Jinsi Ya Kupika Konokono Kama Chakula

We jamaa una hatari. Ungekuwa nchi flani hivi nina uhakika hadi chura ungepeleka puani.
Chura huku niliko analiwa japo sio sana, sema sinaga interest nao japo waliowahi kula chura wanaisifia nyama yake kuwa ni kama ya kuku...

NB: Sio kila chura analiwa, wengine wana sumu kali. chura wanaoliwa ni wale chura wakubwa wa magamba ambao kwa huku tunawaita nhundu. (huwa wakubwa kiasi cha kufikia ukubwa kama kikombe cha ujazo wa nusu lita)

Ipo siku nitaleta uzi jinsi chura huyu anakamatwa hadi kuandaliwa tayari kwa kuliwa.😂😂😂😂
 
Habari!

Twende moja kwa moja kama mada husika. Napenda sana kupika mapishi mbalimbali kulingana na mazingira niliyopo na nini nahitaji.

Sasa wapishi wenzanu wenye uzoefu na pishi la kumpika Konokono kwa chakula tusaidieni kupeana uzoefu.

Pia kama ni aina zote za Konokono unaweza kumfanya kitoweo kwa chakula.

Hii imenishawishi kutokana na eneo niliopo naona kuna Konokono wengi sana sasa kama naweza kuwafanya kitoweo.

Shukrani Ma-chef Cook Wote.
Mimi nitakufundisha mkuu
Umenikumbusha mbali Sana wakati nakaa na bibi yangu alinifundisha

Kwanza tafuta konokono wazima wale wanaokaa migombani au sehemu zenye unyevuunyevu (chukua wa kutosha) kisha tafuta sufulia kubwa waweke then Tia maji waweke jikoni wafunike, mpaka watokote kabisa ukijiridhisha waepue wakiwa hawajapoa tafuta kitu chenye ncha Kali tumia kifaa hicho kutoa mnofu wa konokono kwenye Ganda lake, ukimaliza waoshe vizuri kama unataka kukaanga weka viungo kama nyama ya kawaida kisha weka mafuta jikoni tayari Kwa kukaanga au ukitaka unaweza kuendelea kama nyama ya kawaida

Note
Nyama ya konokono ni Tamu Sana na haina mfupa

Kama unaswali jingine niambie
 
Back
Top Bottom