Jinsi ya kuacha kuvuta sigara (A Guide to Quitting Smoking)

Imebidi nije humu kuomba msaada. Ukweli niko addicted na vitu vitatu. Castle baridi , sigara na JF.

Hivyo viwili havipi shida sana. Kinachonipa shida ni fegi. Nataka kuacha lakini attempt zote zimeshindikana. Wakuu , wale waloweza kuacha naomba michango yenu. HOW CAN I STOP SMOKING?
 
Aisee pole sana... Hata mimi nauta sigara, lakini ninajua kuwa bila kuamua mwenye ni ngumu sana.
1. Nauhakika una company ya wavuta sigara. Wakimbie
2. Usiwache kwa mpigo bali punguza idadi
3. Tafuta kitu kingine cha kula wakati una sikia kiu ya fegi.
Mangineyo ni nia yako....
 
Na matatizo mengineyo mchungaji sylvester gamanywa atakuwa na maombezi kabambe
ya kukemea na kukataa mateso yanayowatesa watanzania pamoja na magonjwa yasiotibika
starehe ndogo ndogo na kubwa...matatizo ya familia yaani ndoa ,Watoto wasio na heshima ,na matatizo ya kibiashaara,makazini,na mengine mengi njoo barabara ya tegeta shuka kituo cha interchick uliza kanisa la BCS kwa Askofu gamanywa
Mungu anakwenda kuondoa mateso yako anaitaji imani na Toba
ijumaa Saa Tatu usiku mpaka kuminamoja
Mungu awabariki
 
Wadau wazima? moja ya ada mbaya kabisa ni uvutaji sigara. Kwa mujibu wa madaktari na ripoti nyingi za kibita uvutaji sigara una madhara mengi. Nina jamaa zangu wengi ambao wanadai kwamba, mara kadhaa wamejaribu kuacha kuvuta sigara lakini bila mafanikio. Labda kwa wale ambao ni wavutaji wanaweza kutujulisha je ni kweli ni vigumu kuacha kuvuta sigara? Je kuna ambao walikuwa ni wavutaji na sasa wameacha kuvuta sigara. Si vibaya wakatufahamisha vipi walifanikiwa kuacha kuvuta sigara ili wavutaji wanaotaka kuacha na kushindwa kufanya hivyo kama wanavyodai waweze kunufaika. Njia nzuri za kuacha kuvuta sigara ni zipi?
 
Mkuu kuna therapy inaitwa hypnosis, kuna baadhi ya matherapist wanafanya service ya ku-hypnotize watu.
Mojawapo ya faida za hypnosis ni kuondoa kumbukumbu ambazo zimejijenga toka mtu anapozaliwa, hizi kumbukumbu hujenga baadhi ya tabia/mazoea/hulka ikiwemo uvutaji sigara. Kumbukumbu hizi (subconcious mind) huweza kuondolewa au kupunuzwa madhara yake kwa njia ya hypnosis. Angalizo: Hypnosis hutakiwa kufanyiwa na mtu unaemuamini kwa maana mtu akiwa hypnotised anakuwa subconcious hivyo anaeku-hypnotise huweza kukupa command yeyote ambayo lazima utaifuata hata kama ni jambo baya.
 
[h=2]Msaada wadau...Jinsi ya kuacha kuvuta sigara[/h]
Wadau wazima? moja ya ada mbaya kabisa ni uvutaji sigara. Kwa mujibu wa madaktari na ripoti nyingi za kibita uvutaji sigara una madhara mengi. Nina jamaa zangu wengi ambao wanadai kwamba, mara kadhaa wamejaribu kuacha kuvuta sigara lakini bila mafanikio. Labda kwa wale ambao ni wavutaji wanaweza kutujulisha je ni kweli ni vigumu kuacha kuvuta sigara? Je kuna ambao walikuwa ni wavutaji na sasa wameacha kuvuta sigara. Si vibaya wakatufahamisha vipi walifanikiwa kuacha kuvuta sigara ili wavutaji wanaotaka kuacha na kushindwa kufanya hivyo kama wanavyodai waweze kunufaika. Njia nzuri za kuacha kuvuta sigara ni zipi?
 
muite Yesu akufungue kutoka kwenye hicho kifungo. Kuanzia kesho anza kufunga kula, fanya sala na maombi, elekeza kilio chako kwa Mungu naye atakufungua na kukuweka huru, nawe utakuwa huru kwelikweli
 
Anza kujishughulisha na kutafuta mademu. Unajua wanawake wengi huwa hawapendi sigara, kwahiyo ukiwa nao watakuwa wanakuambia ''sweety acha sigara''
 
Usiache Mkuu! Kuanzia Tarehe Mosi Julai zitauwa na mchanganyiko wa Blue Band, Maziwa na Asali kwa afya za wavutaji. Usiache uhondo waja ati!
 
muite Yesu akufungue kutoka kwenye hicho kifungo. Kuanzia kesho anza kufunga kula, fanya sala na maombi, elekeza kilio chako kwa Mungu naye atakufungua na kukuweka huru, nawe utakuwa huru kwelikweli

Naunga mkono hoja asilimia mia kwa mia. hiyo ndiyo njia rahisi kuliko zote!
 
Usiache Mkuu! Kuanzia Tarehe Mosi Julai zitauwa na mchanganyiko wa Blue Band, Maziwa na Asali kwa afya za wavutaji. Usiache uhondo waja ati!

pole sana, mazara hayapungui kwa kuweka harufu nzuri au ladha nzuri sumu ni sumu tu!
 
Dawa ya tatizo hilo anayo aliyekuumba, na aliyekukomboa. kama unahitaji kukombolewa jitahidi umfuate mwokozi Yesu. siyo utani, yeye anaweza tena utashangaa wala hutaamini. uvutaji wa sigara unashikiliwa na roho wachafu hivyo unahitaji roho mwenye nguvu kuwadhibiti hao roho wachafu. ukimfuata Roho mtakatifu yeye aweza yote!.
mfuate mchungaji yeyote akusaidie (mchungaji wa makanisa ya kiroho).
 
Inasikitisha, ina maana hakuna mwenye mawazo ya maana mbona mnakatisha tamaa.au ndio kusema wana JF wamefilisika namna hii? inasikitisha na kutia kichefuchefu
 
Inasikitisha, ina maana hakuna mwenye mawazo ya maana mbona mnakatisha tamaa.au ndio kusema wana JF wamefilisika namna hii? inasikitisha na kutia kichefuchefu

Hapa wengi ni wavutaji nikiwemo mimi. Sasa ushaurike vipi wakati nasi tunauhitaji huo msaada wa kuacha? Kama kichefu chefu umetuletea mwenyewe . Acha kutudharau bana.
 
sasa nimefahamu, kumbe nimepeleka kesi ya mbuzi kwa fisi. nisamehe; uungwana kama mtu hana cha kusema bora anyamaze kuliko kuongea pumba.kwa mfano mwendabure anasema: Usiache Mkuu! Kuanzia Tarehe Mosi Julai zitauwa na mchanganyiko wa Blue Band, Maziwa na Asali kwa afya za wavutaji. Usiache uhondo waja ati! mwisho wa kunukuu, kweli haya ni mawazo ya kumpatia mtu sema wewe mfamaji (usioisha kutapatapa)
 
au huyu womanizer anasema? Anza kujishughulisha na kutafuta mademu. Unajua wanawake wengi huwa hawapendi sigara, kwahiyo ukiwa nao watakuwa wanakuambia ''sweety acha sigara'' mwisho wa kunukuu. sema mfamaji hili nalo ni wazo kama sio kichefuchefu ni nini? soma pia maoni yaliyotolewa kabla hujaanza kunishambulia kwa makombora yasiyofika mbali. ala we vipi?
 
Womanizer anaona mademu ndio dili. kama alivyosema mkirua, unakimbia kansa na kuukimbilia ukimwi. du, mawazo mengine hayana hata mizani?
 
Waone washauri nasaha wanajua jinsi ya kushauri ili uache kuvuta bila msongo wa mawazo.
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom