Jinsi ya kutengeneza mwili bila kuingia Gym

Binafsi enzi hizo nilikua napiga kwa sequence maalum.
Kwanza nilianza kwa kupiga push ups za kutanua kifua. Ambazo unapanga matofali mawili kushoto na kulia kwako au vipande vya mbao kisha unakua mikono waiweka juu na kupiga push-ups huku kifua kikiingia katikati.
Nilikua napiga push-ups 50 na nilienda mizunguko 6.
Break ya round na round nilikua na piga squats 100.

Zoezi namba 2 nilikua napiga push-ups za kubana kifua huku mikono nikiibana level ya mabega napo idadi ya push-ups ni kama round one na reps ni sita.

Zoezi namba tatu hapa nilikua naikutanisha mikono kisha natengeneza shepu kama ya kopa.
Nilikua napiga push-ups 3 in 1(yani kila push ups tatu nilizihesabu kama moja) huku kila nikishuka chini kifua kina gusa ile kopa.
Zoezi hili lilikua maalum kwa kujenga msuli wa nyuma ya mkono, kujenga kifua cha juu na kuziba yale matundu ya shingoni,kuujenga mgongo na kua na mwonekano wa kupasuka pasuka.
Nilikua napiga push-up 20 na round 5.

Baada ya hapo nilipiga Zoezi la kujenga shoulders ambalo mara nyingi niliipigia kitandani.
Unachuchumaa kitanda kikiwa nyumba yako kisha mikono una irudisha nyuma na kushika ubao wa kitanda.
Zoezi hili unapiga taratibu na unatakiwa upige push ups hizi 60 *5.

Ukimaliza unaenda mlangoni na kupiga pull ups kwa ajili ya kujenga msuli wa mbele ya mkono.
Pia weza ligeuza kujenga msuli wa nyuma ya mkono.

Baada ya kushughulikia sehemu zote nilikua napiga zoezi la kutengeneza six packs.
Hili zoezi ni gumu kulielezea ila unakaa chini.
Kisha unainyanyua miguu yako unakua kama V. Baada ya hapo unaweka mikono yako kifuani na kuanza kupeleka miguu mbele kama unasukuma kitu bila kuishusha. Unapiga mbele 30,kushoto 30,kulia 30 then unageuka na kupiga push-ups 100 za basketball ili kujenga misuli ya mkono wa chini, zile nyama chini ya kiwiko chako.

Then unahamia kwenye mazoezi ya miguu ukimaliza unajikumbushia kata mbili tatu za wingchun then unapiga sparring na swahiba wako kujiweka fiti tu.
bro u a beast!!!
 
Kamanda eti pili pili ina madhara kwenye mazoezi?
Maana baadhi wanasema inakata pumzi!!!
Ndimu je?
Mimi situmii pilipili kabisa hivyo hili siwezi kukuthibitishia ila ndimu haina ubaya kwangu ndiyo juisi ya haraka niliyokua nakunywa nikimaliza mazoezi.

Ila hata kuhusu pilipili naamini ni stori tu.
 
Umeongea ukweli mkuu.
Ila Tukiachilia mbali swala la genetics kwa baadhi ya watu, wengi wetu tukila balanced diet ni kunenepa na mwisho kujipa kitambi.
Hapo ndipo shida ilipo sie wengine tukila mboga mboga mwili unakaa vyema ila ukileta mambo ya balance diet ndambi hilo!!
je maini ya ngombe hayana madhara?
 
Hapo ndipo shida ilipo sie wengine tukila mboga mboga mwili unakaa vyema ila ukileta mambo ya balance diet ndambi hilo!!
je maini ya ngombe hayana madhara?
Unafanya mazoezi kwa mtindo gani? Casual au hardcore?
 
Kuna article moja ilionesha kua kufanya mazoezi jioni ni vizuri zaidi kushinda asubuhi.
Binafsi ninaweza kufanya mazoezi kabla ya kulala.
Unafanya kabla the au baada ya chakula cha usiku?
Je Yafaa kufanya ukiwa umeshashiba?
 
Unafanya kabla the au baada ya chakula cha usiku?
Je Yafaa kufanya ukiwa umeshashiba?
Sijawahi kufanya mazoezi nikiwa nimeshiba kwakua kipindi naingia gym muda wangu ulikua ni saa 12 alfajiri mpaka saa 3 au saa 10 jioni mpaka saa 1.

Hiyo siyo mida ambayo nakua nimeshiba.
 
Unafanya mazoezi kwa mtindo gani? Casual au hardcore?
Naweza sema ni beginner Nakimbia Jogging dakika 30, push up za kawaida 20*3, sit up nikiwa nimezuia miguu kwenye tofali 50, leg raises *50, flute kick *50.'
Nataka ondoa Kifriji na kupunguza mwili plus 6Pack shida huku JNHPP Msosi ni wali /ugali nyama+harage kila siku.
Asubuhi naskip maana ni mikato na viazi vitamu....
Ushauri please hakuna chaguo hata vya kununua kuna chapati na vitumbua tu
 
Naweza sema ni beginner Nakimbia Jogging dakika 30, push up za kawaida 20*3, sit up nikiwa nimezuia miguu kwenye tofali 50, leg raises *50, flute kick *50.'
Nataka ondoa Kifriji na kupunguza mwili plus 6Pack shida huku JNHPP Msosi ni wali /ugali nyama+harage kila siku.
Asubuhi naskip maana ni mikato na viazi vitamu....
Ushauri please hakuna chaguo hata vya kununua kuna chapati na vitumbua tu
Ukifuatilia page ya tatu au ya nne utakuta kuna watu wamequote uzi orijino kabla haujafutwa na maelezo yake yote.

Pia kuna uzi niliandika kwa ajili ya mazoezi ya tumbo


Na wenyewe hauna maneno ila kuna watu waliniquote so utapata maelezo.

Kuondoa tumbo kunaanza na cardio kama vile kujog, kamba na aerobics. Kwa lengo la kuondoa tumbo nashauri baada ya muda uongeze juhudi katika mazoezi yako kwa kuongeza idadi na muda wa kufanya mazoezi.

Chakula unachokula siyo tatizo, tatizo lipo katika namna unayofanya mazoezi. Actually unatrain casually, so ongeza reps.
 
Kamanda eti pili pili ina madhara kwenye mazoezi?
Maana baadhi wanasema inakata pumzi!!!
Ndimu je?
Pilipili kwl inakata pumzi bro wang anacheza mpira akilaga msosi wa mchana hatumii kabisa pilipili na kama akitumiaga namuonaga uwanjan anavyokuw anahema kama mbwa
 
Back
Top Bottom