Jinsi ya Kusajili kampuni katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Usijali Mkuu

Sisi pia ni Registered Tax Consultants, hivyo ntakujibu

1. Makato ya kodi kwa kampuni ni 30% ya faida ghafi unayopata kwa mwaka mzima. Kodi hii utaijua baada ya kufanya mahesabu ya mizania

2. Tukirejea katika mfano wako, kama tulivyosema hapo juu ni kuwa kodi itakokotolewa kutoka ktk faida ghafi kwa mwaka mzima na sio robo ya mwaka. Kwa mfano kama mil 6 ni faida ghafi kwa mwaka utazidisha na 30% = 1.8mil na gawa kwa awamu nne za ulipaji kodi ie Ending Machi 31, Juni 30, Septemba 30 na Disemba 31 kila awamu utalipa 450,000.
Nashukuru mkuu!

Ila nasikia kuna income tax, witholding tax na mengine mengi mpaka nimeshindwa kuelewa!

So ina maana makato ni hiyo 30% kwenye faida ghafi kwa mwaka mzima basi au kuna nyingine tofauti na hiyo 30%?

Thanks in adwance mkuu
 
MAKALA: Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu kodi kwa mtu anayeanza biashara

Pitia mada hii utapata faida kubwa sana kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu ktk masuala ya kodi japo tuliiweka kitambo kdg
Kiwanda kama kiwanda kina lipa kodi zipi na zipi nimepitia huo uzi wa elimu juu ya kodi sema nimeona una vitu vingi ngoja niulize jambo la kodi hapa


Kiwanda kidogo kina aina ngapi za kodi, na pia kwa kuwa shareholder mwenzangu ambae yupo nje ha nchi yeye atakua ana share kubwa kidogo je huu wekezaji atatambulika yeye ndiyo mwenye kiwanda na je kodi kwa hapo watachaji vipi TRA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kiwanda kama kiwanda kina lipa kodi zipi na zipi nimepitia huo uzi wa elimu juu ya kodi sema nimeona una vitu vingi ngoja niulize jambo la kodi hapa


Kiwanda kidogo kina aina ngapi za kodi, na pia kwa kuwa shareholder mwenzangu ambae yupo nje ha nchi yeye atakua ana share kubwa kidogo je huu wekezaji atatambulika yeye ndiyo mwenye kiwanda na je kodi kwa hapo watachaji vipi TRA

Sent using Jamii Forums mobile app

Sawa Mkuu
Kwa kampuni inakuwa na kodi zifuatazo:
1. Kodi ya mapato 30%
hii nikodi ambayo utailipa kwa namna mbili, ikiwa mwanzo utaanza kulipa kwa kujikadiria ie Provision Tax na baada ya kukamilika mwaka utaandaa mahesabu ya mizania kisha kuangalia ulichilipa awali ni sahihi au laah kwa mujibu wa faida/hasara uliyopata kutokana na mapato

2. Kodi ya zuio WHT
Zimegawanyika utalipa 10% kwa mikataba na gawio na pia utalipa 5% kwa huduma

3. PAYE na SDL
Hizi ni kodi kampuni yako itawajibika kusimamia ulipwaji sahihi wa PAYE kama mishahara itakuwa zaidi ya 270+k na pia kulipa SDL kama wafanyakazi watakuwa zaidi ya wanne

4. Kodi ya ongezeko la thamani - VAT 18%
Hii kama mauzo yatakuwa mil 100 au kuzidi itabidi usajili na kulipa kutokana na mizani ya mauzo na manunuzi katika biashara yako

5. Ushuru wa stempu 1%
Kampuni italipia katika masuala ya kurasimisha mikataba
 
Sawa Mkuu
Kwa kampuni inakuwa na kodi zifuatazo:
1. Kodi ya mapato 30%
hii nikodi ambayo utailipa kwa namna mbili, ikiwa mwanzo utaanza kulipa kwa kujikadiria ie Provision Tax na baada ya kukamilika mwaka utaandaa mahesabu ya mizania kisha kuangalia ulichilipa awali ni sahihi au laah kwa mujibu wa faida/hasara uliyopata kutokana na mapato

2. Kodi ya zuio WHT
Zimegawanyika utalipa 10% kwa mikataba na gawio na pia utalipa 5% kwa huduma

3. PAYE na SDL
Hizi ni kodi kampuni yako itawajibika kusimamia ulipwaji sahihi wa PAYE kama mishahara itakuwa zaidi ya 270+k na pia kulipa SDL kama wafanyakazi watakuwa zaidi ya wanne

4. Kodi ya ongezeko la thamani - VAT 18%
Hii kama mauzo yatakuwa mil 100 au kuzidi itabidi usajili na kulipa kutokana na mizani ya mauzo na manunuzi katika biashara yako

5. Ushuru wa stempu 1%
Kampuni italipia katika masuala ya kurasimisha mikataba
Okey sawa sawa na je kwa kuwa partner wangu ni wa nje ya nchi na mwenye hisa kubwa, hapo TRA wataichukulia kama kampuni ni ya mwekezaji wa nje ya nchi na watamkadiliaje mapato ya kodi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Okey sawa sawa na je kwa kuwa partner wangu ni wa nje ya nchi na mwenye hisa kubwa, hapo TRA wataichukulia kama kampuni ni ya mwekezaji wa nje ya nchi na watamkadiliaje mapato ya kodi

Sent using Jamii Forums mobile app
Naam
1. Hapana hachukuliwi kama kampuni mali yake bali ni mali yenu wote wanahisa
2. Makadirio huwasilishwa mwisho wa mwaka kwa wakurugenzi wote wewe ba hy jamaa wa nje. Mtafanya 'assessment' ya kipato cha kila mkurugenzi kisha atalipa kodi kutokana na mapato ambayo huenda yanapatikana kutokana na kiwanda na shughuli nyinginezo binafsi za nje ya kiwanda
 
Naam
1. Hapana hachukuliwi kama kampuni mali yake bali ni mali yenu wote wanahisa
2. Makadirio huwasilishwa mwisho wa mwaka kwa wakurugenzi wote wewe ba hy jamaa wa nje. Mtafanya 'assessment' ya kipato cha kila mkurugenzi kisha atalipa kodi kutokana na mapato ambayo huenda yanapatikana kutokana na kiwanda na shughuli nyinginezo binafsi za nje ya kiwanda
Umenisaidia sana kweli umeiva mzee baba, una knowledge ya kutosha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habar za mchana.

Naomba kuuliza je mtu anaefanya biashara ya kununua madini kwa wachimbaji wadogo ambao hawana risit au kufanya biashara ya kuchimba madini kisha ukauza kwa madalali au soko kuu je mtu kama huyu analipaje kodi ukiangalia anapochimba au kununua hapati risit?

Shukran
 
Ahsanteee
Karibu sana
Habar za mchana.

Naomba kuuliza je mtu anaefanya biashara ya kununua madini kwa wachimbaji wadogo ambao hawana risit au kufanya biashara ya kuchimba madini kisha ukauza kwa madalali au soko kuu je mtu kama huyu analipaje kodi ukiangalia anapochimba au kununua hapati risit?

Shukran
 
Habar za mchana.

Naomba kuuliza je mtu anaefanya biashara ya kununua madini kwa wachimbaji wadogo ambao hawana risit au kufanya biashara ya kuchimba madini kisha ukauza kwa madalali au soko kuu je mtu kama huyu analipaje kodi ukiangalia anapochimba au kununua hapati risit?

