuwa ni mtu mwaminifu na mchapakazi.
Akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika kiwanja cha Bomani, mjini Monduli jana. alisema wananchi wa Monduli wanapaswa kumchagua Lowassa ili awe Mbunge wao. Rais Kikwete aliwataka wananchi wa Monduli mkoani Arusha, kusahau matukio yaliyopita dhidi Lowassa.
Lowassa aliwahi kuwa Waziri Mkuu baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani mwaka 2005, lakini alijiuzulu kutokana na kashfa ya zabuni ya mkataba wa kufufua umeme wa dharura uliyoihusisha kampuni ya Richmond Development Corporation.
“Nawaomba wakazi wa Monduli, kura zenu zote mpeni mgombea huyu (Lowassa), kwani ni mchapa kazi na ndiye aliyewaletea ukombozi na anayeendelea kufanya hivyo,” alisema.
Alisema kazi aliyoifanya Lowassa inafahamika kwa wakazi wa jimbo hilo, hivyo hawahitaji kuambiwa kwamba ndiye pekee anayefaa kuwa Mbunge.
“Lowassa amewasaidia mambo mengi, na pia ni kiongozi mzuri ambaye nina uhakika hamtakaa kupata kiongozi kama huyu, ambaye atawaongoza vyema,” alisema.
Alisema japo kuwa kuna vyama vingi vimejitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, lakini kati ya vyama hivyo hakuna kinachofanana na CCM kwa ubora. Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, CCM imefanya mambo makubwa, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule za sekondari za kata, ambazo ni moja ya ahadi zake alizotoa.
Aliahidi kuwa kila shule ya kata itapewa walimu watano na kuongeza vyuo vikuu.
Alisema anataka Wamasai waende shule badala ya kuchunga ng'ombe tu na ifikie mahali hata rubani wa ndege na viongozi wakubwa na kampuni mbalimbali wawe Wamasai.
Akizungumzia watu wanaopitapita kuwadanganya Wamasai, Kikwete alisema wamekuwa wakijitokeza watu wanaojidai kutaka kuwasaidia Wamasai ili kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
“Unajua mimi nasema serikali inawapenda na tumeandaa mpango mzuri kwa ajili ya watoto wa Kimasai, hivyo msidanganyike na watu hawa wenye vituo vya misaada ambao wanakuja na kujidai kuwa wanataka kuwasaidia … ni waongo,” alisema.
Alisema watu wa aina hiyo wanafika jimboni humo na katika maeneo mengine kuwapiga picha na kuzipeleka nje kwa ajili ya kuomba misaada kwa lengo la kujinufaisha binafsi.
Alisema watu hao wamekuwa wakidanganya kuwa serikali ya Tanzania haiwajali wala haiwasaidii watu wa pembezoni wakiwemo Wamasai.
Rais Kikwete alisema serikali ya CCM imetenga zaidi ya Sh. milioni 800 kwa ajili ya kurekebisha barabara za Monduli ziwe katika kiwango cha lami.
Aliahidi kuwa serikali imejipanga kuvuta maji katika sehemu nyingi zisizokuwa na maji ili yapatikane kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo.
Alisema serikali itawafidia wafugaji waliopata madhara katika mwaka ulioisha kutokana na njaa iliyowakumba na kusababisha mifugo mingi kufa.
Naye Lowassa aliwataka wananchi wa jimbo hilo kumpa kura za ndiyo Rais Kikwete, kwa vile amechangia kwa kiasi kikubwa kuleta maendeleo jimboni humo.
Rais Kikwete alifanya mikutano katika maeneo ya Ngaramtoni, Longido, Namanga na Monduli.
Alisema lengo la serikali yake kuanzisha shule za sekondari za kata ni kuhakikisha kuwa jamii nzima inapata elimu bila ubaguzi.
Kuhusu soko la mifugo, alisema katika kipindi cha miaka mitano ikiwa CCM itaingia madarakani, itahakikisha inajenga minada.
Alisema watalaamu wameishatumwa kufanya utafiti ili kuanza kutekeleza kazi hiyo.
Habari hii imeandikwa na Woinde Shizza, Monduli na Hellen Mwango, Longido Arusha.




CHANZO: NIPASHE
 
Mnyonge mnyongeni, haki yake mpeni!.
Ukiondoa tuhuma za richmonduli,
Lowassa kweli ni :-
Mchapa kazi kuliko JK!
Mtendaji kuliko JK!,
Mfuatiliaji kuliko JK!
Ila hata yale mengine, pia ni kuliko JK! (JK alikuwa anajionyesha wazi wazi, EL, kimya kimya!)
Hivyo hawa wote ni wale wale!.
 
Monduli%281%29.jpg

Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, akimnadi mgombea ubunge wa Jimbo la Monduli, Edward Lowassa, kwa wapiga kura wa jimbo hilo wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo jana.



Mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amemsifu Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kuwa ni mtu mwaminifu na mchapakazi.
Akihutubia katika mkutano wa kampeni uliofanyika kiwanja cha Bomani, mjini Monduli jana. alisema wananchi wa Monduli wanapaswa kumchagua Lowassa ili awe Mbunge wao. Rais Kikwete aliwataka wananchi wa Monduli mkoani Arusha, kusahau matukio yaliyopita dhidi Lowassa.
Lowassa aliwahi kuwa Waziri Mkuu baada ya Rais Kikwete kuingia madarakani mwaka 2005, lakini alijiuzulu kutokana na kashfa ya zabuni ya mkataba wa kufufua umeme wa dharura uliyoihusisha kampuni ya Richmond Development Corporation.
“Nawaomba wakazi wa Monduli, kura zenu zote mpeni mgombea huyu (Lowassa), kwani ni mchapa kazi na ndiye aliyewaletea ukombozi na anayeendelea kufanya hivyo,” alisema.
Alisema kazi aliyoifanya Lowassa inafahamika kwa wakazi wa jimbo hilo, hivyo hawahitaji kuambiwa kwamba ndiye pekee anayefaa kuwa Mbunge.
“Lowassa amewasaidia mambo mengi, na pia ni kiongozi mzuri ambaye nina uhakika hamtakaa kupata kiongozi kama huyu, ambaye atawaongoza vyema,” alisema.
Alisema japo kuwa kuna vyama vingi vimejitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, lakini kati ya vyama hivyo hakuna kinachofanana na CCM kwa ubora. Rais Kikwete alisema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, CCM imefanya mambo makubwa, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule za sekondari za kata, ambazo ni moja ya ahadi zake alizotoa.
Aliahidi kuwa kila shule ya kata itapewa walimu watano na kuongeza vyuo vikuu.
Alisema anataka Wamasai waende shule badala ya kuchunga ng'ombe tu na ifikie mahali hata rubani wa ndege na viongozi wakubwa na kampuni mbalimbali wawe Wamasai.
Akizungumzia watu wanaopitapita kuwadanganya Wamasai, Kikwete alisema wamekuwa wakijitokeza watu wanaojidai kutaka kuwasaidia Wamasai ili kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
“Unajua mimi nasema serikali inawapenda na tumeandaa mpango mzuri kwa ajili ya watoto wa Kimasai, hivyo msidanganyike na watu hawa wenye vituo vya misaada ambao wanakuja na kujidai kuwa wanataka kuwasaidia … ni waongo,” alisema.
Alisema watu wa aina hiyo wanafika jimboni humo na katika maeneo mengine kuwapiga picha na kuzipeleka nje kwa ajili ya kuomba misaada kwa lengo la kujinufaisha binafsi.
Alisema watu hao wamekuwa wakidanganya kuwa serikali ya Tanzania haiwajali wala haiwasaidii watu wa pembezoni wakiwemo Wamasai.
Rais Kikwete alisema serikali ya CCM imetenga zaidi ya Sh. milioni 800 kwa ajili ya kurekebisha barabara za Monduli ziwe katika kiwango cha lami.
Aliahidi kuwa serikali imejipanga kuvuta maji katika sehemu nyingi zisizokuwa na maji ili yapatikane kwa ajili ya matumizi ya binadamu na mifugo.
Alisema serikali itawafidia wafugaji waliopata madhara katika mwaka ulioisha kutokana na njaa iliyowakumba na kusababisha mifugo mingi kufa.
Naye Lowassa aliwataka wananchi wa jimbo hilo kumpa kura za ndiyo Rais Kikwete, kwa vile amechangia kwa kiasi kikubwa kuleta maendeleo jimboni humo.
Rais Kikwete alifanya mikutano katika maeneo ya Ngaramtoni, Longido, Namanga na Monduli.
Alisema lengo la serikali yake kuanzisha shule za sekondari za kata ni kuhakikisha kuwa jamii nzima inapata elimu bila ubaguzi.
Kuhusu soko la mifugo, alisema katika kipindi cha miaka mitano ikiwa CCM itaingia madarakani, itahakikisha inajenga minada.
Alisema watalaamu wameishatumwa kufanya utafiti ili kuanza kutekeleza kazi hiyo.
Habari hii imeandikwa na Woinde Shizza, Monduli na Hellen Mwango, Longido Arusha.




CHANZO: NIPASHE

Kikwete na wana CCM mmesahau kuwa Kikwete alisema “Nawaomba wakazi wa Monduli, kura zenu zote mpeni mgombea huyu (Lowassa), kwani ni mchapa kazi na ndiye aliyewaletea ukombozi na anayeendelea kufanya hivyo"
 
kweli akiba yamaneno inahitajika alipokuwa kigoma alisema kuwa mwenye richmond ni yule anaetembea na lisu amesahau kuwa mwaka 2010 yeye alikua nae. jambo jema nikuwa maamuzi ya walio wengi wanamtaka awe rais nami nataka awe rais wangu na nimeandaa sherehe fupi ya kujipongeza kwa ushindi wa kishindo nimalize kwa kusema peopleeeeeeees!!
 
Asante sana kwa huu MVINYO wa kale. Hakika umekwiva!

Nafarijika sana kujua kuwa hata Rais Kikwete ana imani kubwa sana na Lowassa
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom