Daisy Llilies
JF-Expert Member
- Apr 19, 2019
- 1,017
- 2,154
Tulisafiri na jirani yangu tukitokea Morogoro, tulifika wote Kibaha lakini baada ya hapo siku muona. Nilifika nyumbani salama, nilipitia kwa Mangi nikikumbuka nyumbani sukari ilibaki kidogo, pale kwa Mangi nilikutana na mama mke wa jirani yangu. Tulisalimiana vizuri na alishangaa kuwa hajaniona hivi karibuni, nilimwambia nilipangiwa kazi Morogoro huu ni mwezi wa pili na field ni ya miezi mitatu, lakini mbona baba Donner nilikuwa nae safarini, alishangaa, lini nilimjibu leo hii tulitoka wote Morogoro.
Baba Donner bwana kumbe alipitia anakokujua mwenyewe, amefika nyumbani saa tano usiku, amemkuta mama Donner amevimba kuwa Daisy alisema tumesafiri pamoja na yeye aliingia tangu saa kumi hapa, wewe ulikua wapi.
Saa sita usiku, mlango unagongwa, baba Donner anataka nimueleze maneno niliyomuambia mkewe, wote wakiwa wameongozana, kisuto hiki nitakimudu vipi, niliwaambia siongei mpaka mwana sheria wangu awepo na mjumbe wa nyumba kumi.
Zogo lilipozidi baba Donner aliaga na kusema atarudi kesho asubuhi, yule mwanamke vipi, mimi nilimpa hints kumbe kwa kua ndoa yake ina shake walitaka kunifanya mimi ndiye mchawi wa ndoa yao.
Baba Donner bwana kumbe alipitia anakokujua mwenyewe, amefika nyumbani saa tano usiku, amemkuta mama Donner amevimba kuwa Daisy alisema tumesafiri pamoja na yeye aliingia tangu saa kumi hapa, wewe ulikua wapi.
Saa sita usiku, mlango unagongwa, baba Donner anataka nimueleze maneno niliyomuambia mkewe, wote wakiwa wameongozana, kisuto hiki nitakimudu vipi, niliwaambia siongei mpaka mwana sheria wangu awepo na mjumbe wa nyumba kumi.
Zogo lilipozidi baba Donner aliaga na kusema atarudi kesho asubuhi, yule mwanamke vipi, mimi nilimpa hints kumbe kwa kua ndoa yake ina shake walitaka kunifanya mimi ndiye mchawi wa ndoa yao.