Enlightened one
JF-Expert Member
- Jun 20, 2019
- 349
- 191
Lo amaa kweli !! Dunia imefika mwisho,yaani watu wanafundisha uchaw hadhran bila hata aibu
ebu nyinyi wachawi mtuondolee matunguri yenu
ebu nyinyi wachawi mtuondolee matunguri yenu
Habari yako mkuu.Kufa Huwezi Wala Hakuna Kiumbe Anaeweza Kukata Silver Cold Ile Zaidi Ya Kupata Amri Kutoka Kwa Mwenyezi Mungu Sawa Na Mtu Kufa Usingizini Au Ndotoni....
Unachoona Ni Kile Utakachohitaji Kuona Kwenye Ulimwengu Wa Roho Na Kukumbuka Ni Lazima Maana Kama Umeweza Kujua Umetoka Nje Ya Mwili Ukirudi Kila Kitu Utakumbuka Hii Ni Tofauti Na Ndoto Kwamba Uote Usikumbuke...
"Its Your Mind Mkuu We Talk About Here"
Rakims
hi ndgu imekaa je mbona wanatuogopesha wanasema kuna mambo ya kufa kufa hapo pamekaejeASTRAL PROJECTION/Mental Projection.FAIDA ZAKE:
Ni Ule Uwezo Wa Mtu Kutengana Na Mwili Wake Ki Fikra Katika Imani Husemwa Kiroho.
au pale ambapo mwili unakuwa umetengana na fahamu zako.
Utokaji huu wa nje ya mwili upo wa aina mbili au tatu na wenyewe ni wa roughly watu wanafundisha kwa maelezo marefu na mapana hali ya kuwa ni kitu kifupi tu watu wanatakiwa kujua jinsi ya kutoka na mengine kujifunza huko huko.
View attachment 420199
1. Kujitambua kuwa wewe hufi na kuondoka moja kwa moja: Hili ni tukio litakalo kubadilishia maisha. Mamilioni ya watu wamekua wakithibitisha kuwa mtu akifa hapotei moja kwa moja bali kuna maisha mengine ambayo ataishi wale wasioamini life after dealth.
2. Kuongeza uwezo mzuri wa kulala:
Hii husaidia mtu kulala katika hali ya usalama na kupata nguvu inayozungumziwa baada ya kulala na kujua ni ipi sababu kubwa ya kulala tunalala ili miili yetu ipumzike roho zetu zianze kuishi.
3. Kuongeza nguvu ya majariwa:
Hii inaongeza kipawa cha unabii na uwezo mkubwa wa kumsoma mtu akili hufahamika kama kama mind reading au telepathy, kasimama hapo wewe unaongea na roho yake.
4. Kujiendeleza Kimaisha:
Ukiwa nje ya mwili inakuthibitishia kuwa wewe ni zaidi ya binadamu wa kawaida hivyo hukuongezea akili ya utendaji zaidi kwa kutumia maajabu na si nguvu tena.
5. Inakuongezea kukomaa kiroho:
Watu wengi wamekuwa na roho nzuri baada ya kuishi na kiumbe zaidi ya asiekuwa mwanadamu.
6. Inaongeza heshima ya maisha:
Hii hukufanya umuheshimu kila kiumbe na umuhurumie hata paka maana kule una uwezo wa kuongea hata na wanyama pia.
7. Inaongeza akili kumbukumbu na ubunifu:
kupitia ufahamu utakao kuwa nao kwa zoezi hili inaeleweka kwamba utakuwa umefungua sehemu za ubongo wako za fahamu zinazodeal na akili pamoja na kumbukumbu.
8. Kukuwezesha kupata majibu yako mwenyewe kwa spiritual guide:
kutoka nje ya mwili kutakujibia maswali mengi ambayo ulikua huwezi kuyajibu katika ulimwengu wako wa kiroho.
9. Kuondoa woga wa kufa:
kuhofia kifo ni kuhofia jambo usilolijua.utakapotoka utaona kwamba kumbe nina uwezo wa kuishi maisha ya pili hata nikifa.
10. Kutambua na kuelewa mambo ya kale yaliyopita:
utajifunza jinsi ya kupanua ubongo wako haya kuzungumza na historia za kale ingawa unaweza kuona pia tukio lijalo ila hii ni kwa wenye power ya precognition na retrocognitions.
11. Kupaa na kufurahi:
Ulimwengu wa roho hata anga sio mpaka. unaweza kupaa nyuma ya mawingu. na ukapaa kama puto. unataka kuwa na macho ya ndege mjini? la shaka! au unataka kupaa na kuogelea kama samaki dolphin na hata kuruka kama ndege, au kudumbukia ndani na kuogelea kama samaki!
ukitaka unaweza hata kufika kwenye sayari za juu na zile ambazo bado hazijawa discovered wazungu walifanya zamani sana hii na kwenda huko kabla hata ya kurusha ndege, unaweza kwenda popote duniani na nje ya dunia hata kuwatembelea marafiki kila corner ya ulikmwengu
12. Kuthibitisha kwamba mwili wako utakufa ila akili au nafsi yako itabaki tu
13. utayaona mengi maisha yako yaliopita na kuyachezea na utakuwa na nafasi ya kuona kila kitu ambacho unatakiwa kufanya ufanikiwe:
Pia hii yaweza kuwa tiba kubwa kwa magonjwa yasiyotibika kwa maana unaingia hata sehemu ambazo zimefichwa hasa na waweza kula dawa yeyote.
14. Kukutana Na Malaika wako wawili
Utawaona hawa hatua ya kwanza kutoka na kukuongoza kwa mengi ukitaka kuwaona.
japokuwa hawaonekani moja kwa moja ila kama vivuli
15. Kuongeza Nguvu ya miujiza
Kutoka huku kutakufanya uongeze nguvu zako za miujiza kama vile
kuona vitu visivyoonekana kwenye real world, kuskia sauti za mawazo ya mtu, kujua kinachotokea dk kadhaa zijazo, kumlazimisha mtu kufanya utakacho (mind control), kuhisi jambo fulani linatokea, nguvu ya unabii,
16. Kuona aura ya kila kitu na nguvu zingine nyingi tu. haya yote yatakutokea kwa maana umezidi mpaka wa ubongo wako hapa ndio tunaanza kuona more than a normal brain function(waweza kuwa genius pia ukitumia vizuri, anyway usitumie manguvu yote hovyo utaanza kuhisi kuchanganyikiwa fuata hatua kwa hatua.
17. kujaza busara akilini.
hii hukufanya uzidishe busara katika akili yako na amani kuu katika roho yako
18. Kuongeza tamaa ya kupata majibu
Kutoka nje ya mwili kutakufanya kujibu maswali na kujua zaidi kwamba wewe ni nani? upo wapi? na unafanya nini? na unaenda wapi? ukijua hayo hutabadilika mfumo wako wa maisha?
19. Kuwaona waliokufa
Hapa utakutana na ndugu zako uliokuwa ukiwapenda waliotangulia mbele za haki. Kukutana nao huku kutakusaidia sana kuwasaidia kama kuwalipia madeni na kukuonyesha mali walizoficha kama walikua wanakupenda.
20. Kujiongezea maajabu ya maisha
hapa utajifunza mengi kuona kila kiumbe kisichoonekana kupajua sehemu watu na nyumba kabla hujaenda
21. Kupona
Ukitoka nje ya mwili unakuwa umejitibu hapa utaweza kujitibu mwenyewe na wengine na wanyama pia.
Na Hizo bado ni baadhi tu:
View attachment 420282HATUA ZA KUFUATA:
Ni Aina Ya Nguvu Ambayo Huwa Nayo Watu Wote Isipokuwa Katika 100%
65% Ni Watu Wasioijua
25% Ni Watu Wanaoijua
10% Ni Watu Wanaoitumia
Hatua za kufuata ili uweze kutoka nje ya mwili
Kuna Njia Mbili Za Kutoka Nje Ya Mwili Hapa Nitaielezea Moja.
Njia Hizo Ni:
1; Kutoka nje wewe binafsi
2: Kutoka nje ya mwili kwa msaada wa mlio(Binaural beats)
View attachment 420201
HATUA ZA KUFUATA KWA NJIA YA KWANZA:
NI RAHISI TU.!
Ukiwa katika hali ya utulivu na utayari na amani na pia kujiamini kuwa leo nitaweza kutoka kwa mara ya kwanza,
1; Oga Na Vaa Nguo Safi Zisizo Bana yaweza kuwa hata night dress ambayo ni laini au nguo yoyote itakayokufanya uwe vema na huru katika kufanya jambo hili,
2: Lala Chali Mgongo Ukiwa Umenyooka Vema huku umefumba macho, hakikisha hukazi mwili wala kufanya focus yoyote katika mwili wako ili uweze kufanya vema na kwa usawa na utulivu,
View attachment 420202
3: wakati ukiendelea kuutafuta utulivu utapata vishawishi vya kujigeuza au kujitingisha usiweke mawazo yako huko usiweke wazo moja wala usilenge wazo sehemu moja wala usitengeneze picha yoyote akilini wewe tulia tu. Kumbuka ili kufanikisha zoezi lolote la kiroho UTULIVU,UTULIVU,UTULIVU pekee ndio jambo au kitendo au maamuzi pekee ya kukufanikishia jambo la kiroho, usijishike wala kujitingisha wewe tulia tu UTULIVU ndio kitu kiwe kinachozunguka kwenye akili yako na mwili wako na pumzi yako TULIA. utaanza kuhisi uzito kwenye viungo mbali mbali vya mwili wako hasa kichwa.
4: Usitingishe Macho Wala Kuchezesha Mwili Wako. tulizana usiogope wala usihofu kwa maana hakuna cha kukuogopesha kwa wakati huo zaidi ya mwili wako ni sawa na mtu aliyelala usingizi.
5: Subiri Na utulizane Kwenye Pumzi yako ( Hapa unakuwa unaupa taarifa ubongo wako kuwa mwili wote umeshalala au upo kwenye state ya ndoto)
6: ukiweza kujizuia Kujigeuza Geuza Au Kujikuna Ubongo Utajua Umelala Na Utaruhusu Mwili Kuachia Kinga Ya Paralysis Au Ganzi Salama Ya Mwili Mzima.
Ambayo Huwa Inakinga Miili Yetu Kutokujiumiza Wakati wa Kuota Mfano: sleep walking(unaota huku unatembea) au wakati unapigana ndotoni usiweze kupiga au kujiumiza.
7: Wakati Hali Hii Inatokea Hapo Ndipo Unaweza Kujitenga na mwili wako ambao umepata ganzi.
tatizo hapa huwa lipo katika kujua ni upi mwili sahihi maana bado miili miwili inakuwa imeshikana
ukiamka na mwili wako wa ganzi kila kitu utakuwa umevuruga na utaamka kwenye mwili wenye ganzi (hii mimi ninauzoefu nayo pia unajiona upo macho lakini mwili hauamki wala kucheza unaganda ni kawaida ila huwa ni inashtusha kidogo. haichukui muda ni kama sekunde 10 ukianza kujishtua au kujitingisha ila inashangaza kidogo na kukutisha kama ni mwoga kwa maana unaweza hisi utakuwa hivyo moja kwa moja.
Sasa Je Utajua Vipi Kati Ya Miili Hii Upi Ni Sahihi?
Mbinu Rahisi Ipo Hivi Ukifikia Kwenye Hatua Hiyo Ya Kutoka. tengeneza picha Kwamba Una Mikono Mipya Na Miguu Mipya..
na ukishaingia kwenye hali hiyo hutokea set ya mingine na ndio unaweza kutumia kwa kutoka.
Lakini kwa wengine hii huwa ngumu sasa hapo unatakiwa uangalie dali na kuhisi ikiwa ni pamoja na mbinu kuwa kamba inashuka na kukukuta unaishika kisha unahisi inakuvuta na kukufanya uelee
9: Baada Ya Hapo Inuka Katika Mwili Wako huo na Sogea Mbele Hatua Tano Geuka Nyuma na Uangalie Mwili Wako Uliouacha.
10: Hongera Umeweza Fanya Chochote Unachojiskia Hakina Madhara Kwenye Real World....
lakini vipo ambavyo vinaonekana in real world play safe there.
Lakini pia kwa wanaoanza ni bora asiende mbali aishie karibu na nyumbani kisha azunguke zunguke ili azoee mazingira ya mwili huo na hali hiyo.
ANGALIZO:
View attachment 420205
Wakati Unautizama Mwili Wako Uliouacha Kuna Kitu Kina Kuwa Kimekuunga Na Ule Mwili Kama Silver cold Hivi Nyeupe Ya Kama Wingu Hiyo Ndio Hukusaidia Kurudi Hata Kama Umepotea Njia.....
View attachment 420206
kama una swali ambalo ni personal na upo nje ya forum:
Wasiliana nami kupitia email hii:
Rakimsspiritual@gmail.com
au namba hii ya mtu aliye karibu nami
+255626085437
Kwa haya na mengineyo pia tembelea
Rakims Spiritual
Rakims
Tungur siyo lazima liwe kibuyu kwani wazungu hutumia matunguri katika ulogi?umeona tunguli hapo?
Duu asa kilichokuleta apa n nnLo amaa kweli !! Dunia imefika mwisho,yaani watu wanafundisha uchaw hadhran bila hata aibu
ebu nyinyi wachawi mtuondolee matunguri yenu
Wadhungu wachawi balaa ila matunguli hawanaTungur siyo lazima liwe kibuyu kwani wazungu hutumia matunguri katika ulogi?
Wadhungu wachawi balaa ila matunguli hawana
hizo ni hatua za awali..hukutakiwa kurudi mapema namna hyoSir Rakims !
Nimejaribu Astral projection sijafanikiwa Moja kwa moja
Tatizo itakuwa nini?
Nilitoka nikaona mwili Wangu unakoroma kama unakata roho nikarudi fasta iyo ni kawaida au ndo nilikuwa nakufa?
Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna kufa mkuu kama ni hivyo kila anaelala akitoka bila dhamira angekuwa anakufa. popote kwenye jambo la mafanikio vitisho lazima viwe vingi ili watu washindwe, wanaoweza wazidi kuwatawalaje
hi ndgu imekaa je mbona wanatuogopesha wanasema kuna mambo ya kufa kufa hapo pamekaeje
Umejifunza na benefits zake, kwanini usifanye sasa kwa kujua na kujiamrishaKuna wakati nilikuwa natoka mara kwa mara, sio kwa kupenda lakini. Nilikuwa kila nikilala baada ya muda najiona napaa na kwenda sehemu mbali mbali kama ndege. I
Aisee..Iliiogopesha kwa sababu kua wakati mwigine nilikuwa napata shida wakati wa kurudi, na nikirudi nakaa kwa muda siwezi kufanya kitu chochote, nashindwa kunyanyuka, hata kukunja kidole, ingawa nasikia kila kitu kinachoendelea.
Ukiwa umerudi hapo unakuwa upo kwenye paralysis it just a normal case mkuuIliiogopesha kwa sababu kua wakati mwigine nilikuwa napata shida wakati wa kurudi, na nikirudi nakaa kwa muda siwezi kufanya kitu chochote, nashindwa kunyanyuka, hata kukunja kidole, ingawa nasikia kila kitu kinachoendelea.