Jiulize; Ethiopia wana Dreamliner zaidi ya 20, SGR, barabara nzuri, flyover nyingi, lakini bado watu wake wanafia kwenye malori wakizamia Bondeni!

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Ni afadhali CCM wameamua kukaa kimya kuhusu kujisifia kwamba wameleta maendeleo nchini sijui wamenunua Dreamliner mbili, wamejenga flyover Tazara na nyingine Ubngo kwa hiyo wameleta maendeleo Tanzania, na hiyo iwe sababu ya kuwachagua tena. Maendeleo kwa ajili ya nani? Bibi yangu kule kwetu Kishimundu?

Inakuwaje CCM wanashindwa kuwa na macho ya kuona kwamba karibu kila mwezi hapa nchini Wa-Ethiopia wanakamatwa kwenye malori wakisafirishwa kimagendo kwenda Afrika Kusini, na wengine kufia ndani ya malori hayo na maiti zao kutupwa porini?

Kama kuwa na SGR, floover, Dreamliner sijui ni maendeleo, kwa nini Wa-Ethiopia kwa maelefu wanazikimbia Dreamliner zao 25, Boeing 777 zaidi ya 16, Airbus 350-900 mpya 14, SGR, flyovers kila mahali, l na kuzamia Afrika Kusini?

Iweje Tanzania tunakuwa wepesi wa kusema tunamuenzi Nyerere huku tunasahau maneno yake kwamba maendeleo sio kuwa na majengo au barabara za ghorofa au ndege? Kwa nini tunasahau Nyerere alikataa kwa miaka mingi Tanzania kuwa na Television akisema kuna mambo muhimu ya kufanya kwanza?

Tafadhali niambieni bibi yangu kule Kishimundu atafaidika vipi na Mfugale flyover hapa Dar es Salaam, au daraja la juu ya bahari, na hapo mtakuwa mmenishawishi kwamba Tanzania tumeendelea sana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita!
 
Akili za kimasikini hizi, kwa sababu bibi yako afaidiki kwahiyo na wengine nao wasifaidike, mangapi ambayo wewe unafaidika nayo, na wenzako hawafaidiki na wametulia tuu.

Vipi watu walioajiliwa kwenye hiyo miradi inayojengwa na watakoajiriwa baada ya kukamilika ushawafikiria? vipi ajira zilizotokana na hizo ndege ushazifikiria? wafanyabiashara na wakazi wa maeneo miundombinu imeboreshwa wanavyoweza kwenda na kurudi kwa wepesi kwenye shughuli zao za kila siku, ushawafikiria au kwako muhimu ni bibi yako tuu.
 
1601897559900.png
 
..usisahau kwamba Ethiopia wamewekeza kwenye VIWANDA kuliko Tanzania.

..tatizo la Waethiopia ni idadi kubwa ya watu wao, hivyo uwekezaji ktk vitu umekuwa outpaced na population growth.

..tatizo lao lingine ni kwamba hawajawekeza vya kutosha ktk KILIMO na UFUGAJI sekta zinazogusa wananchi walio wengi.
 
Akili za kimasikini hizi, kwa sababu bibi yako afaidiki kwahiyo na wengine nao wasifaidike, mangapi ambayo wewe unafaidika nayo, na wenzako hawafaidiki na wametulia tuu.

Vipi watu walioajiliwa kwenye hiyo miradi inayojengwa na watakoajiriwa baada ya kukamilika ushawafikiria? vipi ajira zilizotokana na hizo ndege ushazifikiria? wafanyabiashara na wakazi wa maeneo miundombinu imeboreshwa wanavyoweza kwenda na kurudi kwa wepesi kwenye shughuli zao za kila siku, ushawafikiria au kwako muhimu ni bibi yako tuu.
...akii zako wewe....za kijinga
 
Iweje Tanzania tunakuwa wepesi wa kusema tunamuenzi Nyerere huku tunasahau maneno yake kwamba maendeleo sio kuwa na majengo au barabara za ghorofa au ndege? Kwa nini tunasahau Nyerere alikataa kwa miaka mingi Tanzania kuwa na Television akisema kuna mambo muhimu ya kufanya kwanza?

..."Nyerere alikuwa mwongo na aliishi kiujanja ujanja" Alisikika bosi mmoja akipayuka.
 
..usisahau kwamba Ethiopia wamewekeza kwenye VIWANDA kuliko Tanzania.

..tatizo la Waethiopia ni idadi kubwa ya watu wao, hivyo uwekezaji ktk vitu umekuwa outpaced na population growth.

..tatizo lao lingine ni kwamba hawajawekeza vya kutosha ktk KILIMO na UFUGAJI sekta zinazogusa wananchi walio wengi.
Kwa hiyo!
 
Kwahiyo huko kijijini kwa Bibi yako wasijengewe barabara nzauri na waaiwekewe umeme kila nyumba kwakua tu wewe hapo mbagala hautaona faida yake😀😀😀


Kuwa mpinzani inahitaji kujitoa ufahamu kweli
 
..."Nyerere alikuwa mwongo na aliishi kiujanja ujanja" Alisikika bosi mmoja akipayuka.
Baada ya vita na Uganda Nyerere alisema tuvumilie tufunge mikanda kwa miezi 18 tu na uchumi utarudi sawa - miaka minne baadae bado tulikuwa tunatumia majani ya mipapai kufua nguo na kula ugali wa njano toka USA, uji bila sukari, Colgate za magendo toka Kenya, sabuni za kuogea toka Malawi na Zambia nk lakini anatuchekesha na tunaendelea kuwa na furaha. Hebu mwambie Raisi yeyote wa sasa atufanye hivyo leo kama hajaonja joto ya jiwe
 
Kwahiyo huko kijijini kwa Bibi yako wasijengewe barabara nzauri na waaiwekewe umeme kila nyumba kwakua tu wewe hapo mbagala hautaona faida yake😀😀😀


Kuwa mpinzani inahitaji kujitoa ufahamu kweli
Nadhani wewe ndio huna akili - niambie nichague kati ya barabara nzuri kijijini kwa bibi yangu na Dreamliner yako ambayo wewe kama mimi hujawahi kupanda
 
..usisahau kwamba Ethiopia wamewekeza kwenye VIWANDA kuliko Tanzania.

..tatizo la Waethiopia ni idadi kubwa ya watu wao, hivyo uwekezaji ktk vitu umekuwa outpaced na population growth.

..tatizo lao lingine ni kwamba hawajawekeza vya kutosha ktk KILIMO na UFUGAJI sekta zinazogusa wananchi walio wengi.
Mbona china ina watu lukuki lakini wako vizuri?,tatizo la ethiopia hakuna siasa safi..
 
..usisahau kwamba Ethiopia wamewekeza kwenye VIWANDA kuliko Tanzania.

..tatizo la Waethiopia ni idadi kubwa ya watu wao, hivyo uwekezaji ktk vitu umekuwa outpaced na population growth.

..tatizo lao lingine ni kwamba hawajawekeza vya kutosha ktk KILIMO na UFUGAJI sekta zinazogusa wananchi walio wengi.
Naona Umeacha Ukibendera Kwenye Mada hii ume post Vuzuri
 
Ethiopia imejengwa na Mchina hiyo.....

Watakufa na mikopo ya wachina.
 
Akili za kimasikini hizi, kwa sababu bibi yako afaidiki kwahiyo na wengine nao wasifaidike, mangapi ambayo wewe unafaidika nayo, na wenzako hawafaidiki na wametulia tuu.

Vipi watu walioajiliwa kwenye hiyo miradi inayojengwa na watakoajiriwa baada ya kukamilika ushawafikiria? vipi ajira zilizotokana na hizo ndege ushazifikiria? wafanyabiashara na wakazi wa maeneo miundombinu imeboreshwa wanavyoweza kwenda na kurudi kwa wepesi kwenye shughuli zao za kila siku, ushawafikiria au kwako muhimu ni bibi yako tuu.
Kwa uongozi unaodai upo kwa ajili ya wanyonge ni wazi nitahoji. Mnyonge gani anapitisha gari lake kwenye flyover, anapanda Dreamliner?
 
..usisahau kwamba Ethiopia wamewekeza kwenye VIWANDA kuliko Tanzania.

..tatizo la Waethiopia ni idadi kubwa ya watu wao, hivyo uwekezaji ktk vitu umekuwa outpaced na population growth.

..tatizo lao lingine ni kwamba hawajawekeza vya kutosha ktk KILIMO na UFUGAJI sekta zinazogusa wananchi walio wengi.
huku nako tumeambiwa tufiatue tu watoto
 
Back
Top Bottom