JK akasirika

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
itabidi upangue wizara nyingi...siyo maliasili na utalii pekee ili kurudisha crebility yako kwa Watanzania.

JK akasirika

2007-11-19 17:18:18
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Kuna habari kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bw. Jakaya Kikwete amekasirishwa na vitendo vinavyofanywa na baadhi ya maafisa wa ngazi za juu katika Wizara ya Maliasili na Utalii nchini na yuko mbioni kuwapangua wote wizarani hapo.

Kwa mujibu wa taarifa toka kwa chanzo chetu kimoja, ni kwamba hazitapita siku nyingi kabla Rais hajapitisha panga kali katika wizara hiyo ili kuweka mambo sawa.

``Rais ana taarifa za mambo mengi yanayofanywa kinyume na sheria wizarani hapo? kwakweli anakasirishwa na namna watu waliopewa dhamana kubwa ya kulitumikia taifa wanavyolihujumu taifa.

Wengi atawaopangua na wengine wanaweza kumwaga unga katika muda mfupi ujao,`` kikasema chanzo chetu.

Chanzo hicho kimeongeza kuwa baadhi ya maafisa wasio waaminifu wanaweza kuchukuliwa hatua kali zaidi za kisheria.

Inaelezwa zaidi kuwa miongoni mwa yale yaliyomkasirisha Rais na hata kuamua kutaka kuchukua hatua ya kupangua vigogo kibao wizarani hapo ni pamoja na kushamiri kwa biashara haramu ya magogo ambayo hufanywa kiujanjaujanja na baadhi ya maafisa wa juu wizarani hapo.

Katika hatua nyingine, Rais Jakaya Kikwete amekaririwa jana akisema kuwa maafisa wasio waaminifu katika Wizara ya Malisili na Utalii watachukuliwa hatua stahili katika muda usiokuwa mrefu kuanzia sasa.

``Ninazo taarifa kuwa kuna baadhi ya maofisa wasiokuwa waadilifu ndani ya wizara? hawa wamekuwa wakijihusisha na biashara haramu ya magogo, sasa wajiandae kwa kuwa watachukuliwa hatua zinazostahili siku si nyingi,`` amekaririwa akisema Rais jana wakati akiwa kwenye ziara yake mkoani Lindi.

Amesema maofisa hao wasiokuwa waadilifu wamesababisha kupakwa matope hata wale walio waaminifu.

JK akasema kuwa wilaya za Kilwa na Rufiji ndizo zilizoshamiri kwa biashara hiyo ya uvunaji magogo kinyume cha sheria.

Amesema kinachosikitisha zaidi ni kuwa watu hao wamekuwa wakivuna hata miti michanga na ile isiyokomaa.

SOURCE: Alasiri
 
Ni yale yale kama ya wala rusha nawafahamu wote nawapeni muda wa kujirekebisha. Kisha akaja na majina ya watu wanao jihusisha na biashara haramu ya madawa ya kulevya. Nakumbuka kuna siku Polisi wake walitudanganya mpaka wakatangaza kuwa wana list ya majina stini na mali zao, mpaka leo kimya.

Pesa haramu hiyo ndiyo iliyompa uraisi.

Naona anaendelea kuchezea akili za watanzania
 
Akiletewa issues za BOT anasema hakuna ushahidi hivyo tuiachie serikali kupitia vyombo vyake ifuatilie. Sasa imekuwaje hili la magogo ndiyo kuwa issue kubwa kupita nyingine??? YALE YALE USANII!!
 
huyu hakufaa kuwa rais kumbe siku zote alikuwa chekacheka leo anakasirika nini mbona wakati Severe anawahamisha katibu mkuuPamba na waziri Dialo hakuonyesha hasira?
Ohhhh Kikwete mtumbwi wako umepasuka maji lazima yatakuzamisha tu huwezi kukwepa safari hii ndio mwisho wa uongo wako, umekwama!
 
Nadhani Mpaka kusema hivi,Ndoa ya Muungwana na BWana kasungura ina mgogoro mkubwa,Suala la MAliasili ilnamgusa severe ambaye ni rafiki yake na Ndanda pia mama Meghji..
Mie nina uhakika Kabla ya DEsemba lazima Muungwana aje na List mpya
 
Ni bora kuanza na wafanyakazi wapya ktk wizara ya ardhi kwani hii wizara inanuka rushwa.nitaunda kamati kila wilaya ilikubaini wale wote waliogawa viwanja(kimoja)kwa zaidi mtu mmoja,pia nitafuatilia ilikubaini wale wote waliuza maeneo ya wazi na kuakikisha yanarudishwa.
Haya ni maneno ya jk alipotembelea wizara ya aridhi.hakuna lilofanyika zaidi ya usanii leo anakuja na mengine tena,jamani ninyi washauri wake wa karibu mwambieni rais wenu aache kutoa kauli za namna hiyo zinazidi kupandisha hasira za wadanganyika na kushusha hadhi yake kama rais.
 
JK YOU MUST BE SERIOUS ....KAMA RAIS HUTAKIWI KUCHIMBA MKWARA ..ooh nawafahamu ..maafisa waovu..HUNA HAJA YA KUMBEMBELEZA MTU ..KAMA UMESHAJIRIDHISHA WEWE TOA TAMKO KUWA WANASTAAFISHWA KWA MANUFAA YA UMMA...USIJEUKAISHIA TENA KUFUKUZA KAZI WATU KWA MAKOSA UKABAKI UNAUMIA...
KUMBUKA WANANCHI BADO WANA KUMBUKUMBU YA WALE WALIOKULA PESA WAKARIPOTIWA NA CAG[CONTROLLER AND AUDITOR GENERAL]..UKASEMA SIKU ZAO ZINAHESABIKA NA HADI LEO HUJAFANYA LOLOTE...

RAIS NI CHEO KIKUBWA SANA ....KAULI YAKO NI SHERIA NDOGO,...AU HUJAJIAMINI KWAMBA WEWE NDIO RAIS....
 
JK YOU MUST BE SERIOUS ....KAMA RAIS HUTAKIWI KUCHIMBA MKWARA ..ooh nawafahamu ..maafisa waovu..HUNA HAJA YA KUMBEMBELEZA MTU ..KAMA UMESHAJIRIDHISHA WEWE TOA TAMKO KUWA WANASTAAFISHWA KWA MANUFAA YA UMMA...USIJEUKAISHIA TENA KUFUKUZA KAZI WATU KWA MAKOSA UKABAKI UNAUMIA...
KUMBUKA WANANCHI BADO WANA KUMBUKUMBU YA WALE WALIOKULA PESA WAKARIPOTIWA NA CAG[CONTROLLER AND AUDITOR GENERAL]..UKASEMA SIKU ZAO ZINAHESABIKA NA HADI LEO HUJAFANYA LOLOTE...

RAIS NI CHEO KIKUBWA SANA ....KAULI YAKO NI SHERIA NDOGO,...AU HUJAJIAMINI KWAMBA WEWE NDIO RAIS....

Mkuu PM,

Kikwete bado anaplay kati ya uwaziri wa mambo ya nje na urais.

Au kwa lugha mpya ya JF, Kikwete bado ana-vascodagamarize hii dunia for the second time! Kila siku anasema kuwa ana list ya wala rushwa, wauza madawa, mafisadi, na kamati zinaundwa kila siku kuchunguza kile ambacho kamati zingine zimeshindwa kupata kutoka kwenye original tume ya kuchunguza uundwaji wa kamati na tume teule... gooosh I need a drink!
 
Mkuu PM,

Kikwete bado anaplay kati ya uwaziri wa mambo ya nje na urais.

Au kwa lugha mpya ya JF, Kikwete bado ana-vascodagamarize hii dunia for the second time! Kila siku anasema kuwa ana list ya wala rushwa, wauza madawa, mafisadi, na kamati zinaundwa kila siku kuchunguza kile ambacho kamati zingine zimeshindwa kupata kutoka kwenye original tume ya kuchunguza uundwaji wa kamati na tume teule... gooosh I need a drink!

just a suggestion !
1098147497_whoop-ass1.jpg
 
Mkuu PM,

Kikwete bado anaplay kati ya uwaziri wa mambo ya nje na urais.

Siyo mambo ya nje tu hila naona anafaa kwenda kutoa Lectures pale Chuo cha diplomasia. Mtu anaushahidi tosha kuwa siyo waaminifu anakuja kutwambia nini wananchi kuwa atarusha kombora.

Kinachotakiwa siyo maigizo ni utendaji tu basi, anatakiwa awaondoe mara moja bila kulalamika kwa wananchi.
 
Siyo mambo ya nje tu hila naona anafaa kwenda kutoa Lectures pale Chuo cha diplomasia. Mtu anaushahidi tosha kuwa siyo waaminifu anakuja kutwambia nini wananchi kuwa atarusha kombora.

