Jinsi nilivyotaka kutapeliwa kwenye Crypto-Currency: Chukua Tahadhari, itakusaidia

Heaven Seeker

JF-Expert Member
May 12, 2017
478
1,047
Wakuu,

Kwanza kabisa, ieleweke wazi kuwa sipo hapa kupinga kuhusu Crypto-Currency trading, Forex Trading na jamii zote za mambo kama haya. Mie mwenyewe naendelea kujifunza ili nijue kwa undani na huenda siku moja nikawa expert wa hizi mambo. Lengo kubwa ni ku-share utapeli niliokumbana nao kwa baadhi ya matapeli wanaotaka pesa kirahisi ili kuokoa hata mtu mmoja asije akatapeliwa.

Sasa buana, mimi ni member wa Clubhouse, kama ujuavyo Clubhouse unaweza ku-connect na Dunia kwa haraka zaidi, nadhani ni kuliko Social media yoyote ile. Ni suala tu la wewe kuchagua Club (room) ya nchi gani unataka kuwa member na ukawa connected huko kufuatilia kinachojiri.

Sasa moja ya malengo ya mwaka huu niliyojiwekea ni kujifunza kwa undani ili nijue vizuri haya masuala ya crypto et al. Maana nimekuwa nikisikia stories nyingi sana na kwakuwa katika majukumu yangu nabakiwa na muda, nimeona si vibaya ikawa ni moja ya jambo naloweza kujifunza kupata knowldge. Ili nisiwe mwepesi wa kupinga pinga kila jambo kumbe sina taarifa za kutosha. Kwahiyo ili kutimiza lengo, nikawa nimejiunga Clubhouse kwenye groups (rooms) zinazoelezea masuala hayo kutoka nchi za Marekani na Uingereza. Nilikuwa nimeshafuatilia kidogo Youtube na Twitter kwenye space kutoka kwa wanaofahamu na kufanya mambo hayo kwa wadau wa Bongo land. Nikaona si vibaya kupanua wigo wa kujifunza zaidi ndio maana nikajiunga na hizo rooms za Uingereza na Marekani.

Kwahiyo kwenye profile yangu nikaandika mbwembwe za hapa na pale kama ilivyo profiles/bio za wengine. Members wa Clubhouse watakuwa wameelewa nachomaanisha. Miomngoni mwa niliyoandika kwenye profile/bio ni interests zangu za kujiunga Clubhouse ambapo, pamoja na mambo mengine, nikawa nimeandika kuwa nataka kujifunza zaidi kuhusu Digital business and E-Commerce et al. Ebwana eeeh, kilichojiri sasa... Endelea kufuatilia...

Tangu nimejiunga ni kama wiki 2 hivi, mwanzoni nilikuwa natumia anonymous account ila badae nikaona ngoja niweke real account maana niliona inaweza kuwa fursa ya kukutana na watu potential huku Duniania.

Sakata linaanzia hapa
Kumbe kila nikiingia kusikiliza hayo madini ya Crypto huko kwenye rooms ambazo nipo huwa kuna matapeli wanafanya inspection ya kila member, wanakuwa wanachungulia na kujua wewe una interests gani. Yaani kwa wastani hizo DMs sijui mnaita Backchannels ama kwa lugha rahisi inbox, huwa napokea zisizopungua 3 za hao matapeli kila siku. Imagine nimejiunga rooms za US na UK tu, ingekuwaje ningejiunga na Nchi nyingine wanazozungumza Kiingereza?

SIFA ZAO.
1. Wanakuwa hawana followers wengi na account zao ni mpya.
2. Majina yao yana utata na kwa kiasi kikubwa wanaanadika majina Fake
3. Instagram pages zao zina followers wengi ila ukiangalia posts hazizidi 10. Hii ina maanisha wana-hack accounts za watu kisha wanazitumia kufanya utapeli.
4. Wana lugha flani hivi za kukushawishi tena very professional. Yaani usipokuwa makini unaliwa.

Tuendelee sasa.
Kwahiyo mie mwanzo sikujua kinachoendelea maana sina muda mwingi sana tangu nijiunge. Na kwakuwa nina muda kidogo huku kwa Mabeberu nimeanza ku-adapt hali ya kumuamini mtu kwa haraka na kujaribu kuwa postive. Japo simaamishi kuwa namwamini kila mtu. Kwa mazingira niliyopo kuwaamini watu kwenye hii community nilipo ni kama culture tu. Ni jambo la kawaida. Sijawa exposed sana huko nje kwenye mambo mengi mengi sana kiasi cha kukumbana na kadhia nyingi kiviile. (Najua kuna watakao sema najifanya nimebadilika ama najaribu kuonesha kuwa sie Wabongo siyo waaminifu na siyo positive, ila nia yangu siyo hiyo na hii ni mada nyingine tutaijadili siku nyingine ikihitajika). Kwahiyo mwanzoni sikuwa nime-notice kabisa. Nikawa na-reponds positively.

Naendelea na kisa.

Sasa nikawa nimepokea hizo DMs buana, akaniambia crypto trading inavyokuwa na akasema ana-make pesa nyingi na kwamba watu wengi hawa-make pesa kutokana na sababu kuwa hawana experience yakutosha. Ila yeye anaweza kuniasaidia kufanya trading na nitakuwa nampa commission yake kama 10% hivi ya faida. Nikasema ngoja niendelee kumfuatilia nione wakati huo nikiwa sijamgundua kama ni tapeli. Akasema tubadilishane namba ili tuwasiliane kwa karibu zaidi. Nikawa nimempa buana, si unajua sisi wabongo tulivyo wepesi kuwaamini wazungu. Akawa amenipa namba na nikaona ni ya US. Nilivyocheki instragram profile yake nikakuta amepost mambo hayo ya crypto posts kama 10 hivi na account ina followers wasiopungua 3000.

Kilichoendelea.
Akazungumza swagga nyingi kisha akanambia nifungue account kwenye website flani hivi nilivyoicheki nikaona kweli inahusika na hizo mamboz. Nikafungua kweli. Akanambia kinachofuatia sasa ni ku-fund account yangu kwa USD 500. Nikamwambia sina, akasema naweza kuanza na USD 200. Mwingine alinimbia ataniazima USD 100 mie niweke 200. Duh.! Hapo kwenye kutuma pesa ndio huwa sipo mrahisi kiviiiile. Nikasema ngoja nifanye ka-research kafupi kwanza. Nikaingia Youtube kujua namna gani Scammers wanafanya Scamming kwenye crypto et al. Nikapata hints nyingi nyingi nikaona kuna mojawapo inataka kufanana na kisa changu japo ni tofauti kidogo. Nikavuta pumzi kidogo. Nikatulia makalio kwanza. Nikasema hebu nijipe muda kidogo. Japo alikuwa kama ashafanikiwa kunishawishi maana niliona pesa mbona naweka kwenye profile yangu na situmi mahala? Natapeliwaje sasa.?

Naendelea usichoke.
Sijakaa sawa nikapokea DM kwa tapeli mwingine kwa maelezo hayo hayo. Nikajifanya sijui kinachoendelea na akaaendelea kufunguka na akanipa namba ya simu nikaicheki nikajua ni ya state nyingine huko huko US. Nikapokea DMs tena na tena, yaani kwa wiki nzima mpaka sasa nimepokea DMs kama 15 hivi. Walipofikia watu watatu ndio nikagundua huu ni utapeli tayari. Nikacheeka, nikasema sawa nimejifunza jambo na mie, si mbaya kujua mambo yanayoendelea huku Duniani.

Sifa zao (Nyongeza)
1. Ukimwambia umpigie mzungumze live anakataa, atakwambia sijui yupo tight ofsin na braabraa nyiiingiiiii.
2. Wengine wakishajua unatoka nchi gani, ili uweze kumwamini, anajiunga CLUB (rooms) za nchi yako kabisa. Nilichungulia mmoja wapo nikakuta amejiunga Club za chama kimoja sitakitaja, yaani kajiunga kama rooms 3 hivi za chama hicho. Tena kawa-follow watu prominent kabisa nawajua kama wawili. Tapeli mmoja nimeona yaani kuna a prominet person na yeye kam-follow huyo tapeli. Sasa usipokuwa makini unaliwa kabisa maana unaweza kumwamini kidogo. Nilivyojaribu kumuuliza kama anafahamu kiswahili akasema hapana. Nikamuuliza mbona umejiunga kwenye rooms za Tanzania? Akanambia stori ndeefu, kiufupi akasema eti alikuwa anataka kuja bongo kufanya research kwahiyo akaona aanze ku-connect na wabongo. Duh. Utapeli professional.
3. Utasikia wanakwambia kuwa ukiweka USD 500 ndani ya wiki unapata USD 2500. Ukiweka USD 1000 unapata USD 10,000 kwa wiki. Aisee, yaani simple like that? Kama ingekuwa simple basi kila mtu angekuwa tajiri na watu wasingefanya kazi za kutoa jasho. Sikatai kuwa cypto ama Forex hupati faida, ila siyo kirahisi kihivyo.
4. Mwingine nilivyomwambia kuwa hakuna mtu anaweza kupata faida za namna hiyo, akaja na gear kuwa wao unapata faida ya 30%. Utapeli mtupu.
5. Mwingine anakung'ang'aniza umtumie adress yako, namba za simu. Hapo unaenda kupigwa kuwa makini. Maana huku kwa Mabeberu address ni kitu mojawapo sensitive sana.

Mwisho.
Tapeli mwingine akanambia nifungue wallet kwenye Bitcoin.com, mwingine kwenye Crypto.com. kisha wanakwambia Ku-fund account yako. Baada ya hapo wanasema watakuunganisha na hizo website zao ambazo ni kama brokers, hapo nadhani ndipo wanaenda kukupiga sasa. Kwakuwa sikufikia mwisho, sijui wanakupiga kwa style gani, ila hutumi pesa japo unafanya malipo kwenye account yako uliyofungua kisha baada ya hapo naona wanakuunganisha na links zao ambapo ndio unapigwa sasa.

Wakuu, maelezo yamekuwa mengi sana na sijasema yote ila ili kukatisha maneno nimeona niweza kushea hapa ili kuokoa watu wasije wakatapeliwa. Kuwa makini.
 
Wakuu,

Kwanza kabisa, ieleweke wazi kuwa sipo hapa kupinga kuhusu Crypto-Currency trading, Forex Trading na jamii zote za mambo kama haya. Mie mwenyewe naendelea kujifunza ili nijue kwa undani na huenda siku moja nikawa expert wa hizi mambo. Lengo kubwa ni ku-share utapeli niliokumbana nao kwa baadhi ya matapeli wanaotaka pesa kirahisi ili kuokoa hata mtu mmoja asije akatapeliwa.
Kila siku mnaambiwa,
Fanyeni kazi, achaneni na pesa za kudownload,
Hamtaki kuelewa!!!

Mtapigwa sana huko kwenye digital currency.
 
Wakuu,

Kwanza kabisa, ieleweke wazi kuwa sipo hapa kupinga kuhusu Crypto-Currency trading, Forex Trading na jamii zote za mambo kama haya. Mie mwenyewe naendelea kujifunza ili nijue kwa undani na huenda siku moja nikawa expert wa hizi mambo. Lengo kubwa ni ku-share utapeli niliokumbana nao kwa baadhi ya matapeli wanaotaka pesa kirahisi ili kuokoa hata mtu mmoja asije akatapeliwa.
Jifunze forex, baadae uwe na mtaji minimum Sana $500 anza kutrade u tao na faida yake
 
Wakuu,

Kwanza kabisa, ieleweke wazi kuwa sipo hapa kupinga kuhusu Crypto-Currency trading, Forex Trading na jamii zote za mambo kama haya. Mie mwenyewe naendelea kujifunza ili nijue kwa undani na huenda siku moja nikawa expert wa hizi mambo. Lengo kubwa ni ku-share utapeli niliokumbana nao kwa baadhi ya matapeli wanaotaka pesa kirahisi ili kuokoa hata mtu mmoja asije akatapeliwa.