Shukran
Salama Mkuu

Ni hivi kabla ya kuanza biashara yyt ile unatakiwa ukasajili Namba Maalum ya Mlipa Kodi ie TIN kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania ie TRA

Hii namba ndiyo itakuwezesha kulipa kodi. Baada ya kusajili kama ni mfanyabiashara na mauzo yk kwa mwaka yanazidi mil 4 utakadiriwa kiasi cha kodi cha kulipa kwa mwaka mzima. Hii haijalishi utakuwa wapata risit au laah. Japo sheria ya kodi imeweka wazi juu ya kutoa na kupata risit pindi unapofanya biashara.

Kupata risit ya mashine ie EFD Receipt inategemea wanunua kwa mfanyabiashara mwenye mapato kiasi gn kwa mwaka. Sheria imeweka wazi kama mauzo ni/zaidi ya mil 14 mfanyabiaahara hy analazimika kutoa risit ya mashine. Na kama ni chini ya hapo basi analazimika kutoa risiti ya mkono

Sasa kwa suala lako kodi ya madini utalipa kama ilivyoainishwa juu ktk makadirio na pia utalipia ushuru wa serikali ktk minada ya madini ya serikali

Pia pitia hapa kwa elimu ya kodi zaidi

MAKALA: Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu kodi kwa mtu anayeanza biashara
 
Salama Mkuu

Ni hivi kabla ya kuanza biashara yyt ile unatakiwa ukasajili Namba Maalum ya Mlipa Kodi ie TIN kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania ie TRA

Hii namba ndiyo itakuwezesha kulipa kodi. Baada ya kusajili kama ni mfanyabiashara na mauzo yk kwa mwaka yanazidi mil 4 utakadiriwa kiasi cha kodi cha kulipa kwa mwaka mzima. Hii haijalishi utakuwa wapata risit au laah. Japo sheria ya kodi imeweka wazi juu ya kutoa na kupata risit pindi unapofanya biashara.

Kupata risit ya mashine ie EFD Receipt inategemea wanunua kwa mfanyabiashara mwenye mapato kiasi gn kwa mwaka. Sheria imeweka wazi kama mauzo ni/zaidi ya mil 14 mfanyabiaahara hy analazimika kutoa risit ya mashine. Na kama ni chini ya hapo basi analazimika kutoa risiti ya mkono

Sasa kwa suala lako kodi ya madini utalipa kama ilivyoainishwa juu ktk makadirio na pia utalipia ushuru wa serikali ktk minada ya madini ya serikali

Pia pitia hapa kwa elimu ya kodi zaidi

MAKALA: Mambo muhimu ya kuzingatia kuhusu kodi kwa mtu anayeanza biashara
Nashukuru sana kiongozi.
Nimepata mwangaza.
 
Happy New Week,

#Jipatie

Logo kwa Tsh. 35000,

Flyers na Posters kwa 20000,

Brochures kwa 30000,

Business Card pc 110 kwa 35000

Tunafanya kazi zote za Graphic Designing,

Pia tunafanya Video Editing & Making.

Tucheki #0620275619

#NipeDili #ayendamethusela
 
Swali.
1) Je private LLC zinatakiwa ku file tax returns pia? Kama ndio zinatakiwa hata kama kampuni haikufanya kazi ktk kipindi hicho cha huo mwaka wa fedha? Na taratibu zikoje?

2) Taratibu za kufungua & kuendesha holding company ni zipi?
 
UTANGULIZI
Kuanzia tarehe 1 Februari 2018 #BRELA ilitangaza kuanza kutumika kwa mfumo wake wa kuwawezesha wamiliki wa makampuni na biashara kusajili na kuwasilisha returns BRELA. Pia BRELA ilishatangaza kwamba mnamo tarehe 25 Machi 2018 mfumo wake wa awali wa OBRS uliokuwa unaruhusu kusajili jina la biashara na kufanya clearance ya jina la kampuni kupitia website ungefungwa rasmi ili kuuruhusu mfumo mpya wa #ORS wenye uwezo wa kusajili majina ya biashara na makampuni kufanya kazi rasmi.

