Jinsi ya kuishi na Mwanaume/Mwanamke mwenye hasira

Frumence M Kyauke

JF-Expert Member
Aug 30, 2021
630
1,245
Nani hajawahi kupata hasira kwa mwenza wake? hakuna mtu, Si ndio? ni katika sehemu yoyote ya mahusiano, lakini tumekuwa tukiamini kwamba Hasira ni mbaya, na kwa sababu hio hatutakiwi kuwa na hasira.

Kwa hio hatujui jinsi ya kuishi na mke au mume mwenye Hasira. ni kweli , ni moja ya njia nzuri ukiwa ni mwenye hasira kwa mwenza wako. kitu gani zaidi kinatokea? Hasira yako inaweza kuwa ni kitu kizuri kwenye mahusiano yako. inaweza kuonekana kama kuchanganya hivi, lakini kuwa mke au mume mwenye hasira inaweza kuwa isiwe kitu kibaya.

Kwa nini, ngoja tuendelee kusoma hapa.

Hasira ni Kawaida.
Hasira huja kutokana na kitendo kilichotokea wakati huo, lakini mara nyingi sana, Tunakosa nafasi ya kuelezea hisia zetu za hasira zinapokuja. Na yote hio hutokea kwa sababu ya kuogopa au kuona aibu kuwa na hasira.kwa hio , kwa akili tulizonazo,Tunaficha hasira. Na tusiposhughulikia hilo , hasira inatushughulikia!

Kwa mfano ,Hasira ndogo inaweza kugeuka ikawa hasira kubwa- kitu ambacho ni hatari na kinaharibu mahusiano yeyote,iache ikutane na urafiki, zaidi ya yote , hasira isiotarajiwa inaweza kuleta mambo kama huzuni, matatizo ya moyo, nimetaja tu kidogo. Lakini kama tusipoelezea hasira kila inapowezekana , tunakuwa kwenye hatari zadi ya kupata matatizo ya maumivu ya kichwa, shinikizo la damu, matatizo ya utumbo na zaidi.

Nafikiri ni lazima nisema kwamba tunapobaki na hasira , tunalimbikiza matatizo mapya kila siku. lakini hasira huenda inatokea wakati ambao kuna kitu kinatakiwa kubadilika. ni kama dalili ya kawaida, ishara kwetu ya kutengeneza kitu kipya au kuweka sawa jambo fulani.

Hasira Sio Kitu Kibaya.
Kwa hio kama tunavyoona Hasira sio kitu cha kawaida, pia ni kitu kizuri ambacho unaweza kushangaa jinsi inavyoleta dalili au ishara ya jambo fulani muhimu kwako.

Jaribu hiki. Wakati mwingine ukisikia hasira kuhusu kitu fulani , pata muda wa kutulia kidogo , halafu jiulize kwa nini kinakupa hasira hicho kitu.Utagundua kuwa hasira yangu inapigania kitu fulani – labda huenda unajisikia kuumia, huna usalama, mpweke, umeogopeshwa au hatia. jichunguze ndani zaidi, na jiulize kwa nini unajisikia hivyo.

Fahamu moyoni mwako na ujiambie kuwa , hasira huna muda ndani yangu, na uielewe sawasawa kwa sababu kutunza hasira ni mbaya kwako na kwenye mahusiano yako.

Na kama ukifahamu hasira yako ina ishara za tatizo kubwa, utaweza kuanza kuponya hio misingi ya tatizo. ujiruhusu kukasirika lakini bila ya kujilaumu au kujijaji mwenyewe. na hii itakuweka vizuri kwa vile umeonyesha hasira yako kwa mwenza wako.

Kuwa na utulivu ni dalili za kutubadilisha tabia zetu badala ya kulaumu watu kutobadilisha tabia zao. ni chaguo lako la kubeba hasira au kujielezea ili kuondokana na hilo tatizo.

Hasira Hujenga.
Nina uhakika kuwa vyovyote vile mke au mume au rafiki mwenye hasira huwezi kufikiri kuwa hasira itakupa afya na kuwa mtu wa kuleta mazuri , lakini kuna maajabu hutokea unapotumia hio hasira kwa utulivu .

Hii sio nguvu mbaya , ni nguvu ya kujenga. tunatakiwa tu kuchagua kutumia kwa njia nzuri, na tunapofanya hivyo, tutakuja na mawazo mazuri ya kukabiliana na tatizo.

Kwa hio angalia hasira yako kwa ndani zaidi. mfano kama mwenza wako anapenda kutupa nguo kila sehemu, na wewe hilo linakuudhi , ni vizuri kukaa na kumweleza kuwa anaweza kufanya kitu unachotaka afanye. Kuna wengine wengine sijui wakoje wakienda chooni hawaflash. na kila siku mke akienda kusafisha anakuta uchafu . na kitendo hicho kinampa hasira . hivi vitu ni vya kurekebishana kama ukikaa kwa utulivu na kufikiria jinsi ya kuongea nae.

Unaweza kufikiria huo mfano ni rahisi , lakini kitu kikubwa ni kwamba tunahitaji kujifunza jinsi ya kupata solution ndogo ndogo kwanza, hio ndio njia ya kuweza kushughulikia tatizo kubwa la hasira. na utakuwa na nguvu ya kulithibiti tatizo la hasira.