Sasa buana, mimi ni member wa Clubhouse, kama ujuavyo Clubhouse unaweza ku-connect na Dunia kwa haraka zaidi, nadhani ni kuliko Social media
Ujinga wako tu usisingizie cryptocurrency mbona hata kwenye vitunguu na viwanja mnapigwa ko vitunguu ni scarm ,acha ujinga kiongozi
 
Duh, ahsante Mkuu. Ahsante kwa kunipiga nyundo. Ila ujinga ni hali ya kutokuwa na maarifa ya jambo flani. Kwakuwa nimeongeza maarifa nadhani ujinga utakuwa umenipungua, au unasemaje Mkuu?
Maarifa yanatafutwa sehemu sahihi na inayoaminika sio kila sehemu

Period
 
Wala sio wazungu hao kwa experience yangu hao kama ni 15 basi 10 ni wanaijeria wanatumia namba za USA sometimes hata picha za wazungu unaweza kuta ni mwanaume anatumia picha na jina la kike izo account zao zinakuwa anonymous na ukiwashtukia wanafuta na kuunda nyingine ila kwa platfom kama telegram app moja unakuwa na account hata 5

Usikubali kutuma pesa izo ishu soma uelewe kwanza
 
Sasa hapo ulikuwa unadeal na crypto currency kivipi mkuu mbona maelezo yote harafu ni pumba ....


Mimi nikajua labda umenunua Bitcoin ukakuta ni fake ,labda umenunua Tron ,Shiba Inu ,etherium ,ukakuta ni fake ....

Nikajua labda umefungua account binance ukaweka hela ikapotea ,nikajua labda umenunua coin badae ukakuta haina thamani ......


Mbona sijaona ulipo nunua coin (digital currency)?????


Hapo mbona sijaona sehemu ulipojikita kwenye crypto currency ....

Unajua mkuu wewe ni mweupe kichwani kabisa kuhusu crypto currency ....


Mtu anayejua crypto ,hawezi andika maneno yote hayo bila kutaja ,trust wallet ,binance ,hotbit ,na wallet mbalimbali zinazotumika kutunza hizo coin na kufanya exchange ....


Kiufupi wewe jamaa hujui kitu kuhusu crypto currency ,ni mweupe kabisa ....

Mada yako sijui imejikita wapi ,kwa sababu sijaona sehemu uliyonunua coin ,sijui ulitaka kuwatumia hao wazungu hela ili iweje ,sijui uwape $200 then watakupa $500 hivi kweli kwa mtu anayejua crypto anaweza andika huo uharo .....someni someni jamani ,acheni mihemko


......N.B ..Kwenye crypto currency kama utataka kufanya trade upate pesa za haraka ,kaa ukijua upo mbioni kupoteza mtaji wako ....kama utaamua kununua coin na kuhold ,kwa zaidi ya miaka 3 kaa ukijua unaenda kuwa millionea hio ndio Siri ya crypto currency....
 
Sasa hapo ulikuwa unadeal na crypto currency kivipi mkuu mbona maelezo yote harafu ni pumba ....


Mimi nikajua labda umenunua Bitcoin ukakuta ni fake ,labda umenunua Tron ,Shiba Inu ,etherium ,ukakuta ni fake ....

Nikajua labda umefungua account binance ukaweka hela ikapotea ,nikajua labda umenunua coin badae ukakuta haina thamani ......


Mbona sijaona ulipo nunua coin (digital currency)?????


Hapo mbona sijaona sehemu ulipojikita kwenye crypto currency ....

Unajua mkuu wewe ni mweupe kichwani kabisa kuhusu crypto currency ....


Mtu anayejua crypto ,hawezi andika maneno yote hayo bila kutaja ,trust wallet ,binance ,hotbit ,na wallet mbalimbali zinazotumika kutunza hizo coin na kufanya exchange ....


Kiufupi wewe jamaa hujui kitu kuhusu crypto currency ,ni mweupe kabisa ....

