Lucchese DeCavalcante
JF-Expert Member
- Jan 10, 2009
- 5,471
- 734
Kila mtu katika ulimwengu huu ukimuuliza swali hili JE UNATAKA KUWA TAJIRI? Jibu utakalo lipata hapo ni NDIO. Ndoto hii huwa katika vichwa vya watu wengi ambao bado waiona ni ndoto tu na haiwezii kuwa kweli. Baada ya kusoma makala hii fupi tunaamini kuwa utaweka jitihada na wewe za kufikia ngazi hiyo ya utajiri.
SHINDA BAHATI NASIBU: Utajiri pia unategemeana na bahati. Tumeshudia watu mbalimbali nchini wakiingia katika utajiri kwa kushinda bahati nasibu mbalimbali. Ushindi wa milioni 100 mara nyingi humfanya mtu hatakama alikuwa ameajiriwa basi kuacha kazi na kujiajiri. Hii pia ni aina mojawapo yakuwa tajiri kwa gafla.
KUZA KIPAJI CHAKO: Kila mtu anakipaji chake binafsi kazi kubwa ipo katika kukitambua kipaji hicho. Kipaji kama kipaji kinatakiwa kiweze kuonyeshwa katika soko ili kiweze kukusaidia kukupa utajiri. Watu wengi wameacha shule nakuamua kufuata vipaji vyao na sasa ni matajiri wakubwa katika ulimwengu wasasa. Mfano mkubwa ni waimbaji wanamichezo, mamodel, na waburudishaji. Kwa kulijua hilo basi jaribu kutafuta kipaji chako hata kama umekaa hapo ofisini ukiwa na laptop yako.
ANZISHA BIASHARA: Kama unamapenzi na uvumilivu unaweza kuanzisha biashara yako na kuiendeleza na kuwa na maisha mazuri. Ukilisoma soko vizuri kabla hujaamua kuingia au kukopa fedha katika taasisi za fedha unaweza kuiona fursa ambayo itakupa mwanga juu ya biashara yako. Mapenzi ulionayo juu ya biashara yako itakupa utajiri usiotarajia.
KAMATA FURSA ILIYOPO: Fursa hata siku mmoja haiji mara mbili. Hiiyo inakupa umakini wakuwa macho iliuweze kuiona hiyo fursa, hata siku moja usikubali fursa ikupite tena kama ipo ndani ya uwezo wako. Je utajuaje au utaitafutaje fursa? Unachotakiwa kujua ni fursa zimekuzunguka tumia mda wako na utulivu katika kuziangalia zipo.miaka 8 iliyopita Nani alijua kuwa biashara ya utoaji huduma ya kuosha magari ingekuja kuwa fursa kubwa wakati huu, lakini wale walioona hiyo fursa sasa wanapesa nzuri tu na mpaka watu wanaanza kuiga wao labda walishafikiria kuiacha.
Haya umeshajua njia za kuweza kuwa tajiri ni juu yako kuwa tajiri au kubakia maskini..