Kinachotakiwa siyo maigizo ni utendaji tu basi, anatakiwa awaondoe mara moja bila kulalamika kwa wananchi.

kwi kwi kwi kwi,

chuo cha diplomasia, yaani inabidi tu nichukue my lunch break mapema hapa! Mimi nadhani Kikwete anafaa amfuate Lowassa kwenye chuo cha sanaa na maigizo kule Lindi or somewhere unkown!
 
kwi kwi kwi kwi,

chuo cha diplomasia, yaani inabidi tu nichukue my lunch break mapema hapa! Mimi nadhani Kikwete anafaa amfuate Lowassa kwenye chuo cha sanaa na maigizo kule Lindi or somewhere unkown!

haya sasa, kinywaji ulishapewa !
na lunch yako hii hapa !
Stella_and_Henry_Hot_Dogs_2.JPG
 
Naona ulifaaa kuweka nguruwe hapo - mkuu wa meza! maana vinyama vidogo kama hivyo ulivyoweka vinawafaa watoto wa mama!
 
ni kweli pamoja na mananasi na mafenesi yenu wewe na mwenzako !

mbuzi katoliki mbona anapanda tu kwangu sijui kwa wengine !
 
ni kweli pamoja na mananasi na mafenesi yenu wewe na mwenzako !

mbuzi katoliki mbona anapanda tu kwangu sijui kwa wengine !

Kada acha bwana kututoa kwenye mada.

Suala ni kwamba hivi Muungwana kuna haja kweli ya kutwambia kuwa anajua watendaji wanafanya mchezo mbaya? Mbona alisha twambia anajua wauza unga, je kuna nini kilichofanyika? Je na hawa itakuwa hivi, mimi nafikiri rais mzuri ni yule anayepata ushahidi anareact mara moja.

Vinginevyo ni usanii!
 
Kada hacha bwana kututoa kwenye mada.

Suala ni kwamba hivi Muungwana kuna haja kweli ya kutwambia kuwa anajua watendaji wanafanya mchezo mbaya? Mbona alisha twambia anajua wauza unga, je kuna nini kilichofanyika? Je na hawa itakuwa hivi, mimi nafikiri rais mzuri ni yule anayepata ushahidi anareact mara moja.

Vinginevyo ni usanii!

sikuwa na maana ya kuwatoa kwenye mada, ila huyo binti hapo alikuwa ana njaa mara kinywaji ( si unajua watoto wa bongo bana, iz me iz want a drink kwa saaaana ukiwapeleka posta tu bosi wewe) eniwei, hayo ya rais sina uhakika sana lakini vile vile sidhani kama alitoa time frame ya kushughulikia hayo masuala, cha msingi ni kwamba kama atafail kufanya alichoahidi, basi hapo ndio itakuwa wakati muafaka wa kuuliza hayo maswali !

lakini kama utamjudge wakati hakutoa time frame that will only back fire !
 
lakini kama utamjudge wakati hakutoa time frame that will only back fire !

Mimi huwa nachukia sana watu ambao hawajari muda. Unajua Tanzania ni nchi masikini sana pamoja na raslimali tulizo nazo na pia ni nchi tegemezi omba omba(Refer EL, 2007 na dependence ya bajeti kwa donars).

Sasa JK aliona hilo na akaja na Usanii wa Kasi mpya na nguvu mpya, wananchi wakashangilia sana.

Sasa akiona madudu na muda unakwenda anakuja kutwambia na wewe unatwambia time frame, je mtu akitoa hukumu kuwa fulani ni msanii utetezi utaupata wapi?
 
Mimi huwa nachukia sana watu ambao hawajari muda. Unajua Tanzania ni nchi masikini sana pamoja na raslimali tulizo nazo na pia ni nchi tegemezi omba omba(Refer EL, 2007 na dependence ya bajeti kwa donars).

Sasa JK aliona hilo na akaja na Usanii wa Kasi mpya na nguvu mpya, wananchi wakashangilia sana.

Sasa akiona madudu na muda unakwenda anakuja kutwambia na wewe unatwambia time frame, je mtu akitoa hukumu kuwa fulani ni msanii utetezi utaupata wapi?

mzee kwanza punguza hasira !

halafu kama maendeleo unataka kufaidi wewe mzee, SAHAU !! ni aidha uchakarike weee hadi kijasho cha ..............kitoke ili vizazi vyako baadae vienjoi kama walivyofanya mababu na mabibi zetu kipindi cha ukoloni maana chakarika zao ndio tunafaidi sisi wa vizazi hivi, sasa kama unasema unachukia time frame mzee, maybe tanzania is not the right country and place for you to be in ! wazee wetu kipindi kile laiti wangekuwa wanachukia time frame basi nadhani hadi hivi sasa tungekuwa under colonial rule !

wee chakarika mzee, na usijali kuenjoy wewe hayo maendeleo bali vizazi vijavyo ! sore kama hupendi nilichosema !
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom