Rais Kikwete hatahudhuria Mei mosi
na khamis mkotya
RAIS Jakaya Kikwete, hatakuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha sherehe za Mei mosi zitakazofanyika kitaifa mkoani Iringa.
Mwaliko wa sherehe hizo ulipelekwa kwake na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA). Uamuzi huo wa Rais, umeelezwa kwamba umetokana na majukumu mengi ya kitaifa yanayomkabili.
Kutokana na uamuzi huo, TUCTA imeeleza kusononeka kwa maelezo kuwa kuwapo kwa Rais katika maadhimisho hayo ni muhimu.
Pia Rais Kikwete amelalamikiwa kwamba amekataa kauli mbiu iliyokuwa imependekezwa na TUCTA kwa ajili ya sherehe za mwaka huu.
Kauli mbiu iliyopelekwa kwa Rais ilikuwa ikisema: Maisha bora yanawezekana tukiutokomeza ufisadi. TUCTA wanadai kwamba maneno hayo hayakumfurahisha Rais Kikwete.
Aidha, TUCTA imeeleza kushangazwa na uamuzi wa Rais kukataa kuhudhuria mkutano wa 96 ulioitishwa na Shirika la Kazi Duniani (ILO), utakaofanyika Geneva, Uswisi.
Imeelezwa kwamba kiongozi huyo ameahirisha kwenda huko kutokana na kubanwa na vikao vya bajeti inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni Juni mwaka huu.
Naibu Katibu wa TUCTA, Nicholas Mgaya, alitoa maelezo hayo alipozungumza na MTANZANIA ofisini kwake jana, kuhusu maandalizi ya sherehe za Mei mosi.
Mgaya alisema mwaliko ulipelekwa kwa Rais Kikwete Februari, mwaka huu kupitia Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Kwa mujibu wa Mgaya, wiki mbili zilizopita Shirikisho, kupitia wizara hiyo, lilipata taarifa kuwa Rais hatoweza kushiriki, badala yake atawakilishwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
"Tumesikitishwa hatua hiyo kwa kuwa inaonyesha anaanza kujitenga na wafanyakazi. Tunakubali Waziri Mkuu, lakini kwa shingo upande," alisema na kuongeza;
Kuhusu mkutano wa Geneva, Mgaya alisema Rais Kikwete alikuwa amealikwa na kwamba alipewa hadhi ya kufungua mkutano huo utakaofanyika Juni, mwaka huu kutokana na nafasi yake ya Uenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU).
Kwa mujibu wa Mgaya, mwaliko wa ILO kwa Rais Kikwete kushirikia katika mkutano huo ilikuwa ni nafasi nzuri inayoijengea sifa Tanzania.
"Hatujaridhika na sababu zilizotolewa na Ikulu kwamba Rais hatahudhuria mkutano huo. Ina maana Rais hana wataalamu hadi asimamie bajeti mwenyewe?, alihoji.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, amejibu malalamiko ya TUCTA kwa kusema Rais ameona kuwa baada ya kuhudhuria Mei mosi mwaka 2006 mkoani Shinyanga na mwaka 2007 mkoani Mwanza, ameona sasa ni busara kutoa nafasi kwa mmoja wa wasaidizi wake.
Rais ana kawaida ya kutoa maelekezo ili awakilishwe katika shughuli mbalimbali. Hivi karibuni utakumbuka alifanya hivyo kwa kuwakilishwa na Makamu wa Rais nchini Uingereza na Denmark, alisema.
Rweyemamu alisema ni kweli Rais alialikwa katika mkutano wa ILO, lakini kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi ya kitaifa, ameomba asihudhurie, badala yake ameshauri apangiwe ziara ya kutembelea makao makuu ya chombo hicho kwa wakati mwafaka.
Alisema ameomba asihudhurie mkutano huo kwa vile Juni kutakuwa na vikao vya bajeti, na yeye akiwa Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, anapaswa kuwapo wakati huo, bajeti ya nchi ni kitu nyeti sana, alisema Rweyemamu.
Kuhusu kauli mbiu, Mkurugenzi huyo alikanusha vikali madai ya kufutwa ile iliyohusu ufisadi.
Rais hawezi kufuta kauli mbiu, wataitumia hiyo hiyo waliyoipendekeza, alisema.
Source: Mtanzania
Ukiona mtu aliyekuwa na kiherehere cha kujikweza mbele ya wafanyakazi anaanza kuvuta miguu basi elewa kwamba nchi inaelekea kumshinda. Hana majibu ya Risala ya Wafanyakazi, Tume ya mapendekezo ya mishahara mpaka leo hii haijulikani report yake na kibaya zaidi dongo ya kauli mbiu limemuweka pabaya kwa kuwa lina ukweli kwa 100%. TUCTA wanatakiwa waendelee kivyao na warushe madongo hewani hata kama hakutakuwa na kiongozi wa serikali ili mradi msg itakuwa sent and delivered. Atakaeona dongo limemgusa basi atajua namna ya kulikwepa ama kujiweka mbali nalo, lakini JK hana ubavu wa kulikwepa. Tunachotaka sasa ni TUCTA iwe kiini cha mabadiliko ya fikra kwa watanzania kwa kuwa ina matawi sehemu zote mpaka vijijini. Huko ndiko kuliko na kura zinazowapa kiburi CCM kiasi kwamba wanaona kelele za mpangaji haziwanyimi usingizi japo siku hizi naona wanakesha hata kama hawakubali hilo!
na khamis mkotya
RAIS Jakaya Kikwete, hatakuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha sherehe za Mei mosi zitakazofanyika kitaifa mkoani Iringa.
Mwaliko wa sherehe hizo ulipelekwa kwake na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA). Uamuzi huo wa Rais, umeelezwa kwamba umetokana na majukumu mengi ya kitaifa yanayomkabili.
Kutokana na uamuzi huo, TUCTA imeeleza kusononeka kwa maelezo kuwa kuwapo kwa Rais katika maadhimisho hayo ni muhimu.
Pia Rais Kikwete amelalamikiwa kwamba amekataa kauli mbiu iliyokuwa imependekezwa na TUCTA kwa ajili ya sherehe za mwaka huu.
Kauli mbiu iliyopelekwa kwa Rais ilikuwa ikisema: Maisha bora yanawezekana tukiutokomeza ufisadi. TUCTA wanadai kwamba maneno hayo hayakumfurahisha Rais Kikwete.
Aidha, TUCTA imeeleza kushangazwa na uamuzi wa Rais kukataa kuhudhuria mkutano wa 96 ulioitishwa na Shirika la Kazi Duniani (ILO), utakaofanyika Geneva, Uswisi.
Imeelezwa kwamba kiongozi huyo ameahirisha kwenda huko kutokana na kubanwa na vikao vya bajeti inayotarajiwa kuwasilishwa bungeni Juni mwaka huu.
Naibu Katibu wa TUCTA, Nicholas Mgaya, alitoa maelezo hayo alipozungumza na MTANZANIA ofisini kwake jana, kuhusu maandalizi ya sherehe za Mei mosi.
Mgaya alisema mwaliko ulipelekwa kwa Rais Kikwete Februari, mwaka huu kupitia Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana.
Kwa mujibu wa Mgaya, wiki mbili zilizopita Shirikisho, kupitia wizara hiyo, lilipata taarifa kuwa Rais hatoweza kushiriki, badala yake atawakilishwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
"Tumesikitishwa hatua hiyo kwa kuwa inaonyesha anaanza kujitenga na wafanyakazi. Tunakubali Waziri Mkuu, lakini kwa shingo upande," alisema na kuongeza;
Kuhusu mkutano wa Geneva, Mgaya alisema Rais Kikwete alikuwa amealikwa na kwamba alipewa hadhi ya kufungua mkutano huo utakaofanyika Juni, mwaka huu kutokana na nafasi yake ya Uenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU).
Kwa mujibu wa Mgaya, mwaliko wa ILO kwa Rais Kikwete kushirikia katika mkutano huo ilikuwa ni nafasi nzuri inayoijengea sifa Tanzania.
"Hatujaridhika na sababu zilizotolewa na Ikulu kwamba Rais hatahudhuria mkutano huo. Ina maana Rais hana wataalamu hadi asimamie bajeti mwenyewe?, alihoji.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salvatory Rweyemamu, amejibu malalamiko ya TUCTA kwa kusema Rais ameona kuwa baada ya kuhudhuria Mei mosi mwaka 2006 mkoani Shinyanga na mwaka 2007 mkoani Mwanza, ameona sasa ni busara kutoa nafasi kwa mmoja wa wasaidizi wake.
Rais ana kawaida ya kutoa maelekezo ili awakilishwe katika shughuli mbalimbali. Hivi karibuni utakumbuka alifanya hivyo kwa kuwakilishwa na Makamu wa Rais nchini Uingereza na Denmark, alisema.
Rweyemamu alisema ni kweli Rais alialikwa katika mkutano wa ILO, lakini kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi ya kitaifa, ameomba asihudhurie, badala yake ameshauri apangiwe ziara ya kutembelea makao makuu ya chombo hicho kwa wakati mwafaka.
Alisema ameomba asihudhurie mkutano huo kwa vile Juni kutakuwa na vikao vya bajeti, na yeye akiwa Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, anapaswa kuwapo wakati huo, bajeti ya nchi ni kitu nyeti sana, alisema Rweyemamu.
Kuhusu kauli mbiu, Mkurugenzi huyo alikanusha vikali madai ya kufutwa ile iliyohusu ufisadi.
Rais hawezi kufuta kauli mbiu, wataitumia hiyo hiyo waliyoipendekeza, alisema.
Source: Mtanzania
Ukiona mtu aliyekuwa na kiherehere cha kujikweza mbele ya wafanyakazi anaanza kuvuta miguu basi elewa kwamba nchi inaelekea kumshinda. Hana majibu ya Risala ya Wafanyakazi, Tume ya mapendekezo ya mishahara mpaka leo hii haijulikani report yake na kibaya zaidi dongo ya kauli mbiu limemuweka pabaya kwa kuwa lina ukweli kwa 100%. TUCTA wanatakiwa waendelee kivyao na warushe madongo hewani hata kama hakutakuwa na kiongozi wa serikali ili mradi msg itakuwa sent and delivered. Atakaeona dongo limemgusa basi atajua namna ya kulikwepa ama kujiweka mbali nalo, lakini JK hana ubavu wa kulikwepa. Tunachotaka sasa ni TUCTA iwe kiini cha mabadiliko ya fikra kwa watanzania kwa kuwa ina matawi sehemu zote mpaka vijijini. Huko ndiko kuliko na kura zinazowapa kiburi CCM kiasi kwamba wanaona kelele za mpangaji haziwanyimi usingizi japo siku hizi naona wanakesha hata kama hawakubali hilo!