Jitibu na mchanganyiko huu

Baba Vladmir

JF-Expert Member
Aug 31, 2021
248
381
Ni matumaini yangu kuwa wanajukwaa wenzangu hamjambo kabisa na mnaendelea na mapambano juu ya maisha yenu kama nifanyavvo mimi.Kwa wale wenye changamoto kiafya poleni sana Mungu ni mwema siku zote.

Rejea mada tajwa hapo juu;

Andaa mizizi ya mlonge kadri unavyoweza,kwa ajili ya kuelekeza napendelea uandae angalau mizizi mitatu yenye ukubwa wa kati ambayo ukikatakata inaweza kujaa angalau sifuria ya kupika kilo moja ya mchele na kuendelea.Andaa angalau nusu kilo ya tangawizi.Mchanganyo wa mwisho andaa limao/ ndimu nusu kilo.

Kata mzizi wako wa mlonge katika vipande vidogovidogo,kata limao/ndimu katika vipande vidogovidogo(kwa zile limao kubwa unaweza kukata kwa vipande vinne,kwa zile ndogo ni mara mbili tu) Twanga tangawizi yako ili iweze kupondeka vizuri.

Weka mchanganyo wote kwenye sifuria kubwa na ulijaze maji(angalau kwa mchanganyo huo sifuria yenye kutoa lita kumi).Injika mchanganyo wako kwenye jiko lako na hakikisha unachemka vizuri na kutokota(usitokoteshe kupita kiasi)

Baada ya kuchemsha ipua na subiri mchanganyo wako upoe vizuri na kisha chuja kwa ajili ya matumizi.Kwa mchanganyo huo jitahidi usipungue lita kumi.

Tumia kila siku gilasi moja asubuhi mchana na jioni,mchanganyiko huu usiutumie kwa watoto chini ya umri wa miaka sita.

Mchanganyo huu unatibu magonjwa yafuatayo:
#Matatizo yote ya mfumo wa upumuaji.

#Huondoa sumu mwilini na kusafisha kabisa damu,kuondoa lehemu kwenye mishipa ya damu,hivyo kuongeza na kurahisisha msukumo wa damu.

#Uzito kupita kiasi.

#Matatizo na maumivu ya mishipa ya damu.

#Husafisha mkojo na kibofu cha mkojo,hivyo unatibu kabisa matatizo ya UTI sugu

#Shinikizo la juu damu na magonjwa ya moyo na kisukari.

#Maumivu ya mwili wote

#Upungufu wa nguvu za kiume na huongeza maradufu hamu ya tendo la ndoa

#Tumbo kujaa gesi

#Matatizo ya tumbo na uvimbe

#Baridi yabisi

#Matatizo ya hedhi kwa wanawake na matatizo mengine mengi ambayo siwezi kuyaorodhesha hapa yote.

Unaweza kutumia mchanganyo huu kwa matumizi ya wiki mbili na kuendelea na matokeo yake utayaona.

MUNGU awabariki sana!
 
Kubwa kabisa, nawatahadharisha wale wanao sumbuliwa na vidonda vya tumbo (Ulcers) msithubutu kabjsa kabisa kutumia mchanganyiko huu ni hatari zaidi kwa afya na uhai wenu

Mmeta mada kasahau au kafanya kusudi, kwa sasa yangu ni hayo tu ndugu wasomaji.
 
Huu hautaleta madhara kwa figo huko mbeleni? Maana mitishamba inasemekana ni visababishi mojawapo vya kufeli kwa figo sababu ya matumizi yake bila kufahamu kipimo sahihi
 
Huu hautaleta madhara kwa figo huko mbeleni? Maana mitishamba inasemekana ni visababishi mojawapo vya kufeli kwa figo sababu ya matumizi yake bila kufahamu kipimo sahihi
Mfano wa maandalizi nilioutoa hapa unazingatia uwiano wa material na kiasi cha maji katika mchanganyo,lengo la kutumia kiasi hicho cha maji ni kuondoa/ kupunguza concentration inayoweza kuipa mzigo mkubwa figo katika kuchuja maji hayo

Kwa hiyo unapoandaa ni lazima uzingatie kiasi cha material na wingi wa maji!
 
Mfano wa maandalizi nilioutoa hapa unazingatia uwiano wa material na kiasi cha maji katika mchanganyo,lengo la kutumia kiasi hicho cha maji ni kuondoa/ kupunguza concentration inayoweza kuipa mzigo mkubwa figo katika kuchuja maji hayo

Kwa hiyo unapoandaa ni lazima uzingatie kiasi cha material na wingi wa maji!
Asante sana.
Na hii mizizi ya Mlonge inapatikana wapi Mkuu?
 
Kubwa kabisa, nawatahadharisha wale wanao sumbuliwa na vidonda vya tumbo (Ulcers) msithubutu kabjsa kabisa kutumia mchanganyiko huu ni hatari zaidi kwa afya na uhai wenu

Mmeta mada kasahau au kafanya kusudi, kwa sasa yangu ni hayo tu ndugu wasomaji.
CHONDE MLETA MAADA. ONGEA CHOCHOTE KUHUSU HII SHIDA, KUNA UKWELI HAPO?
 
Hiyo inajulikana, tangawizi na limao (zote zina acid) hazipatani na vidonda vya tumbo...lakini ni dawa nzuri
Ni kweli vidonda vya tumbo havipatani kabisa na vyakula vyenye uchachu(acid) kama limao,ndimu,pilipili nk.Lakini kwa mahitaji ya dawa kwa mgonjwa mwenye tatizo hilo maandalizi yanahitaji uangalifu wa hali ya juu,maana yake ni kwamba lazima kiwango cha solvent(maji) kiwe ni kikubwa kuliko material yaliyo ndani ya mchanganyo ili kupunguza kiwango cha acid, kwa mtu wa vidonda vya tumbo itabidi atumie mchanganyo kwa muda mrefu zaidi kwa sababu mchanganyo wake utakuwa na kiasi kidogo cha material na siyo mkali kama ulivyo kwa mwingine!

NB Ukiona unatumia na kukupa shida ni vema ukaachana nao mara moja,kama ilovyo kwa matumizi ya dawa zingine(unasitisha dozi mara moja)
 
Mizizi ya mlonge unapata wapi huku maeneo ya sinza mkuu??

Mchanganyiko ni mkubwa sana, Fanya calculation vizuri, ili upunguze uwiano hapo
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom