JK aanza kunyooka..

KadaMpinzani

JF-Expert Member
Jan 31, 2007
3,715
86
KIKWETE_S.jpg


:: Akataa nchi kuwa shamba la wajinga
:: Aagiza wababaishaji wageni wasipewe kazi
:: Mkandarasi Sam Nujoma aonjeshwa joto
:: Awageukia TANROADS na bomoabomoa zao

Na Godfrey Dilunga, Singida

RAIS Jakaya Kikwete (pichani) sasa amewageukia wanataaluma na watendaji wa Serikali katika kuhakikisha udhibiti wa fedha za umma unaimarika, akisema “nchi haiwezi kuendelea kuwa shamba la wajinga.”

Rais alitoa msimamo wake huo kwa kauli kali, mara baada ya kusomewa taarifa ya ujenzi wa barabara mbalimbali nchini, ikiwamo ya Dodoma-Singida, hususan kipande cha Isuna-Manyoni, chenye urefu wa kilomita 55, jana.

Taarifa hiyo ilisomwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omari Chambo, katika eneo la Isuna, barabara kuu ya Dodoma-Singida.

Katika taarifa yake iliyoamsha ari ya Rais kutaka fedha za umma alizoziita “fedha za masikini,” Chambo alisema baadhi ya makampuni ya ujenzi wa barabara nchini yameshindwa kutimiza wajibu wao kikamilifu.

Alisema hatua ambazo Serikali imechukua dhidi ya kampuni hizo ni pamoja na kuwafukuza baadhi ya makandarasi na wengine kuwakata fedha ya tozo. Aliwataja wakandarasi waliofukuzwa na Serikali kuwa ni pamoja na aliyekuwa akijenga barabara ya Dodoma-Singida, Kigoma-Lusahunga (mkoani Kagera) na kipande cha barabara ya Mbwemkuru-Lindi. Kwa upande wa makandarisi watakaokatwa fedha za tozo ni pamoja na anayejenga barabara ya Sam Nujoma, Dar es Salaam.

Akimzungumzia mkandarasi huyo, Chambo alisema; “Si busara kumfukuza kwa wakati huu, bali adhabu anayopewa na Serikali ni kukatwa fedha za tozo.”

Baada ya taarifa hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Korne, alipanda jukwaani na kumkaribisha Rais kuzungumza na wananchi waliokusanyika katika eneo hilo, ambalo pia Rais aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa kipande hicho cha barabara.

Akitumia maneno makali kuonyesha kukerwa na makandarasi na namna fedha za umma zinavyotumika ovyo, Rais alisema: “Kinachowaponza ni kutafuta mkandarasi wa gharama nafuu mno isiyolingana hata na tathmini yenu.”

Akasema: “Bure ina gharama. Kilichotokea ni fundisho. Thamani ya ujenzi wa barabara mnaijua kwa sababu mnatakiwa kwanza mfanye tathmini ya awali, sasa mkandarasi anajitokeza kwa bei nafuu kuliko tathmini yenu mnamkimbilia, mnampa tenda. “Baadaye kazi inafika katikati analalamika gharama za ujenzi zimepanda, fedha haitoshi…mnaanza makubaliano mapya. Msiwape kazi makandarasi wa namna hii.

“Kwanza...hivi hamna namna ya kuwaadhibu. Nadhani sasa wakitokea makandarasi wa namna hii, ambao wengi ni wa kigeni wasipewe tena kazi popote nchini.

“Lazima tuonyeshe kuwa wakali. Hawa wananyonya fedha zetu. Sisi ni nchi masikini, wao wanatoka nchi tajiri. Simamieni ukweli na haki kumpata mkandarasi, si kukimbilia tu unafuu msio na uhakika nao.

“Lazima watendaji muonekane mna uchungu na fedha za wananchi,” alisema Rais na baadaye kwa kauli ya ukali alisema: “Tusipofanya hivi siku zote tutakuwa shamba la wajinga.”

Aliendelea kutamka; “Nasisitiza iwe fundisho, haya yasijiridie, msiwe mbumbumbu, mmesoma…mnajua thamani ya barabara, kwa nini mtu awadanganye kujenga kwa gharama yenye unafuu wa kupindukia?”

Hata hivyo, katika hatua nyingine, Rais Kikwete aliwageukia watendaji wa Wakala wa Barabara wa Serikali (TANROAD) na Wizara ya Miundombinu, akiwashangaa kuacha watu wakijenga katika hifadhi za barabara na wanapoanza kuishi wanawataka kuhama.

“Hivi nyie, mtu anachimba msingi mnamuangalia, tena mnapita hapo, anapandisha ukuta, anapaua…anahamia, hatua zote hizo mnamuangalia tu, baadaye akishahamia mnamtaka kuondoka. Sasa hawa wanavunja sheria mnawaangalia kuweni makini,” alionya Rais.
 
