Delightie
Senior Member
- Feb 7, 2014
- 138
- 196
Habari wapendwa,ni matumaini yangu mu wazima wa afya njema.Leo nataka niwaelekeze kupika mboga ya majani ya maboga kiurahisi na matamu sana,japo najua kila MTU ana style yake ya kuyapika.
MaHITAJI:
1.Majani ya maboga fungu hata 2 kutegemeana na ukubwa wa familia.
2.Hoho.
3.Kitunguu maji
4.Karoti
5.Mafuta ya kupikia
6.Karanga za kusaga(kipome) kwa wenzangu wa nyanda za juu kusini.
7.Chumvi
JINSI YA KUPIKA:
1. Chambua,osha vizuri halafu katakata mboga zako.
2. Chukua sufuria weka mboga yako,weka na mafuta ya kupika kiasi ukitakacho.
3. Andaa kitunguu,hoho,karoti pia weka vyote kwa pamoja juu ya mboga.
4. Weka chumvi na maji kiasi yatakayo tosha kuivisha mboga na karanga utazoweka baadae,ila yasizidi mboga,maana mboga ya majani INA tabia ya kunywea au kusinyaa ikichemka.
5. Bandika jikoni,baada ya dk 8 angalia kama viungo ulivoweka vimesinyaa.
6. Geuza mboga yako iache iive kama dk 5 tena.
7. Baada ya hapo weka karanga zako kulingana na wewe unavopenda(kama Mimi napenda karanga nyingi kwenye hii mboga).unapoweka unakoroga mpka zichanganyike na mboga vizuri.
8. Iache mboga iendelee kuchemka kama dk 5 usiifunike,maana karanga INA tabia ya kushika chini ya sufuria,koroga ili zisishike chini.
9. Hakikisha harufu ya karanga ile mbichi haisikiki,mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.
INAPENDEZA in UGALI,WALI HATA NDIZI MSHALE AU MZUZU ZILE MBICHI,UKIWA NA PARACHICHI PEMBENI.
MaHITAJI:
1.Majani ya maboga fungu hata 2 kutegemeana na ukubwa wa familia.
2.Hoho.
3.Kitunguu maji
4.Karoti
5.Mafuta ya kupikia
6.Karanga za kusaga(kipome) kwa wenzangu wa nyanda za juu kusini.
7.Chumvi
JINSI YA KUPIKA:
1. Chambua,osha vizuri halafu katakata mboga zako.
2. Chukua sufuria weka mboga yako,weka na mafuta ya kupika kiasi ukitakacho.
3. Andaa kitunguu,hoho,karoti pia weka vyote kwa pamoja juu ya mboga.
4. Weka chumvi na maji kiasi yatakayo tosha kuivisha mboga na karanga utazoweka baadae,ila yasizidi mboga,maana mboga ya majani INA tabia ya kunywea au kusinyaa ikichemka.
5. Bandika jikoni,baada ya dk 8 angalia kama viungo ulivoweka vimesinyaa.
6. Geuza mboga yako iache iive kama dk 5 tena.
7. Baada ya hapo weka karanga zako kulingana na wewe unavopenda(kama Mimi napenda karanga nyingi kwenye hii mboga).unapoweka unakoroga mpka zichanganyike na mboga vizuri.
8. Iache mboga iendelee kuchemka kama dk 5 usiifunike,maana karanga INA tabia ya kushika chini ya sufuria,koroga ili zisishike chini.
9. Hakikisha harufu ya karanga ile mbichi haisikiki,mboga yako itakuwa tayari kwa kuliwa.
INAPENDEZA in UGALI,WALI HATA NDIZI MSHALE AU MZUZU ZILE MBICHI,UKIWA NA PARACHICHI PEMBENI.