Jipatie Nakala yako: Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania by Nyerere

Hii yawezekana ndio sababu CCM hawataki wananchi wengine wakipate?

Hakijaonekana bado. Chama Cha Mapinduzi, kwa sababu ya uzito wa historia yake, hadhi ya jina lake, mfumo wa wavu wake, mazoea ya watu, na ubovu wa vyama vya upinzani, kinaweza kuendelea kuchaguliwa na Watanzania, pamoja na kansa ya uongozi wake. Au watu wanaweza wakachoka, wakasema, "potelea mbali:" wakachagua Chama chochote, ili mradi tu watokane na kansa ya uongozi wa CCM. Hainifurahishi kuyasema haya, lakini uhai wa nchi yetu unataka yasemwe. - Nyerere
 
Kwa kuweka kitabu hiki hapa, sijui mmewakosesha wahusika mapato kwa kiasi gani. Na sijui swala la copyright linakuwaje. Pale Great thinkers infringe copyright.
 
Kwa kuweka kitabu hiki hapa, sijui mmewakosesha wahusika mapato kwa kiasi gani. Na sijui swala la copyright linakuwaje. Pale Great thinkers infringe copyright.

not really.. hii haikuwa kwa ajili ya faida.... ni public domain..
 
Nilikuwa nimeamua kuchukua likizo na JF lakini imenibidi nikatize likizo yangu kwa sababu ya hii thread. Asante sana Mkuu SubiriJibu umenikumbusha mbali na hapa natokwa machozi nikitafakari hatma ya nchi yangu niipendayo Tanzania inavyonajisiwa hivi sasa na viongozi limbukeni. Mungu atusaidie, amina.
 
Nilikuwa nimeamua kuchukua likizo na JF lakini imenibidi nikatize likizo yangu kwa sababu ya hii thread. Asante sana Mkuu SubiriJibu umenikumbusha mbali na hapa natokwa machozi nikitafakari hatma ya nchi yangu niipendayo Tanzania inavyonajisiwa hivi sasa na viongozi limbukeni. Mungu atusaidie, amina.

Mbona unataka kukimbia Mag3, ukiwa kama mdau unaweza kubadilisha hii forum pia kwa kuleta sred za maana kama hizi
 
Nilikuwa nimeamua kuchukua likizo na JF lakini imenibidi nikatize likizo yangu kwa sababu ya hii thread. Asante sana Mkuu SubiriJibu umenikumbusha mbali na hapa natokwa machozi nikitafakari hatma ya nchi yangu niipendayo Tanzania inavyonajisiwa hivi sasa na viongozi limbukeni. Mungu atusaidie, amina.

- Wakipewa nafasi na sisi wananchi, ambao kama unayosema ni kweli basi ni malimbukeni kuliko hata hao viongozi, kwa sababu wanachanguliwa na sisi wananchi, au? Likizo imeisha mkuu? karibu sana tumkome nyani!

FMEs!
 
- Wakipewa nafasi na sisi wananchi, ambao kama unayosema ni kweli basi ni malimbukeni kuliko hata hao viongozi, kwa sababu wanachanguliwa na sisi wananchi, au? Likizo imeisha mkuu? karibu sana tumkome nyani!

FMEs!

Viongozi hawa hawapewi nafasi na wananchi, wanahakikisha wanajipa hizo nafasi kwa kutumia njia zozote zile. Ndio maana Mwalimu kwa wakati fulani aliwaita wahuni hawa kwani hata pale wananchi watakapowakataa, watatafuta jinsi ya kujihalilishia nafasi zao. Wapo watakaofanya juu chini kujaribu kufuta historia hata ikibidi kukana kauli zao wenyewe au kung'ang'ania uongozi hadi kufa. Ndio mkuu FMes, likizo imeisha na sasa Mag3 nimerudi tumkone nyani kisawasawa bila kumtazama uso, a luta continua.
 
when it comes to suala la mwl.JKN.......wengi hukurupuka pasipo hata ku-read btn the lines.....!At least baada ya kusoma mawazo yake kwenye kitabu chake hiki nadhani mawazo ya wengi humu ndani towards him yatabadilika! HEY GREAT THINKERS......WHAT DO YOU THINK OF THE MAN....?
 
