KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 18,126
- 32,812
Habari ndugu wapendwa na natumaini sote tu wazima wa afya na walio na mitihani ya maradhi au changamoto mbali mbali Mungu awapiganie ili sote tuishi kwa raha na kukiri utukufu wa Mungu.
Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.
Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.
Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.
Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.
Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.
Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.
Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.
Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.
Nimeamua kuileta habari hii ambayo ilinitokea mimi mwenyewe ili iwe kama funzo kwa wengine wenye mioyo ya kusaidia wanadamu wenzao wenye uhitaji lakini badala yake wanakutana na matapeli.
Nakumbuka siku fulani miezi kadhaa nyuma nilipanda dala dala kituo cha Mwembechai nikiwa naelekea Sinza, pembeni yangu alikuwa ameketi kijana mmoja wa makamo hivi huku mkono wake wa kulia akiwa ameushikilia huku akigugumia kwa maumivu makali.
Kilio chake kilivuta hisia zangu kama mwanadamu na kutaka kujua zaidi alipatwa na jambo gani, basi katika maelezo yake machache na alinifunulia kile kiganja kilichokuwa kimevimba kwa kutunga usaha mzito huku akisema kuwa hana msaada wowote nikadhamiria kumsaidia.
Alisema kuwa alikuwa anahitaji kiasi kama 15,000/= ili akapasuliwe ule uvimbe na kusafishwa kidonda. Yeye alisema ni dereva wa magari madogo ya mizigo na maskani yake ni pale Manzese Bakhresa kwa hali hiyo anashindwa kufanya shughuli zake za udereva hivyo kukosa kipato na kupelekea kudhoofu kutokana na lishe duni, pale nilimpatia kiasi kama 20,000/= ili akajitibie na nikampatia mawasiliano yangu ili awe ananipa maendeleo ya kidonda chake na kwa msaada zaidi.
Baada ya pale tukawa tunawasiliana na yule kijana kuhusu maendeleo ya kidonda chake na nikawa kila siku namtumia 7,000/= kwa ajili ya kujikimu huku akijiuguza kidonda chake, baada ya masiku kadhaa nikamuuliza wewe unatokea mkoa gani akaniambia anatokea mkoa wa Tanga. Nikamwambia kwanini nisimpe nauli arudi Tanga kwa wazazi kupumzika akijiuguza taratibu mpaka atakapotengemaa ndipo arejee mjini maana kwa mujibu wa maelezo yake ni kwamba hata pakulala hana maana alifukuzwa baada ya kushindwa kulipia pango, basi tukakubaliana kesho yake ajiandae ili nimtumie nauli ili aende nyumbani kupumzika, kesho yake nikamtumia 50,000/= nikiamini itamtosha nauli ya Tanga na hela kidogo ya kujikimu.
Baada ya masaa kama 7 nikiamini ameshaondoka mjini kwenda Tanga, akanipigia Simu kwa namba ya mtu mwingine maana yeye hakuwa na simu, aliniambia kuwa ameshafika Stendi Kange lakini amepungukiwa na nauli maana amebakiwa na 5,000/= hivyo mpaka afike kwao hiyo hela haitoshi. Kuanzia hapo akili yangu ikawa na mashaka kwa kuwa Tanga napafahamu inawezekana vipi kutoka Dar mpaka Tanga atumie 45,000/= ? Sikumtumia hela nilimwambia nipo bize kidogo.
Baada kama dakika 10 nikatumia namba nyingine kumpigia yule aliyenipigia nilimpa msichana aongee naye ili nijue yupo wapi, ikagundua kuwa yule alikuwa Manzese darajani na hakuwa Tanga, nikawapigia watu waliokuwa wanampa simu niongee naye na nilipokuwa nawatumia kumtumia hela, wote wakanithibitishia kuwa yule jamaa yupo Pale pale Dar na alikuwa ni muokota makopo ya plastiki maarufu na pia mtumiaji mkubwa dawa za kulevya hata wakati namtumia fedha walijua mimi ni ndugu yake na mara nyingi anautumia mkono wake uliojaa usaha kujipatia kipato huo ndio ukawa mwisho wa mimi na yeye, na yote niliyomsaidia nikamwachia Mungu.
Nb;
Tuwe macho na tunaodhania wanahitaji misaada.