Jinsi ya kuiibia Serikali bila kukamatwa!

Pumbafu kabisa wewe ,unadhani sisi biashara hatufanyi???? Wewe ni mmoja ya majizi kwa mfumo huuu
Maneno yako tu yanakutambulisha wewe ni mtu wa namna gani.

Hapa tunaongelea biashara na siyo uchuuzi ambao kuna uwezekano mkubwa, ndiyo unaoufanya.
 
...Kwenye hundi ya malipo unaongeza/kupunguza 0 au 00 mfano hundi ya malipo ya shs 1,000,000/= unaongeza 0 inakuwa 10,000,000/= milioni tisa, yes 9,000,000/= 'zako na wenzako'!

...Unarekodi makontena 10 wakati idadi halisi yaliyoingia ni 100, hapo umepunguza sifuri moja, cha juu au 'idadi' ya makontena (90) tisini yaliyosalia 'mnakula na wenzako'.

...anapewa Sheraton 5yrs tax holiday, miaka mitano mingine anapewa Royal Palm 'tunu hiyo', miaka kumi na tano baadae Movenpick nao wanafaidi 'tunu hiyo hiyo', ...bure tu? hapana, kuna commission fulani inakwenda kwa mfuko,

Usanii wa kubadili majina/makampuni ya 'wawekezaji' ni katika 'kula na kipofu bila kumshika mkono!'. i.e Richmonds to Dowans et al...

...kwa wale wataoshangaa hii ndio bongo bwana, mwendo mdundo!
Duhhh!!!
 
Njia bora zaidi ni kushirikisha wenzako hasa wale wanaoweza kuinfluence mambo ya kijinga ya kukamatana.

Sio uwashirikishe kwa kuwaita muibe, uwashirikishe baada au wakati unaendelea kuiba.
 
Nasikia kuna katabia ka viongozi wetu kwenda kwenye mikutano ambayo hailingani na vyeo vyao, na pia baadhi ya mabalozi wetu huko nje,

mkutano ni wa maofisa wa chini, lakini waziri mzima analilia kwenda tu, anachukua posho, halafu akifika kule hawezi kuingia kwenye mkutano kwa sababu ni maofisa wa ngazi za chini, mkuu anabaki huko majuu maana alishachukua posho tayari ya mkutano wa mwezi mzima, anapiga mitaa huko majuu na shopping baadaye anarudi bongo na kuzungumza na waandishi wa habari juu ya mafanikio ya mkutano huo, ambao hakuhudhuria,

nasikia pia kuna baadhi ya mabalozi wetu huko nje nao wana hiyo tabia ya kulazimisha safari hata zisizowahusu, ili mradi tu wapate posho na kusafiri, mwisho kulitia taifa letu hasara na in fact huu ni wizi wa mchana kweupe!
Nimecheka hapo unaposema "anaporudi anaitisha mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia mafanikio ya mkutano huo ambao hakuhudhuria.
 
Hiyo ya kubadili jina au umiliki wa mradi ni uwongo. Huwezi kupata fedha kwa kubadili jina la mradi au umiliki wa mradi. Maneno hayo yanazungumzwa na mbumbumbu wa biashara.

Msamaha wa kodi hutolewa kwa mradi na siyo kwenye jina la mradi. Kama mradi ni ule ule hata ungebadili majina mara 1000 haitabadili nafuu ya kodi au muda wa msamaha wa kodi kwa mradi husika. Lakini kwa sababu watanzania wengi hawajui kabisa biashara wakiona jina au mmiliki wa mradi amebadilika, utasikia, 'tayari jamaa wamekwishakula', ujinga mtupu! Nchi ya wapiga majungu. Nchi ambayo mtu ambaye hawezi hata kueleza madini maana yake nini lakini anaamini anaweza kuwaelezea watu uchumi wa madini, au mtu asiyejua hata maana ya X- Ray lakini anaamini ana uwezo wa kuhutubia watu namna ambayo mgonjwa aliyevunjika mfupa anatakiwa kutibiwa!
Usitake kupotosha watu mkuu, hata kwenye sheria ya kodi tu neno "mradi" halijatumika.
 
Kuna course ya siri sana ambayo huwa inafundisha mambo ya namna ya kuiibia serikali course hii inaitwa 'THEFTOLOGY'
THEFTOLOGY ni muunganiko wa maneno mawili yaani ' theft' which means steal na logy/ology ambayo ni Greek word which means 'the study',therefore 'Theftology is the study of stealing (Ni kujifunza namna ya kuiba hasa kuiibia serikali)

HOW THEFTOLOGY IS APPLIED? (NI JINSI GANI THEFTOLOGY INAFANYA KAZI?)
Hapa inapotokea labda m2 kama Waziri kutoka Wizara Fulani anataka kuiibia serikali anafanya hivi;
1.Anatafuta jengo la MTU binafsi (kama ni waziri wa ujenzi) na jengo hili linakuwa ni jengo la mamilioni
2.Anamtafuta mwenye jengo kwaajili ya kutengeneza 'fake case baada ya kuwa wameshapga gharama halisi za jengo'
3.Anawatafuta majaji watakao simamia hyo case itakayoanzishwa.
Kwa hyo Waziri,Mwenye jengo na majaji wanakutana kwa siri kisha wanatengeza mazingira ya kuanzisha hii 'fake case' kama hivi;
Waziri mwenye dhamana husika atatangaza kuwa jengo fulani linapaswa kubomolewa atatuma mpaka tingatinga kwaajili ya kazi kuanza,lakn kwa kuwa ni very culculated movie mwenye jengo atakuja na hati ya zuio kutoka mahakamani (Kumbuka kuwa kuna majaji wameingizwa kwenye hii game).Baada ya mahakama kutoa hati ya zuio kitakachofuatia ni kusitisha ubomoaji na kuanzishwa kwa case kati ya Wizara ya ujenzi na mmiliki wa jengo, kesi hii inaweza kusikilizwa hata kwa miezi kadhaa au miaka na hatimaye mwenye jengo atashinda kesi,mahakama itaamuru alipwe kwa kupotezewa muda wake kama mfanyabiashara na wizara itamlipa so, kama malipo ni million 1,500 basi waziri atachukua millioni 500,majaji 500,mwenye jengo million 500 na kesi inaisha.Ndyo maana kwa Africa Mara nyingi mtu binafsi akipelekana mahakamani na serikali basi mwisho wa mchezo lazma serikali ishindwe
Kwa hapa kwetu bongo njia rahc ya kuiibia serikali ni kupitia mzabuni ambayo huwa ipo hivi;
Unaagiza vifaa vinavyoweza kuisha kutoka kwa mzabuni mfano kama upo kwenye idara ya elimu unaagiza box tatu za chaki lakn kwenye covering letter,muhtasari na kwenye cheque za kumlipa mzabuni unaandka box 57 za chaki kwa kuwa ni vitu vya kuisha hata wakaguz wakija hawawez kukwambuia "tuletee na chaki zilizoisha tuzione"
NB:Lengo langu si kufundsha wizi ila ni kuwafumbua watu macho ili wajue mambo haya yapo na yanatendeka kila sku na kila mahali
 
Maneno yako tu yanakutambulisha wewe ni mtu wa namna gani.

Hapa tunaongelea biashara na siyo uchuuzi ambao kuna uwezekano mkubwa, ndiyo unaoufanya.
Kama brela unasajiri makampuni ya uchuuzi sawa! We endelea na makampani yako yakupiga super profit acha wachuuzi tuendeleee kuchuuza!
 
Usitake kupotosha watu mkuu, hata kwenye sheria ya kodi tu neno "mradi" halijatumika.
Fanya utafiti, utaujua ukweli. Misamaha ya kodi hutolewa wakati uwekezaji wa miradi mipya. Mradi unapouzwa na kununuliwa na mwekezaji mpya au mwekezaji wa mwanzo anapotaka kubadilisha jina, haihesabiki kama ni uwekezaji mpya. Mradi unaendelea na benefits zile zile za mwanzo. Kama mwekezaji wa mwanzo alikuwa hajarudisha mtaji wake, akaja mwekezaji mpya kwenye mradi ule ule, akaongeza uwekezaji, kipindi cha msamaha wa kodi kitaongezeka kutokana na mtaji uliongezeka. Na hiyo haina uhusiano na jina la kampuni.

Mabadiliko ya majina ya hoteli kama ile iliyokuwa ikiitwa zamani Kilimanjaro au Sheraton Hotel, sidhani kama yana uhusiano na ukwepaji kodi bali ilitokana na mabadiliko ya wamiliki. Ni jambo la kawaida sana katika biashara hizi kubwa za kimataifa, makampuni kununuliwa, kufilisika au kuungana. Mmiliki mpya au partner mpya (na hasa kama amekuwa na umiliki mkubwa) atapenda kuitambulisha biashara yake kwa brand yake.

Kwenye biashara inalengwa faida. Kama nimejenga hotel, nimepata msamaha wa kodi mpaka nitakaporudisha mtaji wangu au nimepewa msamaha wa kodi wa jumla, msamaha wa kodinwa miaka 5. Hotel niliijenga kwa TZS 50 billion. Mwaka wa 3 kuna kampuni imekuja inataka kununua hotel yangu kwa TZS 100 billion. Kwa nini nisiiuze. Nitalipwa TZS 100 billion, nitailipa serikali tax gain. Aliyeinunua atapeleka ombi la kubadilisha jina na kuendelea na msamaha wa kodi wa miaka iliyobakia. Kuna kosa gani? Au aliyeinunua anaamua kufanya expansion, ameongeza kiwango cha uwekezaji, hatalipa kodi mpaka mtaji niliouwekeza mimi na ule wa kwake itakapokuwa imerudi. Kunapofanyika hivyo, kuna kosa gani?

Zamani hakukuwa na tax unapouza project yako lakini baadaye sheria ilibadilika. Leo hii mradi wowote ukiuzwa kuna tax ya serikali.

Tuondoe dhana kuwa kila kunapofanyika mabadiliko ya jina, kuna watu wamepiga hela.
 
Kama brela unasajiri makampuni ya uchuuzi sawa! We endelea na makampani yako yakupiga super profit acha wachuuzi tuendeleee kuchuuza!
BRELA wanasajili makampuni yote ya uwekezaji na uchuuzi pia. Unaweza kuwa kampuni ya ku-supply stationery. Stationery unachukua India au China unapeleka kwenye ofisi mbalimbali. Huo ni uchuuzi. Na kuna wakati uchuuzi unaweza kukupa super profit kumshinda mwekezaji.
 
Mkuu MMM,

Kwanza nakubaliana na Ngabu na wengine kutoa angalizo kuwa kuziweka hadharani mbinu/njia za wizi kunaweza kuwa na madhara ambayo yatakula kotekote.

Lakini mimi nina tatizo na hicho kinachoitwa "Serikali". Ukichunguza Serikali na matendo yake unaweza usiumie wala kujali ikiibiwa lakini nchi/wananchi wakiibiwa unaweza kuumia sana. Sasa kama wewe unataka kuisaidia Serikali nikuulize yafuatayo:-

1) Wakati Serikali inanyang'anya mashamba, mali/fedha na majumba ya watu toka awamu ya kwanza mpaka hii ya tano je unadhani ni haki na sahihi?

2) Unadhani kwa unyang'anyi huo wa Serikali (calling a spade a spade), Nchi/Wananchi wa Tanzania wamefaidika nini/vipi?

3) Azimio la Arusha ni moja ya doa na laana kwa nchi hii (without apology). Kwa kudhulumu kwa njia zile haramu mali halali za watu binafsi na kuzifanya za Serikali/Umma unadhani lile lilikuwa jambo jema au haki? Je machozi na damu ya waliodhulumiwa unadhani havitudhuru mpaka leo?

4) Tumemsikia Mh Rais wiki iliyopita akisema kuwa "...mtu anaweza kupotea lakini hela ya Serikali haiwezi potea kamwe...." Yaani fedha ina thamani kuliko mtu na utu. Kwa matendo na maneno yake anathibitisha kuwa kuna watu wamepotea na ni kweli kabisa kwenye awamu hii yametokea mengi tu; lakini ni kosa na uovu mkubwa kuliko unavyoweza kukubali. Ina maana hawa watawala wa sasa ni zaidi ya materialists wa hatari mno, ukipingana na maslahi yao kwisha.

NB: Serikali ni utashi wa mtu + utashi na maslahi ya kikundi cha watu wachache tu. Nchi ni ya wananchi/wakaazi wote.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom