Jiulize hili..

Mtama

Member
Nov 8, 2010
63
0
Hivi umewahi kujiuliza hasa maisha ni kitu gani?Au unaenda enda tu?Je maisha ni kusoma,kuoa/kuolewa,kupata watoto kuzeka kisha kufa??Au kuna kitu kingine kinatakiwa kufanywa ili kukamilisha kitu kinachoitwa maisha,mi naamini Mungu hajatuumba tuje kusoma,ndoa,watoto kisha kuzeeka na kufa,kuna kitu kingine zaidi tuwe tunajua au hatujui,wewe wasemaje?
 
Mungu ametuumba binadamu kwa sababu ametupenda na amependa kutushirikisha upendo wake ili tumjue, tumpende, tumtumikie na mwisho wa maisha haya turudi kwake mbinguni.
 
Maisha ni historia yako yote , ulipo kuwa jana , ulipo leo na utakapokuwa kesho yote ni maisha. Usije jidanganya eti sijaanza maisha .maisha ya kiumbe chochote huanzia kinapoumbwa hadi kufa..
 
Maisha ni GAME, baada ya game, Kuna kuulizwa ulichezaje!!!, mbona kucheza RAFU, mbona kacheza ***** *****, yoooote hayo uwe tayari kumjibu Maanani.
 
Ebwana kweli MUNGU si mwadamu hata atuumbe bila sababu. Sababu ni moja tu ametuumba ilikuitenda na kuifuata kweli yake katika maisha yetu. Ila jaribu kutafakari maana hii ya maisha: MAISHA NI MTIRIRIKO WA SHIDA NA MATATIZO MENGI NA CHECHEMBE KIDOGO ZA BURUDANI.:smile-big:
 
maisha ni kuishi and that's it...........let's not fear what we don't know or have prove of it.........:hippie:
 
Hivi umewahi kujiuliza hasa maisha ni kitu gani?Au unaenda enda tu?Je maisha ni kusoma,kuoa/kuolewa,kupata watoto kuzeka kisha kufa??Au kuna kitu kingine kinatakiwa kufanywa ili kukamilisha kitu kinachoitwa maisha,mi naamini Mungu hajatuumba tuje kusoma,ndoa,watoto kisha kuzeeka na kufa,kuna kitu kingine zaidi tuwe tunajua au hatujui,wewe wasemaje?


Swali lako ni zuri sana kama mtu atakaa chini na kujiuliza, maana binadamu pamoja na ugunduzi wake wa vitu vyote uvionavyo leo hii bado hajatumia hata robo ya uwezo wa akili yake katika kufikiri.Wengi wetu hata tuwe tumesoma kiasi gani tunakuwa tunafuata yale yaliyokwishafanywa na watu wengine ni kama vile tunakariri.Ni bora mwanadamu akakaa chini na kutafakari nini maana ya maisha na jinsi ya kuyaendeleza.
 
kweli sijui maisha ni nini mimi naishi tu ...... kwangu mimi maisha ni mafumbo.... leo nafumbua kesho ni siku nyingine....
 
Mungu hawezi kufanya kitu pasipo sababu kama tunafutata maelekezo katika Vitabu vyake Vitakatifu basi sababu kubwa ya sisi kuumbwa ni KUMUABUDU YEYE TU,kutokana na mapenzi makubwa ya Mungu kwa watu wake akaamua kutufanyia wepesi kwa kila jambo tufanyalo hivyo maisha ni KUABUDU MUNGU.
 
Ukiyafikiria hayo yote utakufa muda c wako bana
:bowl::tape::doh::nono::smile-big:
A%20S%20angry.gif
:hippie::yield:
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom