ndege JOHN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2015
- 19,550
- 44,702
Asikwambie mtu kukaa maskani yoyote Ni msala maana mamwera muda wowote wanatimba na mapira kutujaza.kama una roho nyepesi usikae kabisa we chukua mzigo stori nyingine kwenu,kula pia kwenu.mimi mpaka nafikia hapa nilipo nimedakwa Mara tano na polisi
Mara ya kwanza nipo mitaa ya Riverside tuko wakushi Kama sita hivi Mimi nilikuwa nanyonga kitu,ghafla bin vuu wazee wanne wamekuja tukashindwa kukimbia tukafungwa wawili wawili kwenye mashati wawili wakafungwa na pingu.tukapelekwa kituo kidogo Cha kibangu.
Sema siku hio wapiga debe(masarange) wengi walikua wamekamatwa kwa hiyo boss wa bus akaja kututoa wote ilibidi tukomae kwamba na sisi Ni wapiga debe.tukatolewa wote baada ya masaa Kama ma nne hivi.
Mara ya pili nakamwatwa Niko msasani B Club Niko na wahuni flani mida ya mchana na marasta pia walikuwepo walikuja wazee na defender mbili lakini uzuri mmiliki wa lile eneo alikuja akatutoa kwa shillingi 300000.
Mara ya tatu Niko vingunguti hapa sikukamatwa lakini Cha moto nilikiona maana nilikimbizana na Askari Kama dakika kumi hivi ye mwenyewe akachoka nimemtoa baru kuanzia vingunguti mpaka barakuda kugeuka nyuma nikaona nimemwacha mbali.kwa jinsi nilivyopagawa ilibidi nipande gari la kwenda kimanga afu kibaya nauli sikuwa nayo.konda alinielewa lakini alinionea huruma ninavyohema na kutoka jasho
Mara ya nne Niko mitaa ya perfect vision pale ubungo.siku hio nilichomeshwa maana niliondoka maskani lakini nikawa nimechukua kete moja nikailipue ma getoni.Nimetembea ile navuka daraja la kwenda mawasiliano nikashangaa watu wawili warefu wamenipiga bega nikadakwa kupigwa search wakanikamata na kiberiti bangi hawakuiona.nimefika kituoni SI ndio ikadondoka bahati mbaya.Ikawa msala kituo chenyewe Cha urafiki.hio kesi ndio ilikuwa kubwa kuliko kesi zote maana nilitoka kwa shillingi laki na nusu.
Mara ya tano Niko makoka mitaa ya kibangu mbele mbele.siku hio.asubuhi TU unaambiwa wamekuja na vi Noah vyeusi tukakamatwa watu watatu tukapelekwa mbez kwa yusufu kituo Cha polisi tulikaa kule siku tatu.nilivyopewa tu dhamana sikuwahi kurudi Tena hata kureport uzuri hio kesi sikutoa hata Mia.
Nyingine Niko mikasa club pale Riverside tukashangaa amekuja mshikaji kajifanya anataka kazi kumbe Ni Askari tumeanza kuvuta naye tukashangaa wameingia watu watatu SI ndio wakatupiga chini ya ulinzi..ilibidi nimpigie simu mpenzi wangu anitumie 20000 fasta nimalizane nao.
Kwa hiyo ndugu zangu tunakumbana na misukosuko mingi Sana ndo maana siku hizi maskani sitembelei kabisa nikienda nachukua mzigo wangu Kama Ni za 5000 za kunitosha kwa siku tatu au nne naishia zangu magetoni.
Mara ya kwanza nipo mitaa ya Riverside tuko wakushi Kama sita hivi Mimi nilikuwa nanyonga kitu,ghafla bin vuu wazee wanne wamekuja tukashindwa kukimbia tukafungwa wawili wawili kwenye mashati wawili wakafungwa na pingu.tukapelekwa kituo kidogo Cha kibangu.
Sema siku hio wapiga debe(masarange) wengi walikua wamekamatwa kwa hiyo boss wa bus akaja kututoa wote ilibidi tukomae kwamba na sisi Ni wapiga debe.tukatolewa wote baada ya masaa Kama ma nne hivi.
Mara ya pili nakamwatwa Niko msasani B Club Niko na wahuni flani mida ya mchana na marasta pia walikuwepo walikuja wazee na defender mbili lakini uzuri mmiliki wa lile eneo alikuja akatutoa kwa shillingi 300000.
Mara ya tatu Niko vingunguti hapa sikukamatwa lakini Cha moto nilikiona maana nilikimbizana na Askari Kama dakika kumi hivi ye mwenyewe akachoka nimemtoa baru kuanzia vingunguti mpaka barakuda kugeuka nyuma nikaona nimemwacha mbali.kwa jinsi nilivyopagawa ilibidi nipande gari la kwenda kimanga afu kibaya nauli sikuwa nayo.konda alinielewa lakini alinionea huruma ninavyohema na kutoka jasho
Mara ya nne Niko mitaa ya perfect vision pale ubungo.siku hio nilichomeshwa maana niliondoka maskani lakini nikawa nimechukua kete moja nikailipue ma getoni.Nimetembea ile navuka daraja la kwenda mawasiliano nikashangaa watu wawili warefu wamenipiga bega nikadakwa kupigwa search wakanikamata na kiberiti bangi hawakuiona.nimefika kituoni SI ndio ikadondoka bahati mbaya.Ikawa msala kituo chenyewe Cha urafiki.hio kesi ndio ilikuwa kubwa kuliko kesi zote maana nilitoka kwa shillingi laki na nusu.
Mara ya tano Niko makoka mitaa ya kibangu mbele mbele.siku hio.asubuhi TU unaambiwa wamekuja na vi Noah vyeusi tukakamatwa watu watatu tukapelekwa mbez kwa yusufu kituo Cha polisi tulikaa kule siku tatu.nilivyopewa tu dhamana sikuwahi kurudi Tena hata kureport uzuri hio kesi sikutoa hata Mia.
Nyingine Niko mikasa club pale Riverside tukashangaa amekuja mshikaji kajifanya anataka kazi kumbe Ni Askari tumeanza kuvuta naye tukashangaa wameingia watu watatu SI ndio wakatupiga chini ya ulinzi..ilibidi nimpigie simu mpenzi wangu anitumie 20000 fasta nimalizane nao.
Kwa hiyo ndugu zangu tunakumbana na misukosuko mingi Sana ndo maana siku hizi maskani sitembelei kabisa nikienda nachukua mzigo wangu Kama Ni za 5000 za kunitosha kwa siku tatu au nne naishia zangu magetoni.