Vinywa vinatamka ukweli na kuonyesha hali ya matumaini lakini AKILI, MIKONO na MIGUU havionyeshi kutenda katika kusimamia kauli hizo. Wakandarasi wengi hususani WACHINA wameonyesha dharau kubwa kwa Taifa letu kwani kazi wanazopewa wanajifanyia kwa viwango na wakati watakao wao pasipo kuzingatia makubaliano yaliyowekwa. Wafukuzwe na sio kudai tu kwamba wanakatwa fedha za TOZO ambazo hatujui zinakokwenda huku TAIFA likizidi kuingia gharama kubwa katika ujenzi wa miundombinu yake hususani Barabara. Mbona wakati wa MAGUFULI alikuwa anawatimua pasipo kusubiri amri ya RAIS?.
 
mabadiliko ya ghafla huwa yanasababisha maafa mengi sana ni sawa kuweka maji ya moto kweye glass huwa ina fasuka kutokana na tofauti ya halijoto (thermo aggitation) saasa akipitiliza yanaweza yakawa kama ya mzee wa bulawayo. inabidi awe gradually. tunauzoefu wa kunyonywa kwa enzi ndio maana wahenga walituandalia misemo ya uvumilivu huku tukiwa tunaelimishana haki zetu.tusije tukaendelea sana mpaka ifike kipindi hatumiliki gari ingawa tunaliendehsa(lease), hatumiliki nyumba ingawa tunaishi na kuilipia(mortage)., hatumiliki pesa ingawa tunatmia (credit card) hatujivuni watoto ingawa tume zaa( child support)
 
Hajaongea kitu cha tofauti na siku zote na ndo maana serikali yake ikapewa jina la ze comedy, tunataka vitendo kuonyesha kuwa ameanza kubalika na sio maneno matupu.
 
"Lazima tuonyeshe kuwa wakali. Hawa wananyonya fedha zetu. Sisi ni nchi masikini, wao wanatoka nchi tajiri. Simamieni ukweli na haki kumpata mkandarasi, si kukimbilia tu unafuu msio na uhakika nao.

"Lazima watendaji muonekane mna uchungu na fedha za wananchi," alisema Rais na baadaye kwa kauli ya ukali alisema: "Tusipofanya hivi siku zote tutakuwa shamba la wajinga."


maneno juu ya mstari,

ila kwa 'mswahili' maneno laini matendo nayo yatabakia hayo hayo, Mh Rasi angeondoa hayo maneno "tuonyeshe", na "Muonekane" yabakie matamshi...

..."lazima kuwa wakali..."

..."lazima watendaji muwe na uchungu na fedha za wananchi"


...naamini ujumbe ungewagusa zaidi, anyway, labda ndio style ya lugha yake.
 
Haya ni yaleyale ya kupiga makelele ya kumfukuza mwizi wakati umejibanza ndani ,unasema tu kapita huku kaendea kule kisha unarudi ndani asubuhi unauliza kama mifanikiwa kumkamata yule mwizi wa jana,pengine wewe ndie ulimpa hifadhi.
Mheshimiwa Kikwete makelele yako yamekuwa mengi na kadili siku zinavyoendelea ndio inaelekea sasa unatuwekea zogo kwa kutuelekeza wapi mwizi wetu yupo , hivi muheshimiwa Muungwana huoni kama hawa wezi unao ndani au huhisi kama hawa wezi umewaficha na kuwaelekeza wengine njia alioelekea.
Huu si wakati wa kufahamishana na kuelezana huu ni wakati wa utekelezaji na uwajibikaji ,hayo mambo ya wananchi kujenga sehemu ambazo ni hifadhi ya njia hayakuanza jana wala juzi ,na sababu kuu ni ahadi hewa zinazoekwa na serikali bila ya kujiwekea muda ,unatoa ahadi utajenga barabara baada ya mwaka mmoja inapita miaka kumi hakuna chochote wala alama kama sehemu fulani itajengwa barabara,huu ni uzembe unaofanywa na watekelezaji ,unapoamua kupitisha bara bara basi hata plani za viwanja ikiwa zitajengwa nyumba inabidi ziwepo,yeyote anaejenga aonyeshe mchoro aliopewa na baraza la mji.
Muungwana watekelezaji wako ndio wa kuwashughulikia na sio makandarasi ambao wana mikataba mifukoni mwao ,wanaweza wakaipeleka serikali yako mahakamani kwa jinsi walivyotulia na makaratasi ya mikataba ndani ya mifuko yao ,si unaona hizo feza ya umeme inavyoendelea kuchotwa hadi leo na haijulikani inakwenda wapi.Sasa hata hizo za barabara nazo zitaenda kwenye njia hizo hizo.
 
