Jinsi ya kupika maandazi laini ya kuoka [baked]

Abu Haarith

JF-Expert Member
Oct 16, 2015
314
165
maandazilainibaked.jpg.jpg


Vipimo
Vikombe 3 vya unga
Kikombe 1 maziwa ya dafudafu (warm)
½ kikombe sukari
½ kikombe maziwa ya unga
Mayai 2
Kijiko 1 cha chai baking powder
½ kijiko cha hiliki ya unga
1/3 kikombe mafuta
Mchanganyiko wa hamira
2 vijiko vya kulia hamira
1 kijiko cha kulia unga
½ kikombe maji
1 kijiko cha chai sukari
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Weka mchanganyiko wa hamira katika bakuli dogo kisha koroga na acha uumuke kiasi dakika 5.
Kidokezo: Ukitaka hamira iumuke haraka: Washa microwave kiasi dakika 3 bila ya kitu ndani yake. Kisha weka mchanganyiko wa hamira ndani uache uumuke basi mara moja utaumuka.
Mchanganyiko Wa Maandazi
  1. Changanya vitu vyote katika bakuli la kukandia unga la umeme kisha tia mchanganyiko wa hamira.
  2. Washa mashine ikande unga kwa mpigo wa wastani (medium speed) kwa muda wa dakika 8 takrbian mpaka donge la unga liwe laini.
  3. Paka mafuta au unga mikononi kisha toa donge la unga ugawe madonge 9.
  4. Tandaza kila donge huku unanyunyizia unga ili usigande. Likisha tandazika likawa duara ya kiasi lisiwe nene, kata donge sehemu 4 za shape ya pembe tatu.
  5. Pakaza mafuta katika treya na nyunyizia unga kisha panga maandazi uwache nafasi yasije kugandana yatakapoumuka.
  6. Funika kwa karatasi ya plastiki au kitambaa kusikuweko na uwazi wa kuingia hewa. Acha yaumuke muda wa saa 1 au 1 ½ kutegemea hali ya hewa.
  7. Yachome (bake) katika moto wa wastani kwa dakika 10 takriban huku unaangaza mpaka yageuke rangi khafifu ya dhahabu.
  8. Epua yakiwa tayari panga katika sahani
Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

Kupata maelezo ya mapishi mbali mbali bonyeza hapa Muislamu: Mapishi
 
mie nikipata kumi pamoja na chai ya maziwa chupa moja nitakushukuru sanaaa. nitaomba dua kwa ajili yako
 
Wana bodi, kwa wale wenye kufahamu/uzoefu wa namna ya kuoka maandazi, vifaa (machines) vinavyotumika ktk kufanikisha kupata 'product' hyo, ikiwa ni pamoja na gharama zote za kuanzisha mrdi huo, namna ya kuunzisha na mazingira yanayofaa kufanya shughuli hyo. ....... Tafadhari sana naomba anifahamishe ..... Tufanikiwe kwa pamoja.

Ahsante
 
Msaada namna ya kupika andazi kubwa kabisa na ikaiva ndani vizuri
1.PIMA UNGA WA NGANO KIASI UPENDACHO KILO 1-3
PIMA MAFUTA YA KUPIKIA 1/2 LITA
YACHEMSHE KWA DAKIKA 5
3.MIMINA MAFUTA HAYO YA MOTO KATIKA UNGA ULIO UANDAA
4.WEKA VIUNGO VYAKO KATIKA UNGA ULIO UWEKA MAFUTA
5.CHANGANYA KWA MIKONO YAKO KWA MTINDO WA KUISAGA HADI UNGA UCHANGANYIKE VEMA
6.WEKA MAJI KISHA CHANGANYA HADI ULAINIKE
7.UACHE UUMUKE KISHA PIKA MAANDAZI YAKO HATA UKATE KUBWA KAMA MLIMA NDANI LITAIVA MKUU
 

Similar Discussions

5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom