Jinsi ya kuflash simu za kichina (android phones)

May 11, 2020
9
14
Kama kichwa cha post kinavyosema, nataka ujue ni jinsi gani ya kuweza kuflash simu yako ya Android kwa kutumia Proglam mbalimbali kulingana na tatizo binafsi.

Hapa kwanza nitaelezea simu mbalimbali kulingana na aina ya chipset zake

= => Tecno

= => Infinix

= => Gionee

= => Innjoo

= => Itel

= => Elephone

= => Jiayu

= => Oppson

= => THL

= => Pipo

= => Oppo

= => Chuwi

= => Yusun Copy za samsung, copy za htc, copy za sony kama (XBO) n.k. hizi chipset zake ni =MTK
  1. itel, copy za tecno na copy nyingine za samsung, hzo ni SPD

Matatizo ni kama simu imefikia hatua inawaka haimalizi. kwa maana kama ni tecno inaishia katika logo ya tecno. cha kufanya ni kuingia hapa MTK FLASH FILES.

Utadownload mafile kulingana na aina ya simu yako na model yako. ukimaliza itakubid uingie hapa udownload driver hizi hapa Mtk usb flashing drivers

Utadownload hii program kwa ajiri ya kuflash ambayo inaitwa Sp flash tool
kumbuka haya mafile unapoyadownload mengine yatakuwa katika mfumo wa ZIP au RAL kwahyo itakubidi uyaextract.

Ukishayaextract andaa simu simu yako kwa kuichaji simu yako hadi 50% at least. fungua folder la sp flash tool humo ndani utakuta mafile mengi ila wewe fungua file linaloitwa flash tool lililopo katika mfumo wa application.

Angalia kulia katika browser list utaona browse to load scatter file. itafungua window mpya kwa ajili ya kuselect scatter. hapo utaenda katika folder uliloextract file la simu yako then utachagua mfano kama ni mtk 6572 itakuwa hivi- (MT6572_Android_scatter_emmc) utalifungua hilo na litaload mafile yote unayotakiwa kuyaflash katika simu yako alafu utaclick katika Download.

Hapo toa betri katika simu subil sekunde kama tatu rudishia bonyeza batani ya kupunguzia sauti na chomeka simu yako katika computer bila kuachilia hyo batani, ukiona msitali mwekundu unapita hadi mwisho achia batani. utapta wa blue alafu utafatia wa njano huo ukimaanisha imeanza kuflash. Hapo tulia uisikilizie hadi imalize. ambapo ikimaliza inaonyesha tick. ukishaona tick chomoa simu yako toa betri na rudshia tena iwashe kawaida.
  • Hapa tena nazungumzia jinsi ya kuziflash hizo za aina ya piri aina ya SPD. Mara nyingi katika kazi zangu nimekutana nazo za aina ya (Itel) hizi Proglam yake ni hii hapa SPD FLASH TOOL
  • Mafile ya hizo simu yanapatikana hapa SPD FLASH FILES
  • Driver za hzo simu kwa ajiri ya kuflashia ni hizi hapa SPD FLASHING DRIVER
Hizi utatakiwa kuifungua hiyo upgrade tool kutoka katika folder uliloliextract na utaenda katika alama ya kwanza kulia inayoonyesha (load package) utraiclick tena itafungua window itakayokuwa inakutaka ukaload file unalotakiwa kuliflash katika simu yako. kwahyo utatafuta hlo folder ulipoliextract file la simu yako na utaliload katika hiyo program.

likishaingia itakubid uclick katika alama ya kama play itakayokuwa inaonyesha haya maandishi pindi unaposogeza mshale wa mouse yako- (start download) hgapa utatumia njia ile ile ya kushikilia batani ya kushusha au kupandisha sauti katika kuconnect kama mtk. usisahau kabla ya yote kuinstall driver za simu yako husika. maana bila driver huwezi kufanya lolote.

kwa mara nyingne nitarudi kufundisha jinsi ya kuflash simu za samsung smartphones.
Kwa msaada wa kujua mobile software au kutengenezewa simu yako tuwasiliane 0718968027
 
Hivi ukiflash sinu si unabadili hadi IMEI mkuu? Je, is't legal to flash a phone? Yaan kisheria ikoje? Maana nishaona jamaa kadakwa kwa kuflash simu.

Naomba msaada kwa hili tafadhali
 
Sasa Wewe Ndio Unataka Wazizime

Stock ROM Zote Zinaflashiwa Na Sp Na Ukiona Sp Imeahindwa Basi Box Nyingine Zote Cracked Haziwez Mpaka Uwe Na Paid.

Ku Format Preloader Unachagua Wewe, Sp ROM Yako Ikiwa Hata Na Block 1 Imemis Inakataa Kufanya Update Itakuletea BROM Error.

Simu Yoyote Uliyoizima Ukitaka Kuwasha Tafuta Stock ROM NA SP Inawaka Ikigoma Ujue Hiyo ROM Sio Yake Au Tumia KOLO PIN POINT METHOD.
Mkuu unataka wazime simu za wateja hii Sp Flash naiogopa sana kuna muda inaua simu, iki format preloader harafu ika fail, bora ungewapa alladin, miracle crack. Harafu hizi spd kwenye hiyo tools kuna zingine huwa haziendi.
 
Hivi ukiflash sinu si unabadili hadi IMEI mkuu? Je, is't legal to flash a phone? Yaan kisheria ikoje? Maana nishaona jamaa kadakwa kwa kuflash simu.

Naomba msaada kwa hili tafadhali
Kuflash simu hubadili imei,japo kuna scenario unaweza kukuta na imei nayo imebadilika...hapo utapaswa kuandika upya imei ya simu husika..

Kuflash simu sio kosa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm niko nje ya Mada mkuu.
PC yang nikifungua mafile inaandka
directx failed to initialize please install the correct drivers for your video card..

Nn shda apo
 
kwamba nipige tu window nyingine mkuu
hapana, kama unatumia windows 10 nenda settings>Update and security> chek for update. Inaweza chukua MB za kutosha but n uhakika, pia unaweza kupakua manually driver unazohitaji na directx. kufanya hivo chomeka sim afu search computer Management then Device manager then chek kama MTP itaonesha sign ya error then right click chagua update driver chagua search automatically for update driver software.
JPEG_20200527_170941_4834370855473489062.jpg
JPEG_20200527_171056_8435253327472453307.jpg
JPEG_20200527_171125_2613756332556175702.jpg


Sent from my TA-1020 using JamiiForums mobile app
 
hapana, kama unatumia windows 10 nenda settings>Update and security> chek for update. Inaweza chukua MB za kutosha but n uhakika, pia unaweza kupakua manually driver unazohitaji na directx. kufanya hivo chomeka sim afu search computer Management then Device manager then chek kama MTP itaonesha sign ya error then right click chagua update driver chagua search automatically for update driver software.View attachment 1460823View attachment 1460825View attachment 1460826

Sent from my TA-1020 using JamiiForums mobile app
Nashkuru kaka lakini natumia window 7
 
Back
Top Bottom