Jinsi ya kutengeneza mwili bila kuingia Gym

Katika kila uzi nilikua naonyesha beginner aanzeje, ajipe mapumziko kati ya zoezi moja na jingine kwa muda gani na nilionyesha mazoezi ambayo beginner anaweza kuanza nayo kabla hajajumuisha mazoezi yote.

Mfano katika uzi huu nilionyesha push ups ambazo beginner hazimfai hapa mwanzo..

Dawa ni kwenda slow na kuongeza vitu kadri muda unavyoenda. Sikuahidi kua kesho utaweza kujikuna mgongoni ila nakuahidi maumivu yatakua robo ya siku zingine.
Safi sana kwa maelezo mazuri, kuna gym nilianzia kipindi naanza tizi nikipigishwa vyumaa maninaaa as if ni pro kesho kutwa yake mikono imevimba na mwili kama sio wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sina formula, nilikua nakula kawaida tu kwa kuzingatia protin, wanga etc.

What matters ni mazoezi.
Hapana. Wataalamu wanasema mazoezi ni 20% tu na utaratibu wako wa kula ni 80%. Kama unafakamia macalories mengi kuliko unayounguza hata uwe unalala gym hakuna uzito utakaopoteza. Mazoezi na utaratibu mzuri wa chakula ni lazima viendane sawa.
 
maelezo yako mazuri sana, kinachitakiwa ni kuyafuata na kutekeleza, pale tutakapokuwa tuna kwama tutakuuliza
 
Hapana. Wataalamu wanasema mazoezi ni 20% tu na utaratibu wako wa kula ni 80%. Kama unafakamia macalories mengi kuliko unayounguza hata uwe unalala gym hakuna uzito utakaopoteza. Mazoezi na utaratibu mzuri wa chakula ni lazima viendane sawa.
Chief niamini mimi. What matters ni mazoezi, mazoezi ya mtindo wa hardcore hata kama unashindia wanga kila muda hardcore exercises itakuweka sehemu poa sana.
 
Hapana. Wataalamu wanasema mazoezi ni 20% tu na utaratibu wako wa kula ni 80%. Kama unafakamia macalories mengi kuliko unayounguza hata uwe unalala gym hakuna uzito utakaopoteza. Mazoezi na utaratibu mzuri wa chakula ni lazima viendane sawa.
Hapa ni mimi nikiwa nasoma. Nahisi unajua namna mwanafunzi anavyokula, anakua hana format ya nini kije au nini kisije..

tapatalk_1546614276791.jpeg
 
Je kwenye kwa haya matizi naweza kujaza kabisaa bila kugusa gym..
Nna siku ya tano toka nianze nahisi kama kuzoea hivi je nipumzike au niendelee??
 
Safi kabisa..
Ila bado naamini kuna mazoezi yale ya kupalilia, kufyeka, kulima, bustani, ufugaji, kufua nguo zako mwenyewe, kusaidia usafi wa boma lako, kukata fence n.k n.k. kwamba ni mazoezi tosha yanayokupa na yatajenga mwili wako vizuri tu kama ukiyafanya...Ni bora nguvu zako zitumike huko kuliko kupiga ma push ups yasiyosaidia familia...
 
Je kwenye kwa haya matizi naweza kujaza kabisaa bila kugusa gym..
Nna siku ya tano toka nianze nahisi kama kuzoea hivi je nipumzike au niendelee??
Umefanya mazoezi gani kwa siku tano?
 
Inakuaje wadau?

Nimeanza mazoezi ya kunyanyua uzito (I hate saying vyuma) mwaka 2013. Katika mazoezi hua tunasema majukumu ndiyo mchawi wa mazoezi, hivyo majukumu ya chuo yalikua yakinifanya nisiingie gym vile ninavyotaka iwe.
Wakati mwingine unajikuta unakosa pesa ya kuingia gym hivyo unajikuta huna option zaidi ya kukaa nyumbani ukiangalia ulivyoviingiza kwa wiki sita vikipukutika.

Lakini kwa muda nimekua nikitumia njia ambayo inanifanya kuubakisha mwili kwa kuujaza na kuukata.
Best of all, hili zoezi unaweza ukafanya popote na ndani ya dakika 45 (kutegemea na unavyotaka kua challenged).

Ili kuyafikia malengo ya hapo inabidi tufanye haya mazoezi kwa kutumia mtindo unaoitwa Tabata Protocol.

Zoezi tutakalolifanya litakua ni push ups (pushapu).

Na kanuni yetu itakua;

Zoezi moja litajumuisha seti nne.
Seti moja itajumuisha reps 20.
Kupumzika kati ya seti na seti ni sekunde 10.
Kupumzika kati ya zoezi moja na jingine ni dakika moja.

Anza na Pushap za Kawaida.
Hii ni ile aina ya pushap ambayo watu wengi wameizoea. Kama alizopiga Magufuli ila wewe usikunje ngumi.
View attachment 462249
Utaanza kwa kwenda juu ukishuka chini hiyo ni moja, utafanya hivyo mara 20. Utapumzika sekunde 10 na kurudia tena mara nne.

Hapo tunakua tumemaliza zoezi moja tunaenda jingine.

Pushap za miguu ikiwa imeinuka.
Mimi hua naweka miguu kitandani, unaweza ukaiweka kwenye stuli, jiwe au hata ndoo ukiigeuza juu chini. Pale daraja la Manzese miguu hua inawekwa kwenye ngazi.
View attachment 462252
Utaanza kwa kwenda juu ukishuka chini hiyo ni moja, utafanya hivyo mara 20. Utapumzika sekunde 10 na kurudia tena mara nne.

Hapo tunakua tumemaliza zoezi la pili, tunaenda jingine.

Tunakuja na Spartan Pushap.
Mikono yako inatakiwa ipishane, mmoja uwe mbele kushinda mwingine. Lakini ukiwa unaenda juu mkono uliokua mbele utaurudisha nyuma na uliokua nyuma unaupeleka mbele.
View attachment 462253
Utaanza kwa kwenda juu ukishuka chini hiyo ni moja, utafanya hivyo mara 20. Utapumzika sekunde 10 na kurudia tena mara nne.

Hapo tunakua tumemaliza zoezi la tatu tunaenda jingine.

Tunamalizia na Pushap za Magoti kugusa Chini.
Unaweka mikono kama unataka kupiga pushap alizopiga Magufuli, ila magoti yako yatakua yamegusa chini na usikunje ngumi kama Magufuli.
View attachment 462255
Utaanza kwa kwenda juu ukishuka chini hiyo ni moja, utafanya hivyo mara 20. Utapumzika sekunde 10 na kurudia tena mara nne.

Hapo tunakua tumemaliza zoezi letu.

NB.
-Utavuja sana jasho ndani ya dakika moja
-Kama hujawahi kufanya mazoezi, usifanye spartan pushap na hii ya magoti kugusa chini kwa sasa mpaka utakapozoea. Pia punguza idadi ya seti na reps, jiongezee na muda wa kupumzika.
-Natumia uzoefu na kujifunza kwa wengine, sijasomea, ushauri wangu siyo wa kidaktari.
-Comment workout yako tupate kujifunza.


Update:
Tafadhali usiniquote na kuniuliza juu ya hii mada
mm huwa push up zangu nazipiga wakati nagegeda
 
91 Reactions
Reply
Back
Top Bottom