JK akabidhi kadi za CCM 1138 ktk ziara yake LINDI.

the horse

JF-Expert Member
Sep 27, 2011
652
441
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amewapokea na kuwakabidhi kadi wanachama wapya 1138 walipojiunga na Chama Cha Mapinduzi, katika wilaya za Liwale na Nachingwea Mkoani Lindi.


Mwenyekiti Huyo wa Chama Tawala aliwapokea wanachama hao wapya baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wake wa hadhara katika uzinduzi wa Boma la Wananchi Nachingwea na mkutano wa Hadhara Liwale, ambapo wanachama hao wapya walikabidhiwa kadi za chama na kisha kuapishwa kwa Imani na Ahadi za Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi.


Mheshimiwa Rais yupo katika ziara ya Kikazi Mkoani humo ambapo alishiriki maazimisho ya siku ya Ukimwi Duniani tarehe 01[SUP]st[/SUP] Dec 2012 kisha kufanya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo ya wananchi Mkoani Lindi pamoja na kusikiliza na kutatua kero mbalimbali na Changamoto zinazoikabili Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.


Mheshimiwa Rais anaendelea na Ziara yake Mkoani umo ambapo leo yupo katika wilaya ya Kilwa ambayo iko chini ya Mheshimiwa Abdallah Ulega aliyekuwa Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Pwani. Mheshimiwa Rais anategemea kumalizia ziara yake wilayani Kilwa,alasiri ya leo, tarehe 5[SUP]th[/SUP] Dec 2012.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amewapokea na kuwakabidhi kadi wanachama wapya 1138 walipojiunga na Chama Cha Mapinduzi, katika wilaya za Liwale na Nachingwea Mkoani Lindi.


Mwenyekiti Huyo wa Chama Tawala aliwapokea wanachama hao wapya baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wake wa hadhara katika uzinduzi wa Boma la Wananchi Nachingwea na mkutano wa Hadhara Liwale, ambapo wanachama hao wapya walikabidhiwa kadi za chama na kisha kuapishwa kwa Imani na Ahadi za Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi.


Mheshimiwa Rais yupo katika ziara ya Kikazi Mkoani humo ambapo alishiriki maazimisho ya siku ya Ukimwi Duniani tarehe 01[SUP]st[/SUP] Dec 2012 kisha kufanya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo ya wananchi Mkoani Lindi pamoja na kusikiliza na kutatua kero mbalimbali na Changamoto zinazoikabili Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.


Mheshimiwa Rais anaendelea na Ziara yake Mkoani umo ambapo leo yupo katika wilaya ya Kilwa ambayo iko chini ya Mheshimiwa Abdallah Ulega aliyekuwa Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Pwani. Mheshimiwa Rais anategemea kumalizia ziara yake wilayani Kilwa,alasiri ya leo, tarehe 5[SUP]th[/SUP] Dec 2012.
Hiyo ziara ya kiserikali mnaifanya ya kichama mnajisifu kugawa kadi kwa matumizi mabaya ya rasilimali za umma.Kuna haja sasa kutenganisha shughuli za vyama vya siasa na serikali ili kuepusha matumizi yasiyo na manufaa na taifa.
 
Si ajabu hao ni mashemeji wanatafuta chakula tu.
 
shughuli za chama kwa fedha za serikali,..ajali za barabarani zimepungua sana zingetuondolea kadhia yote
 
Baadhi ya watu hawajafahamu mgawanyio wa majukumu kati ya Chama na serikali, kimsingi JK akiwa kama Rais bado anatambulika kwa wana-CCM kama Mwenyekiti wa Chama Chao, hakuna makosa na ni uelewa mbovu kutaka Rais asishiriki shughuli za kichama anapozunguka katika ziara zake.

Anao uwezo na wala hakuna kipengele cha sheria kinachomzuia kufanya shughuli hizo za kichama awapo ziarani. Hili halina utata, mbona inapotokea Mawaziri ama Manaibu Waziri kuambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnnauye katika Ziara zake haiwi ni tatizo, kwanini iwe tatizo kwa Rais pekee.

Sidhani kuwa jambo hili ni la msingi sana kulipinga.
 