KIKWETE_S.jpg


:: Akataa nchi kuwa shamba la wajinga
:: Aagiza wababaishaji wageni wasipewe kazi
:: Mkandarasi Sam Nujoma aonjeshwa joto
:: Awageukia TANROADS na bomoabomoa zao

Na Godfrey Dilunga, Singida

RAIS Jakaya Kikwete (pichani) sasa amewageukia wanataaluma na watendaji wa Serikali katika kuhakikisha udhibiti wa fedha za umma unaimarika, akisema “nchi haiwezi kuendelea kuwa shamba la wajinga.”

Rais alitoa msimamo wake huo kwa kauli kali, mara baada ya kusomewa taarifa ya ujenzi wa barabara mbalimbali nchini, ikiwamo ya Dodoma-Singida, hususan kipande cha Isuna-Manyoni, chenye urefu wa kilomita 55, jana.

Taarifa hiyo ilisomwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu, Omari Chambo, katika eneo la Isuna, barabara kuu ya Dodoma-Singida.

Katika taarifa yake iliyoamsha ari ya Rais kutaka fedha za umma alizoziita “fedha za masikini,” Chambo alisema baadhi ya makampuni ya ujenzi wa barabara nchini yameshindwa kutimiza wajibu wao kikamilifu.

Alisema hatua ambazo Serikali imechukua dhidi ya kampuni hizo ni pamoja na kuwafukuza baadhi ya makandarasi na wengine kuwakata fedha ya tozo. Aliwataja wakandarasi waliofukuzwa na Serikali kuwa ni pamoja na aliyekuwa akijenga barabara ya Dodoma-Singida, Kigoma-Lusahunga (mkoani Kagera) na kipande cha barabara ya Mbwemkuru-Lindi. Kwa upande wa makandarisi watakaokatwa fedha za tozo ni pamoja na anayejenga barabara ya Sam Nujoma, Dar es Salaam.

Akimzungumzia mkandarasi huyo, Chambo alisema; “Si busara kumfukuza kwa wakati huu, bali adhabu anayopewa na Serikali ni kukatwa fedha za tozo.”

Baada ya taarifa hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Korne, alipanda jukwaani na kumkaribisha Rais kuzungumza na wananchi waliokusanyika katika eneo hilo, ambalo pia Rais aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa kipande hicho cha barabara.

Akitumia maneno makali kuonyesha kukerwa na makandarasi na namna fedha za umma zinavyotumika ovyo, Rais alisema: “Kinachowaponza ni kutafuta mkandarasi wa gharama nafuu mno isiyolingana hata na tathmini yenu.”

Akasema: “Bure ina gharama. Kilichotokea ni fundisho. Thamani ya ujenzi wa barabara mnaijua kwa sababu mnatakiwa kwanza mfanye tathmini ya awali, sasa mkandarasi anajitokeza kwa bei nafuu kuliko tathmini yenu mnamkimbilia, mnampa tenda. “Baadaye kazi inafika katikati analalamika gharama za ujenzi zimepanda, fedha haitoshi…mnaanza makubaliano mapya. Msiwape kazi makandarasi wa namna hii.

“Kwanza...hivi hamna namna ya kuwaadhibu. Nadhani sasa wakitokea makandarasi wa namna hii, ambao wengi ni wa kigeni wasipewe tena kazi popote nchini.

“Lazima tuonyeshe kuwa wakali. Hawa wananyonya fedha zetu. Sisi ni nchi masikini, wao wanatoka nchi tajiri. Simamieni ukweli na haki kumpata mkandarasi, si kukimbilia tu unafuu msio na uhakika nao.

“Lazima watendaji muonekane mna uchungu na fedha za wananchi,” alisema Rais na baadaye kwa kauli ya ukali alisema: “Tusipofanya hivi siku zote tutakuwa shamba la wajinga.”

Aliendelea kutamka; “Nasisitiza iwe fundisho, haya yasijiridie, msiwe mbumbumbu, mmesoma…mnajua thamani ya barabara, kwa nini mtu awadanganye kujenga kwa gharama yenye unafuu wa kupindukia?”

Hata hivyo, katika hatua nyingine, Rais Kikwete aliwageukia watendaji wa Wakala wa Barabara wa Serikali (TANROAD) na Wizara ya Miundombinu, akiwashangaa kuacha watu wakijenga katika hifadhi za barabara na wanapoanza kuishi wanawataka kuhama.

“Hivi nyie, mtu anachimba msingi mnamuangalia, tena mnapita hapo, anapandisha ukuta, anapaua…anahamia, hatua zote hizo mnamuangalia tu, baadaye akishahamia mnamtaka kuondoka. Sasa hawa wanavunja sheria mnawaangalia kuweni makini,” alionya Rais.