Hatua 10 za kufuata ili kusajili jina la biashara imeelezwa hapa chini, tafadhali fuatilia.

Kwa wale wanaohitaji kusajiliwa kampuni au jina la biashara chapu chapu tafadhali wasiliana nami kupitia kwenye ukurasa huu wa mawasiliano

HATUA 10 ZA USAJILI
Hatua #1: Taarifa za msajili, mmiliki au wamiliki wa biashara

  1. Kitambulisho cha Taifa kwa wenyeji na Passport kwa wageni
  2. Simu ya kiganjani
  3. Barua pepe yaani email
Hatua #2: Taarifa za biashara
  1. Aina ya biashara mtu binafsi, washirika au shirika
  2. Jina la biashara
Hatua #3: Ofisi ya biashara (Business Location)
  1. Aina ya eneo (Aidha limepimwa au la)
  2. Kama halijapimwa tayarisha anuanii ya makazi yenye mfumo huu, jina la Mkoa, Wilaya, Kata, kijiji, kitongoji na ueleze kama eneo lipo karibu na alama zipi ambazo hazihamishiki kama shule ya msingi nk. Usiweke alama ambazo hazina uhakika wa kudumu hapo maana brela watazikataa.
  3. Kama limepimwa tayarisha yafuatayo: Jina la Mkoa, Wilaya, Kata, kijiji/mtaa, barabara, namba ya kiwanja, namba ya kitalu na namba ya nyumba, sanduku la posta, simu ya ofisi/kiganjani na barua pepe (email)
Hatua #4: Shughuli za Biashara (Business Activities)
Hatua #5: Taarifa za Wamiliki (Business Owner’s Information) pamoja na Akaunti ya Benki kama ipo
  1. Aina ya mmiliki kama ni mtu au taasisi
  2. Asili yake kama ni mwenyeji au mgeni
  3. Kitambulisho cha taifa kama ni mwenyeji au passport kama ni mgeni
  4. TIN
  5. Simu ya kiganjani
  6. Barua pepe yaani email
  7. Anuani ya makazi kwa kila mmiliki kwa kufuata mfumo wa anuani ya ofisi hapo juu
Hatua #6: Taarifa za Akaunti ya Benki Zingine kama ipo (Business Bank Account Information)
  1. Aina ya mmiliki kama ni mtu au taasisi
  2. Asili yake kama ni mwenyeji au mgeni
  3. Kitambulisho cha taifa kama ni mwenyeji au passport kama ni mgeni
  4. TIN
  5. Simu ya kiganjani
  6. Barua pepe yaani email
  7. Anuani ya makazi kwa kila mmiliki kwa kufuata mfumo wa anuani ya ofisi hapo juu
Hatua #7: Taarifa za Wawakilishi (Person who can update ORS Information)
  1. Aina ya mmiliki kama ni mtu au taasisi
  2. Asili yake kama ni mwenyeji au mgeni
  3. Kitambulisho cha taifa kama ni mwenyeji au passport kama ni mgeni
  4. TIN
  5. Simu ya kiganjani
  6. Barua pepe yaani email
  7. Anuani ya makazi kwa kila mmiliki kwa kufuata mfumo wa anuani ya ofisi hapo juu
Hatua #8: Viambatanisho (Attachments in PDF)
Viambatanisho vinavyotakiwa kuambatanisha kwenye maombi (zote katika pdf) ni:-
  1. Consolidated form iliyosainiwa wamiliki wote wa biashara
  2. Viambatanisho vingine vinakuja - Mkataba wa washirika kama wamiliki ni zaidi ya mtu mmoja
Hatua #9: Ada za usajili na kufaili (Different Fees)
Aina za ada ni kama ilivyoonyeshwa hapa chini
  1. Kusajili biashara = TZS. 15,000
  2. Kuhifadhi nyaraka na = TZS. 5,000/mwaka
Hatua #10: Namna ya kulipa ada (Payment Methods)
Malipo ya ada yanafanyika kwa njia kuu tatu ambazo ni
  1. Kuweka Benki: Kwa njia ya kuweka Fedha kwenye Tawi la Benki /Wakala wa Benki
    Nenda kwenye Tawi lolote la Benki / Wakala wa Benki ya CRDB /NMB kwa kutumia Namba ya Kumbukumbu ya Malipo uliyopewa kupitia PO yako
  2. Kwa njia ya Simu ya Mkononi: Tumia mtandao wa simu wa AirTell Money / Tigopesa/ MPesa/ HalloPesa kwa kuweka namba ya Kampuni 888999 na Kumbukumbu ya Malipo uliyopewa kupitia PO yako
  3. Kwa njia ya Kuhamisha Fedha: Unaweza kuhamisha Fedha moja kwa moja kutoka katika Benki yoyote kwenda kwenye Akaunti zetu zilizoko katika Benki ya NMB/ CRDB kwa njia ya TISS /SWIFT kwa kujaza: Namba ya Akaunti na Kumbukumbu ya Malipo uliyopewa kupitia PO yako
Kumbuka: Utaratibu wa malipo aidha kwa simu au benki utapewa ukishafikia hatua husika ya malipo

Soma zaidi kuhusu jinsi ya kufanya malipo BRELA Kupitia Simu Yako

HITIMISHO NA USHAURI
Brela sasa hivi hawataki usajili kwa njia ya zamani, yaani kupeleka karatasi ngumu na kusubiri mlangoni kwa siku 6. Pia BRELA hawakubali mtu asiye na kitambulisho cha Taifa yaani #NIDA kusajili kampuni au jina la biashara.
Taarifa zilizotolewa hapo juu ni zile za lazima ambazo bila hizo huwezi kumalizia usajili na au usajili unaweza kukawia

Nashauri yafuatayo:
  1. Nashauri kama unataka kusajiliwa kampuni au jina la biashara kwa haraka wasiliana nasi kwa kutumia mawasiliano
  2. Kama huna kitambulisho cha Taifa na umeshaandikisha ili kupata kitambulisho cha Taifa, tembelea ofisi zozote za NIDA karibu na wewe ili wakupe angalau namba yako ya kitambulisho ili uweze kukitumia ukiambatanisha na Kibali cha BRELA ili Kupata Kitambulisho cha NIDA kwa haraka.
  3. Nashauri pia kama bado hujajiandikisha ni vyema ukawahi, hata kupitia kwenye eneo ambalo zoezi linaendelea ili uwahi kwa maana serikali imeanza kuzuia kupata huduma za public kama huna kitambulisho. ambatanisha pia Kibali cha BRELA ili Kupata Kitambulisho cha NIDA kwa haraka.
  4. Mwisho nashauri hizi taarifa zote uwe nazo mkononi kwa sababu huu mfumo wa usajili wa ORS unakupa siku sita (6 days) tu kukamilisha usajili kama baada ya hizo siku bado, taarifa zote zinafutika na itakubidi uanze upya from the scratch.
Kwa wale wanaohitaji kusajiliwa kampuni au jina la biashara chapu chapu tafadhali wasiliana nami kupitia kwenye ukurasa huu wa mawasiliano

Bofya hapa: Hatua 10 Rahisi za Kusajili Kampuni Kupitia Website ya BRELA
Broo nomba muongozo taratibu za kujisajiri TBS.
 
NAUZA CARWASH MPYA YA KISASA
MAELEZO: UJENZI, MACHINE ZOTE, VYOMBO, SIMTANK, KODI n.k
JUMLA: TZS 8,000,000

LOCATION: KINONDONI BLOCK 41
CALL: 0717 26 33 77
 
ETJ BANNER NW.jpg
SAJILI KAMPUNI YAKO SASA
 
Back
Top Bottom