Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Yote tisa, hivi huu mtindo wa kampuni za madini kuwa na viwanja vya ndege ambapo wanaweza kusafirisha dhahabu moja kwa moja hadi nje ya nchi una manufaa gani kwa taifa? Hivi ni kweli hawa watu kutoka Geita wanashindwa kuruka hadi uwanja wa ndege wa Mwanza ambapo kuna Ushuru na Forodha? Maana hata Meremeta nao walikuwa na uwanja wa ndege vile vile hadi leo hatujua walisafirisha kiasi gani cha dhahabu kwenda Afrika ya Kusini; wameacha mashimo tu!!
Lakini kuna namna ya kuhalalisha uwepo wa viwanja hivi vya ndege
- kusafirisha wafanyakazi
- Kusafirisha vitendea kazi mbalimbali
- Kusafirisha vipuri
Hata hivyo nimeshindwa kuelewa kama viwanda vingine navyo vinaweza kutumia sababu hizo hizo kuwa na viwanja vyao vya ndege. Nimejiuliza kwa mfano kwanini tusiweke utaratibu kuwa labda mahali ambapo wanaweza kuwa na uwanja wa ndege ni pale ambapo hapawezi kufikika kwa ndege kati ya saa moja hivi au kulazimisha viwanja hivyo vya ndege visiwe vya makampuni bali kampuni kama ya madini ijenge kiwanja cha ndege cha umma ambacho kitatumiwa na umma vile vile. Kwa mfano hicho cha Geita kisiwe cha kampuni bali chini ya TCAA (sijui kama kilivyo sasa kinamilikiwa na GGM au vipi).
Sijui ni makampuni mangapi ya madini yana viwanja vyao vya ndege vya kimataifa nchini. Hili linahusu pia kampuni za uwindaji...
Lakini kuna namna ya kuhalalisha uwepo wa viwanja hivi vya ndege
- kusafirisha wafanyakazi
- Kusafirisha vitendea kazi mbalimbali
- Kusafirisha vipuri
Hata hivyo nimeshindwa kuelewa kama viwanda vingine navyo vinaweza kutumia sababu hizo hizo kuwa na viwanja vyao vya ndege. Nimejiuliza kwa mfano kwanini tusiweke utaratibu kuwa labda mahali ambapo wanaweza kuwa na uwanja wa ndege ni pale ambapo hapawezi kufikika kwa ndege kati ya saa moja hivi au kulazimisha viwanja hivyo vya ndege visiwe vya makampuni bali kampuni kama ya madini ijenge kiwanja cha ndege cha umma ambacho kitatumiwa na umma vile vile. Kwa mfano hicho cha Geita kisiwe cha kampuni bali chini ya TCAA (sijui kama kilivyo sasa kinamilikiwa na GGM au vipi).
Sijui ni makampuni mangapi ya madini yana viwanja vyao vya ndege vya kimataifa nchini. Hili linahusu pia kampuni za uwindaji...