Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,172
JK yaelekea haelewi misingi ya kuandika katiba mpya kuwa yapaswa kuwa ni shirikishi kuanzia uteuzi wa wale watakayoyakusanya maoni ya wananchi........................uamuzi wa JK kuunda Tume yake mwenyewe ambayo haitokani na wadau na ambayo haina nguvu ya kisheria inamaanisha lengo lake ni kuiwekea viraka katiba iliyopo.....................kama wale waliomtangulia waliopachika viraka 15 kwa katiba iliyopo.......................Hii yamaanisha ya kuwa..........
Maoni ya wananchi yatachakachuliwa kama yalivyochakachuliwa siku zilizopita...........
Huko nyuma tume za Raisi ziliundwa na zikapeleka mapendekezo yake kwa vyombo vya kisheria kwa marekebisho lakini havikuweza kuandaa katiba mpya........Sababu kuu ni kuwa wananchi wenyewe kupitia Bunge lao hawakushirikishwa katika kusimamia mchakato mzima ila ni Ikulu au Ofisi moja tu ya Raisi ndiyo iliyosimamia na kuratibu mchakato mzima..........
..........na huu mchakato wa JK lengo lake ni kuhakikisha ya kuwa CCM tu ndiyo itakuwa na uamuzi wa mwisho juu ya sura ambayo marekebisho ya katiba yatakavyokuwa na kwa hili nchi hii siyo wageni.......................
Tume ya Nyalali iliyoundwa na Raisi Mwinyi pamoja na kuwa ilisimamiwa na Jaji Mkuu iliishia kuona mapendekezo yake ya sheria 40 za kidhalimu kuishia kwenye makaratasi tu.......................
Hii yote ilitokana na hapakuwepo sheria ambayo iliipa nguvu tume hiyo kuwa mapendekezo yake yatajadiliwa moja kwa moja na Bunge bila ya kukarabatiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu....................
Wakati wa Mkapa tuliona "WHITE PAPER"....hakuna raia hata mmoja leo anayeweza kusema hivi ni vigezo vipi ambavyo Ikulu ilivitumia katika kuhakikisha ya kuwa mapendekezo ya marekebisho ya 13 ya Katiba yaliamuliwa na kupelekwa Bungeni
Tunachohitaji ni...............Bunge na wala ofisi ya Raisi kusimamia mchakato huo.......
1) Bunge kupitisha sheria ya mchakato mzima wa uandaaji wa ukusanyaji wa maoni ya raia wote, utaratibu mzima utakavyofuatwa kuhakikisha hakuna ambaye ataweza kuchakachua maoni tajwa........................
2) Wajumbe wa Tume wafanye maombi rasmi baada ya nafasi hizo kutangazwa na Ofisi ya Bunge kwenye vyombo vya habari...................
3) Maoni ya Wananchi kupelekwa kwa Mwanasheria Mkuu na yeye anapaswa kuyaundia muswada bila marekebisho yoyote yale..................
4) Bunge linaweza kuyarekebisha kama theluthi mbili ya Bunge lote linaafiki marekebisho hayo...................
5) Sheria ya kura ya maoni iundwe ili kuruhusu raia kuwa na sauti ya mwisho juu ya katiba hiyo ambayo kweli itakuwa ni mpya........................
Nje ya utaratibu huu katiba iliyopo itakuwa imewekwa viraka na JK kama maraisi waliomtanguliwa walivyofanya kwa kujiundia Tume ya Katiba ambayo waliibabatiza ni ya wadau wote bila ya kuwapa watanzania kushiriki katika kuichagua....................au kuiunda na Tume hiyo kutokuwa na ubavu wa kisheria.........
Maoni ya wananchi yatachakachuliwa kama yalivyochakachuliwa siku zilizopita...........
Huko nyuma tume za Raisi ziliundwa na zikapeleka mapendekezo yake kwa vyombo vya kisheria kwa marekebisho lakini havikuweza kuandaa katiba mpya........Sababu kuu ni kuwa wananchi wenyewe kupitia Bunge lao hawakushirikishwa katika kusimamia mchakato mzima ila ni Ikulu au Ofisi moja tu ya Raisi ndiyo iliyosimamia na kuratibu mchakato mzima..........
..........na huu mchakato wa JK lengo lake ni kuhakikisha ya kuwa CCM tu ndiyo itakuwa na uamuzi wa mwisho juu ya sura ambayo marekebisho ya katiba yatakavyokuwa na kwa hili nchi hii siyo wageni.......................
Tume ya Nyalali iliyoundwa na Raisi Mwinyi pamoja na kuwa ilisimamiwa na Jaji Mkuu iliishia kuona mapendekezo yake ya sheria 40 za kidhalimu kuishia kwenye makaratasi tu.......................
Hii yote ilitokana na hapakuwepo sheria ambayo iliipa nguvu tume hiyo kuwa mapendekezo yake yatajadiliwa moja kwa moja na Bunge bila ya kukarabatiwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu....................
Wakati wa Mkapa tuliona "WHITE PAPER"....hakuna raia hata mmoja leo anayeweza kusema hivi ni vigezo vipi ambavyo Ikulu ilivitumia katika kuhakikisha ya kuwa mapendekezo ya marekebisho ya 13 ya Katiba yaliamuliwa na kupelekwa Bungeni
Tunachohitaji ni...............Bunge na wala ofisi ya Raisi kusimamia mchakato huo.......
1) Bunge kupitisha sheria ya mchakato mzima wa uandaaji wa ukusanyaji wa maoni ya raia wote, utaratibu mzima utakavyofuatwa kuhakikisha hakuna ambaye ataweza kuchakachua maoni tajwa........................
2) Wajumbe wa Tume wafanye maombi rasmi baada ya nafasi hizo kutangazwa na Ofisi ya Bunge kwenye vyombo vya habari...................
3) Maoni ya Wananchi kupelekwa kwa Mwanasheria Mkuu na yeye anapaswa kuyaundia muswada bila marekebisho yoyote yale..................
4) Bunge linaweza kuyarekebisha kama theluthi mbili ya Bunge lote linaafiki marekebisho hayo...................
5) Sheria ya kura ya maoni iundwe ili kuruhusu raia kuwa na sauti ya mwisho juu ya katiba hiyo ambayo kweli itakuwa ni mpya........................
Nje ya utaratibu huu katiba iliyopo itakuwa imewekwa viraka na JK kama maraisi waliomtanguliwa walivyofanya kwa kujiundia Tume ya Katiba ambayo waliibabatiza ni ya wadau wote bila ya kuwapa watanzania kushiriki katika kuichagua....................au kuiunda na Tume hiyo kutokuwa na ubavu wa kisheria.........
Last edited by a moderator: