Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,001
- 9,862
Katika ulimwengu wa Teknolojia wa sasa watoto wanalazimika kuwa na vifaa kama simu, laptops nk ili kuwezesha mawasiliano ya mzazi na mtoto.
Kwa kiasi kikubwa wazazi wanadhana kwamba vifaa hivi vinaweza kumuharibu mtoto hivyo wengine huwanyima watoto vifaa hivyo ambapo wanakuwa wamewanyima haki ya kupata taarifa.
Mtoto kuwa na simu janja sio tatizo, tatizo ni namna ambavyo ataitumia. Na katika hilo kunahitaji muongozo wa mzazi. Lakini kwa sasa wazazi hawako muda wote na watoto ili kuwachunga katika matumizi yao.
Ili mzazi kuwa na uwezo wa kuchunga matumizi ya simu janja au laptop kwa mtoto atahitaji kuwa na vifaa vingine ambavyo inaweza kuwa ni Google Family Link For children and teen au hata baadhi ya antivirus ambazo zinatoa huduma ya Parental Control.
Huduma hizo zinaweza kumfanya mzazi aweze kujua na kuzuia anachofanya mtoto kwenye simu yake hata kama hayupo naye jirani. Mzazi anaweza akapanga muda wa mtoto wake kuwa mtandaoni, kuzuia baadhi ya Apps nk.
Vitu hivyo unaweza kufanya bila kuwa na mtoto jirani, mathalani mzazi uko nyumbani, mtoto yuko shuleni na ukaweza kuzuia vitu ambavyo anavifanya kwenye simu. Hapa utakuwa umemuachia mtoto haki ya mawasiliano lakini umedhibiti matumizi yake.
Baadhi ya apps ambazo unaweza kuzitumia kudhibiti matumizi ya simu kwa mtoto
Kwa kiasi kikubwa wazazi wanadhana kwamba vifaa hivi vinaweza kumuharibu mtoto hivyo wengine huwanyima watoto vifaa hivyo ambapo wanakuwa wamewanyima haki ya kupata taarifa.
Mtoto kuwa na simu janja sio tatizo, tatizo ni namna ambavyo ataitumia. Na katika hilo kunahitaji muongozo wa mzazi. Lakini kwa sasa wazazi hawako muda wote na watoto ili kuwachunga katika matumizi yao.
Ili mzazi kuwa na uwezo wa kuchunga matumizi ya simu janja au laptop kwa mtoto atahitaji kuwa na vifaa vingine ambavyo inaweza kuwa ni Google Family Link For children and teen au hata baadhi ya antivirus ambazo zinatoa huduma ya Parental Control.
Huduma hizo zinaweza kumfanya mzazi aweze kujua na kuzuia anachofanya mtoto kwenye simu yake hata kama hayupo naye jirani. Mzazi anaweza akapanga muda wa mtoto wake kuwa mtandaoni, kuzuia baadhi ya Apps nk.
Vitu hivyo unaweza kufanya bila kuwa na mtoto jirani, mathalani mzazi uko nyumbani, mtoto yuko shuleni na ukaweza kuzuia vitu ambavyo anavifanya kwenye simu. Hapa utakuwa umemuachia mtoto haki ya mawasiliano lakini umedhibiti matumizi yake.
Baadhi ya apps ambazo unaweza kuzitumia kudhibiti matumizi ya simu kwa mtoto