Jinsi ya kutoka nje ya mwili (Astral Projection)

Rakims

JF-Expert Member
Jun 4, 2014
4,982
4,481
ASTRAL PROJECTION/Mental Projection.

Ni ule uwezo wa mtu kutengana na mwili wake kwa fikra katika imani Husemwa Kiroho.
Pale ambapo roho yako inakuwa imetengana na mwili wako wa nyama.

Utokaji huu wa nje ya mwili upo wa aina mbili au tatu na wenyewe ni wa roughly watu wanafundisha kwa maelezo marefu na mapana hali ya kuwa ni kitu kifupi tu watu wanatakiwa kujua jinsi ya kutoka na mengine kujifunza pale wanapokuwa wameshatoka ndio maana huitwa OOBE yaani Out Of Body Experience.
Baada ya wewe kutoka nje ya mwili umeexperience nini?
Na kile ulichoexperience wewe sio kukiweka sheria maana kila mtu anaweza kutoka nje ya mwili ikiwa atapata muongozo mzuri sasa kuna watu tofauti tofauti wanaweza kutoka nje ya mwili nao wakaja na makala zao za kukurupuka na Experience zisizo na kichwa wala miguu wengine experience zao ni za dhana.

images (2).jpg


FAIDA ZAKE:

Hakuna chochote utakachopenda au kuthubutu kufanya pasipo kujua faida wala hasara au Athari zake zifuatazo ni faida chache anaweza kupata yoyote mwenye kuthubutu kutoka nje ya mwili:

1. Kujitambua kuwa wewe hufi na kuondoka moja kwa moja: Hili ni tukio litakalo kubadilishia maisha. Mamilioni ya watu wamekua wakithibitisha kuwa mtu akifa hapotei moja kwa moja bali kuna maisha mengine ambayo ataishi wale wasioamini life after dealth.

2. Kuongeza uwezo mzuri wa kulala:
Hii husaidia mtu kulala katika hali ya usalama na kupata nguvu inayozungumziwa baada ya kulala na kujua ni ipi sababu kubwa ya kulala tunalala ili miili yetu ipumzike roho zetu zianze kuishi.

3. Kuongeza nguvu ya majariwa:
Hii inaongeza kipawa cha unabii na uwezo mkubwa wa kumsoma mtu akili hufahamika kama kama mind reading au telepathy, kasimama hapo wewe unaongea na roho yake.

4. Kujiendeleza Kimaisha:
Ukiwa nje ya mwili inakuthibitishia kuwa wewe ni zaidi ya binadamu wa kawaida hivyo hukuongezea akili ya utendaji zaidi kwa kutumia maajabu na si nguvu tena.

5. Inakuongezea kukomaa kiroho:
Watu wengi wamekuwa na roho nzuri baada ya kuishi na kiumbe zaidi ya asiekuwa mwanadamu.

6. Inaongeza heshima ya maisha:
Hii hukufanya umuheshimu kila kiumbe na umuhurumie hata paka maana kule una uwezo wa kuongea hata na wanyama pia.

7. Inaongeza akili kumbukumbu na ubunifu:
kupitia ufahamu utakao kuwa nao kwa zoezi hili inaeleweka kwamba utakuwa umefungua sehemu za ubongo wako za fahamu zinazodeal na akili pamoja na kumbukumbu.

8. Kukuwezesha kupata majibu yako mwenyewe kwa spiritual guide:
kutoka nje ya mwili kutakujibia maswali mengi ambayo ulikua huwezi kuyajibu katika ulimwengu wako wa kiroho.

9. Kuondoa woga wa kufa:
kuhofia kifo ni kuhofia jambo usilolijua.utakapotoka utaona kwamba kumbe nina uwezo wa kuishi maisha ya pili hata nikifa.

10. Kutambua na kuelewa mambo ya kale yaliyopita:
utajifunza jinsi ya kupanua ubongo wako haya kuzungumza na historia za kale ingawa unaweza kuona pia tukio lijalo ila hii ni kwa wenye power ya precognition na retrocognitions.

11. Kupaa na kufurahi:
Ulimwengu wa roho hata anga sio mpaka. unaweza kupaa nyuma ya mawingu. na ukapaa kama puto. unataka kuwa na macho ya ndege mjini? la shaka! au unataka kupaa na kuogelea kama samaki dolphin na hata kuruka kama ndege, au kudumbukia ndani na kuogelea kama samaki!

ukitaka unaweza hata kufika kwenye sayari za juu na zile ambazo bado hazijawa discovered wazungu walifanya zamani sana hii na kwenda huko kabla hata ya kurusha ndege, unaweza kwenda popote duniani na nje ya dunia hata kuwatembelea marafiki kila corner ya ulikmwengu

12. Kuthibitisha kwamba mwili wako utakufa ila akili au nafsi yako itabaki tu

13. utayaona mengi maisha yako yaliopita na kuyachezea na utakuwa na nafasi ya kuona kila kitu ambacho unatakiwa kufanya ufanikiwe:
Pia hii yaweza kuwa tiba kubwa kwa magonjwa yasiyotibika kwa maana unaingia hata sehemu ambazo zimefichwa hasa na waweza kula dawa yeyote.

14. Kukutana Na Malaika wako wawili
Utawaona hawa hatua ya kwanza kutoka na kukuongoza kwa mengi ukitaka kuwaona.
japokuwa hawaonekani moja kwa moja ila kama vivuli

15. Kuongeza Nguvu ya miujiza
Kutoka huku kutakufanya uongeze nguvu zako za miujiza kama vile
kuona vitu visivyoonekana kwenye real world, kuskia sauti za mawazo ya mtu, kujua kinachotokea dk kadhaa zijazo, kumlazimisha mtu kufanya utakacho (mind control), kuhisi jambo fulani linatokea, nguvu ya unabii,

16. Kuona aura ya kila kitu na nguvu zingine nyingi tu. haya yote yatakutokea kwa maana umezidi mpaka wa ubongo wako hapa ndio tunaanza kuona more than a normal brain function(waweza kuwa genius pia ukitumia vizuri, anyway usitumie manguvu yote hovyo utaanza kuhisi kuchanganyikiwa fuata hatua kwa hatua.

17. kujaza busara akilini.
hii hukufanya uzidishe busara katika akili yako na amani kuu katika roho yako

18. Kuongeza tamaa ya kupata majibu
Kutoka nje ya mwili kutakufanya kujibu maswali na kujua zaidi kwamba wewe ni nani? upo wapi? na unafanya nini? na unaenda wapi? ukijua hayo hutabadilika mfumo wako wa maisha?

19. Kuwaona waliokufa
Hapa utakutana na ndugu zako uliokuwa ukiwapenda waliotangulia mbele za haki. Kukutana nao huku kutakusaidia sana kuwasaidia kama kuwalipia madeni na kukuonyesha mali walizoficha kama walikua wanakupenda.

20. Kujiongezea maajabu ya maisha
hapa utajifunza mengi kuona kila kiumbe kisichoonekana kupajua sehemu watu na nyumba kabla hujaenda

21. Kupona
Ukitoka nje ya mwili unakuwa umejitibu hapa utaweza kujitibu mwenyewe na wengine na wanyama pia.

Na hizo bado ni baadhi tu:
astral-travel-compressed.jpg

Ni aina ya uwezo ambao huwa nao watu wote kwa 100%
Lakini

65% Ni watu wasiojua na wala hawaamini kama inawezekana

25% Ni watu wanaojua na wanaamini inawezekana

10% Ni watu wanaoju na wanaamini lakini vile vile wameshaweza na wanatumia katika maswala mbali mbali.

Hatua za kufuata ili uweze kutoka nje ya mwili


JINSI YA KUFANYA:
Ili kuweza kutoka nje ya mwili kuna njia kuu mbili lakini hapa nitapenda kuelezea moja ambayo ni nzuri zaidi na salama zaidi.


1: Kutoka nje ya mwili ukiwa wewe binafsi.

2: Kutoka nje ya mwili kwa msaada wa sauti yaani (Binaural beats)

astral-projection.jpg


HATUA ZA KUFUATA KWA NJIA YA KWANZA:

NI RAHISI TU!

Ukiwa katika hali ya utulivu na utayari na amani na pia kujiamini kuwa leo nitaweza kutoka kwa mara ya kwanza,

HATUA ZA KUFUATA:
1; Oga vaa nguo safi zisizo bana yaani yaweza kuwa hata night dress ambayo ni laini au nguo yoyote itakayokufanya uwe vema na huru katika kufanya jambo hili,

2: Lala chali mgongo ukiwa umenyooka vema huku umefumba macho,
hakikisha hukazi mwili wala kufanya focus yoyote katika mwili wako ili uweze kufanya vema na kwa usawa na utulivu, kuna muda utahisi unashindwa na koo lako linajaa mate usihofu ni hisia tu maana hata ukimeza mate inakuwa ni kama umeanza upya

images (4).jpg


3: wakati ukiendelea kuutafuta utulivu utapata vishawishi vya kujigeuza au kujitingisha usiweke mawazo yako huko usiweke wazo moja wala usilenge wazo sehemu moja wala usitengeneze picha yoyote akilini wewe tulia tu.
Kumbuka ili kufanikisha zoezi lolote la kiroho UTULIVU,UTULIVU,UTULIVU pekee ndio jambo au kitendo au maamuzi pekee ya kukufanikishia jambo la kiroho,
Usijishike wala kujitingisha wewe tulia tu UTULIVU ndio kitu kiwe kinachozunguka kwenye akili yako na mwili wako na pumzi yako iwe inapumua neno moja tu TULIA.
utaanza kuhisi uzito kwenye viungo mbali mbali vya mwili wako hasa kichwa.

4: Usitingishe macho wala kuchezesha mwili wako.
tulizana usiogope wala usihofu kwa maana hakuna cha kukuogopesha kwa wakati huo zaidi ya mwili wako ni sawa na mtu aliyelala usingizi maana hata kama mwili wako utakuwa na maumivu sehemu basi hujipoza wenyewe kwa ganzi salama na hata kama mwili ukitaka kupata tatizo wenyewe utakuweka sawa kujidhuru ni jambo ambalo halipo ukiwa umelala aliyekuumba alihakikisha usalama wako wakati umelala.

5: Subiri na utulizane kwenye pumzi yako lakini pia ifikie muda hata pumzi nayo utakuwa huna habari nayo maana nayo kuna muda dakika kadhaa baada ya zoezi inakuwa kero kuifuatilia (Hapa unakuwa unaupa taarifa ubongo wako kuwa mwili wote umeshalala)

6: ukiweza kujizuia kujigeuza geuza au kujikuna na kujitingisha Ubongo wako utatambua umelala na utaruhusu mwili wako kuachia Ganzi Salama ya mwili mzima.
Utahisi kama kitu kinakuvaa kutoka miguuni inaenda inapanda itakapofika kifuani utahisi uzito katika kifua chako zaidi na utahisi kama umewekewa kimzigo pumzi itaanza kuja kwa kasi kidogo hapo ndio unatakiwa kumaintain mapigo ya moyo wako usiache yapige kwa kukutia hofu na kukujaza mashaka tulia na weka furaha kwamba upo karibu kufanikiwa,


ikifika kichwani ndio sehemu pekee ambayo unaweza kufanikisha au kuribu zoezi zima maana kuna muda inaweza kukupindisha kichwa pembeni au inaweza kudidimiza kichwa chako ganzi hiyo ambayo huwa inakinga miili yetu kutokujiumiza wakati wa kuota

Mfano:
Sleep walking(unaota huku unatembea) au wakati unapigana ndotoni usiweze kujipiga au kujiumiza.

7: Wakati hali hii inatokea hapo ndipo unaweza kujitenga na mwili wako ambao umepata ganzi.
tatizo hapa huwa lipo katika kujua ni upi mwili sahihi maana bado miili miwili inakuwa imeshikana
ukiamka na mwili wako wa ganzi kila kitu utakuwa umevuruga na utaamka kwenye mwili wenye ganzi
(hii mimi ninauzoefu nayo pia unajiona upo macho lakini mwili hauamki wala kucheza unaganda ni kawaida ila huwa ni inashtusha kidogo).
haichukui muda ni kama sekunde 30 ukianza kujishtua au kujitingisha ila inashangaza kidogo na kukutisha kama ni muoga kwa maana unaweza hisi utakuwa hivyo moja kwa moja.

Sasa Je Utajua Vipi Kati Ya Miili Hii Upi Ni Sahihi?

Mbinu Rahisi Ipo Hivi Ukifikia Kwenye Hatua Hiyo Ya Kutoka. tengeneza picha Kwamba Una Mikono Mipya Na Miguu Mipya..
na ukishaingia kwenye hali hiyo hutokea set ya mingine na ndio unaweza kutumia kwa kutoka.

Lakini kwa wengine hii huwa ngumu sasa hapo unatakiwa uangalie Dali na kuhisi ikiwa ni pamoja na mbinu kuwa kamba inashuka na kukukuta unaishika kisha unahisi inakuvuta na kukufanya uelee.
Lakini kwa sisi wazoefu ukifika kwenye ganzi unavisualize kuinuka unainuka.

9: Baada ya hapo utahisi unaelea na hatua kadhaa simama wima tizama kitandani mwili wako uliouacha ukiuona basa tizama silver cord kama ipo imekuunganisha na mwili wako. ukiiona basi jua upo nje ya mwili lakini usipoona mwili wako na silver cord huioni basi jijue unaota na haupo nje ya mwili hapo pia unaweza kufurahia na ndoto yoyote unayotaka kuiota lakini pia unaweza kutoka nje ya mwili ukiwa ndani ya ndoto nimeeliza jinsi ya kufanya kwenye makala ya kucid dream nje ya mwili katika blog yangu.

10: Hongera umeweza fanya chochote unachojiskia hakina madhara kwenye Ulimwengu wa nyama kwa kuwa wewe ndio umeanza lakini kwa masters kinakuwa na Athari.
lakini vipo ambavyo vinaonekana in real world nakushauri ufanye unayofanya salama kuna mengi utajua ya kufurahisha na mengine ya kusikitisha play safe there.


ANGALIZO:
Lakini pia kwa wanaoanza ni bora asiende mbali aishie karibu na nyumbani kisha azunguke zunguke ili kuweza kuzoea mazingira ya mwili huo na hali hiyo.


3638238241_527c68904b_z.jpg

Wakati unatizama mwili wako utakapoiona silver cord inakuwa inaonekana kama utando huo pichani.

download.jpg



1423494076425.jpg



Kwa haya na mengineyo:
Tembelea:

Rakims

quote_341.jpg
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Rakims na MziziMkavu, naombeni sana wakati mnatoa hili somo, pia muwape angalizo muhimu hao wanafunzi wenu, kuwa mchezo huu pia ni sawa na kuijaribu sumu kwa kuilamba!. Waambieni nguvu zinazotumika kuyafanya haya sio nguvu za Mungu ni nguvu za giza!. Wapeni kabisa masharti ya kuzingatia, wakikosea ndio safari jumla!, asubuhi unakutwa ulitangulia ukiwa usingizini!.

Masharti ni haya.
  1. Fanya hivyo ukiwa umelala peke yako chumbani, na kabla hujaanza ujinga huo, hakikisha umefunga mlango kwa funguo, kwa sababu akitokea mtu akakuamsha kwa kukutingisha kwa nguvu na kuchange ile position yako hata ya milimita moja, ile cord ni kama utando wa buibui, inakatika, wewe unakuwa ndio basi tena!.
  2. Unaweza kukutana na "the under world" ukaona maisha hayo ya astra plane (ni maisha ya kichawi) ndio bora zaidi kuliko real world, hivyo cord ikakatika, huku unakutwa ndio basi tena!, wewe ni safari jumla!, zinageuka mchawi!.
  3. Hizi ni highest stages za meditation ambazo haziruhusiwi kufanywa na beginners, na hazifanywi un supervised bila supervisor na supervision, vinginevyo ni safari jumla!.
  4. Yote utakayoyashuhudia kwenye astra body, unaweza kuyafanya by simply opening up the "third eye!"
  5. Hizi ndizo the first stages za wachawi!.
Wito wangu mimi wa wafuatiliaji wa haya makitu, kama hujui unataka nini, au utoke out of body ili kuachieve nini, please don't try this or do it!. Mtu asikudanganye kuwa its very fun to go out of body, is not fun!. Too much knowledge on anything is harmful, please don't try unless you are very sure of what going into, and you are trying to do and what to achieve and not doing it for fun!, na ujue unaingia kwenye ulimwengu wa majini na ushetani!.

Paskali
 
Pasco Ni kweli unayoyasema ndio maana kuna mambo mengine hayafai watu kufundishwa akikosea ndio anakufa moja kwa moja mimi huwa sipendi kujaribu kitu kwa njia ya Riski.

Mimi huwa inatokea sio kila siku kusafiri wakati nipo ndani ya usingizi nikikusudia huwa ndio ninasafiri na sio kwa nia mbaya bali kutembea na kujionea mwenyewe ulimwengu jinsi ulivyo ingawa ukizoea utaona raha lakini sio nzuri kusafiri ndani ya ndoto unaweza unakokwenda usirudi tena ulipo toka. nimekuelewa Mkuu Pasco.
 
Last edited by a moderator:
ASTRAL PROJECTION/Mental Projection......

Ni Ule Uwezo Wa Mtu Kutengana Na Mwili Wake Ki Fikra Katika Imani Husemwa Kiroho...

I respect your viewpoints Rakims, but I'm afraid you're taking allegiance with ignorance and diabolical celestial beings. The article in itself is full with speculation and unfounded assertion.

Your idea is based on your faith beliefs and dogmas, in contrast, your thread is more fiendish and supports witchcraft. My question is: are you open to the possibility that your belief system might be distorted and from not God? 
 
Kusafiri na kuona dunia jinsi ilivyo kwani watu waaokwenda angani wanakwenda kufanya nini huko miaka ya nyuma?

Kumbuka ulimwengu mnaojaribu kuuelezea hapa si ulimwengu wa kifizikia...

Je sasa hizo safari uzisemazo hatma (destination) yake ni kutaka kwenda wapi?

Pia ukimsoma vizuri Pasco kaeleza kuwa hata mwili wako binafsi unakuwa huna mamlaka nao tena bila shaka hata nafsi...

Je kwa wakati huo ni mamlaka ipi inayokuwa ikiongoza nafsi yako?
 
Last edited by a moderator:
Kumbuka ulimwengu mnaojaribu kuuelezea hapa si ulimwengu wa kifizikia...

Je sasa hizo safari uzisemazo hatma (destination) yake ni kutaka kwenda wapi?

Pia ukimsoma vizuri Pasco kaeleza kuwa hata mwili wako binafsi unakuwa huna mamlaka nao tena bila shaka hata nafsi...

Je kwa wakati huo ni mamlaka ipi inayokuwa ikiongoza nafsi yako?
Spirit Mkuu Watu8 mambo haya hutoyaweza tuachie sisi wenyewe tunayoyafanya.Mambo ya Ngoswe Muachie ngoswe mwenyewe wewe angalia mambo yako yanavyokwenda. Usijaribu hiyo Elimu ya hali ya juu sio kila mtu anaweza kujaribu unaweza kupoteza maisha yako ukikosea japo kidogo.
 
Hehehe...

Spirit Mkuu Watu8 mambo haya hutoyaweza tuachie sisi wenyewe tunayoyafanya.Mambo ya Ngoswe Muachie ngoswe mwenyewe wewe angalia mambo yako yanavyokwenda.

Usijaribu hiyo Elimu ya hali ya juu sio kila mtu anaweza kujaribu unaweza kupoteza maisha yako ukikosea japo kidogo.
 
Back
Top Bottom