Logikos
JF-Expert Member
- Feb 26, 2014
- 12,435
- 19,452
Kapteni aliyekuwepo palepale alidhani imeangukia upande wake..., refa pia alidhani hivyo ila watu ambao hawakuwepo pale wala yule ambaye hakuangalia ndio baadae alidhani iliangukia kwake sababu mwenzake alishangilia ?Robo fainali
Yanga walikutana na Asante Kotoko na wakatoka sare 1-1 mechi zote mbili hatimaye ikaamuliwa irushwe shilingi ili iamue nani aende nusu fainali.
Makapteni wote wawili wakishuhudia shilingi ikarushwa hata hivyo kapteni wa Asante kotoko alifanya udanganyifu kwani kabla shilingi haijatua alijifanya kushangilia na kumfanya kapteni wa Yanga Abdulrahaman kuamini kuwa shilingi imeangukia upande wake.
Ndipo Yanga ikadhulumiwa nafasi ya kuwa timu ya kwanza kuingia nusu fainali, rekodi iliyokuja kuwekwa na watani zao Simba mwaka 1974.
kitwana Manara akaingia kwenye orordha ya wafungaji bora akiwa mfungaji bora namba tisa mwenye magoli mawili.