...hao watakuwa ni shemeji zake,sinasikia raisi kaoa huko au kumbukumbu zangu hazijatulia?!....
 
Baadhi ya watu hawajafahamu mgawanyio wa majukumu kati ya Chama na serikali, kimsingi JK akiwa kama Rais bado anatambulika kwa wana-CCM kama Mwenyekiti wa Chama Chao, hakuna makosa na ni uelewa mbovu kutaka Rais asishiriki shughuli za kichama anapozunguka katika ziara zake. Anao uwezo na wala hakuna kipengele cha sheria kinachomzuia kufanya shughuli hizo za kichama awapo ziarani. Hili halina utata, mbona inapotokea Mawaziri ama Manaibu Waziri kuambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnnauye katika Ziara zake haiwi ni tatizo, kwanini iwe tatizo kwa Rais pekee. Sidhani kuwa jambo hili ni la msingi sana kulipinga.

Inatakiwa ujue katika mfumo wa vyama vingi Rais anapokuwa katika shughuli za kiserikali lakini akaingiza siasa moja kwa moja anakuwa anawanyima fursa watanzania ambao ni wa vyama vya upinzani au wasio na vyama kushiriki kikamilifu katika hizo ziara zake ikiwa ni pamoja na kutoa maoni, na mawazo yao juu ya maendeleo ya Taifa hili.
 
Inatakiwa ujue katika mfumo wa vyama vingi Rais anapokuwa katika shughuli za kiserikali lakini akaingiza siasa moja kwa moja anakuwa anawanyima fursa watanzania ambao ni wa vyama vya upinzani au wasio na vyama kushiriki kikamilifu katika hizo ziara zake ikiwa ni pamoja na kutoa maoni, na mawazo yao juu ya maendeleo ya Taifa hili.

Hakuna ukweli wa moja kwa moja katika hili kwa maana katika baadhi ya maeneo Rais akliweza kusimama na kuongea na wananchio katikja vijiwe vya CUF kama katika kata ya MIGURUWE wilaya ya KILWA ambapo bila kujali kuwa yeye ni MwanaCCM na haikuwa katika Ratiba ya Msafara wa Rais lakini alipofika katika Maskani hiyo ya CUF na kuwakuta wanaCUF wamejaa eneo hiloMheshimiwa Rais aliamuru Msafara Usimame na asalimiane na wanachama wa CUF katika eneo hilo. Jambo hili linawezekana kutoa tafsir kuwa RAIS anafanya kazi yake kwa Ufahamu na Uelewa kuwa yeye ni wa watanzania wote lakini pia anajitambua kuwa yeye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.
 
Bado kuna mkanganyiko mkubwa katika ufahamu wa watu katika mgawanyo wa majukumu ya Rais kama Rais na Kama Mwenyekiti wa Chama.,nafikiri ni busara sasa watu waanze kupewa elimu ya kutosha.
 
Baadhi ya watu hawajafahamu mgawanyio wa majukumu kati ya Chama na serikali, kimsingi JK akiwa kama Rais bado anatambulika kwa wana-CCM kama Mwenyekiti wa Chama Chao, hakuna makosa na ni uelewa mbovu kutaka Rais asishiriki shughuli za kichama anapozunguka katika ziara zake.

Anao uwezo na wala hakuna kipengele cha sheria kinachomzuia kufanya shughuli hizo za kichama awapo ziarani. Hili halina utata, mbona inapotokea Mawaziri ama Manaibu Waziri kuambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnnauye katika Ziara zake haiwi ni tatizo, kwanini iwe tatizo kwa Rais pekee.

Sidhani kuwa jambo hili ni la msingi sana kulipinga.

Loh Rais kupokea kadi za wananachama, Kazi ya Nape na Kinana itakuwa nini?
 
Katika Ziara hiyo ya Ndugu Jk..,wanaCCM wanayo haki na wajibu zaidi kuhudhuria na kumpokea sawa na wanachi wengine.,utofauti wa kuwa chama tawala cheye serikali lazima uonekane waziwazi na wapinzania waone kuwa hawa ni watawala na watambue kuwa wao ni wapinzani.

Ni ziara ya Rais lakini klatika Protocal lazima atajwe Mwenyekiti wa Chama Tawala wa Eneo husika katika Utambulisho, lazima atajwe MNEC pia.
 
Katika Ziara hiyo ya Ndugu Jk..,wanaCCM wanayo haki na wajibu zaidi kuhudhuria na kumpokea sawa na wanachi wengine.,utofauti wa kuwa chama tawala cheye serikali lazima uonekane waziwazi na wapinzania waone kuwa hawa ni watawala na watambue kuwa wao ni wapinzani.

Ni ziara ya Rais lakini klatika Protocal lazima atajwe Mwenyekiti wa Chama Tawala wa Eneo husika katika Utambulisho, lazima atajwe MNEC pia.

Anatuchuna ngozi kwa kumaliza rasimali za serikali kwa kujenga chama mfu hao wafuasi kamera ziliwakimbia hatujaonywesha ati nadhani figure imechakachuliwa
 
JK akabidhi kadi za CCM 1138 ktk ziara yake LINDI
Yeah, alikuwa anakabidhi kadi mpya baada ya zile za mwanzo kuwa zimechakaa, na amekabidhi kwa wanachama wale wale wa zamani (sio wapya). Hata mimi kitambulisho changu cha kupigia kura kimechakaa, ningependa JK aje anikabidhi kipya!
 
tatizo la kikwete ni mtu wa kamba sana, ndiyo maana alitaka tumuanmini kwamba. katika kikao kikuu cha CCM ni watu wawili tu wasiyo mkubali. tena hao wana chuki binafsi. kwa hiyo akiongea kitu chukua mawili kumi ni kamba tupu
 
Hakuna ukweli wa moja kwa moja katika hili kwa maana katika baadhi ya maeneo Rais akliweza kusimama na kuongea na wananchio katikja vijiwe vya CUF kama katika kata ya MIGURUWE wilaya ya KILWA ambapo bila kujali kuwa yeye ni MwanaCCM na haikuwa katika Ratiba ya Msafara wa Rais lakini alipofika katika Maskani hiyo ya CUF na kuwakuta wanaCUF wamejaa
eneo hiloMheshimiwa Rais aliamuru Msafara Usimame na asalimiane na wanachama wa CUF katika eneo hilo. Jambo hili linawezekana kutoa tafsir kuwa RAIS anafanya kazi yake kwa Ufahamu na Uelewa kuwa yeye ni wa watanzania wote lakini pia anajitambua kuwa yeye ni Mwenyekiti wa CCM Taifa.

CUF si ndio Wake zao wa Ndoa! (tafsr sahihi)
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amewapokea na kuwakabidhi kadi wanachama wapya 1138 walipojiunga na Chama Cha Mapinduzi, katika wilaya za Liwale na Nachingwea Mkoani Lindi.


Mwenyekiti Huyo wa Chama Tawala aliwapokea wanachama hao wapya baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wake wa hadhara katika uzinduzi wa Boma la Wananchi Nachingwea na mkutano wa Hadhara Liwale, ambapo wanachama hao wapya walikabidhiwa kadi za chama na kisha kuapishwa kwa Imani na Ahadi za Mwanachama wa Chama Cha Mapinduzi.


Mheshimiwa Rais yupo katika ziara ya Kikazi Mkoani humo ambapo alishiriki maazimisho ya siku ya Ukimwi Duniani tarehe 01[SUP]st[/SUP] Dec 2012 kisha kufanya Ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo ya wananchi Mkoani Lindi pamoja na kusikiliza na kutatua kero mbalimbali na Changamoto zinazoikabili Serikali ya Chama Cha Mapinduzi.


Mheshimiwa Rais anaendelea na Ziara yake Mkoani umo ambapo leo yupo katika wilaya ya Kilwa ambayo iko chini ya Mheshimiwa Abdallah Ulega aliyekuwa Mwenyekiti wa Vijana Mkoa wa Pwani. Mheshimiwa Rais anategemea kumalizia ziara yake wilayani Kilwa,alasiri ya leo, tarehe 5[SUP]th[/SUP] Dec 2012.

hiyo ziara anafanya kama kiongozi wa nchi au kama m/kiti wa ccm?manake tumezoea kuona rasilimali za taifa hili zikitumika ndivyo sivyo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom