Jinsi ya kuepuka maambukizi ya v.V.U wakati wa sex

KANYEGELO

JF-Expert Member
Nov 12, 2019
2,149
4,752
JINSI YA KUEPUKA MICHUBUKO WAKATI WA TENDO LA NDOA ILI KUZUIA MAAMBUKIZI YA VIRUSI VYA UKIMWI(V.V.U)

Sio kila anayefanya ngono na mgonjwa wa ukimwi anapata maambukizi, kuna watu wameishi na wagonjwa wa ukimwi miaka na kuzaa watoto lakini bado hawakupata maambukizi haya ya virusi vya ukimwi.

Tafiti zinaonyesha kwamba ukilala na muathirika wa ukimwi basi uwezekano wakupata maambukizi ni asilimia 0.002 mpaka asilimia 1, kwa maana nyingine ni kwamba kati ya watu 100 mpaka 500 wanaolala na waathirika wa ukimwi ni mmoja anayepata maambukizi.
Hatari ya maambukizi huongezeka kwa asilimia 1 mpaka 1.4 kwa watu ambao wanafanya ngono kinyume na maumbile.
Kama ingekua kila anayelala na muathirika wa ukimwi na yeye anapata basi watu wangeisha kwani sisi wote tumeunganishwa kwenye mnyororo mmoja wa ngono bila kujuana.
Pamoja kwamba mnaweza kupima kabla ya kuanza mahusiano kitu ambacho kweli ni muhimu, bado Kuna haja ya kuendelea kua makini kwani watu wengi sio waaminifu na waathirika wengi ni wanandoa na watu ambao wako kwenye mahusiano sababu yakuaminiana sana.
yafuatayo ni mambo unayoweza kufanya kuzuia michubuko na kukuepusha maradhi ya mbalimbali ikiwemo ukimwi.

MAANDALIZI MAZURI:-
Hakikisha mwanamke ameloa vya kutosha muda wote wa tendo la ndoa na hii ni matokeo mazuri ya kumuandaa vizuri kabla ya tendo la ndoa na ukiona ukavu umeanza basi sitisha na muandae tena, kamwe usikubali kuendela na tendo la ndoa wakati unasikia uke ni mkavu kabisa au unasikia maumivu.

TUMIA VILAINISHI:-
watu wengi wanaamini vilainishi ni kwa ajili ya kuingiliwa kinyume na maumbile kitu ambacho sio kweli.
kama mwanamke unaona umeshindwa kuloana kwa sababu ambao ziko nje ya uwezo wako basi unaweza kutumia vilainishi hivi kuepuka michubuko.
kama wewe ni kijana ambaye hua unashiriki tendo la ndoa basi sio vibaya kua nayo nyumbani.

EPUKA NGONO YA KUKOMOA:-
kama mwanaume achana na mawazo yakumkomesha mwanamke, huwezi kumkomesha mwanamke kwa sex, ile sehemu mtoto anapita, wewe ni nani? fanya mambo yako kaa pembeni.
Ni rahisi sana kumridhisha mwanamke kwa round moja tu au mbili, ukizidi hapo mara nyingi anakua mkavu na kukauka.
ndio maana maambukizi yako juu kwa vijana kuliko wazee ambao hawana muda wala nguvu za kukomesha.

FANYA TARATIBU:-
Usidanganywe na video za ngono, mwanamke anaweza kuridhika sana kwa tendo la ndoa la taratibu kuliko ile ya fujo ambayo umeaminishwa kuiamini.
kufanya ngono taratibu kunaongeza msisimko, maji mengi ukeni na kupunguza uwezekano wa kuchubuka kwani unatumia nguvu kidogo sana kuingia na kutoka.

KUA MSIKIVU:-
kama kuna staili ambayo unaona ukimuweka mwenza wako anasikia maumivu au analalamika basi achana nayo, mwanamke akianza kusikia maumivu anakosa hamu ya tendo na kukauka haraka huku akisubiri umalize tu avae nguo
.
HAKIKISHA ANAFIKA KILELENI:-
jaribu kua mtundu na kuhakikisha mwenza wako anafika kileleni siku zote, kumfikisha kileleni siku zote kunamfanya mwanamke aloane sana na kupunguza sana uwezekano wa kuchubuka.
bahati nzuri mwanamke anaweza kuingia kileleni hata mara nne au tano wakati mwanaume akifika kileleni mara moja au mbili.
usioshe uke na maji kama bado unaendelea; mwanamke anaweza kuosha uke wake kabla ya tendo la ndoa, sio kitu kibaya kwani maandalizi hayajaanza.
Lakini kwenda kuosha tena baada ya mshindo wa kwanza unapafanya kule kua kugumu na kukavu kwani maji sio laini, hivyo utaleta ukavu ambao haukuepo mwanzoni.

USILAZIMISHE:-
kama mwanamke amechoka au ana sababu nyingine yeyote ya kutojisikia kufanya ngono basi usitumie nguvu kwani utajikuta umelala na mtu mkavu, mara nyingi watu ambao wanabakwa au kubaka huambukizwa maambukizi ya ukimwi sababu ya kufanya ngono na watu ambao hawakua tayari.
mwisho; tendo la ndoa sio vita, jipe muda wa kutosha kujiandaa kiakili na kimwili kabla ya kushiriki, hii itakuletea raha na kukuzuia na magonjwa mbalimbali ambayo ni hatari sana kwa mwili wako.

sent from toyota Allex
 
Waambie hao
Screenshot_20200109-200200.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah vijana tunaangamizana wenyewe kwa wenyewe embu ulete na takwimu za vijama wanaokufa kwa maambukizi ya virus vya ukimwi ili mtu achaguee maana naskia wanaumee ndo tunaongoza kufa
 
Mimi nina kinyaa siwezi kurudia tendo kama hatujakwenda kunawa au kuoga.

Yani nipizie kwenye uke halafu nirudie tena humo humo pasipo kunawa au kuoga-Never!
 
KANYEGELO,
Kwa uongo huu utaua wengi.
Risk ya kupata HIV unapolala na mwenye nayo bila kinga ni zaidi ya 80%. Tafiti zilizoko hadi sasa watu wanaoishi na wenza wenye ukimwi lakini wenyewe wakawa hawana ukimwi ni chini ya 15% ya couples za waathirikia. Yaani ukichukua waathirika wote wa HIV na wenza wao, utakuta 15% ya wenza hawajaathirika (na hapo hatuna uhakika na sex life yao, wengine utakuta walishaacha kufanya zamani ndipo mmoja wao akaenda kuutafuta huko nje).
Kondom yenyewe hupunguza maambukizi kwa 98%, kwa hiyo hata ukitumia kondomu unabaki na uwezekano wa 2%, kwa mnaojua probability mtaelewa kwa nini watu wanashauriwa kutumia kondom, ni kwamba katika kuokoa watu 100 ni sahihi kukubali kupoteza wawili ili 98 wapone.
Na haya niliyoandika wala hayahitaji elimu sana, hata huku mitandaoni uki google tu unapata taarifa za kukutosha kabisa kuepukana na upotofu. Au basi kama uko karibu na wataalamu waulize upate taarifa sahihi kuliko kueneza uongo, hii ni kama kulisha watu sumu.
 
Back
Top Bottom