JK aikwepa Mei Mosi... Rais Kikwete hatahudhuria Mei mosi

Hana jipya la kuwambia wafanyakazi,maana Maisha bora yameyeyuka.Falsafa yake inatumika tena kumkaanga.EPA haina majibu,Mawaziri wake wanajiziulu n.k

Nyongeza ya mshahara kwa njia ya kisayansi(aliunda tume kutafiti) imekwama?Maana tume ilifanya utafiti na mapendekezo yametolewa hayatekelezeki.Na TUCTA wanahitaji kima cha chini 315k

Kukimbia wajibu si kusuluhisha tatizo.

Mkuu hawa mawaaziri hawajiuzulu, wamanchi wanawafukuza.... ni kelele zetu ndio zinawatoa...
 
Safari imeanza hiyo, tunaisubiri ripoti nyingine ya REDET tuone ameporomoka kiasi gani

REDET ya nani? ya yule fisadi, dikiteta na muuaji Mukandala ambaye ameshidwa kusimamia demokrasia kwenye chuo anachoongoza?

Hiyo REDET report imekufa kwenye kufika (dead on arrival).
 
Watanzania, tusimlaumu sana JK kwani taabu hizi zote na mzigo huu kaachiwa na Mkapa, kuwa miwaziri mizi, ujue kama asingeiteua kweli angejiweka pabaya, sasa tunamtaka aende pale Iringa akaseme nini jamani? Kikwete ana nia njema tuu ila hawa maswahiba zake ndiyo wanamuangusha

Hata yule mwizi aliyepigwa na wananchi wenye hasira kali pale Manzese wiki iliyopita, alisema kuwa alikuwa na nia nzuri ya kuipa cell phone ili apate pesa za kutibia mtoto wake mgonjwa.

Sijui nia nzuri ya Kikwete hapa ni kama hii!??????
 
tukta msimwalike waziri mkuu, nashauri mumualike mzee Mwinyi. Mpeni jukwaa la Kitaifa Rais Mwinyi kama walivyofanya wenzenu mwaka 1995 walipoamua kumkaribisha Rais Nyerere.
 
Kwanza alianza kuwakimbia Watanzania wanaoishi nje hasa US, sasa anaanza kukimbia hata walio Tanzania! Achia ngazi mambo yanakushinda.
 
Mwaka huu atakimbia sana,Maana hata hiyo taarifa yake ya kila mwisho wa mwezi kwenye luninga,bado itapimwa kwa yale atakayo sema.Niliwahi kusikia kuna mwingine alirudishiwa air port akitaka kukimbia nchi baada ya kushindwa kuongoza.

Mwisho wa mwezi April atuwekee ile Hotuba ya ufunguzi wa bunge mara baada ya kuapishwa kuwa mkuu wa kaya ili ajikague ni wapi alipoanguka atubu na kurejea.
 
Mwanakijiji,
Nyerere alialikwa 1995 kwa kuwa wale waliomualika waliamini kuwa anaweza kuwa na kitu cha kuwaeleza, na ninakumbuka alitoa hotuba ambayo naamini kuwa ni moja kati ya hotuba nzuri alizowahi kuzitoa na it is still relevant todate. Sasa unafikiri akialikwa Mwinyi atawaambia nini hao waalikaji?
 
gagnija, na hilo ndilo lengo langu, tumpe Mwinyi jukwaa azungumze na Taifa badala ya kumfuata fuata nyumbani. Tuone je na na yeye ana ujasiri wa kusema ukweli mbele ya wenye nguvu?
 
Watanzania, tusimlaumu sana JK kwani taabu hizi zote na mzigo huu kaachiwa na Mkapa, kuwa miwaziri mizi, ujue kama asingeiteua kweli angejiweka pabaya, sasa tunamtaka aende pale Iringa akaseme nini jamani? Kikwete ana nia njema tuu ila hawa maswahiba zake ndiyo wanamuangusha

Hivii wewe ukiwa na swahiba anaekuangusha utaendelea kumlea? ina maana watu wenye akili Tanzania ni Chenge, Lowasa, Karamagi, ... kati ya Watanzania milioni 40 kwa sasa. wenye uwezo wa kuwa mawaziri ni hao tuu.. Kauli yako inaonyesha ni jinsi gani watanzania tupo wavivu kufikiria
 
kikwete mwaka huu atakimbia mengi, na atawakimbia wengi.
na angeenda kwenye mkutano wa mei mosi angesema nini? samahanini lakini kila niliyemchagua kwenye nafasi ya uwaziri fisadi?
lazima kwa hali ilivyo akwepe watu. na bado....ndo kwanza mwanzo huu

Wabongo kwa umbeya!!!, Nongwa!!, majungu!!! mpaka lini????? Haya yametokea wapi? Haya semeni basi mgeni wa Mei Mosi atakuwa nani? Kwani ni lazima kila Mei Mosi Rais aseme? Waziri Mkuu, Waziri wa Kazi, Makamu wa Rais wakizungumza haitoshi? Kwanza huyu JK kila mwezi anazungumza yeye tu, mwaka huu awaachie na wenzake wasikike.
 
tukta msimwalike waziri mkuu, nashauri mumualike mzee Mwinyi. Mpeni jukwaa la Kitaifa Rais Mwinyi kama walivyofanya wenzenu mwaka 1995 walipoamua kumkaribisha Rais Nyerere.

Lets go for a change TUCTA...kila siku mboga za majani tu kwanini msimualike Dr Slaa mkabadili kidogo chakula?...kwanza ujumbe wenye mlipendekeza wenye kulenga vita dhidi ya ufisadi. Na yeye ni Mbunge, waziri Kivuli na Kiongozi wa upinzani.

Asha
 
Msanii amepatikana, ipo siku atakiri hadharani kwamba mambo yameshamshinda, na wapambanaji tupo tutampokea kijiti ili kukifikisha pale watanzania wanapotaka kifike, arobaini yake naona haiko mbali inakaribia sana tu washikaji.

We ni Hamad Yussuf naibu katibu mkuu wa CHADEMA kwetu Zanzibar au ni mtu mwingine? Hebu niambie basi jamani kama ni wewe nikupongeze

Asha
 
Asha Abdallah.. hata Dr. Slaa ni vizuri tu.. kwanini lazima wawe ni viongozi wa serikali? Imekuwa ni yale yale ya kwenye kufungua makanisa, mashule, majengo basi wanaoalikwa ni viongozi wa serikali tu... why?
 
Sasa rais wa jamhuri tena yetu ya Tanzania, anapoanza kukwepa wafanyakazi wa jamhuri something is not right, lakini hakuna siri ya zaidi ya mtu mmoja very soon tutayajua yanayojiri huko ndani maana hapa something is not very right............ na fumbo mfumbie mjinga maana mwerevu.......!

Yaaani sasa mkulu hataki tena zile ziara za wizarani na masokoni, na mahospitalini, kulikoni?

Tutaona mengi mwaka huu, anapoalikwa na MAFISADI anakuwa na muda lakini waliompigia kura hawathamini tena Tutafika tu.
 
Ni kweli Rais hana sera za Mei Mosi. Hata sera za kila mwezi naona atakuwa kaishiwa. Ni wakati muafaka sasa ajitenge na mafisadi ili aweze kutekeleza majukumu yake bila wasiwasi.
Lakini swali je ni kweli aweza kujitenga na mafisadi wakati ni marafiki zake wa karibu? NI sawa na Mkushi hawezi kubadili ngozi yake
 
Wabongo kwa umbeya!!!, Nongwa!!, majungu!!! mpaka lini????? Haya yametokea wapi? Haya semeni basi mgeni wa Mei Mosi atakuwa nani? Kwani ni lazima kila Mei Mosi Rais aseme? Waziri Mkuu, Waziri wa Kazi, Makamu wa Rais wakizungumza haitoshi? Kwanza huyu JK kila mwezi anazungumza yeye tu, mwaka huu awaachie na wenzake wasikike.

Awe Rais wa Jamhuri ya Muungano, aliyetoa ahadi lukuki ambazo alijua hazitekelezeki. MaMkwe huu si umbeya na si majungu amekwepa hana nondo za maswali yaliyo ktk risala si unajua mwaliko unaendana na risala. Mda wa yeye kuachia mwingine bado mpaka asawazishe mambo yenye utata alioanzisha yeye.
 
wajameni nchi imemshinda mkwere huyo alidhani nchi ni kama kuongoza nyumba yake..na wizara moja....ndio atie akili ikulu hakugombaniwi..atii...alikuwa anakimbiliaa nini na umri ule na uzoefu wake ule wa 1995?????ingekuwaje kama angepewa umri ule?na bado anatakiwa kulipa fadhila na pesa za walizotumia waliomuweka.......2010 mbona haifiki haraka tuone ngoma ????
 
Kama mwinyi atahutubia , sina haja ya kusikiliza, maana najua atasema nini (Mahakama ya kadhi...!)
 
Sasa rais wa jamhuri tena yetu ya Tanzania, anapoanza kukwepa wafanyakazi wa jamhuri something is not right, lakini hakuna siri ya zaidi ya mtu mmoja very soon tutayajua yanayojiri huko ndani maana hapa something is not very right............ na fumbo mfumbie mjinga maana mwerevu.......!

Yaaani sasa mkulu hataki tena zile ziara za wizarani na masokoni, na mahospitalini, kulikoni?



Umesema maneno yote sina la kuogeza ES .JK tulijua mbwe mbwe hizi zitaisha .Sasa atatfuta kila sababu kila kona .Alidhani ukada unakubalika kila kona siyo ? Urais ni kazi nzito na sasa atajua .Lakini huwa hana jamaa anacheka na saa tatu tu unaambiwa hakuna simu maana Rais kesha lala .Saa tatu usiku kwa hii Nchi iliyo jaa washikaji zake wa vijisenti .
 
Back
Top Bottom