Jinsi wageni watakavyo leta vita Tanzania!

Menejimenti SCI yatuhumiwa


na Mwandishi Wetu


amka2.gif

WAFANYAKAZI wa Kampuni ya SCI Tanzania Limited wameutuhumu uongozi wa kampuni yao kwa kukiuka taratibu za ajira na za uhamiaji.
Wakiongea juzi katika ofisi za gazeti hili, walisema wamefikia hatua ya kutoa malalamiko yao hadharani baada ya viongozi wao kuanza kuwafukuza kazi bila kuwalipa stahili zao na kuajiri raia wa kigeni kinyume cha taratibu.
Wafanyakazi hao ambao waliomba majina yasitajwe gazetini kwa kuhofia usalama wa ajira zao, walisema kumekuwa na mkakati wa siri wa kunyakua ajira za wazawa na kuwapa wageni.
Walisema, licha ya kuajiri wageni, taratibu za ajira zimekuwa hazifuatwi na baadhi ya maofisa wa Uhamiaji wamekuwa wakifika katika ofisi hizo na kufanya mazungumzo ya siri na mkurugenzi wao waliyemtaja kwa jina la Ravishankar Rajamani kisha wanaondoka.
“Tumekwishafikisha malalamiko yetu Uhamiaji kuwa katika kampuni hii kuna wageni ambao hata hawana ujuzi wala uzoefu wa kazi, lakini wamepewa kazi zisizo za kitaalamu huku wakiwa hawana hata vibali vya kufanya kazi nchini. Maofisa Uhamiaji wanakuja, wanaongea na bosi wanaondoka kimya kimya,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.
Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Rajamani alisema suala hilo amekwishazungumza na maofisa wa Uhamiaji na kulimaliza. Ramajani alisema, Uhamiaji wanazo taarifa kuwa ana wafanyakazi ambao hawajapata vibali, lakini utaratibu wa kupatiwa unaendelea na kwamba anayo ruhusa kutoka kwa maofisa hao ya kuendelea kuwatumia wakati taratibu za kuwapatia vibali vya kufanya kazi nchini zikiendelea. Jitihada za kumpata Mkurugenzi wa Uhamiaji kuzungumzia suala hilo juzi na jana hazikufanikiwa kwa maelezo yaliyotolewa na mmoja wa wasaidizi wake aliyekataa kutaja jina lake, kwamba ana kazi nyingi za nje wiki hii.
 
Menejimenti SCI yatuhumiwa


na Mwandishi Wetu


amka2.gif

WAFANYAKAZI wa Kampuni ya SCI Tanzania Limited wameutuhumu uongozi wa kampuni yao kwa kukiuka taratibu za ajira na za uhamiaji.
Wakiongea juzi katika ofisi za gazeti hili, walisema wamefikia hatua ya kutoa malalamiko yao hadharani baada ya viongozi wao kuanza kuwafukuza kazi bila kuwalipa stahili zao na kuajiri raia wa kigeni kinyume cha taratibu.
Wafanyakazi hao ambao waliomba majina yasitajwe gazetini kwa kuhofia usalama wa ajira zao, walisema kumekuwa na mkakati wa siri wa kunyakua ajira za wazawa na kuwapa wageni.
Walisema, licha ya kuajiri wageni, taratibu za ajira zimekuwa hazifuatwi na baadhi ya maofisa wa Uhamiaji wamekuwa wakifika katika ofisi hizo na kufanya mazungumzo ya siri na mkurugenzi wao waliyemtaja kwa jina la Ravishankar Rajamani kisha wanaondoka.
“Tumekwishafikisha malalamiko yetu Uhamiaji kuwa katika kampuni hii kuna wageni ambao hata hawana ujuzi wala uzoefu wa kazi, lakini wamepewa kazi zisizo za kitaalamu huku wakiwa hawana hata vibali vya kufanya kazi nchini. Maofisa Uhamiaji wanakuja, wanaongea na bosi wanaondoka kimya kimya,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.
Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Rajamani alisema suala hilo amekwishazungumza na maofisa wa Uhamiaji na kulimaliza. Ramajani alisema, Uhamiaji wanazo taarifa kuwa ana wafanyakazi ambao hawajapata vibali, lakini utaratibu wa kupatiwa unaendelea na kwamba anayo ruhusa kutoka kwa maofisa hao ya kuendelea kuwatumia wakati taratibu za kuwapatia vibali vya kufanya kazi nchini zikiendelea. Jitihada za kumpata Mkurugenzi wa Uhamiaji kuzungumzia suala hilo juzi na jana hazikufanikiwa kwa maelezo yaliyotolewa na mmoja wa wasaidizi wake aliyekataa kutaja jina lake, kwamba ana kazi nyingi za nje wiki hii.


patamu hapa ngoja tuone sheria inasemaje
 
Hapa ofisini kwangu menejimenti imeajiri afisa utawala (senior administrator) mkenya. Huyu bwana kaanza kazi jana.

Hili jambo limenikera sana kwa maana ninajua kuwa kuna watanzania wa kutosha wenye sifa (kielimu na kiutendaji) ambao wangeweza kujaza nafasi hiyo.

Wakati tangazo la nafasi ya kazi lilipotoka magazetini, watu mbali mbali waliomba hiyo kazi. Usaili ulifanyika na utawala katika hekima zake ukaamua kumpa kazi huyu mkenya.

Swali:

1. Je sheria za ajira zinasemaje juu ya ajira zinazoweza kujazwa na watanzania kujazwa na "wageni"?

2. Je kuna namna ambavyo naweza kujenga hoja na kuushurutisha utawala hapa ofisini kwangu kusitisha ajira ya huyu mkenya na kuhakikisha mtanzania mwenye sifa (kielimu na kiutendaji) anapewa hiyo kazi?

Binafsi kitendo hiki kimenikera sana na ningependa kuwa tofauti kwa kujaribu kurekebisha jambo hili hapa ofisini kwangu nikitumaini na wengine wakafuata hivyo na tukawa watu wa maendo zaidi kuliko maneno / majadiliano.

Angalizo:
Kama hamna njia ambaya ninaweza kurekebisha hali hii maadam imekwisha tokea naomba mnisaidie naweza kufanya nini ili hali hii isitoke kwa ajira nyingine hapa ofisini kwangu.

Natanguliza shukurani

Nyau
 
Hapa ofisini kwangu menejimenti imeajiri afisa utawala (senior administrator) mkenya. Huyu bwana kaanza kazi jana.

Hili jambo limenikera sana kwa maana ninajua kuwa kuna watanzania wa kutosha wenye sifa (kielimu na kiutendaji) ambao wangeweza kujaza nafasi hiyo.

Wakati tangazo la nafasi ya kazi lilipotoka magazetini, watu mbali mbali waliomba hiyo kazi. Usaili ulifanyika na utawala katika hekima zake ukaamua kumpa kazi huyu mkenya.

Swali:

1. Je sheria za ajira zinasemaje juu ya ajira zinazoweza kujazwa na watanzania kujazwa na "wageni"?

2. Je kuna namna ambavyo naweza kujenga hoja na kuushurutisha utawala hapa ofisini kwangu kusitisha ajira ya huyu mkenya na kuhakikisha mtanzania mwenye sifa (kielimu na kiutendaji) anapewa hiyo kazi?

Binafsi kitendo hiki kimenikera sana na ningependa kuwa tofauti kwa kujaribu kurekebisha jambo hili hapa ofisini kwangu nikitumaini na wengine wakafuata hivyo na tukawa watu wa maendo zaidi kuliko maneno / majadiliano.

Angalizo:
Kama hamna njia ambaya ninaweza kurekebisha hali hii maadam imekwisha tokea naomba mnisaidie naweza kufanya nini ili hali hii isitoke kwa ajira nyingine hapa ofisini kwangu.

Natanguliza shukurani

Nyau


Kabla hatujakusaidia nini ufanye, tuambie mweye kampuni ni local investor au foreigner?
If foreigner from where!

Njimba
 
Hapa ofisini kwangu menejimenti imeajiri afisa utawala (senior administrator) mkenya. Huyu bwana kaanza kazi jana.

Hili jambo limenikera sana kwa maana ninajua kuwa kuna watanzania wa kutosha wenye sifa (kielimu na kiutendaji) ambao wangeweza kujaza nafasi hiyo.

Wakati tangazo la nafasi ya kazi lilipotoka magazetini, watu mbali mbali waliomba hiyo kazi. Usaili ulifanyika na utawala katika hekima zake ukaamua kumpa kazi huyu mkenya.

Swali:

1. Je sheria za ajira zinasemaje juu ya ajira zinazoweza kujazwa na watanzania kujazwa na "wageni"?

2. Je kuna namna ambavyo naweza kujenga hoja na kuushurutisha utawala hapa ofisini kwangu kusitisha ajira ya huyu mkenya na kuhakikisha mtanzania mwenye sifa (kielimu na kiutendaji) anapewa hiyo kazi?

Binafsi kitendo hiki kimenikera sana na ningependa kuwa tofauti kwa kujaribu kurekebisha jambo hili hapa ofisini kwangu nikitumaini na wengine wakafuata hivyo na tukawa watu wa maendo zaidi kuliko maneno / majadiliano.

Angalizo:
Kama hamna njia ambaya ninaweza kurekebisha hali hii maadam imekwisha tokea naomba mnisaidie naweza kufanya nini ili hali hii isitoke kwa ajira nyingine hapa ofisini kwangu.

Natanguliza shukurani

Nyau

EAC.... Tunawafungulia waingie... ilhali nasi tumelala fofofo!!!
 
Labda waunde EWURA YAKUDHIBITHI AJIRA KWA FOREIGNER!! Have'nt see wachina kama kawa in the city??
 
Labda waunde EWURA YAKUDHIBITHI AJIRA KWA FOREIGNER!! Have'nt see wachina kama kawa in the city??

EWURA?? Hapana bana, hawa jamaa chakachua imewashinda sasa tukiunda lichombo kama hilo tena itakuwa ni ufisadi juu ya ufedhuli.

Hadi sasa kuna immigration dept., Wizara ya kazi na ajira, TIC na mazaga zaga mengine meeengi lakini bado tu wabangladesh, wafilipino, wakenya, wachina na kila aina ya raia wa kigeni wamejaa nchini kuanzia kwenye meli za uvuvi na abiria(mf.Azam Marine-wafilipino wamejazana), mahotelini na kwenye mabenki ndipo wakenya wanatamba, viwandani kumejaa wahindi, wapakistani, walebanese n.k, ukienda migodini ndio usiseme kabisaa, funga kazi kariakoo wachina wanatamba kila nyumba. Watanzania tumelala fofofofofofofofo................
siku tukiamka, kama cameroun jana!!
 
Pole ndugu NYAU,
Hata mimi hiki kitendo kinanikera sana, Nafanya kazi ktk Mojawapo ya Migodi ya hapa nchini lakini kuna EXPERT wengi sana na hawana chochote kichwani cha ajabu baadhi ya wengine wanadiriki kuja kukuuliza kuwasaidia baadhi ya kazi na hakuna wanachotuzidi sisi, Nenda kwenye malipo ni kufuru tupu humkaribii analipwa zaidi ya mishahara yako ya miaka miwili. Hao wachina, wafilipino ndo usiombe kabisa wanaajiriwa kama madereva na tuna vyuo vingi kila siku vitoa madereva wengi mitaani.
Kwa huyu Mkenya hayo ndo matunda ya mchakato wa jumuiya ya Africa Mashariki na huu ni mwanzo watakuja wengi kutunyang'anya kazi zetu.
Mimi nafikiri tugeuke zimbabwe sasa.
 
Kama alivyosema Mwita Maranya hili ni suala la kushughulikiwa na Wizara ya Kazi na Wizara ya Uhamiaji ambazo zinahusika katika kutoa kibali kwa kuajiriwa mgeni katika nafasi za kazi. Lakini ubaya wa Tanzania hela inatembea na sheria haifuatwi. Tutakuja kujikuta siku moja utabiri wa Mwalimu Nyerere umetimia kuwa tumekuwa kama Wahindi wekundu walivyojikuta Marekani. Nchi yao lakini inamilikiwa na wageni.
 
Hili suala ni gumu. Mi kwanza ningetaka kujua hizo sera na sheria zilizopo zinasemeje.

Kusema tu kazi wasipewe wageni nadhani si sahihi maana kuna waTz wengi nje ya nchi wanafanya kazi na wenyeji wao hawapati hizo ajira.

Mi nadhani tatizo kubwa hapa ni suala la kimuundo zaidi. Kama serikali yetu kila siku inavyojibidiisha kuwakabidhi wageni uchumi wetu kwa kisingizio cha uwekezaji, hali itazidi kuwa mbaya zaidi. Suala la msingi lilikuwa ni serikali kuacha hii akili matope ya kuwapa wageni wawekeze kwene kila kitu. Huwezi ukamruhusu mtu awekeze kwa 100% halafu ukamdhibiti kwene kuajiri, atakuona kichaa..maana atakuuliza unapata wapi nguvu ya kunipangia staff wangu wakati hukuwekeza hata thumni?

Pia kuna suala la udhibiti hafifu, hili tu si kwa uhamiaji na vibali vyao vya ukazi bali kila kona kila taasisi watu wanalalamika juu ya kutokuwajibika kwa vyombo na mamlaka husika.
 
Hili suala ni gumu. Mi kwanza ningetaka kujua hizo sera na sheria zilizopo zinasemeje.

Kusema tu kazi wasipewe wageni nadhani si sahihi maana kuna waTz wengi nje ya nchi wanafanya kazi na wenyeji wao hawapati hizo ajira.

Mi nadhani tatizo kubwa hapa ni suala la kimuundo zaidi. Kama serikali yetu kila siku inavyojibidiisha kuwakabidhi wageni uchumi wetu kwa kisingizio cha uwekezaji, hali itazidi kuwa mbaya zaidi. Suala la msingi lilikuwa ni serikali kuacha hii akili matope ya kuwapa wageni wawekeze kwene kila kitu. Huwezi ukamruhusu mtu awekeze kwa 100% halafu ukamdhibiti kwene kuajiri, atakuona kichaa..maana atakuuliza unapata wapi nguvu ya kunipangia staff wangu wakati hukuwekeza hata thumni?

Pia kuna suala la udhibiti hafifu, hili tu si kwa uhamiaji na vibali vyao vya ukazi bali kila kona kila taasisi watu wanalalamika juu ya kutokuwajibika kwa vyombo na mamlaka husika.

Hayo yote ni sahihi mkuu. Lakini hatuwezi kuacha hivyo hivyo, lazima tuchukue hatua. Ni kufuatilia Uhamiaji na Wizara ya Kazi. Mimi bahati mbaya sijakutana na hawa watu unwanted illegal, mitaa yangu nakutana na walimu kutoka Uganda, nawaacha kwa vile ni walimu, mnajua wenyewe kazi za ualimu tulivyozinyanyapaa toka huko nyuma na sasa inakula kwetu.

Siwezi kufukuzisha Mwalimu wala daktari (the real ones) ila wengine patachimbika. Kama kuna mtu ana hao watu tusiowahitaji ani PM nitimize wajibu wangu kama raia mwema! Hatuhitaji afisa utawala wala mhasibu kutoka nchi jirani katika nji hii!

Kuna wachina wanatengenezea magodoro nyumbani (kiwanda kidogo), wamepanga karibu na mtaa wangu..will follow up nijue kama wanalipa kodi au wako kwenye regime gani. Maana minimum ya foreigner investor ni USD 300,000, sasa siju wanazitimiza au namna gani.
 
Serikali imetahadharishwa kuwa makini na wimbi la wageni, hususan kutoka Bara Asia, ambao wamekuwa wakiingia nchini kinyemala na kisha kupora ajira za Watanzania.
Akichangia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mbunge wa Viti maalum (CCM), Riziki Lulida, alidai kwamba anazo habari za Waasia, wengine wakiwa hawajaingia nchini kihalali, kufanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania.
Alisema tabia ya umakini mdogo wa serikali, umesababisha wawekezaji wengi kuigeuza Tanzania kama shamba la bibi ambapo huja kuchuma huku wananchi wakiwa hawafaidiki na uwekezaji huo.
Rulida alitahadharisha kwamba kutokana na mkoa wa Lindi ambao umepata hadhi ya manispaa na miundombinu yake imeimarika, hasa baada ya barabara zake kupitika na daraja la umoja kufunguliwa, wawekezaji wengi, baadhi wakiwa wababaishaji, wameelekeza huko pua zao.
“Lindi sasa kila mtu anakutaka. Kuna ardhi nzuri na yenye rutuba na kuna madini na hivyo wawakezaji wababaishaji wameshaanza kupakimbilia. Lazima serikali iwe macho,” alisema. Mbunge wa Viti Maaulum (Chadema), Halima Mdee, aliitaka CCM kukiri kwamba imeshindwa kutekeleza sehemu kubwa ya ilani yake na hivyo kukiri hilo na kuwaomba radhi Watanzania.
Alisema Ilani si sera, ni ahadi kwa wapiga kura, hivyo lazima upinzani uitumie kuona kama imetekelezwa kwani wananchi waliichagua CCM wakiamini kwamba watafanyiwa kama yaliyomo kwenye ahadi hiyo. Alitoa mfano kwamba wakati ilani hiyo inaahidi kwamba ifikapo mwaka 2010 kilimo kitakuwa kimepanda kwa asilimia 10, takwimu zinaonyesha kwamba kimepanda kwa asilimia tatu na heri hata mwaka uliopita ambapo kilipanda kwa asilimia 4.
Wabunge katika michango yao jana waliitaka serikali kuchukua hatua zaidi katika kuwabana wabadhirifu wa mali ya umma, ikiwa ni pamoja na kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima.
Mbunge wa Chunya (CCM) Victor Mwambalasa, aliitaka serikali kutimiza kauli zake kwa kuacha kununua magari ya bei mbaya yanayofikia hadi Sh. milioni 200.
Mdee alizungumzia sera ya ubinafishaji kwamba inatakiwa kuangaliwa upya kwani kati makampuni zaidi ya 300 yaliyosajiliwa, 60 yamemekaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG) na kugundua kwamba ni 12 tu ndio yanayofanya kazi.



CHANZO: NIPASHE
 
Wabunge nao ndio wanaochangia mambo haya. Kwa nini wasitoe miswada ya kulinda ajira za watanzania? wanakuwa kama wapiga debe ambao wanaongea kwa pembeni. Ni swala la bunge kutunga shrai imara zinazolonda ajira za watanzania. sasa hivi zaidi ya nusu za kazi zote katika makampuni ya wanaoitwa "wawekezaji," ambao hata hawalipi kodi za nchi, zimechukuliwa na watu wa nje. Watanzania wanapewa kazi za hovyo hovyo tu wakati zile nzuri zote zinrusha nje ya dirisha. wabunge wetu hatoa sheria yoyote inayolinda ajira, leo hii uchaguzi unakaribia eti ndipo wanaibuka na filimbi zisizokuwa na lolote..
 
Wabunge nao ndio wanaochangia mambo haya. Kwa nini wasitoe miswada ya kulinda ajira za watanzania? wanakuwa kama wapiga debe ambao wanaongea kwa pembeni. Ni swala la bunge kutunga shrai imara zinazolonda ajira za watanzania. sasa hivi zaidi ya nusu za kazi zote katika makampuni ya wanaoitwa "wawekezaji," ambao hata hawalipi kodi za nchi, zimechukuliwa na watu wa nje. Watanzania wanapewa kazi za hovyo hovyo tu wakati zile nzuri zote zinrusha nje ya dirisha. wabunge wetu hatoa sheria yoyote inayolinda ajira, leo hii uchaguzi unakaribia eti ndipo wanaibuka na filimbi zisizokuwa na lolote..


Wanayasema haya kwa kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi. Kwani hili la ajira za Watanzania kuvamiwa na wageni toka nchi mbali mbali halikuanza leo lipo tangu enzi za Mkapa. Wapo bungeni kulinda maslahi yao tu vinginevyo wangeishapeleka puta Serikali katika swala hili miaka mingi iliyopita. Wachina, Wahindi wa kutoka India, Bangladesh, Pakistan, na Waafrika kutoka nchi mbali mbali wanazidi kumiminika nchini kila kukicha na wengi hawa wanachukua ajira za wazawa au kufanya biashara ambazo hastahili kufanywa na wageni. Pale uhamiaji sijui kwa kweli wanafanya kazi gani maana mipaka yetu inakuwa kama haina mwenyewe na wahamiaji haramu wanapeta tu na kuendelea kuitana kwa wingi.
 
[QUOTE=Kanyabwoya;955423]Hayo yote ni sahihi mkuu. Lakini hatuwezi kuacha hivyo hivyo, lazima tuchukue hatua. Ni kufuatilia Uhamiaji na Wizara ya Kazi. Mimi bahati mbaya sijakutana na hawa watu unwanted illegal, mitaa yangu nakutana na walimu kutoka Uganda, nawaacha kwa vile ni walimu, mnajua wenyewe kazi za ualimu tulivyozinyanyapaa toka huko nyuma na sasa inakula kwetu. Siwezi kufukuzisha Mwalimu wala daktari (the real ones) ila wengine patachimbika. Kama kuna mtu ana hao watu tusiowahitaji ani PM nitimize wajibu wangu kama raia mwema! Hatuhitaji afisa utawala wala mhasibu kutoka nchi jirani katika nji hii! Kuna wachina wanatengenezea magodoro nyumbani (kiwanda kidogo), wamepanga karibu na mtaa wangu..will follow up nijue kama wanalipa kodi au wako kwenye regime gani. Maana minimum ya foreigner investor ni USD 300,000, sasa siju wanazitimiza au namna gani.[/QUOTE]

kanyabwoya, Hawa watu si wa kutafuta ni wa kufikia tu ila tunaowahifadhi ni sisi wenyewe, mimi nilitolea mfano wa "Mining Industry" kuwa tuna Wafilipino kibao kwenye mining wanafanya kazi za udereva wakati tunavyuo vinamwaga kila siku mitaani, Hawa watu wanajulikana na tunao, tukubali kuwa ofisi zetu za uhamiaji hazifanyi kazi ipasavyo, Kwani hatuwezi kuwafundisha wazawa wafanye kazi hizi mpaka expert
anayelipwa pesa nyingi ya karibu wazawa 10???.
 
Wanayasema haya kwa kuwa huu ni mwaka wa uchaguzi. Kwani hili la ajira za Watanzania kuvamiwa na wageni toka nchi mbali mbali halikuanza leo lipo tangu enzi za Mkapa. Wapo bungeni kulinda maslahi yao tu vinginevyo wangeishapeleka puta Serikali katika swala hili miaka mingi iliyopita. Wachina, Wahindi wa kutoka India, Bangladesh, Pakistan, na Waafrika kutoka nchi mbali mbali wanazidi kumiminika nchini kila kukicha na wengi hawa wanachukua ajira za wazawa au kufanya biashara ambazo hastahili kufanywa na wageni. Pale uhamiaji sijui kwa kweli wanafanya kazi gani maana mipaka yetu inakuwa kama haina mwenyewe na wahamiaji haramu wanapeta tu na kuendelea kuitana kwa wingi.

Nakukubalia kuwa Serikali yetu haiwafatilii hao Wageni toka Asia kwa sababu wengi waohao wa Asia wanatowa pesa kuwapa wakubwa wa Serikali mpaka hii Serikali iliyokuwepo isiwepo tena katika uongozi ndipo hayo matatizo yataondoka. Na kwa juhudi za sisi Wenyewe Wananchi kuwachaguwa Viongozi bora sio Mafisadi.
 
Wabunge nao ndio wanaochangia mambo haya. Kwa nini wasitoe miswada ya kulinda ajira za watanzania? wanakuwa kama wapiga debe ambao wanaongea kwa pembeni. Ni swala la bunge kutunga shrai imara zinazolonda ajira za watanzania. sasa hivi zaidi ya nusu za kazi zote katika makampuni ya wanaoitwa "wawekezaji," ambao hata hawalipi kodi za nchi, zimechukuliwa na watu wa nje. Watanzania wanapewa kazi za hovyo hovyo tu wakati zile nzuri zote zinrusha nje ya dirisha. wabunge wetu hatoa sheria yoyote inayolinda ajira, leo hii uchaguzi unakaribia eti ndipo wanaibuka na filimbi zisizokuwa na lolote..
Kichuguu,
Sheria za kulinda ajira ya Watanzania zipo. Ni kazi ya Kapuya kuhakikisha kuwa zinafuatwa na kazi ya Masha kuhakikisha kuwa wageni wasio halali hawapewi vibali vya kuishi nchini na kufanya kazi. Tumeshafahamu mchawi wetu ni nani.
 
leave the kenyan alone. alitia bidii na akapata kazi sasa wewe chuki ya nini? dont be a hater just raise your hustle to the next level and mybe then u will get a better job too.

as i always say, this is a dog eat dog world. the weak lose and only the fittest and the strongest survive. which one are you????

you tanzanians need to toughen up and compete with others instead of being a bunch of whinning and crying babies, hating and blaming kenyans and other foreigners for all that is wrong with your country. GROW THE HELL UP!!!!

 
leave the kenyan alone. alitia bidii na akapata kazi sasa wewe chuki ya nini? dont be a hater just raise your hustle to the next level and mybe then u will get a better job too.

as i always say, this is a dog eat dog world. the weak lose and only the fittest and the strongest survive. which one are you????

you tanzanians need to toughen up and compete with others instead of being a bunch of whinning and crying babies, hating and blaming kenyans and other foreigners for all that is wrong with your country. GROW THE HELL UP!!!!


DEAR NYANG'AU,

Tz is OUR country..the country of our forefathers and grandgrandgrand children, na tunayo haki ya kusema CHOCHOTE kuhus NCHI YETU na hamna nyang'au mwenye haki ya kutuambia VINGINEVYO.

Whether madai yetu ni ya haki au si ya haki, NCHI NI YETU NA TUTAFANYA VYOVYOTE VILE KUHUSU NCHI YETU!!
 
ukienda bandarini kurasini kuna kiwanda cha METL, wahindi wageni wanapewa kazi na hawana vibali wakati waswahili ni maday worker wanapanga foleni asubuhi ili kujua wana kazi au la. mtu anakuwa dayworker miaka mitatu.
halafu huyu jamaa ndio mbunge na anajidai mzalendo sijui uzalendo wake uko wapi
 
Back
Top Bottom