Natafuta kitabu kilichoandikwa na J.K. Nyerere, "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania" kwa Kiswahili au Kiingereza.

Jitihada za kukipata mitaa ya Dar zilishindikana baada ya kuambiwa 'udaku' kwamba kimepigwa marufuku kinamna. Madukani mwa vitabu mwote nilimopita kukiulizia waliniona juha, kana kwamba 'kila mtu anajua' kitabu kilipigwa marufuku.

Madai hayo ni ya kweli au uzushi tu wa uchaguzi?

Shida yangu ni nakala moja tu ya kitabu hicho kwa ajili ya rejea ya kitaaluma.

Natanguliza shukrani.

Mlenge

=============
UPDATE:

Kwa msaada wa mkuu SubiriJibu kitabu kimepatikana, nakala inaweza kupatikana chini hapa

Safi sana, hiki ni cha kuprinti na kusoma vizuri, Mungu amweke Mwl mahali pema peponi, nadhani haki miliki haitaleta shida.
 
Mwalimu anaendelea kusema katika UWHT..

Viongozi wetu wakuu hawawezi kukiuka Uamuzi na msimamo wa Chama kizima, halafu wadai kuungwa mkono na viongozi wa chini yao au na wanachama kwa jumla. Kwa kweli tunatazamia kuwa viongozi hao watapingwa kwa nguvu kabisa, na kama hapana budi kufukuzwa. Huko ndiko kuwajibika. Bila hivyo viongozi wetu watafanya wapendavyo bila kuwa na wasiwasi. Watapinda, watapuuza, watavunja maamuzi na msimamo wa chama bila kuwa na hofu yoyote. Wenye hofu watakuwa ni viongozi wa chini na wanachama wa kawaida watakaofanya ujasiri wa kuwapinga viongozi wakuu. Maana hao wataonekana kuwa ni wakorofi na wachochezi, na watachukuliwa hatua za nidhamu! .

Na kuendelea kugongomelea msumari:

Kukubali kufanywa vikaragosi vya viongozi ni dalili ya woga, si dalili ya heshima; na woga na heshima ni vitu viwili mbali mbali. Maadili mema hayatudai tuwaogope viongozi wetu.

na kutupa elimu hapa:

Hatuwezi kuachia utamaduni wa woga ukawa ni mbinu au sifa mpya ya uongozi. Na sasa lazima tukiri kwamba utamaduni huu wa woga unaanza kuwa ni sehemu ya tatizo letu la kitaifa.

Na kama nabii pweke jangwani akasema:

Nilisema awali kwamba kansa ya uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi isingekuwa ni jambo la kutisha sana kama tungekuwa tumeanza kuona kizuri cha upinzani kinachoweza kuiongoza nchi yetu badala ya CCM. Ubovu wa uongozi ndani ya CCM ndio uliofanya nikapendekeza tuanzishe mfumo wa vyama vingi. Nilitumaini kuwa tunaweza kupata chama kingine kizuri ambacho kingeweza kuiongoza nchi yetu badala CCM au ambacho kingekilazimisha Chama Cha Mapmduzi kusafisha uongozi wake kwa kuhofia kuwa bila kufanya hivyo kitashindwa katika uchaguzi ujao.

Na kama Musa mbele ya wana Waisraeli walioasi nyikani akasema:

Lakini bado sijakiona chama makini cha upinzani; wala,dalili zozote za kuondoa kansa ya uongozi ndani ya CCM. Bila upinzani mzuri wa nje, na bila demokrasia halisi ndani ya Chama Cha Mapinduzi, Chama hili kitazidi kudidimia chini ya uzito wa uongozi mbovu. Kwa hali yetu ya kisiasa ilivyo nchini, hili si jambo la kutarajia bila ya hofu na wasi wasi!
 
Mlenge,
Kama uko DSM ningekushauri umtafute Walter Bgoya. Yeye alichapisha kitabu cha Mtei. Kama walivyosema waungwana hapo awali, kitabu cha Mwalimu kilichapishwa Zimbabwe baada ya kufanyiwa mizengwe na wenye madaraka kisichapishwe DSM. Ninavyo vyote vya Kiswahili na Kiingereza lakini bahati mbaya niko mbali ya DSM.

Tafadhali naomba uki"scan" na kukiweka kwenye mtandao. Ni muhimu kwa wadau kukipata
 
JKN yeye passion yake ilikuwa Muungano.alikuwa hataki kabisa serikali 3!Mnakumba group 55!Nimecheck hiyo attachment juu juu sidhani inazungumzia tatizo la sasa:Ufisadi!!!Ufisadi.

Tukumbuke JKN ndio alimtaka Mkapa !Angalia family ya Mkapa ilivyofanya:Kufanya biashara ukiwa ikulu na dubious Kiwira deals.

Hatima ya nchi hii sio JKN tena,hata tukisoma kitabu mara mia!Tukumbuke JKN aliua upinzani,kurecover imekuwa shida sana.Assume tungekuwa na akina Slaa tangu uhuru?Upinzani sio vita,ni kuimarisha demokrasia na kukosoana.SISIEM inavyobehave ni kama chama kimoja.Kila mtu anajua kukifund hiki chama fedha inatoka wapi.

I salute wale ambao walitaka kuleta mabadiliko ya kisiasa toka mwanzo.Chief Fundikira,Makwaia,Kasanga Tumbo,James Mapalala na wengineo wengi.
 
Mwalimu anaendelea kusema katika UWHT..



Na kuendelea kugongomelea msumari:



na kutupa elimu hapa:



Na kama nabii pweke jangwani akasema:



Na kama Musa mbele ya wana Waisraeli walioasi nyikani akasema:

Nukuu hizo zimetoa Muhtasari wa ujumbe uliokusidiwa. Hata kama sitasoma chote hapa ndiyo alimaliza kazi. Ndiyo maana kimefichwa na wahusika.
 
Nadhani sasa kiko kwenye posti ya kwanza..
MM Ulianza kupiga type ili uweze kutuletea hiyo nakala hapa? kwa kweli mzee kama umefanya hivyo nikupongeze huu ni moyo wa pekee kuhakikisha watu wanaijua kweli labda siku moja hiyo kweli itawaweka Huru. Ubarikiwe sana mkuu
 
MM Ulianza kupiga type ili uweze kutuletea hiyo nakala hapa? kwa kweli mzee kama umefanya hivyo nikupongeze huu ni moyo wa pekee kuhakikisha watu wanaijua kweli labda siku moja hiyo kweli itawaweka Huru. Ubarikiwe sana mkuu

hapana sikufanya mimi hii kazi. NI kutokana na chanzo cha kuaminika. Shukrani apewe "invisible". Ninachofanya sasa ni kukiweka sawa maana kina makosa mengi ya uchapaji, ni kama first or second draft..

Nyerere hakukawaia kuwaita wapumbavu viongozi uchwara..

Hoja ya pili wanayoisema ni ile ya kura ya maoni. Wanasema: "Kuhusu suala la kura ya maoni, Serikali iliona kwamba utekelezaji wake ni sawa na kufanyya uchaguzi mkuu,jambo ambalo ni gharama kubwa. Aidha, kwa kuzingatia kuwa kura ya maoni hupigiwa suala linalohitaji jibu NDIYO au HAPANA, ni vigumu kupata swali lililo wazi kwa wananchi ambao hawana uzoefu wa utaratibu huu wa kura ya maoni.

Ni vigumu kuelewa kwa nini watu walio tayari kuwabebesha wananchi mzigo wa Serikali Tatu za kudumu, wanahofu gharama za kura ya maoni ya mara moja! Na kama viongozi wetu ni wapumbavu kiasi cha kwamba hawawezi kutunga swali "Je, unataka Serikali Tatu?" Au "Je, unataka Serikali ya Tanganyika?" kazi hiyo wangeweza kuwaachia wataalamu wenye uwezo zaidi. IIa wasiwatukane Watanzania, ambao miaka yote hii wamekuwa wakipiga kura za NDIYO au HAPANA, kwamba ati wakiulizwa swali kama hili watashindwa kulijibu.
 
Kwanza nikiri kuwa ni mmoja wa watu waliomisi hii kitu ila nashukuru kwa kuwekwa hapa hiyo hazina. Aisee huyu mzee aliipenda hii nchi hawa waliopo sasa wanapenda maslahi yao kwa kupitia nchi hii WHAT IS HE WAS ALIVE TODAY?
 
Back
Top Bottom