JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 625
- 938
Angalia kama Tovuti uliyoifungua au kuitembelea ina alama ya kufuli kwenye 'URL' yake. Alama hii hutokea kabla ya 'link' iliyofungua ukurasa huo
Kufuli hili humaanisha kuwa kuna usalama katika mawasiliano yanayofanyika au yatakayofanyika kupitia Tovuti husika
Aina hii ya ulinzi imewekwa kuhakikisha hakuna Mtu anayeza kuingilia tovuti hiyo na kubadili taarifa zinazotumwa kupitia tovuti husika
Tazama mfano pichani
Hakikisha Tovuti uliyotembelea inaanza na HTTPS badala ya HTTP. HTTPS inasimama badala ya maneno Hypertext Transfer Protocol Secure (HTTPS) neno la msingi hapo ni 'Secure' ikimaanisha usalama
Mfano: Kila kiunganishi kutoka katika Tovuti ya JamiiForums lazima itaanza kusomeka hivi: JamiiForums
Aidha, zipo Tovuti nyingi ambazo bado hazijazingatia usalama huu kwani bado zinatumia mfumo wa HTTP hivyo usalama kuwa mdogo zaidi kwa watumiaji wake
Tazama mfano pichani
Lazima Tovuti hiyo itakuwa imeambatanisha Sera ya Faragha (Privacy Policy) kwa ajili ya watembeleaji wake
Sera ya Faragha ni nyaraka inayopatikana kwenye tovuti ikiwaeleza watembeleaji wake ni taarifa zipi zitakusanywa kutoka kwake
Aidha, Sera ya Faragha hueleza jinsi waendeshaji wa tovuti hiyo watakavyo zitumia taarifa hizo
JamiiTalks inakusisitiza kukumbuka kusoma na kuzielewa Sera za Faragha katika Tovuti unazotembelea au kujisajili
Tazama mfano pichani
Kufuli hili humaanisha kuwa kuna usalama katika mawasiliano yanayofanyika au yatakayofanyika kupitia Tovuti husika
Aina hii ya ulinzi imewekwa kuhakikisha hakuna Mtu anayeza kuingilia tovuti hiyo na kubadili taarifa zinazotumwa kupitia tovuti husika
Tazama mfano pichani
Hakikisha Tovuti uliyotembelea inaanza na HTTPS badala ya HTTP. HTTPS inasimama badala ya maneno Hypertext Transfer Protocol Secure (HTTPS) neno la msingi hapo ni 'Secure' ikimaanisha usalama
Mfano: Kila kiunganishi kutoka katika Tovuti ya JamiiForums lazima itaanza kusomeka hivi: JamiiForums
Aidha, zipo Tovuti nyingi ambazo bado hazijazingatia usalama huu kwani bado zinatumia mfumo wa HTTP hivyo usalama kuwa mdogo zaidi kwa watumiaji wake
Tazama mfano pichani
Lazima Tovuti hiyo itakuwa imeambatanisha Sera ya Faragha (Privacy Policy) kwa ajili ya watembeleaji wake
Sera ya Faragha ni nyaraka inayopatikana kwenye tovuti ikiwaeleza watembeleaji wake ni taarifa zipi zitakusanywa kutoka kwake
Aidha, Sera ya Faragha hueleza jinsi waendeshaji wa tovuti hiyo watakavyo zitumia taarifa hizo
JamiiTalks inakusisitiza kukumbuka kusoma na kuzielewa Sera za Faragha katika Tovuti unazotembelea au kujisajili
Tazama mfano pichani