Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Wandugu,
Mimi ni miongoni mwa wananchi waliokuwa na wasiwasi juu ya uwezo wa Jk kuongoza nchi. Kwa jinsi nilivyomfahamu, nilijua anauchukulia urais kama vyeo vingine alivyowahi kukalia. Kikubwa alichokuwa anakitafuta kilikuwa ni 'hadhi' na siyo kuwakomboa wanyonge wa nchi hii. Pamoja na kumshtukia tangu awali kuwa hawezi kuongoza sikutarajia kama uwezo wake kiuongozi ni mdogo kwa kiwango ninachoshuhudia sasa. Watanzania lazima tukiri tuna kiongozi wa ajabu. Baadhi ya wananchi wanasema uongozi wa mzee mwinyi ulipwaya lakini kwa maoni ya wengi sasa wanasema bora hata ya mzee mwinyi. Uongozi wa sasa siyo umepwaya tu, umepwaguka.
Mimi ni miongoni mwa wananchi waliokuwa na wasiwasi juu ya uwezo wa Jk kuongoza nchi. Kwa jinsi nilivyomfahamu, nilijua anauchukulia urais kama vyeo vingine alivyowahi kukalia. Kikubwa alichokuwa anakitafuta kilikuwa ni 'hadhi' na siyo kuwakomboa wanyonge wa nchi hii. Pamoja na kumshtukia tangu awali kuwa hawezi kuongoza sikutarajia kama uwezo wake kiuongozi ni mdogo kwa kiwango ninachoshuhudia sasa. Watanzania lazima tukiri tuna kiongozi wa ajabu. Baadhi ya wananchi wanasema uongozi wa mzee mwinyi ulipwaya lakini kwa maoni ya wengi sasa wanasema bora hata ya mzee mwinyi. Uongozi wa sasa siyo umepwaya tu, umepwaguka.