Mada yako sijui imejikita wapi ,kwa sababu sijaona sehemu uliyonunua coin ,sijui ulitaka kuwatumia hao wazungu hela ili iweje ,sijui uwape $200 then watakupa $500 hivi kweli kwa mtu anayejua crypto anaweza andika huo uharo .....someni someni jamani ,acheni mihemko


......N.B ..Kwenye crypto currency kama utataka kufanya trade upate pesa za haraka ,kaa ukijua upo mbioni kupoteza mtaji wako ....kama utaamua kununua coin na kuhold ,kwa zaidi ya miaka 3 kaa ukijua unaenda kuwa millionea hio ndio Siri ya crypto currency....
Mkuu ni kweli mimi ni mweupe kichwani kuhusu Crypto ndio maana nimesema wazi hapo juu kuwa ndio naanza kujifunza..

Sijui unataka kuthibitisha nini? Kwamba mie si mweupe? Nani kasema nina ufahamu kama ulionao?

Angalia isije ukawa kundi la 'arrogant people'. Ama ukawa na changamoto ya 'overthinking'. BTW; Shukrani kwa mchango wako Mkuu. Naendelea kujifunza niwe 'elite' kama ulivyo.
 
Mkuu ni kweli mimi ni mweupe kichwani kuhusu Crypto ndio maana nimesema wazi hapo juu kuwa ndio naanza kujifunza..

Sijui unataka kuthibitisha nini? Kwamba mie si mweupe? Nani kasema nina ufahamu kama ulionao?

Angalia isije ukawa kundi la 'arrogant people'. Ama ukawa na changamoto ya 'overthinking'. BTW; Shukrani kwa mchango wako Mkuu. Naendelea kujifunza niwe 'elite' kama ulivyo.
Anyway ...

Mimi nitaaminu crypto currency ni utapeli pale nitakapo nunua coin harafu hizo coin zikapotea kwenye wallet ...

Au nifungue wallet yangu nikute coin hazipo ,au wallet yangu yenye coin iwe hacked na kuibiwa coin ....

Tofauti na hapo itakuwa ujinga wangu na kutokuwa na uelewa na crypto currency kama nitakuja na maada kuwa nimempa mtu $100 baada ya wiki atanipa $300 kitu ambacho kwenye crypto hakipo ...

Crypto currency ni kununua coin na kuuza zikiwa zimepanda bro ...

Leo nikiwa na 200 Tron ,hizo Tron zitabaki kwenye wallet miaka yote mpaka nitakapo uza ...nikiwa na 0.005 BTC hakuna atakayeweza zichukua mpaka niuze mwenyewe ...

Tafuta mentor ,akufundishe shule kuhusu crypto currency ,about HOLDING OF COIN and TRADING...baad ya hapo utajua mbichi na mbivu za crypto currency...

Kujisomea mwenyewe YouTube haitoshi believe me ....

Vinginevyo utaendelea kubaki njia panda kuhusu crypto ....
 
Sasa hapo ulikuwa unadeal na crypto currency kivipi mkuu mbona maelezo yote harafu ni pumba ....


Mimi nikajua labda umenunua Bitcoin ukakuta ni fake ,labda umenunua Tron ,Shiba Inu ,etherium ,ukakuta ni fake ....

Nikajua labda umefungua account binance ukaweka hela ikapotea ,nikajua labda umenunua coin badae ukakuta haina thamani ......


Mbona sijaona ulipo nunua coin (digital currency)?????


Hapo mbona sijaona sehemu ulipojikita kwenye crypto currency ....

Unajua mkuu wewe ni mweupe kichwani kabisa kuhusu crypto currency ....


Mtu anayejua crypto ,hawezi andika maneno yote hayo bila kutaja ,trust wallet ,binance ,hotbit ,na wallet mbalimbali zinazotumika kutunza hizo coin na kufanya exchange ....


Kiufupi wewe jamaa hujui kitu kuhusu crypto currency ,ni mweupe kabisa ....

Mada yako sijui imejikita wapi ,kwa sababu sijaona sehemu uliyonunua coin ,sijui ulitaka kuwatumia hao wazungu hela ili iweje ,sijui uwape $200 then watakupa $500 hivi kweli kwa mtu anayejua crypto anaweza andika huo uharo .....someni someni jamani ,acheni mihemko


......N.B ..Kwenye crypto currency kama utataka kufanya trade upate pesa za haraka ,kaa ukijua upo mbioni kupoteza mtaji wako ....kama utaamua kununua coin na kuhold ,kwa zaidi ya miaka 3 kaa ukijua unaenda kuwa millionea hio ndio Siri ya crypto currency....
nafikili hujamuelewa jamaa
ukimsoma tena utamuelewa vizuri lengo la uzi wake nini
kwanza hakuna sehemu alosema CRYPTO ni utapeli
katika maelezo yake amesema kbla hajaanza kununua COIN
alitaka kwanza apate ABC za hizo ishu ndo akaamua kujiunga na na CLUB HOUSE za room za US na UK na katika interest alizoweka ni hayo mambo ya CRYPTOCURRENCY

sasa kuna wajuba wao kazi yao ni kuwapokea watu dizaini yake na kuwaingiza mjini
7bu kubwa hawajui chochote kuhusu hayo mambo ya CRYPTOCURRENCY
na kwa maelezo ya jamaa wana maneno mazuri ikiwa ndio Beginner lazima uingie cha kike

hivyo lengo la uzi wake ni kuwatahadharisha wale wote wanaotaka kuanza wawe makini na utaperi wa aina hiyo unapojiunga katika SOCIAL MEDIA mbalimbali katika kutafuta maarifa ya CRYPTOCURRENCY
 
nafikili hujamuelewa jamaa
ukimsoma tena utamuelewa vizuri lengo la uzi wake nini
kwanza hakuna sehemu alosema CRYPTO ni utapeli
katika maelezo yake amesema kbla hajaanza kununua COIN
alitaka kwanza apate ABC za hizo ishu ndo akaamua kujiunga na na CLUB HOUSE za room za US na UK na katika interest alizoweka ni hayo mambo ya CRYPTOCURRENCY

sasa kuna wajuba wao kazi yao ni kuwapokea watu dizaini yake na kuwaingiza mjini
7bu kubwa hawajui chochote kuhusu hayo mambo ya CRYPTOCURRENCY
na kwa maelezo ya jamaa wana maneno mazuri ikiwa ndio Beginner lazima uingie cha kike

hivyo lengo la uzi wake ni kuwatahadharisha wale wote wanaotaka kuanza wawe makini na utaperi wa aina hiyo unapojiunga katika SOCIAL MEDIA mbalimbali katika kutafuta maarifa ya CRYPTOCURRENCY
Mkuu nashukuru sana kwa kunielewa vema. Comment ya mdau hapo juu imenifanya nifikirie zaidi nikadhani siku hizi nimepoteza uwezo wa kujieleza ' Publicy' kiasi cha watu kutoelewa 'contents' za ninachokuwa nimekusudia. Nikataka nianze upya kujifunza namna ya kujieleza. Ila comment yako imenipa FARAJA sana. Barikiwa sana Mkuu.
 
Play store inatambulika kwa jina hilohilo la clubhouse?
Ndio Mkuu. Kama unashindwa kui-access basi itakuwa ni changamoto ya version ama aina ya simu unayotumia. Kuna baadhi ya simu hazi-accomodate hiyo App especially za kutoka kule kwa Xi Jinping. Hata mie nilijaribu ku-download kwa simu yangu moja tokea huko ikawa haikubali. Ni mpaka nilivyobadili simu ndio nikaipata. Fanya jitihada ujiunge Clubhouse Mkuu. Huko kuna madini mengi sana ndani na nje ya Nchi especiilay kama siyo msomaji sana wa mambo na unapendelea kusikia zaidi. Ni juu yako tu kuchagua unachotaka kukisiskia. Iwe ni Ujasiriamiali, Siasa, Technology, Mindset transformation, Motivation na mambo mengine, ni wewe tu Mkuu.
 
Back
Top Bottom