Kama kweli alivaa hivi jana na alikuwa ana kagua barabara na kuongea na wananchi ,nasema kama alivaa hivi jana na kuzungukwa na wana CCM namna haya ndiyo tunayo yakataa hapa .Lakini hii picha inaonekana ni ya wakati wa kampeni manazi wameitumia kuleta habari hii .
 
Hana lolote kila kukicha magazeti yanampamba kwa hili kwa lile lakini vitendo hatuoni akisha sema na kuondoka hali inaendelea kama kawaida hashupalii mambo kama mzee Ben.Hana jipya huyu maneno tu na atachonga sana.
 
Hana lolote kila kukicha magazeti yanampamba kwa hili kwa lile lakini vitendo hatuoni akisha sema na kuondoka hali inaendelea kama kawaida hashupalii mambo kama mzee Ben.Hana jipya huyu maneno tu na atachonga sana.

Lakini ikifika kwenye uchaguzi tunaishia kusema ..jamaa ana nyota kali sana ndio mana anapendwa....then tunampigia lol
 
Kama kweli alivaa hivi jana na alikuwa ana kagua barabara na kuongea na wananchi ,nasema kama alivaa hivi jana na kuzungukwa na wana CCM namna haya ndiyo tunayo yakataa hapa .Lakini hii picha inaonekana ni ya wakati wa kampeni manazi wameitumia kuleta habari hii .

Kama kweli bado anavaa hivi wakati wa kushughulikia maendeleo, inatakiwa aambiwe tu wakati wa kampeni za uchaguzi umeisha kwisha sasa hivi ni kazi na kutimiza yale aliyoyaahidi.
 
kwani si mwana ccm ?

1. Kwani mambo aliyokua akiyaongelea (e.g ujenzi wa barabara nk) yanagharamiwa na CCM?

2. Kwani CCM ilimlipia per diem siku hiyo?

3. Na yule waziri wa miundombinu aliyekuwa naye huko ziarani alikuwa analipwa per diem na CCM?

4. Kwani magari aliyokwenda nayo huko ziarani yaliwekwa mafuta na CCM? CCM inagharamia service ya hayo magari?

Kama jibu ni NO basi ujue kuwa there's something wrong in the mindsets of the people in question... Kama wanashindwa kutofautisha vitu vidogo namna hii basi mhhh...

Ila I doubt kama kweli alikwenda kinamna hii huko Singida, maana hata ukiangalia bodyguards wake ni wa ki-Chama Cha Mafisadi.
 
Jamani Kikwete Ametajwa Katika Hii Post Kama Ameanza Kunyooka.....! Is It Not Right For Him To Cry For Public Fund? Mheshimiwa Hapa Ameongelea Kuhusu Barabara...... Sisi Twaja Kuhusu Mavazi...... Mavazi Ndo Hoja?
lets Back Kikwete On This....... Bravo Kikwete Bravo Kikwete......! Now You Are Coming....!
 
Jamani Kikwete Ametajwa Katika Hii Post Kama Ameanza Kunyooka.....! Is It Not Right For Him To Cry For Public Fund? Mheshimiwa Hapa Ameongelea Kuhusu Barabara...... Sisi Twaja Kuhusu Mavazi...... Mavazi Ndo Hoja?
lets Back Kikwete On This....... Bravo Kikwete Bravo Kikwete......! Now You Are Coming....!

mzee kuhusu mavazi ya jk, hizo ni kebehi tu watu wasiokuwa na la kupinga. Watu hawawezi kukubali the fact the guy anaanza kunyooka, lakini tutasubiri tu hadi muda utakapofika, watajionea !
 
Hivi JK alipinda lini hadi aanze kunyooka? Nilidhani kuwa JK ni chaguo la mungu kama tulivyoambiwa na viongozi wa dini na wapambe wake wakati wa uchaguzi wa 2005?
 
Hivi JK alipinda lini hadi aanze kunyooka? Nilidhani kuwa JK ni chaguo la mungu kama tulivyoambiwa na viongozi wa dini na wapambe wake wakati wa uchaguzi wa 2005?

JK anaifanyia mazuri hii nchi. Mpeni muda tu asafishe chama chake na kisha ajenge nchi na kuiletea maendeleo. Wapinzani nyie hakuna zuri hata moja ambalo mmeona?
 
JK anaifanyia mazuri hii nchi. Mpeni muda tu asafishe chama chake na kisha ajenge nchi na kuiletea maendeleo. Wapinzani nyie hakuna zuri hata moja ambalo mmeona?

and he is on his way up there ! trust me mzee !
 
Back
Top Bottom