msigazi
JF-Expert Member
- Sep 1, 2017
- 456
- 330
JF nawasalimia kupitia jina la jamhuri,
Nachukua nafasi hii kuleta nasaha zangu kwenu ikiwezekana serikali izipate.
Kuna jambo ambalo nimewaza ni kwanini vitu huwa vinapanda bei bila mpangilio nikagundua kuwa kuna shida kwenye wasimamizi wa bishara.
Kwenye wizara ya viwanda inatakiwa ipitie upya ufuatiliaji wa bidhaa kama wanavyofanya kwenye bidhaa bandia wanatakiwa waangalie hasa masoko.
Natoa mfano
Sukari ya kagera sugar inazalishwa Kagera ajabu ni kuwa bei ya sukari kwa mikoa ya kanda ya ziwa ni bei juu sababu inayosababisha ni kusafirishwa mara mbili. Kupelekwa Dar kwa ajili ya uchapishaji wa TBS nk.
Kwanini wasije moja kwa moja kiwandani wakaweka hizo TBS zao? Na kitu kingine vifaa vya ujenzi viko bei juu mno. Dar unaweza kukuta mfuko wa siment Tsh. 15,000/= lakini huku mikoani tunalia bei ziko juu mno nondo siment na vifaa vyote vya ujenzi.
Kama kuna kitu ambacho serikali wanajisahau ni kuwaachia wawekezaji kupanga bei za vitu. Bila serikali kuweka bei elekezi hasa upande wa vifaa vya ujenzi, mafuta ya kula, sukari nk.
Naiomba serikali iliangalie suala hili kwa jicho la tatu.
Asante.
Nachukua nafasi hii kuleta nasaha zangu kwenu ikiwezekana serikali izipate.
Kuna jambo ambalo nimewaza ni kwanini vitu huwa vinapanda bei bila mpangilio nikagundua kuwa kuna shida kwenye wasimamizi wa bishara.
Kwenye wizara ya viwanda inatakiwa ipitie upya ufuatiliaji wa bidhaa kama wanavyofanya kwenye bidhaa bandia wanatakiwa waangalie hasa masoko.
Natoa mfano
Sukari ya kagera sugar inazalishwa Kagera ajabu ni kuwa bei ya sukari kwa mikoa ya kanda ya ziwa ni bei juu sababu inayosababisha ni kusafirishwa mara mbili. Kupelekwa Dar kwa ajili ya uchapishaji wa TBS nk.
Kwanini wasije moja kwa moja kiwandani wakaweka hizo TBS zao? Na kitu kingine vifaa vya ujenzi viko bei juu mno. Dar unaweza kukuta mfuko wa siment Tsh. 15,000/= lakini huku mikoani tunalia bei ziko juu mno nondo siment na vifaa vyote vya ujenzi.
Kama kuna kitu ambacho serikali wanajisahau ni kuwaachia wawekezaji kupanga bei za vitu. Bila serikali kuweka bei elekezi hasa upande wa vifaa vya ujenzi, mafuta ya kula, sukari nk.
Naiomba serikali iliangalie suala hili kwa jicho la tatu.
Asante.