ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Haya ni baadhi tu ya orodha ya majaribio ambayo binafsi nayaona yanaweza kumfanya JK akose raha hata kama atakuwa bado ana kiburi cha kuendelea na awamu nyingine ya Uongozi.
- Mikopo kwa wajasiliamali kupitia mabilioni ya JK = 0
- Kupunguza ukubwa wa Serikali kwa kuunganisha Wizara na Idara ili kuleta ufanisi = 0
- Kufanya Kilimo chetu kiwe endelevu kupitia umwagiliaji = 0
- Kutoa ruzuku ya pembejeo ili kuboresha kilimo = 0
- Kumleta Maximo kwa gharama kubwa ili kuinua soka la Bongo = 0
- Kuileta Real Madrid = 0
- Kushawishi watanzania waliopo ughaibuni kurejea ili wawekeze nyumbani = 0
- Kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini = 0
- Kuweka mfumo mzuri wa wazawa kunufaika kutokana madini yetu sawa na wawekezaji = 0
- Kuileta Brazil ili kutangaza Tanzannia ikiwemo utalii wetu pia kupata kafaida kidogo = 0
- kuitangaza Tz kwa safari zake kibao za nje ya nchi hasa USA= 0
- Kuleta mkutano wa kimataifa wa Lionel Sullivan hapa Bongo ili kutangaza wajasiliamali wetu = 0
- Kuanzisha vituo vya kukodisha matrekta na kuleta matrekta = 0
- Kujenga madarasa =0
- Kujenga zahanati = 0
- Kuongeza ajira za waalimu na kuboresha maslahi yao = 0
- Kuongeza mishahara ya watumishi wa umma =0
- Kupunguza matukio ya uhalifu = 0
- Kuwachukulia hatua wote watakaojisisha na ufisadi = 1x 0
- Kupunguza kero za foleni = 0
- Kupunguza ajali za barabarani = 0
- Kupunuza foleni kwa utaratibu wa njia tatu = 0
- Kupunguza utegemezi wa wahisani kwenye bajeti ya Serikali = 0
- kupunguza mfumuko wa bei = 0.
- Kuongeza idadi ya akina wanawake katika sekta ya uongozi na utawala
- Kuinua vipaji vya wasanii ikiwemo kuwahusiha katika masuala mbalimbali ya kitaifa kama mradi wa maralia, changia CCM ns kula nao pilau IKULU.
- Mpango wa walimu wa "voda fasta" ambao wengi walifeli ili watumike kuwafundisha wanafuzin kwenye shule za kata..
- Kuwa karibu na wananchi kwenye hitima, misiba na majanga mengine ya kitaifa kwa kuwatembelea kwenye mapagale yao wanayoishi..
- Kuwasaidia vijana kuingia na kujijenga kwenye ulingo wa kisiasa ikiwemo Kijana wake Ridhiwani, Shy- Rose, Nape, Januari Makamba, nk.
- Kushawishi baadhi ya watanzania ughaibuni kurejea nyumbani ili kushika nafasi nyeti akiwemo Tido Mhando pale TBC nk.