Jiunge nami kusema hapana kwa udhalilishaji na ubaguzi anaoufanya mmliki wa clock tower café Iringa

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
13,636
19,733
JIUNGE NAMI KUSEMA HAPANA KWA UDHALILISHAJI NA UBAGUZI ANAOUFANYA MMLIKI WA CLOCK TOWER CAFÉ IRINGA.

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
Nimekuwa mteja wa mgahawa wa Clock Tower Café uliopo barabara ya Dodoma/Uhuru Avenue katika Manispaa ya Iringa tangu uanzishwe mwaka jana. Nimekuwa nikipata huduma ya chakula katika Mgahawa wa Clock Tower nikiwa ama peke yangu au nikiwa na wageni au wateja wangu kwa kuwa ofisi yangu ya Uwakili ipo jirani tu na mgahawa huu. Hata hivyo jana tarehe 9 mwezi Mei mwaka 2019 limetokea tukio ambalo limenisononesha na kunifanya nisiwe tena na hamu ya kupata huduma ya chakula katika mgahawa wa Clock Tower Café wa hapa Iringa.

Jana ilikuwa ni siku ya tatu/ya nne ya mwezi wa Ramadhan. Nami nilikuwa katika saumu lakinijana wakati natoka mahakamani wakati napita Clock Tower Café nilijisikia haja nikaona niinge ili nijisaidie. Mnamo saan 4.00 asubuhi hivi niliingia Clock Tower Café. Nilipoingia nilimkuta Mmiliki wa Clock Tower Café, Iringa akiwa na mfanyakazi wake wa muda mrefu tangu enzi eneo hilo lilipokuwa Iringanet ikitoa huduma za mtandao wa internet. Kama ilivyo desturi niliwasalimia na kuingia ndani nikapita chooni.

Wakati nataka kutoka Clock Tower Café, niliwakuta Mmiliki na mfanyakazi wake wakiwa eneo lile lile na Mmiliki alinikabili kwa ujeuri na katika hali ya udhalilishaji na kashfa kwangu. Mbele ya wateja na wafanyakazi wa Clock Tower Café Iringa alinionyesha kwa sauti ya ukali kama vile mimi ni motto mdogo sana poster yenye maneno “Management reserves the right to refuse admission” iliyobandikwa ukutani. Maneno hayo ya Kiingereza yanamanisha: “Utawala unayo haki ya kumkataza mtu yoyote kuingia”. Na kisha kwa maneno makali akaniambia eti mimi ni mteja mbaya na kamwe hataki kuniona nikiingia au kununua chochote katika mgahawa wake wa Clock Tower Café Iringa na kwamba choo chake sio choo cha umma.

Kwa kweli nilifedheheka sana na kuvunjiwa heshima yangu katika jamii kwa tukio hili na sikuamini kinachotokea. Nimekuwa ninamfahamu Mmiliki huyo wa Clock Tower Café Iringa kwa miaka mingi sana name nimekuwa nikimchukulia kwamba ni jamaa yangu na yeye ananifahamu kwa kina na kazi ninazofanya hapa Iringa na hata baba yake namfahamu na tuna mahusiano mazuri tu kwa miaka mingi. Nimemfahamu Mmiliki huyu wa Clock Tower Cafe Iringa tangu mwaka 2015 nilipokuwa nafanya kazi Iringa na nikiwa mteja wa Iringanet tangu ilipokuwa jingo la Ghorofa pale Mshindo hadi anahamia hapa Barabara ya Dodoma. Kwa upole, nilimsihi na kumkumbusha kwamba tuko ndani ya mwezi wa Ramadhani na si vizuri kunifanyia kitendo cha udhalilishaji lakini alibaki na msimamo wake kuwa hanihitaji mimi wakla wananihusu kuwa wateja wa Clock Tower Café na kwamba niondoke na kamwe nisiingie tena Clock Tower Café Iringa. Ilibidi niondoke kwa aibu kimya kimya kwa unyonge mithili ya mbwa aliyemwagia maji akiogopa hata kubwekawa. Na jambo hili lilinishangaza sana kwa sababu sehemu ya biashara ni sehemu ya umma ambapo kila mtu anaweza kuingia na kutoka.

Kwa kweli tukio hili lininsononesha, kunidhalilisha na kunikumbisha si tukio lilimtokea mmoja wa wagombe Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alipoingia katika Hotel moja Mjini Dar es Salaam, Uongozi wa Hotel ulikataa hata kumhudumia maji ya kunywa na pia unakumbusha madhila ya siku za ukoloni ambapo watu waafrika licha ya kuwa ndiyo wenyeji wa nchi hii walikuwa wanabaguliwa kwa rangi na hadhi yao na kukatazwa kuingia katika mahoteli au migahawa ya watu weupe. Pale jijini Tanga ilikuwa rahisi mbwa kuingia Planters Hotel lakini si Mwaafrika. Na marehemu Mzee Erasto Mang’enya katika kitabu chake kimoja anaeleza madhila haya ya ubaguzi kwa waafrika pamoja na elimu yake na kuwa mjumbe wa Mamlaka ya Mji alikuwa haruhusiwi kuingia katika Hotel za watu weupe kwa kuwa tu alikuwa ni Mwaafrika.

Na ni jambo la kusikitisha zaidi kuona kuwa baada ya zaidi ya nusu karne ya nchi yetu ya Tanzania na pia Visiwa vya Unguja na Pemba kuwa nchi huru, bado wapo watu kama Mmiliki wa Clock Tower Café Iringa ambao wanaona wanayo haki ya kumnyanyasa Mtanzania na kwamba Mwaafrika kwao ni mtu dhalili asiye na hadhi au haki ya kupata huduma katika biashara zao. Jambo hili halivumiliki hata kidogo na kamwe siwezi kukaa kimya katika hili kuona mtu kwa sababu yeye ni Mwaarabu au Mweupe anayo haki ya kumnyanyasa mtu mweusi katika ardhi ya mababu zake. Je mtu mwenye rangi nyeupe akiingia Clock Tower Café kwenda choo kujisaidia na kasha kutoka bila ya kupata huduma yoyote, je Mmiliki huyu angemsemesha katika kama alivyonisemesha mie kijeuri?

Kama Mtanzania na Mwaafrika naona fahari kuwa nimepata bahati ya kutembelea au kuishi katika nchi zingine za Afrika Mashariki, Ulaya (Norway) na Marekani (USA) lakini katika kutembea kwangu kote huko sijawahi kukatazwa kupata huduma hata ya kujisaidia chooni katika mgahawa au Hotel yoyote kokote kule duniani isipokuwa hapa Iringa katika mgahawa huu wa Clock Tower Café. Kote nilipopata huduma hotelini au mgahawani nimekuwa nikipata heshaima ya utu wangu kwa usawa bila ya kujali hali yangu, rangi yangu au Utaifa wangu hata kama nilikuwa Mwaafrika pekee mahali hapo. Kamwe sijawahi kutokewa na tukio la kubaguliwa na kuonekana dhalili na nisiye na hadhi yoyote isipokuwa jana mbele ya Mmiliki, wafanyakazi na wateja wa Clock Tower Café Iringa ndani ya Mji na nchi yangu. Jambo hili halivumiliki na ni lazima kwa vitendo tulikemee.

Msimamo wangu ni kwamba tukio lililonitokea jana kamwe lisimtokee mkazi au mtu yoyote anayetembelea Iringa. Rai yangu ni kuwa wakazi na watu wote wanaotembelea Iringa kamwe tusiingie kupata huduma Clock Tower Café Iringa kwani Mmili hatuhitaji sisi anao wateja wake wenye hadhi ya kupata huduma ya chakula chake na sio sisi wakazi na watu wanaotembelea Iringa. Tusimmudhi tuwache Mmiliki huyu awahudumie wateja wake anaowataka kwa raha zake.

Tuungane pamoja kusema hapana kwa udhahlilishaji na ubaguzi anaoufanya Mmiliki wa Clock Tower Café katika nchi yetu na mji wetu!

Tafadhali mhabarishe na mwingine!

ZUBERI HAMISI NGODA
Iringa, Tanzania
Simu: +255 655 200 200
E-Mail: advocate.ngoda@gmail.com
May 10 , 2019

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
 
Umeandika/Umecopy Mkeka mrefu sanaa
Jinsi wabongo walivyo wavivu,watakuwa Wamesoma na ilipofika Juu juu Waka scroll.

In summary

Hilo bandiko Linahusu Ubaguzi (kwa mujibu Wake)
Muandishi Ni mwanasheria/wakili
anaishi Iringa.
Ni mteja mzuri sana wa Mgahawa uliopo Clock Tower Iringa dodoma road.
Akiwa katika harakati Zake za Kuweka mkono kinywaji,alibanwa na haja Sasa kwa Kuwa Ni mteja wa pale na Ni mwez mtukufuku (ramadhani) akaon ngoja nikaji sitili pale (kujisaidia japo hajasema Kama ilikuwa kubwa au ndogo haha yamkini Kubwa).

wakati kashamaliza kuji hajabisha,ghafla mhudumu akamuambia Kuwa "Yeye c Mteja mzuri na anatakiwa asikanyage Tena pale"

na hiyo ndiyo hoja yake Kuwa. aliambiwa asikanyage Tena hapo.bila sababu ya Maana.
so akaona Kuwa ame baguliwa (C unajua Wanasheria tena?!).

Kupitia Ubaguzi wake akatumia ref za wakati wa ukoloni jinsi watu walivyokuwa wanabaguliwa katika nchi yao.

Ni Hayo TU.
 
Umeandika/Umecopy Mkeka mrefu sanaa
Jinsi wabongo walivyo wavivu,watakuwa Wamesoma na ilipofika Juu juu Waka scroll.

In summary

Hilo bandiko Linahusu Ubaguzi (kwa mujibu Wake)
Muandishi Ni mwanasheria/wakili
anaishi Iringa.
Ni mteja mzuri sana wa Mgahawa uliopo Clock Tower Iringa dodoma road.
Akiwa katika harakati Zake za Kuweka mkono kinywaji,alibanwa na haja Sasa kwa Kuwa Ni mteja wa pale na Ni mwez mtukufuku (ramadhani) akaon ngoja nikaji sitili pale (kujisaidia japo hajasema Kama ilikuwa kubwa au ndogo haha yamkini Kubwa).

wakati kashamaliza kuji hajabisha,ghafla mhudumu akamuambia Kuwa "Yeye c Mteja mzuri na anatakiwa asikanyage Tena pale"

na hiyo ndiyo hoja yake Kuwa. aliambiwa asikanyage Tena hapo.bila sababu ya Maana.
so akaona Kuwa ame baguliwa (C unajua Wanasheria tena?!).

Kupitia Ubaguzi wake akatumia ref za wakati wa ukoloni jinsi watu walivyokuwa wanabaguliwa katika nchi yao.

Ni Hayo TU.
Mwanasheria akikwambia summary ni kurasa kumi, akikwambia anaandika kwa kirefu ni kurasa 100 kuendelea.
asante sana kwa kufupisha, hapo imefupishwa sana .

naomba upige kura hapo juu, tupinge ubaguzi alioanzisha nyerere na mandela
 
Sijajua labda kuna utaratibu umeukiuka wakati unaingia kwa kuchukulia kuwa wewe anakufahamu ni nani katika mji wa Iringa na pengine wewe ni wakili maarufu.

Kwa kuwa wewe ni mwanasheria, unatambua kabisa kuwa tukimhukumu na kumwadhibu huyu mtu kwa kusikiliza upande mmoja pekee, yaani wewe tutakuwa hatujamtendea haki. Ni lazima asikilizwe kwanini ametenda vile.

Pia tukisema kususa biashara yake si tu kwamba tunamuumiza yeye, la hasha! Tunaumiza pia wafanyakazi na wategemezi wao kwani hawatapata mshahara. Pia tunapunguza pato la Taifa kwani huyo ni mlipa kodi.

USHAURI
Mfuate tu kwa ustaarabu na kumuuliza.... sheikh... nini nimetenda kinyume, kisha msameheane na muendeleze mahusiano kwa ustawi wa jamii, Iringa na nchi yetu.

Take care.
CC. jaji mfawidhi
 
Pole sana advocate...
Umeingia mara ngapi kuoata hiyo huduma ya haja ndogo hapo clock tower cafe iringa..??

Wateja mkishaizoea sana ofisi kuna tabia ovu huwa hutokeza,
Wengine kuingia counter
Kuondoka bila kulipa kwa kuwa anafahamika
 
JIUNGE NAMI KUSEMA HAPANA KWA UDHALILISHAJI NA UBAGUZI ANAOUFANYA MMLIKI WA CLOCK TOWER CAFÉ IRINGA.

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
Nimekuwa mteja wa mgahawa wa Clock Tower Café uliopo barabara ya Dodoma/Uhuru Avenue katika Manispaa ya Iringa tangu uanzishwe mwaka jana. Nimekuwa nikipata huduma ya chakula katika Mgahawa wa Clock Tower nikiwa ama peke yangu au nikiwa na wageni au wateja wangu kwa kuwa ofisi yangu ya Uwakili ipo jirani tu na mgahawa huu. Hata hivyo jana tarehe 9 mwezi Mei mwaka 2019 limetokea tukio ambalo limenisononesha na kunifanya nisiwe tena na hamu ya kupata huduma ya chakula katika mgahawa wa Clock Tower Café wa hapa Iringa.

Jana ilikuwa ni siku ya tatu/ya nne ya mwezi wa Ramadhan. Nami nilikuwa katika saumu lakinijana wakati natoka mahakamani wakati napita Clock Tower Café nilijisikia haja nikaona niinge ili nijisaidie. Mnamo saan 4.00 asubuhi hivi niliingia Clock Tower Café. Nilipoingia nilimkuta Mmiliki wa Clock Tower Café, Iringa akiwa na mfanyakazi wake wa muda mrefu tangu enzi eneo hilo lilipokuwa Iringanet ikitoa huduma za mtandao wa internet. Kama ilivyo desturi niliwasalimia na kuingia ndani nikapita chooni.

Wakati nataka kutoka Clock Tower Café, niliwakuta Mmiliki na mfanyakazi wake wakiwa eneo lile lile na Mmiliki alinikabili kwa ujeuri na katika hali ya udhalilishaji na kashfa kwangu. Mbele ya wateja na wafanyakazi wa Clock Tower Café Iringa alinionyesha kwa sauti ya ukali kama vile mimi ni motto mdogo sana poster yenye maneno “Management reserves the right to refuse admission” iliyobandikwa ukutani. Maneno hayo ya Kiingereza yanamanisha: “Utawala unayo haki ya kumkataza mtu yoyote kuingia”. Na kisha kwa maneno makali akaniambia eti mimi ni mteja mbaya na kamwe hataki kuniona nikiingia au kununua chochote katika mgahawa wake wa Clock Tower Café Iringa na kwamba choo chake sio choo cha umma.

Kwa kweli nilifedheheka sana na kuvunjiwa heshima yangu katika jamii kwa tukio hili na sikuamini kinachotokea. Nimekuwa ninamfahamu Mmiliki huyo wa Clock Tower Café Iringa kwa miaka mingi sana name nimekuwa nikimchukulia kwamba ni jamaa yangu na yeye ananifahamu kwa kina na kazi ninazofanya hapa Iringa na hata baba yake namfahamu na tuna mahusiano mazuri tu kwa miaka mingi. Nimemfahamu Mmiliki huyu wa Clock Tower Cafe Iringa tangu mwaka 2015 nilipokuwa nafanya kazi Iringa na nikiwa mteja wa Iringanet tangu ilipokuwa jingo la Ghorofa pale Mshindo hadi anahamia hapa Barabara ya Dodoma. Kwa upole, nilimsihi na kumkumbusha kwamba tuko ndani ya mwezi wa Ramadhani na si vizuri kunifanyia kitendo cha udhalilishaji lakini alibaki na msimamo wake kuwa hanihitaji mimi wakla wananihusu kuwa wateja wa Clock Tower Café na kwamba niondoke na kamwe nisiingie tena Clock Tower Café Iringa. Ilibidi niondoke kwa aibu kimya kimya kwa unyonge mithili ya mbwa aliyemwagia maji akiogopa hata kubwekawa. Na jambo hili lilinishangaza sana kwa sababu sehemu ya biashara ni sehemu ya umma ambapo kila mtu anaweza kuingia na kutoka.

Kwa kweli tukio hili lininsononesha, kunidhalilisha na kunikumbisha si tukio lilimtokea mmoja wa wagombe Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye alipoingia katika Hotel moja Mjini Dar es Salaam, Uongozi wa Hotel ulikataa hata kumhudumia maji ya kunywa na pia unakumbusha madhila ya siku za ukoloni ambapo watu waafrika licha ya kuwa ndiyo wenyeji wa nchi hii walikuwa wanabaguliwa kwa rangi na hadhi yao na kukatazwa kuingia katika mahoteli au migahawa ya watu weupe. Pale jijini Tanga ilikuwa rahisi mbwa kuingia Planters Hotel lakini si Mwaafrika. Na marehemu Mzee Erasto Mang’enya katika kitabu chake kimoja anaeleza madhila haya ya ubaguzi kwa waafrika pamoja na elimu yake na kuwa mjumbe wa Mamlaka ya Mji alikuwa haruhusiwi kuingia katika Hotel za watu weupe kwa kuwa tu alikuwa ni Mwaafrika.

Na ni jambo la kusikitisha zaidi kuona kuwa baada ya zaidi ya nusu karne ya nchi yetu ya Tanzania na pia Visiwa vya Unguja na Pemba kuwa nchi huru, bado wapo watu kama Mmiliki wa Clock Tower Café Iringa ambao wanaona wanayo haki ya kumnyanyasa Mtanzania na kwamba Mwaafrika kwao ni mtu dhalili asiye na hadhi au haki ya kupata huduma katika biashara zao. Jambo hili halivumiliki hata kidogo na kamwe siwezi kukaa kimya katika hili kuona mtu kwa sababu yeye ni Mwaarabu au Mweupe anayo haki ya kumnyanyasa mtu mweusi katika ardhi ya mababu zake. Je mtu mwenye rangi nyeupe akiingia Clock Tower Café kwenda choo kujisaidia na kasha kutoka bila ya kupata huduma yoyote, je Mmiliki huyu angemsemesha katika kama alivyonisemesha mie kijeuri?

Kama Mtanzania na Mwaafrika naona fahari kuwa nimepata bahati ya kutembelea au kuishi katika nchi zingine za Afrika Mashariki, Ulaya (Norway) na Marekani (USA) lakini katika kutembea kwangu kote huko sijawahi kukatazwa kupata huduma hata ya kujisaidia chooni katika mgahawa au Hotel yoyote kokote kule duniani isipokuwa hapa Iringa katika mgahawa huu wa Clock Tower Café. Kote nilipopata huduma hotelini au mgahawani nimekuwa nikipata heshaima ya utu wangu kwa usawa bila ya kujali hali yangu, rangi yangu au Utaifa wangu hata kama nilikuwa Mwaafrika pekee mahali hapo. Kamwe sijawahi kutokewa na tukio la kubaguliwa na kuonekana dhalili na nisiye na hadhi yoyote isipokuwa jana mbele ya Mmiliki, wafanyakazi na wateja wa Clock Tower Café Iringa ndani ya Mji na nchi yangu. Jambo hili halivumiliki na ni lazima kwa vitendo tulikemee.

Msimamo wangu ni kwamba tukio lililonitokea jana kamwe lisimtokee mkazi au mtu yoyote anayetembelea Iringa. Rai yangu ni kuwa wakazi na watu wote wanaotembelea Iringa kamwe tusiingie kupata huduma Clock Tower Café Iringa kwani Mmili hatuhitaji sisi anao wateja wake wenye hadhi ya kupata huduma ya chakula chake na sio sisi wakazi na watu wanaotembelea Iringa. Tusimmudhi tuwache Mmiliki huyu awahudumie wateja wake anaowataka kwa raha zake.

Tuungane pamoja kusema hapana kwa udhahlilishaji na ubaguzi anaoufanya Mmiliki wa Clock Tower Café katika nchi yetu na mji wetu!

Tafadhali mhabarishe na mwingine!

ZUBERI HAMISI NGODA
Iringa, Tanzania
Simu: +255 655 200 200
E-Mail: advocate.ngoda@gmail.com
May 10 , 2019

#SAYNOTOCLOCKTOWERCAFEIRINGAMISTREATMENTOFCLIENTS#
I say no to racism
 
Mkuu mimi sikubaliani na wewe na ninahisi wewe ndo ulikuwa na makosa...choo ni kwa ajili ya watu wanaopata huduma hapo na si kwa ajili ya nyi wapita njia...eti kwa sababu tu ushawahi pata huduma hapo so unaona ndo sehemu ya kwenda kumaliza haja zako mda wowote ukijiskia katika mizunguko yako...choo ni kwa ajili ya watu wanaopata huduma kwa mda ule pale
 
Umeandika/Umecopy Mkeka mrefu sanaa
Jinsi wabongo walivyo wavivu,watakuwa Wamesoma na ilipofika Juu juu Waka scroll.

In summary

Hilo bandiko Linahusu Ubaguzi (kwa mujibu Wake)
Muandishi Ni mwanasheria/wakili
anaishi Iringa.
Ni mteja mzuri sana wa Mgahawa uliopo Clock Tower Iringa dodoma road.
Akiwa katika harakati Zake za Kuweka mkono kinywaji,alibanwa na haja Sasa kwa Kuwa Ni mteja wa pale na Ni mwez mtukufuku (ramadhani) akaon ngoja nikaji sitili pale (kujisaidia japo hajasema Kama ilikuwa kubwa au ndogo haha yamkini Kubwa).

wakati kashamaliza kuji hajabisha,ghafla mhudumu akamuambia Kuwa "Yeye c Mteja mzuri na anatakiwa asikanyage Tena pale"

na hiyo ndiyo hoja yake Kuwa. aliambiwa asikanyage Tena hapo.bila sababu ya Maana.
so akaona Kuwa ame baguliwa (C unajua Wanasheria tena?!).

Kupitia Ubaguzi wake akatumia ref za wakati wa ukoloni jinsi watu walivyokuwa wanabaguliwa katika nchi yao.

Ni Hayo TU.
Hili bandiko siyo refu unless umeishia ngumbaru! Tafadhali usieneze huu utamuduni potefu wa kuogopa kusoma!
 
Huyu jamaa anadai ni wakili ?😲😲😲 Jambo la Aya tatu anaandika gazeti? Sasa sishangai kwa nini Huyo Mmiliki amekufukuza.

Maana umeandika mambo mengi unalia lia na sijui uwakili ambao unataka watu wajue umekusaidiaje. Unafanyaje kazi ikiwa kuandika kifupi tu huwezi unalia lia? Si ukamshtaki mhusika basi mahakamani kuliko kuja mshtaki JF?
 
Wakili wenyewe ndo hawa wa vyuo hivi ninavyoviona? We acha kabisa hamna kitu.... Weupe sana na huu ni mfano tosha. Huyu unamwambiaje akutetee yeye tu kujitetea ameshindwa? Anakuja hapa analia lia asaidiwe.

Kama Wakili unalia lia mitandaoni je wengine wafanye nini?

Kama umeona amevunja sheria we mchukulie hatua ili iwe fundisho kwa wengine,kulia lia mitandaoni sio inshu.
 
Kikubwa usizoee sana ofisi za watu ,,choo kipo kwa ajili ya wateja tu na sio wapita njia ,Iringa vyoo ni vingi tu ,toa 200 acha kuzoea


Kuna hichi choo cha stand kimetazamana na mahala wamachinga wamepanga vitu ,,ukiwa mteja wa kila siku unatoa 100 tu.
 
31 Reactions
Reply
Back
Top Bottom