Jinsi ya Kusajili kampuni katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

nataka kusjili kampuni, naomba mnielekeze juu ya hatua za kufuata na nataka kujua wapi zilipo ofisi za BRELA?
 
ingia kwenye tovuti ya BRELA wametoa maelezo ya kina juu ya usajili wa kampuni. Pia kuna fomu za usajili.
 
Mkuu nenda BRELLA utapata taratibu zote na pia kusajiliwa, isije ingizwa mjini na ofisi na mihuri ya kwenye mikoba.
 
BRELA utapewa maelezo ya nini kinatakiwa ili ufungue kampuni lakin unatakiwa utafute mwanasheria ili akutengenezee hizo nyaraka zinazotakiwa.
 
Mkuu,unaweza kufanya biashara kwa jina lako binafsi bila kwenda BRELA kwa kutumia kitambulisho chako kupata leseni na TIN. Unaweza pia kusajili jina hilo lako kuwa jina la biashara kupitia usajili wa BRELA. Kama unatumia jina lako binafsi sheria inakuruhusu kuto kwenda BRELA. Lakini kama utataka kutumia majina mfano. Mjamaica enterprises, Mjamaica general suppliers, mjamaica industries, Mjamaica ltd nk itabidi uanzie BRELA kusudi ijulikane kama kuna kampuni nyingine lenye jina hilo. Kama unatumia jina lako binafsi na unaona labda kampuni inaweza kuwa kubwa au kuwa inaweka matangazo kwenye vyombo vya habari ni vizuri usajili jina lako BRELA hata kama ni la binafsi. Hii ni kwa sababu mtu mwingine akiwahi kusajili jina hilo (labda anaitwa hivyo pia) hautaweza kuweka matangazo yako kwa sababu anaweza kukushtaki. BRELA ina hakikisha kwamba hakuna kampuni mbili zitakuwa na jina linalo fanana na la kampuni nyingine. Anaye wahi kusajili jina la biashara BRELA basi haitakubalika kamwe kampuni nyingine kuitwa jina hilo hilo. Inakuwa ni jina la kipekee na inasaidia sana kwa sababu mfano ukilipwa kwa cheki inamaanisha mtu yeyote mwenye jina kama lako anaweza kuchukuwa ile cheki na kuingiza kwenye akaunti yake na kulipwa hela yako. Ndio sababu benki wanaitisha vyeti vya BRELA wakati wanafungua akaunti za biashara na wanaenda kufanya search huko huko BRELA kuakikisha ni vyeti vya kweli.

chashi naomba kujua zaidi hapo kwa red
Mi tayari nina biashara ambayo nimeisajili kwa jina langu binafsi, ila sasa nataka kusajiri kama kampuni ili nitumie majina kama ......general supplier. Je BRELA watazikubali documents (TIN na leseni ya biashara) nilizokuwa natumia? au watataka nianze kutafuta mpya?
 
Mkuu mito, nenda na barua BRELA ya kuwaomba wasajili kampuni (andika jina unalotaka kusajili kwenye kichwa cha hiyo barua) wataangalia kwenye rekodi zao na kama hakuna kampuni imesajiliwa tayari kwa jina hilo watakubali na watakupatia fomu za kujaza. Sijui kama hizo document zingine zitasaidia chochote lakini ni bora uwe nazo. Sina hakika hiyo process inachukua mda gani, watakujulisha huko huko. Asante
 
Wakuu nahitaji kufungua kampuni itakayo shughulika na masuala ya IT, makao yake makuu ningependelea yawe Dar na vilevile kuwe na matawi mikoani. Bado sijaandaa ofisi. Kuna uwezekano wa kupata usajili?
Naombeni msaada wa hatua za kufuata ili kwanza ikiwezekana nipate usajili wa jina la kampuni kama inawezekana!!
 
Unaends kwa mwanasheria anakuiandalia memorandum and article of association,kuna gharama unalipia kutokana na maelewano na mwanasheria kwa mimi alinifanyia kilo moja,then zikiwa tayari anaweza kukusaidia kuzipeleka brela kwa malipo kuhusiana na brela visit web yao,ila ktk kuregister kampuni minimum capital inatakiwa uwe na tsh laki 3 by the time naregister 2009.brela watasajili jina kama halitakuwepo ktk orodha yao,fee ni ndogo tu,then watakupa certificate of incorporation then ndo utaitumia kuacquire licence ktk jiji na tin tra
 
Unaends kwa mwanasheria anakuiandalia memorandum and article of association,kuna gharama unalipia kutokana na maelewano na mwanasheria kwa mimi alinifanyia kilo moja,then zikiwa tayari anaweza kukusaidia kuzipeleka brela kwa malipo kuhusiana na brela visit web yao,ila ktk kuregister kampuni minimum capital inatakiwa uwe na tsh laki 3 by the time naregister 2009.brela watasajili jina kama halitakuwepo ktk orodha yao,fee ni ndogo tu,then watakupa certificate of incorporation then ndo utaitumia kuacquire licence ktk jiji na tin tra

Mkuu hapa umenipa mwanga na mimi kwani nina mpango huo hapo baadae
 
Andaa 700k na uni-PM nikuelekeze ofisi mjini. Usajili wa kampuni,certificate of incorportion,memarts,TIN number na business licence vitakuwa tayari in 10 days time.
 
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom