Jinsi ya Kumroga na Kumuongoza Mtu kupitia Kinyago/Mwanasesele

Mgodo visa

JF-Expert Member
Nov 1, 2016
3,550
3,534
Karibuni kwenye Jamvi.
Kama nilivyo eleza katika kichwa cha habari hapo JUU..

Najua na kwa hakika wapo watakao shangaa na kupinga, pia wapo watakao UNGANA nami kwa michango yenye KUELIMISHA na kufunua Bongo za wengine juu ya aina hii ya UCHAWI/UGANGA..

Kabla sijaingia katika MADA husika, ningeomba kidogo nichukue nafasi hii nieleze CHANZO ama ASILI (nguvu) inayo muwezesha Mwanaadamu kuweza kuzikabili CHANGAMOTO za kila siku katika kuendesha /kupitisha uhai wa uwepo wake katika Ulimwengu huu..

Baada ya Mwanaadamu kutua katika SAYARI hii ya Dunia...alijikuta anakabiliwa na changamoto/vikwazo vikubwa vinne (4) katika Uhitaji..
1: Hitaji la MUNGU.
2: Hitaji la viongozi wa dini (Prophecy)
3: HItaji la TABIBU (Mganga)
4: Hitaji la ushirika na mahusiano ya mtu na mtu mwingine..

Kuna msemo wanasema "Katika ulimwengu huu ama Sayari hii ya Binaadamu kuna kila kitu cha kumfaa Kiumbe"...
Ni binaadamu wajuzi wachache walio weza kutumia NADHARIA hii kwa kuifanyia kazi, kiasi ambacho leo hii wametajirika na kujizolea HESHIMA na UMAARUFU katika jamii...

Katika makundi hayo manne...Ningeomba kwa leo nizungumzie hitaji namba 3 -4 (tatu na nne) niweze kuendelea na MADA yangu hapo juu..
The+Doctor+Luke+Fildes+crop.jpg

Mwanaadamu alifikiri sana pale alipo ugua ama kuuguliwa na mpendwa wake..hii ilikuwa ni chanzo cha kuitafuta TIBA..

HITAJI LA TABIBU (MGANGA)
Hapa nisinge penda kuzungumzia matabibu (Dakitari na Manesi) wanao patikana katika Hospitali na vituo vingine vya tiba (dawa zao zinatokana na Mitishamba) japo natambua na kuthamini uwepo wao..
Kinyume chake nitazungumzia matabibu wa tiba ASILI (Sangoma).
Asklepios.3.jpg

Moja ya waanzilishi wa TIBA za Kisasa..

Jamii ya leo sehemu kubwa inakabiliwa na hali mbaya KI- Afya (magonjwa) Umasikini, Usaliti, Ukosefu wa ajira, Kupanda Madaraja (vyeo), Wivu wa maendeleo na Mengine mengi...
voodoo-doll_163.jpg

Mwanasesere akimuwakilisha Bosi na Mkurugenzi wa SHIRIKA/KAMPANI

aid279106-v4-728px-Use-a-Voodoo-Doll-Step-2-Version-2.jpg

Msichana akitekeleza maagizo toka kwa Mganga..jinsi ya Kumdhibiti mpenzi wake kwa kutumia PICHA..

MuslinVoodooDoll-2.jpg

Mahaba niue..Mwanasesere akiakisi picha/umbile la binti atakae dhibiitiwa KIMAPENZI..

Mazingira yamempelekea mwanaadamu kuweka IMANI pembeni na kupiga Magoti kwa SANGOMA kwa lengo la kupata TIBA (Muharobaini) wa matatizo yake..
How-To-Make-A-Voodoo-Doll-For-Revenge.jpg


th5Q9I3CO2.jpg

Sangoma katika nchi za Amerika ya Kusini...anamuwajibisha SEKRITALI mwenye chuki na wageni wa "Mkuu"..

UNAWEZAJE KUMTENGENEZA MTU?
Akiwa ni :-Bosi kazini, Mpenzi wako, Adui yako, Ndugu yako n.k (katika mfumo na muundo) wa Picha..Mwanasesere/mdoli ama Kinyago kwa lengo la mahitaji yako binafsi..
th54GF4YML.jpg

KIvuli ni hazina kubwa katika uchawi..

creepy-doll-08.jpg


Kinyago cha moja ya AMIRI JESHI MKUU (katika Ulinzi)

Ningeomba niishie hapa kwa leo...
Naahidi kuendeleza mada hii J-Mosi kwa ufafanuzi zaidi..

Nakaribisha Mawazo na Maswali..

Made in Jf
Mgodo visa
(C) All right to Jamii Forum
 

Attachments

  • stock-vector-two-businessmen-shaking-hands-admist-the-crowd-of-business-people-193967315.jpg
    stock-vector-two-businessmen-shaking-hands-admist-the-crowd-of-business-people-193967315.jpg
    32.2 KB · Views: 58
too much 'walla walla' hakuna lolote apo other than longolongo tuu!
 
Duuu hiki kinyago cha amiri jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi
kilifaa kwa matumizi ya kuzuia makinikia isitoroshwe
nje ya nchi.

upload_2017-6-8_15-43-21.jpeg
 
Haya mambo yangekuwa ni kweli ningeanza na Jecha kwanza, halafu bashite angefuata, hebu guess nani angefuata baada ya bashite
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom