Jinsi ya Kujiunga na CCJ kwa njia ya Simu

Status
Not open for further replies.
Mkuu nashukuru kwa maelezo ya namna ya kujiunga na chama kipya. Mimi ninaomba msaada kwa machache.

1. Chama hiki kipya kinasimamia sera gani?

2. CCJ ina imani na malengo gani?

3. Kwa ambao hawako ndani ya nchi kwa sasa, wafanyeje ili nao waweze kujiunga na CCJ?

Inawezekana baadhi ya maswali yangu hapo juu yameshawahi kujibiwa hapa jamvini siku za nyuma. Ila naomba univumilie na kunipa majibu, kwani sijawahi kuyapata.

Recta.. sasa hivi CCJ ina katiba na uongozi wa muda; Nimeamua kuambatanisha tena Katiba hiyo hapa japo ilishawekwa tayari.. nimeweka kwenye posti ya kwanza. Suala la sera sasa hivi kuna timu ya kimataifa ambayo inaandika sera na pamoja na hivyo platform ya kitaifa ya uchaguzi pamoja na kuangalia muundo wa CCJ.. Kila kitu kikiwa tayari na usajili wa muda ukipatikana kama tunavyotarajia CCJ kitakuwa ni chama pekee nchini ambacho sera, muundo na itikadi yake inaelekea kuharakisha mabadiliko tunayoyataka ili tuweze kurudisha taifa katika misingi yake na mikononi mwa wananchi.
 
CCJ zao la waraka wa kikatoliki kuwa macho wenye kupenda nchi yetu...maaskofu wana makazi yao vatican wakishawasha moto na kuwagawa they quit..

Hili ni angalizo..angalia kwa makini safu yao kwa wenye akili...

Mara CCJ ni mtoto wa CCM...., CCJ ya Usalama wa taifa........., CCJ imetoka ukatolikini........., CCJ Longolongo........, CCJ kimbilio la vigogo wa CCM......., na mengine meeeengi. Jamani kwangu miluzi hii ni mingi mno imesha nipoteza mwelekeo!!!! Nani mkweli kati yao!!!!?

Maada iliyopo ni namna ya kujiunga kwa urahisi na sio vinginevyo. Ni mwaliko tu bandugu!!

Ni mtazamo wangu tu.
 
CCJ fanyeni kweli na sisi tulio nje ya nchi tunataka kujiunga na CCJ. "Saa ya ukombozi ni sasa"
 
Recta.. sasa hivi CCJ ina katiba na uongozi wa muda; Nimeamua kuambatanisha tena Katiba hiyo hapa japo ilishawekwa tayari.. nimeweka kwenye posti ya kwanza. Suala la sera sasa hivi kuna timu ya kimataifa ambayo inaandika sera na pamoja na hivyo platform ya kitaifa ya uchaguzi pamoja na kuangalia muundo wa CCJ.. Kila kitu kikiwa tayari na usajili wa muda ukipatikana kama tunavyotarajia CCJ kitakuwa ni chama pekee nchini ambacho sera, muundo na itikadi yake inaelekea kuharakisha mabadiliko tunayoyataka ili tuweze kurudisha taifa katika misingi yake na mikononi mwa wananchi.
Nashukuru sana Mkuu.

Umenijibu kwa ufasaha/ukamilifu na kwa haraka sana kama ilivyo kawaida yako.

Nitaipitia Katiba ya chama hiki na kuangalia uwezekano wa kujiunga nacho kama nitaridhika na vipengele muhimu vilivyomo ndani ya Katiba hiyo.

Mkuu Mwanakijiji, kwa kuwa umesema kuwa CCJ ina uongozi wa muda, je unaweza pia kunisaidia kukijua zaidi chama hiki na malego yake? Kwa mfano ningependa kufahamu kama;

1. Kina mipango gani ya kuhakikisha kinapata uongozi wa kudumu kwa mujibu wa Katiba yake,

2. Inawezekana kwa chama hiki kupokea mapendekezo, maoni na tamaa nyingine za watanzania ili kuhakikisha kinajibu hamu za wananchi, kwa chama kinachoweza kutawala na kuleta nuru kwa maendeleo yao na Taifa kwa jumla?

Mkuu, niko interested sana na chama hiki kipya kuliko vilivyopo kwa kuwa vilivyopo vinajulikana na vimeshaonyesha uwezo na misimamo yake katika mambo kadhaa muhimu. Kwa kifupi, vyama vingi vilivyopo havionyeshi kujali sana mahitaji muhimu ya wananchi na vinachokitafuta hakijulikani sana.

Ningefurahi kuona tofauti kubwa kati ya vyama vilivyopo na hiki kinachoanza. Kwa upande wangu sijaridhika sana na siasa za vyama vilivyopo.

Naitakia CCJ nguvu, ukuaji, na uzalendo wa kweli. Watanzania wanahitaji kupata watu na taasisi zinaoweza kuwajali katika kuongoza maisha yao. Walau kwa kuwaelekeza njia za kujikwamua na matatizo yao ya msingi.
 
Mwanakijiji/JF members,

Apology kama swali langu ni la kipuuzi, ila mimi binafsi ninajiuliza je hii kujiandikisha kwa simu haitafanya mtu mmoja kuweza kujiandikisha mara nyingi with different names and locations? je uhakiki wa kujiunga kwa njia hii bila kuwa na proper identification inadhibitiwa vipi? je idadi ya wanachama itakuwa ni ya kweli?
 
Mwanakijiji/JF members,

Apology kama swali langu ni la kipuuzi, ila mimi binafsi ninajiuliza je hii kujiandikisha kwa simu haitafanya mtu mmoja kuweza kujiandikisha mara nyingi with different names and locations? je uhakiki wa kujiunga kwa njia hii bila kuwa na proper identification inadhibitiwa vipi? je idadi ya wanachama itakuwa ni ya kweli?

kila akifanya hivyo anakatwa shilingi 500 so.. tunaweza hata kumuencourage kufanya hivyo..!!! Unalosema linaweza kusemwa hata kwa kadi za kawaida tu.. unafikiria vyama vilivyopo sasa CCM kimojawapo wameunganisha databases zao? Unakumbuka suala la uanachama wa Mengi kwenye CCM ndani ya mji mmoja ambapo kiongozi mmoja wa mkoa akisema Mengi siyo mwanachama wao, na kiongozi wa tawi akiibuka na kusema ndiyo!? Kama kungekuwa hakuna kiingilio basi ingekuwa ni rahisi sana kwa watu kujiandikisha kwa majina mengi.. ili kuinflate namba; lakini kwa vile kuna na malipo unless hao watu wana fedha za kuchezea haiingii akilini kama kuna watu watakuwa na muda wa kujitolea fedha zao kwa namna hiyo.
 
Wakati umefika kwa wananchi kuelewa maana ya mageuzi na upinzani wa kweli, mimi binafsi nina imani kubwa sana na CCJ kuwa italeta mabadiliko makubwa sana katika vyama vya upinzani nchini ikiwapo na kuleta upinzani wa kweli kwa CCM, kwani zama za wizi wa CCM kwa wananchi wa Taifa hili umefikia kikomo.

Tumechoshwa sana na CCM, kwani wametunyonya vya kutosha, wameiba mali na rasilimali zetu kwa kipindi kirefu sana, wamejineemisha vya kutosha, wengi wao na mabepari wakubwa sana, wakimiliki kila chazo cha uchumi ndani ya nchi yetu kwa kutumia Kodi zetu, hakuna maaendeleo yeyeto yaliyopatikana kwa kipindi chote.

Mwananchi yheyote anayetagaza leo hii kugombe uongozi kwa tiketi ya CCM ni lazima achunguzwe kwa umakini? kwani kama ana nia ya kuogembea na kuleta mabadiliko why CCM? kwa kuzingatia kuwa CCM haiwezi kubadilika hata kidogo, lazima mtu huyu atakuwa na agenda ya siri moyoni mwake.

Kwa kweli mimi binafsi nawashukuru watu wote wenye malengo ya kuleta mabadiliko nchini mwetu, ila hakika huwezi leta mabadiliko ndani ya nchi hii kwa kuwa CCM, lazima utoke na kuwa nje ya chama kwa ajili ya kupambana na mtandao mkubwa wa Mafisadi ndani ya CCM

Imefika wakati watanzania tukaamua kwa kauli moja kuwa sasa CCM basi, lazima CCM waondoke, tumechoka na tumechoshwa na matendo yao.
 
Pole Recta.. nitakujibu kama ifuatavyo:

Mkuu Mwanakijiji, kwa kuwa umesema kuwa CCJ ina uongozi wa muda, je unaweza pia kunisaidia kukijua zaidi chama hiki na malego yake? Kwa mfano ningependa kufahamu kama;

1. Kina mipango gani ya kuhakikisha kinapata uongozi wa kudumu kwa mujibu wa Katiba yake,

Uongozi wa kudumu unakuja baada ya kupata usajili wa kudumu. Baada ya kupata usajili wa kudumu basi utafanyika mkutano mkuu wa wanachama ili kuunda uongozi wa kitaifa (yaani kujaza nafasi mbalimbali za jao, za idara, na za vitengo) na vile vile kuweka utaratibu wa kujaza nafasi za uongozi katika matawi.. kupitia rasimu ya katiba mpya n.k n.k Ni kutoka hapo ndipo CCJ itaanza kazi zake kama Chama cha siasa kuelekea uchaguzi mkuu
2. Inawezekana kwa chama hiki kupokea mapendekezo, maoni na tamaa nyingine za watanzania ili kuhakikisha kinajibu hamu za wananchi, kwa chama kinachoweza kutawala na kuleta nuru kwa maendeleo yao na Taifa kwa jumla?

absolutely!! kwa wakati huu focus nzima iko kwenye kupata wanachama wa kutosha, kwenda kuomba usajili wa kudumu, na kusajiliwa. Baada ya hapo milango yote itafunguliwa. Niamini kuwa hakuna chama kitakachofanana kimiundo, malengo na kiutendaji na CCJ. Ukiondoa kufanana kwa jina tu kidogo CCJ kitakuwa ni chama tofauti kabisa vya kisiasa nchini.

Mkuu, niko interested sana na chama hiki kipya kuliko vilivyopo kwa kuwa vilivyopo vinajulikana na vimeshaonyesha uwezo na misimamo yake katika mambo kadhaa muhimu. Kwa kifupi, vyama vingi vilivyopo havionyeshi kujali sana mahitaji muhimu ya wananchi na vinachokitafuta hakijulikani sana.

Umehukumu vyema.. ndio maana CCJ imezaliwa saa na wakati kama huu; kuziba pengo ambalo wengi tumeliona kwa muda mrefu na licha ya kujitahidi kuliziba ndio limezida kupanuka.

Ningefurahi kuona tofauti kubwa kati ya vyama vilivyopo na hiki kinachoanza. Kwa upande wangu sijaridhika sana na siasa za vyama vilivyopo.

Unaungana na karibu Watanzania elfu 10 ambao wanahisia kama hizo
 
Mwanakijiji,

Shukurani sana kwa kusaidia kusambaza huu ujumbe, wasi wasi wangu ni kutmuia wataalamu wa kimataifa, unamaanisha watz wenye uzoefu wa kimataifa? I wish kama watagrow na hizi propaganda zinazoenea. Natumaini kuwa wataalamu watajikita katika hilo nami nitajitahidi kutetea.

Napendelea mabadiliko, napenda kuona CCJ inakuwa na kuwa maarufu na chama dhabiti kushinda hata chama changu CHADEMA. Tathmini yangu ni kuwa mind za watu ndo zimetupelekea hapa tulipo na sidhani kama ni taasisi na mfumo wake. CCJ ni taasisi na watu ni wale wale na ni watanzania. Namna ya kupata wanachama na kutekeleza demokrasia hapa tz ni shaka mojawapo ndani ya matarajio. Kama ni vigumu sana majority kuelewa vision na mission ya Selous but kama wale vinara wananielewa au kinara mmoja ananipinga tayari ni mgogoro na kupoteza imani kwa wahusika.

Kama tukiweza kubadili mindset za watu, tukajenga kuaminiana i believe we can step far ahead.
 
kila akifanya hivyo anakatwa shilingi 500 so.. tunaweza hata kumuencourage kufanya hivyo..!!! Unalosema linaweza kusemwa hata kwa kadi za kawaida tu.. unafikiria vyama vilivyopo sasa CCM kimojawapo wameunganisha databases zao? Unakumbuka suala la uanachama wa Mengi kwenye CCM ndani ya mji mmoja ambapo kiongozi mmoja wa mkoa akisema Mengi siyo mwanachama wao, na kiongozi wa tawi akiibuka na kusema ndiyo!? Kama kungekuwa hakuna kiingilio basi ingekuwa ni rahisi sana kwa watu kujiandikisha kwa majina mengi.. ili kuinflate namba; lakini kwa vile kuna na malipo unless hao watu wana fedha za kuchezea haiingii akilini kama kuna watu watakuwa na muda wa kujitolea fedha zao kwa namna hiyo.

MKK,

Kwani CCJ wameshapata uwanachama wa kudumu?

Kama bado, je moja na conditions ambazo wanaitaji kutekeleza kupata uwanachama wa kudumu ni kupata idadi Fulani ya wanachama kwenye mikoa tofauti?

Na kama that the case, Je hawawezi kutumia hela na mali walizonanzo kuandikisha idadi kubwa ya watu kwa njia ya simu ili wapate huo usajili wa kudumu?
 
Jee ni watanzania wangapi kule nkasi, tandahimba, sirari na loliondo wana habari ya kujiunga na ccj kwa sms?jee kule kwetu wotta kibakwe wana habari ya ccj?twendeni vijijini jamani...
 
Nia na malengo ni mazuri, tuombe mungu tuvuke kwenye usajili. Ukisoma imani ya chama inakupa mwelekeo wa kutatua matatizo sugu yanayotunakabili.
 
Inawezekana unasubiri uone vigogo watoke CCM ndio na wewe ufanye uamuzi na inawezekana unasubiri wengine waanze kuleta mabadiliko ili na wewe udandie mbele ya safari; lakini wengine wangependa kuwa sehemu ya mabadiliko wanayoyataka.. hivyo..

Ni namna rahisi yakujiunga na CCJ kwa haraka na kwa wepesi... Kwa kutumia simu yako:


Ingia kwenye "Message"

Andika neno "Sajili" weka nyota (*)
Andika Jina lako kamili kisha weka (*)
Andika Mkoa unaotoka kisha weka (*)
Andika mtaa unaotoka kisha weka (*)

Halafu tuma kwenda namba
15337

Mara moja utapata namba yako ya kadi, na maelekezo jinsi ya kupata kadi yako..

Ushauri wangu ni kuwa baada ya kupata usajili wa kudumu first move iwe kuwafikia wananchi kwa gharama yeyote. Some people are ready to make it happen. Tunaweza ona tafauti. Kimsingi ni kupunguza imani ya wananchi kwa CCM, ili changamoto zifanyiwe kazi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom