Jinsi nilivyonyanyuka tena baada ya kuanguka kimaisha

Oct 6, 2016
56
152
Wakuu habari zenu mimi sio mwandishi mzuri sana ila nitajitaidi kidogo kuandika kwa ufupi ili niweze ku share nanyi jambo lililonikumba mwaka jana 2020.

Katika haya maisha kuna mambo tunapitia yanatuachia makovu,na hayatuachi salama baadhi yetu,mwaka jana 2020-2021 mwanzoni nilipitia anguko kubwa sana kimaisha.

Picha linaanza covid pandemic ilivyoingia kipindi kile nilikua nina mipango kibao kuikuza biashara yangu na mambo yalienda vizuri sana mwanzoni January 2020 mpaka march mambo yalivurugika vibaya sana niliyumba jumla yani mwez wa tisa nikafunga biashara kuogopa kupoteza mtaji wife akarudi kwao mm nikasepa nikaingia mkoani shamba (ukiondoa ujasiriamali chuo nilisoma kilimo) na nina uzoefu huko wazee wangu wakulima wayback.

Basi bhana nikaingia nikalima pilipili hoho by January 2021 nilipigika mbaya kabisa ilibidi niingie front mm mwenyewe hakuna kibarua nashukuru mzee wangu ana mashamba na visima na mashine za umwagiliaji alinipa sapport sana nilipiga kazi miezi mitatu ya machungu sana nilisemwa vibaya ndugu kejeli kibao me sikujali nilikua kila siku naamkia shamba siku nzima, Mungu ni mwema mwezi wa nne hoho ilikua juu sana roba 130000/= na mvua hazikunyesha sana mwaka huu 2021 nilikua nina uwezo wa kuchuma roba kumi na saba kila baada ya siku kumi yaani kila itaendelea wakuu nikipata muda
 
Tunaendelea
Yaani kila baada ya siku kumi nilikua naingiza 2 milion+ na nilichuma michumo sita,wife alinikimbia kwa dharau sana alipoanza kusikia kwa madogo nimeanza kujikongoja akaanza rudi speed kuanza kuomba msamaha aisee nilimpiga block kila kona mwez wa sita nikaingia tena nikalima maharage ya njano napo mungu akasaidia nimevuna mwez wa tisa nikarudi mjini mungu ni mwema biashara yangu ilikua sio ya vitu vya kuoza niliviifadhi vizur nikaviombea kwa mtu pamoja na vitu vyangu vya home,sikukubali kuuza kitu changu hata kimoja kingine zaidi ya tv yangu ambayo iliniongezea hela ya kujazia mtaji wa shamba kiukweli wazazi ni watu pekee watakua na ww kwenye kila hali niamini mm wazee wangu walitoa sapot ya kila namna kipindi nimedrop sasa nimenunua tv nyingine kubwa 55inch nimefungua biashara nyingine ya pili mkoani kwetu ya kuonesha mpira uzuri ukumbi ulikuepo home mzee ana guest house kwa ndani kuna ukumbi so nikafungua hapo na sio haba wadau wapo ,hatimae maisha yamerudi tena kwenye mstari arakati zinaendelea inawezekana kuna mtu anapitia changamoto kubwa nakusihi usikate tamaa kamwe.
 
Hongera sanaa mkuu kwa upambanaji wako na kutokukata tamaa, Pia kupitia habari yako hii ningependa pia kuwakumbusha tu VIJANA WA KIUME kuwa WANAWAKE WAPO TU NA WALA MWANAMKE ASIWE CHANZO CHA WEWE KUTOTIMIZA LENGO LAKO KATIKA MAISHA, cha umuhimu ni kuyajenga maisha yako kwanzaa. HONGERA!!
 
Tunaendelea
Yaani kila baada ya siku kumi nilikua naingiza 2 milion+ na nilichuma michumo sita,wife alinikimbia kwa dharau sana alipoanza kusikia kwa madogo nimeanza kujikongoja akaanza rudi speed kuanza kuomba msamaha aisee nilimpiga block kila kona mwez wa sita nikaingia tena nikalima maharage ya njano napo mungu akasaidia nimevuna mwez wa tisa nikarudi mjini mungu ni mwema biashara yangu ilikua sio ya vitu vya kuoza niliviifadhi vizur nikaviombea kwa mtu pamoja na vitu vyangu vya home,sikukubali kuuza kitu changu hata kimoja kingine zaidi ya tv yangu ambayo iliniongezea hela ya kujazia mtaji wa shamba kiukweli wazazi ni watu pekee watakua na ww kwenye kila hali niamini mm wazee wangu walitoa sapot ya kila namna kipindi nimedrop sasa nimenunua tv nyingine kubwa 55inch nimefungua biashara nyingine ya pili mkoani kwetu ya kuonesha mpira uzuri ukumbi ulikuepo home mzee ana guest house kwa ndani kuna ukumbi so nikafungua hapo na sio haba wadau wapo ,hatimae maisha yamerudi tena kwenye mstari arakati zinaendelea inawezekana kuna mtu anapitia changamoto kubwa nakusihi usikate tamaa kamwe.
Mtoto wa kishua siyo?
 
Ushauri wangu
1 Usije wacha kilimo hio ndio ngazi ilio
kunyanyua.
2 Sijui maisha yako yalikuwa vipi na wazee wako wakati ukiwa na mke lakini waweke karibu zaidi. Nilicho jifunza kwenye dunia hii wazee tu wanataka ufanikiwe walobakia wanajua siri za nafsi zao.



Lunatic
 
Mm ningependa kujua upo mkoa gan ningependa kushare na wewe juu ya kilimo Cha maharage ya njano

Kama kutaja hapa utaona n shida tafadhari pm yangu iko waz mkuu


...hongera kwa mapambano mkuu happy bado changamoto u nakuja nying jipange tu


..usikate tamaa matatizo ameumbiwa binadamu lazma tukabiliane nayo
 
Back
Top Bottom