ZEE LA HEKIMA
JF-Expert Member
- Aug 10, 2015
- 1,417
- 1,829
Mimi nilivuta kwa zaidi ya miaka 20 na niliacha nikiwa nimeshafikisha paketi.mbili kwa siku. Silu tatu za kwanza ndio ngumu sana lakini ukishazivuka the rest is plain sailing. Ukitaka kuishinda hiyo tabia vizuri siku unaacha nunua sigara zako na kiberiti kabisa. Jipongeze kwa ushindi kwa masaa matatu ya kwanza. Jipongeze kwa masaa matatu yanayofuata. Kisha jiambie kama umeweza kuacha kwa saa sita utaweza kwa saa sita zinazofuata. Ukishindwa kabisa kuacha kuwasha sigara toa sigara kwenye paketi weka mdomoni, toa kiberiti ukiwashe lakini usiwashe sigara. Ukiacha hiyo sigara mdomoni kwa dakika mbili bila kuiwasha una ushindi mkubwa. Siku ya kwanza uzalendo ukikushinda usikate tamaa. Jaribu tena kesho yake. Kila wakati jipongeze kwa idadi ya masas uliyoacha kuvuta. Mtu yeyote anayetaka kuacha kuvuta sigara ajaribu kufanya hivi. Utashinda uvutaji uliolitesa kwa miaka mingi