Jinsi Wachina wanavyopata viungo vya binadamu kwa ajili ya upandikizaji

Papa Mobimba

JF-Expert Member
Dec 6, 2018
1,153
1,359
Siku za hivi karibuni nimekuwa nikisoma kitabu kinaitwa The Slaughter: Mass Killings, Organ Harvesting, and China's Secret Solution to Its Dissident Problem. Kitabu hiki kimeandikwa na bwana Ethan Gutmann huyu ni mwandishi wa habari za uchunguzi. Kitabu hiki alikitoa mwaka mmoja baada ya ripoti nyingine iliyochapishwa na David Mantis pamoja na David Kilgour.

Mahitaji ya viungo vya binadamu nchini China yako juu sana kulinganisha na nchi nyingine pengine hii inatokana na taifa hilo kuwa na idadi kubwa ya watu. Licha ya kwamba mahitaji ya kupata viungo ni makubwa sana lakini muda wa kusubiri kupata kiungo ni mfupi kulinganisha na nchi nyingine. Kwa mfano nchini Marekani utalazamika kusubiri kupata kiungo kwa muda wa siku 1865 (miaka sita), nchini Uingereza ni siku 1095 lakini China ni siku 15 tu.

Je viungo hivyo vinatoka wapi
Wote watatu wanakubaliana kuwa idadi kubwa ya viungo vya binadamu inapatikana kwa njia isiyo kuwa halali. Viungo vingi vinavyuna kwa wafungwa waliohukumiwa kifo kutokana na makosa makubwa hasa yako uhaini, madawa ya kulevya, ujambazi.

Wachunguzi hawa wanaeleza kuwa muda mfupi kabla mtu hajapelekwa kunyongwa huchomwa sindano ya kuzuia damu kuganda. Timu ya Madaktari inakuwa iko tayari. Mara nyingi hawa ni Madaktari wenye uzoefu mkubwa pamoja na spidi ya hali ya juu.

"Baada ya mtu kupigwa risasi, mwili huchukuliwa haraka haraka na kupelekwa katika magari maalumu ambako upasuaji wa kuvuna viungo hufanyika", taarifa zinasema. Ili kuhakikisha viungo haviharibiki madaktari hutumia dakika 20 mpaka 30 kuondoa viungo vyote wanavyohitaji.

Tuhuma kama hizo zimetolewa katika nchi ya India. Ambako huaminika mania ya watu husafirishwa na kuuwa kwa ajili ya viungo vyao. Shirika la Afya duniani linapiga marufuku uvunaji wa viungo usiozingatia haki za binadamu.

Katika nchi nyingi viungo vya binadamu ambavyo hupandikizwa ni pamoja na figo, moyo, maini, ngozi ya jicho, uboho wa kwenye mifupa, mapafu na kadhalika.

Miaka michache iliyopita Tanzania imeanza kutoa huduma za upandikizaji figo. Ni muhimu kuweka sheria mahususi zinakazosimamia masuala ya upatikanaji wa viungo pamoja na matumizi yake.
 
I have a very dreadful story about human body parts harvesting... Huko nje ni kawaida sana na ni biashara haramu inayolipa sana... Sasa hivi soko limegeukia Africa hasa kwa vijana wa kiume wenye nguvu na mabinti walimbwende wasiotumia madawa kung'arisha ngozi zao
 
Huko mochwari kuna siri nyingi sana nzito.
Ukibahatika kufika mochwari mida ya usiku, kuna magari yanapaki usiku usiku wahusika wanaingia ndani na kutoka na vifurushi.

Viuongo vya binadamu imekuwa biashara inayolipa sana miaka hii.
 
Siku za hivi karibuni nimekuwa nikisoma kitabu kinaitwa The Slaughter: Mass Killings, Organ Harvesting, and China's Secret Solution to Its Dissident Problem. Kitabu hiki kimeandikwa na bwana Ethan Gutmann huyu ni mwandishi wa habari za uchunguzi. Kitabu hiki alikitoa mwaka mmoja baada ya ripoti nyingine iliyochapishwa na David Mantis pamoja na David Kilgour.

Mahitaji ya viungo vya binadamu nchini China yako juu sana kulinganisha na nchi nyingine pengine hii inatokana na taifa hilo kuwa na idadi kubwa ya watu. Licha ya kwamba mahitaji ya kupata viungo ni makubwa sana lakini muda wa kusubiri kupata kiungo ni mfupi kulinganisha na nchi nyingine. Kwa mfano nchini Marekani utalazamika kusubiri kupata kiungo kwa muda wa siku 1865 (miaka sita), nchini Uingereza ni siku 1095 lakini China ni siku 15 tu.

Je viungo hivyo vinatoka wapi
Wote watatu wanakubaliana kuwa idadi kubwa ya viungo vya binadamu inapatikana kwa njia isiyo kuwa halali. Viungo vingi vinavyuna kwa wafungwa waliohukumiwa kifo kutokana na makosa makubwa hasa yako uhaini, madawa ya kulevya, ujambazi.

Wachunguzi hawa wanaeleza kuwa muda mfupi kabla mtu hajapelekwa kunyongwa huchomwa sindano ya kuzuia damu kuganda. Timu ya Madaktari inakuwa iko tayari. Mara nyingi hawa ni Madaktari wenye uzoefu mkubwa pamoja na spidi ya hali ya juu.

"Baada ya mtu kupigwa risasi, mwili huchukuliwa haraka haraka na kupelekwa katika magari maalumu ambako upasuaji wa kuvuna viungo hufanyika", taarifa zinasema. Ili kuhakikisha viungo haviharibiki madaktari hutumia dakika 20 mpaka 30 kuondoa viungo vyote wanavyohitaji.

Tuhuma kama hizo zimetolewa katika nchi ya India. Ambako huaminika mania ya watu husafirishwa na kuuwa kwa ajili ya viungo vyao. Shirika la Afya duniani linapiga marufuku uvunaji wa viungo usiozingatia haki za binadamu.

Katika nchi nyingi viungo vya binadamu ambavyo hupandikizwa ni pamoja na figo, moyo, maini, ngozi ya jicho, uboho wa kwenye mifupa, mapafu na kadhalika.

Miaka michache iliyopita Tanzania imeanza kutoa huduma za upandikizaji vifo. Ni muhimu kuweka sheria mahususi zinakazosimamia masuala ya upatikanaji wa viungo pamoja na matumizi yake.
Hapo mwishoni nimeshindwa kukuelewa. Tanzania inatoaje hiyo huduma ya upandikizaji vifo?
 
Hii biashara ni kinyume na haki za binadamu. Sababu binadamu kazaliwa kwa ajili ya kuishi na si kufa...

Soon itaanza kushamiri hapa nchini na wahanga wakubwa ni wale maskini ambao watauza baadhi ya viungo vyao kujipatia pesa za kujikimu na maisha magumu.

Naomba yasifike huku kwetu.
 
Hii biashara ni kinyume na haki za binadamu. Sababu binadamu kazaliwa kwa ajili ya kuishi na si kufa...

Soon itaanza kushamiri hapa nchini na wahanga wakubwa ni wale maskini ambao watauza baadhi ya viungo vyao kujipatia pesa za kujikimu na maisha magumu.

Naomba yasifike huku kwetu.
Kwa sasa hufanyika kwa kile kinachoitwa "kujitolea figo" au "kujitolea moyo"

Sio kwamba haijafika, ila inafanyika sana tu sema kwa kificho.
 
Hii biashara ni kinyume na haki za binadamu. Sababu binadamu kazaliwa kwa ajili ya kuishi na si kufa...

Soon itaanza kushamiri hapa nchini na wahanga wakubwa ni wale maskini ambao watauza baadhi ya viungo vyao kujipatia pesa za kujikimu na maisha magumu.

Naomba yasifike huku kwetu.
Yasifike?
Mbona yapo sana
 
Huko mochwari kuna siri nyingi sana nzito.
Ukibahatika kufika mochwari mida ya usiku, kuna magari yanapaki usiku usiku wahusika wanaingia ndani na kutoka na vifurushi.

Viuongo vya binadamu imekuwa biashara inayolipa sana miaka hii.
Mkuu, sasa Mochwari mbona tayari mwili unakuwa umekaa muda mrefu na tayari kiungo husika kimekufa rasmi, kinawezaje kufanya kazi tena.
 
Motuary kazi kweli , na washirikina nao wapo kazini
Na hivi vituo vya kulea watoto yatima na wanao ishi katika mazingira magumu pia vina husishwa sana na uvunaji wa viungo. Mtu anaanzishaje kituo cha kulelea watoto yatima wakati hakimlipi!!! Au anapata misaada kutoka nje ya nchi, lakini je hawa wafadhiri wao wananufaika vipi?

Mtoto yatima ambae kwa kiasi kikubwa jamii haifahamu uwepo wake pale kituoni, akichinjwa nani atajua?
 
Hii biashara ni kinyume na haki za binadamu. Sababu binadamu kazaliwa kwa ajili ya kuishi na si kufa...

Soon itaanza kushamiri hapa nchini na wahanga wakubwa ni wale maskini ambao watauza baadhi ya viungo vyao kujipatia pesa za kujikimu na maisha magumu.

Naomba yasifike huku kwetu.
Isipokuwepo sheria mahususi,
 
wanafanya poa kuliko mtu anyongwe aoze na viungo bora vikatumike tena hawa watu wako makini sana
 
siwezi pata kazi mochwarii.....inaonekana kunapesa sana, ila kama kweli kuna pesa nawajua watumishi wawili wa mochwari ya arusha na kilimanjaro mbona maisha yao niyachini sana kama kweli kunabiashara hiyo, nazani wangekuwa matajiri.tuache story za vijiweni
 
Back
Top Bottom