Jinsi ya kuiibia Serikali bila kukamatwa!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Nimekaa najiuliza ni jinsi gani watumishi wa serikali kuanzia wa ngazi za chini hadi za juu kabisa wanaweza kuibia serikali na serikali isitambue au ishindwe kuchukua hatua? Inawezekana vipi watu wakawa wanachota fedha za umma kama kuchota maji kwa kata na wakazimeza hata bila ya kuzitafuna? Bila ya shaka kuna mbinu mbalimbali ambazo zinatumika na wajanja hao kula fedha za umma "bila kunawa". Hivi ni mbinu gani zinatumika kuuibia serikali bila ya hata kukamatwa?

NB: Mada hii haina lengo la kufundisha wizi au mbinu za kuuibia serikali bali inataka kuonesha ni mbinu gani zinatumika kuubia serikali. Kama unataka kujua jinsi ya kula fedha za umma, tafadhali jiunge na utumishi wa serikali kwani wapo watu ambao watakuwa tayari kukupa somo "live" as you go along.
 
kupanga safari za nje zisizo na kichwa wala miguu. Mtu moja anakwenda nje mara 10 kwa mwaka na kila safari analipwa usd 15,000 ukizidisha na watu kama 200 walio katika huo mradi unapata kiasi kama cha usd 3,000,000. hao ni wafanyakazi wa chini ambao wanazibwa midomo kwa kupewa hivyo viofa.
 
kupanga safari za nje zisizo na kichwa wala miguu. Mtu moja anakwenda nje mara 10 kwa mwaka na kila safari analipwa usd 15,000 ukizidisha na watu kama 200 walio katika huo mradi unapata kiasi kama cha usd 3,000,000. hao ni wafanyakazi wa chini ambao wanazibwa midomo kwa kupewa hivyo viofa.

..baaab kubwa!

..15,000$ kila safari inatosha kabisa kuondoa umasikini!

..i doubt this!
 
Hizo safari ni za lazima au ni safari hewa.. maana kuna safari za mtu anakwenda halafu kuna safari za mtu anabakia nyumbani kufanya shughuli zake lakini akimaliza anaonesha tiketi ya kwenda Magu, risiti ya hoteli n.k halafu analipwa...
 
Nimekaa najiuliza ni jinsi gani watumishi wa serikali kuanzia wa ngazi za chini hadi za juu kabisa wanaweza kuibia serikali na serikali isitambue au ishindwe kuchukua hatua? Inawezekana vipi watu wakawa wanachota fedha za umma kama kuchota maji kwa kata na wakazimeza hata bila ya kuzitafuna? Bila ya shaka kuna mbinu mbalimbali ambazo zinatumika na wajanja hao kula fedha za umma "bila kunawa". Hivi ni mbinu gani zinatumika kuuibia serikali bila ya hata kukamatwa?
.

...Kwenye hundi ya malipo unaongeza/kupunguza 0 au 00 mfano hundi ya malipo ya shs 1,000,000/= unaongeza 0 inakuwa 10,000,000/= milioni tisa, yes 9,000,000/= 'zako na wenzako'!

...Unarekodi makontena 10 wakati idadi halisi yaliyoingia ni 100, hapo umepunguza sifuri moja, cha juu au 'idadi' ya makontena (90) tisini yaliyosalia 'mnakula na wenzako'.

...anapewa Sheraton 5yrs tax holiday, miaka mitano mingine anapewa Royal Palm 'tunu hiyo', miaka kumi na tano baadae Movenpick nao wanafaidi 'tunu hiyo hiyo', ...bure tu? hapana, kuna commission fulani inakwenda kwa mfuko,

Usanii wa kubadili majina/makampuni ya 'wawekezaji' ni katika 'kula na kipofu bila kumshika mkono!'. i.e Richmonds to Dowans et al...

...kwa wale wataoshangaa hii ndio bongo bwana, mwendo mdundo!
 
mchongoma.. hapo umeniacha hoi.. na hasa hiyo signature yako.. sasa ukaguzi unapofanyika huwa haugundui hayo au inakuwaje ripoti ya mkaguzi mkuu inapokuja na maneno kama "fedha zisizooneshwa zimetumika vipi"... how is that possible...?
 
Nimekaa najiuliza ni jinsi gani watumishi wa serikali kuanzia wa ngazi za chini hadi za juu kabisa wanaweza kuibia serikali na serikali isitambue au ishindwe kuchukua hatua? Inawezekana vipi watu wakawa wanachota fedha za umma kama kuchota maji kwa kata na wakazimeza hata bila ya kuzitafuna? Bila ya shaka kuna mbinu mbalimbali ambazo zinatumika na wajanja hao kula fedha za umma "bila kunawa". Hivi ni mbinu gani zinatumika kuuibia serikali bila ya hata kukamatwa?

NB: Mada hii haina lengo la kufundisha wizi au mbinu za kuuibia serikali bali inataka kuonesha ni mbinu gani zinatumika kuubia serikali. Kama unataka kujua jinsi ya kula fedha za umma, tafadhali jiunge na utumishi wa serikali kwani wapo watu ambao watakuwa tayari kukupa somo "live" as you go along.


...kufundisha wizi kwa wale ambao ndo wameanza inaweza ikawa unintended consenquence...
 
...Kwenye hundi ya malipo unaongeza/kupunguza 0 au 00 mfano hundi ya malipo ya shs 1,000,000/= unaongeza 0 inakuwa 10,000,000/= milioni tisa, yes 9,000,000/= 'zako na wenzako'!

..mkuu,ina maana hizo hundi haziandikwi kwa maneno?ni namba pekee?

..ninavyofahamu deal liko kwenye tender za kupeana!a lot of over invoicing!
 
...sasa ukaguzi unapofanyika huwa haugundui hayo au inakuwaje ripoti ya mkaguzi mkuu inapokuja na maneno kama "fedha zisizooneshwa zimetumika vipi"... how is that possible...?

...ohooo, nawewe unachimba sana sasa, ushaambiwa ukitaka kula na kipofu usimshike mkono,... siri ya urembo ni kunawa haraka haraka na kujifuta mdomo! ...wakaguzi wakija wanakuta Ripoti safiii... kwa jinsi gani basi? nitakudokezea;

...kunakuwa na Bill of landing mbili, Original ndio mfanyabiashara anakwenda nayo TRA long room kulipia makontena yake (10) kumi aliyoyaingiza. Wakati huo huo akienda kuyakomboa bandarini anakwenda na 'iliyopikwa' yenye kuonyesha amekwisha lipia makontena yote mia moja, (yes, 100)!...

...'Mkaguzi' akija anakuta mahesabu saaafi, makontena kumi yamelipiwa ushuru wa (approx) $1000 kila moja, na 'taifa limeingiza' $10,000 saaaaaafi, kumbe kuna wajanja wachache weshakula 10% ya makontena 90 yaliyobakia (approx $ 9,000), mfanyabiashara anapeta kwa faida ya kutolipia $81,000!... na kama mkaguzi atakuja mdomo juu naye atazimwa kwa 'kibahasha' cha kulipia school fees ya mwanawe mwaka mzima! si unajua st Mary's Academy (pale mbagala) siku hizi Annual school fees per kid inadunda milioni kamili!.

...Siku akitokea bosi mbabe 'mwenye meno' TAKURU ambaye ataamuru watumishi wa serikali/umma wataje walivyopata haya ma RANGE ROVER VOGUE, LEXUS, BMW X5, na MERCEDES M CLASS pamoja na majumba yao kama mahekalu yenye marumaru na Viyoyozi , ndio siku hiyo ndipo utapoona vitambi vinabana, na watu wanavyopuputika na BP!
 
..mkuu,ina maana hizo hundi haziandikwi kwa maneno?ni namba pekee?

..ninavyofahamu deal liko kwenye tender za kupeana!a lot of over invoicing!

...ndugu yangu weee... hebu soma hili;

Hoja ni kuchunguza wanaosambaza ama wanachosambaza?

2007-07-06 09:13:29
Na Mhariri

Katika Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma, madai ya kuwepo ubadhirifu mkubwa katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yamezua mjadala mkubwa na mvutano baina ya serikali kwa upande mmoja na kambi ya upinzani kwa upande mwingine.

Inadaiwa kuwa katika ujenzi wa majengo hayo, kiasi cha Dola za Marekani milioni 30.8, sawa na sh. bilioni 40 kimefujwa kupitia akaunti ya madeni ya biashara ya nje.

Inadaiwa kuwa gharama za ujenzi huo, kiasi cha Dola za Marekani 8,000 kwa kila mita ya mraba inayojengwa ni cha juu kuliko hata kama yangejengwa katika jiji la London, Uingereza ama New York, Marekani.

Pia inadaiwa kwamba benki hiyo imeendesha miradi kadhaa mibovu kwa udhamini wa Gavana wake, Bw. Daudi Balali.

Kwa mujibu wa tuhuma hizo, wapo wafanyabiashara na wanasiasa, wakiwemo wabunge, ambao wamefaidika na ubadhirifu huo.

Serikali kwa upande wake imesema kwamba tuhuma hizo zitachunguzwa na wakaguzi wa nje kwa usimamizi wa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), lakini upinzani kwa upande mwingine hauridhiki na msimamo huo.

http://www.ippmedia.com/ipp/nipashe/2007/07/06/93923.html

...nani atayemfunga paka kengele? hii nchi inaliwa mbele, nyuma shoto na kulia, nidhamu hakuna kabisa,

...RUSHWA tangia ilikuwa inanuka mpaka sasa imeanza KUNUKIA watu 'wanajifukizia'!!!
 
sasa haya mambo ya over invoicing yanakwendaje.. kwenye mfano wako huo mchongoma si lazima mkubwa fulani naye awemo ndani ya dili... au watu wa chini mnaweza "kugawiana tenda" bila mkubwa kujua?
 
FinancialTimes interview; Eti Mheshimiwa Rais anasema hajui kwanini Africa ni masikini pamoja na rasilimali zote ilizo nazo....

..... HATA mchongoma ANAJUA KWANINI AFRICA NI MASIKINI!!


SteveD.
 
...si lazima mkubwa fulani naye awemo ndani ya dili... au watu wa chini mnaweza "kugawiana tenda" bila mkubwa kujua?

...mwanakiajiji maskendeli yanayotokea chini, (naamini) yanakuja kwa baraka za wakubwa huko juu,... (isipokua JMK tu, yeye ndio 'wenzake' hawampi chochote maskini).

...ngoja nikale daku mie, usiku mwema.
 
HATA mchongoma ANAJUA KWANINI AFRICA NI MASIKINI!!

SteveD.

...Mkuu Steve D, heshima mbele. Una maana article hii?;

RAIS Jakaya Kikwete amesema haelewi ni kwa nini Tanzania bado ni fukara ingawa imejaliwa rasilimali nyingi za asili kuliko nchi nyingi za bara la Afrika.

Rais Kikwete aliyasema hayo Oktoba 4, mwaka huu mjini Paris Ufaransa katika mahojiano na Mhariri wa masuala ya Afrika wa gazeti la Financial Times, William Wallis na Mwandishi wa gazeti hilo,Tom Burgis.


"...Kiwi cha yule ni chema cha;hata ulimwengu uwishe kwani Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua!"

ALAMSIKI!
 
Nasikia kuna katabia ka viongozi wetu kwenda kwenye mikutano ambayo hailingani na vyeo vyao, na pia baadhi ya mabalozi wetu huko nje,

mkutano ni wa maofisa wa chini, lakini waziri mzima analilia kwenda tu, anachukua posho, halafu akifika kule hawezi kuingia kwenye mkutano kwa sababu ni maofisa wa ngazi za chini, mkuu anabaki huko majuu maana alishachukua posho tayari ya mkutano wa mwezi mzima, anapiga mitaa huko majuu na shopping baadaye anarudi bongo na kuzungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya mkutano huo, ambao hakuhudhuria,

nasikia pia kuna baadhi ya mabalozi wetu huko nje nao wana hiyo tabia ya kulazimisha safari hata zisizowahusu, ili mradi tu wapate posho na kusafiri, mwisho kulitia taifa letu hasara na in fact huu ni wizi wa mchana kweupe!
 
Mkuu FMES, hilo unalolisema kiongozi mmoja aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje inadaiwa ilikuwa na katabia hako sana... ile yeye badala ya kwenda shopping alikuwa "anajipongeza" hotelini....
 
...Mkuu Steve D, heshima mbele. Una maana article hii?;




"...Kiwi cha yule ni chema cha;hata ulimwengu uwishe kwani Kivuli cha fimbo hakimfichi mtu jua!"

ALAMSIKI!

Haswaa, nilimaanisha hiyo article. Africa ilikuwa jumuisho tu lakini the word is Tanzania to be precise.

Hata hivyo naomba unitafsirie maneno yako ya chini, lugha yangu hii sitobisha, saa nyingine inanichenga vibaya sana, na mambo huwa noma kweli kweli kama mafumbo yananijia kutoka kwa wataalam wa lugha kama wewe. Naomba nitangulize shukrani.

SteveD.
 
Hizi zinanikumbusha mwanasheria mmoja wa taasisi ya Fedha, alikuwa anaongea na wafanyakazi wa chini wanafile claims zisizo na kichwa wala miguu, kesi ikienda mahakamani anafanya madudu huyo mfanyakazi anashinda milion kadhaa ambazo hata angestaafu kihalali asingeweza kuzipata, kesi ikiisha anamkatia(mwanasheria) asilimia yake mwendo mdundo.
 
Wakuu wanalipana posho wakiwepo Dodoma kwa kisingizio ni nje ya eneo lao kazi. Wakirudi Dar wanalipana posho tena kwa kisingizio kwamba ofisi zao za kazi ziko Makao makuu Dodoma. Posho mwaka mzima. Kulaleki
 
Back
Top Bottom