palsa
JF-Expert Member
- Apr 24, 2011
- 1,326
- 1,680
Mimi nilikutana na mzee maeneo ya kanisani magomeni na yeye akainiomba nauli..wakati narudi namwona kajibanza sehemu anahesabu hela nyingi🤣Kuna siku moja alinisimamisha mzee mmoja, akaniambia mwanangu nimetoka hospitali naomba nauli nipande bajaji kwa hali yangu siwezi kutembea nikampa. Wakati anaondoka nikajilaumu kwanini nimempa hela ya bajaji wakati obvious hela ya kula atakuwa hana naye ni mgonjwa.
Namfata chap kumuongezea fedha ya chakula, kwa mbali namuona bajaji anazipita bila kupanda mpaka akazimaliza. Mbele akamsimamisha mtu mwingine anamuomba, niliumia.