Jinsi Ya Kuwa Mke Au Mume Mwenye Hasira.
Kabla ya kuonyesha hasira, ni muhimu kwanza kuondoa woga, woga wa kukataliwa na kutokueleweka, na ukumbuke woga ni halali na upo kwa sababu.. Lakini kuwa tayari kuonyesha hasira ya upande mwingine ni iwe dalili nzuri ya uaminifu. unaamini kwamba mahusiano yenu yanasimamia ukweli na uaminifu.

Kwanza kabisa unaweza kujitenga na hasira yako kwa kusema hivi vitu, Najisikia hasira kuhusu hiki kitu na hapo lazima useme kwa nini.” Kitu kingine unaweza kuandaa kuwajibika kwa hisia zako na kuingia kwa nia ya kuleta badiliko zuri.. na mwisho ni kuongea na mwenza wako kwa lugha nzuri ya kueleweka, inayowezekana, itakusaidia usijilaumu wala kulaumiwa na mtakuwa na maongezi mazuri.

Kubadili mpangilio wa akili yako kuhusu hasira na kutumia kwa faida yako, utaleta Amani ya kutosha,mawasiliano mazuri na kuongeza urafiki wa kimapenzi nyumbani kwako.

Nitajitahidi mazoezi haya kila mara na kujitahidi kutafakari kila siku ili ninaposikia hasira niitulize na kuwa na maamuzi mazuri kwenye mahusiano yangu.

images (6).jpeg
 
Pamoja na hayo yote ukiwa na pesa ya kutosha hakuna cha hasira kwa mwanamke au mwanaume. Mwanamke anakuwa na hasira pale ambapo mwanaume huna pesa ya kumtunza yeye na familia.

Kadhalika, mwanaume asiye na pesa huwa na hasira, makasiriko ya ajabu ajabu. Tutafute pesa nyingi kuondoa hasira, viburi, dharau na makasiriko kwa wake zetu wakuu.
 
Pamoja na hayo yote ukiwa na pesa ya kutosha hakuna cha hasira kwa mwanamke au mwanaume. Mwanamke anakuwa na hasira pale ambapo mwanaume huna pesa ya kumtunza yeye na familia.

Kadhalika, mwanaume asiye na pesa huwa na hasira, makasiriko ya ajabu ajabu.

Tutafute pesa nyingi kuondoa hasira, viburi, dharau na makasiriko kwa wake zetu wakuu.
Pesa haiondoi hasira. Wala haimaliz hilo tatizo. Ni tatizo la kisaikologia ambapo mtu anashindwa kudhibit hisia za gafla ambazo ni negative.
Mostly hawa watu wanashindwa ku explain kilichomo wanaishia kuchukia mtu.. but deep down wanataman waeleweke.
 
Pamoja na hayo yote ukiwa na pesa ya kutosha hakuna cha hasira kwa mwanamke au mwanaume. Mwanamke anakuwa na hasira pale ambapo mwanaume huna pesa ya kumtunza yeye na familia.

Kadhalika, mwanaume asiye na pesa huwa na hasira, makasiriko ya ajabu ajabu.

Tutafute pesa nyingi kuondoa hasira, viburi, dharau na makasiriko kwa wake zetu wakuu.
Uko sahihi.
 
Pesa haiondoi hasira. Wala haimaliz hilo tatizo. Ni tatizo la kisaikologia ambapo mtu anashindwa kudhibit hisia za gafla ambazo ni negative.
Mostly hawa watu wanashindwa ku explain kilichomo wanaishia kuchukia mtu.. but deep down wanataman waeleweke.
Siyo kweli mkuu. Mara nyingi ukosefu wa pesa ndiyo husababisha matatizo ya kisaikolojia kama msongo wa mawazo n.k.

Ukiwa financially stable na unazingatia mfumo mzuri wa maisha huwezi ukawa na matatizo ya kisaikolojia hata siku moja.

Kumbuka ili uwe na mfumo mzuri wa maisha ni lazima uwe financially stable. I mean you can afford what you want at any cost and at any time. You can eat whatever you wish to eat, you can go wherever you want to go.
 
Siyo kweli mkuu. Mara nyingi ukosefu wa pesa ndiyo husababisha matatizo ya kisaikolojia kama msongo wa mawazo n.k.

Ukiwa financially stable na unazingatia mfumo mzuri wa maisha huwezi ukawa na matatizo ya kisaikolojia hata siku moja.

Kumbuka ili uwe na mfumo mzuri wa maisha ni lazima uwe financially stable. I mean you can afford what you want at any cost and at any time. You can eat whatever you wish to eat, you can go wherever you want to go.
"Mara nyingi pesa husababisha matatizo ya kisaikolojia"
Nani kasema? Thats is a big NO.

Matajiri , viongoz wakubwa wa serikal hawana msongo wa mawazo?

Kuwa financialy stable kuta minimize baadhi ya vitu lakin haimaanishi matatizo yataacha kuja. Yataibuka mapya day in day out. Tofauti ni jinsi gani una deal nayo
 
Pamoja na hayo yote ukiwa na pesa ya kutosha hakuna cha hasira kwa mwanamke au mwanaume. Mwanamke anakuwa na hasira pale ambapo mwanaume huna pesa ya kumtunza yeye na familia.

Kadhalika, mwanaume asiye na pesa huwa na hasira, makasiriko ya ajabu ajabu. Tutafute pesa nyingi kuondoa hasira, viburi, dharau na makasiriko kwa wake zetu wakuu.
Ukweli mtupu..
 
Back
Top Bottom