Konzo Ikweta
JF-Expert Member
- Oct 3, 2013
- 735
- 1,464
Alipojiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani ya nchi mwaka 83 kama sijakosea nafasi yake aliteuliwa mzee mmoja kutoka Zanzibar anaitwa mzee Natepe kushika Uwaziri wa Mambo ya ndani ya nchi.
Natepe alipoingia tu ofisini alimtaka Waziri aliyemtangulia kutoka katika nyumba ya Waziri ili yeye aweze kukaa hapo kama Waziri.
Ilikuwa shida kidogo maana Waziri aliyeondoka bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka na Natepe kutoka.
Ikampasa Mzee Mwinyi kutoka kwa haraka na siku anatoka pale nyumbani alikuwa amenunua mabati 150 na mifuko ya saruji 100 ya kwake wala sio mali ya Serekali.
Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya Serekali kweli mzee Mwinyi akaviacha akaondoka.
Baada ya miezi kadhaa tu mzee mwinyi akateuliwa kuwa Rais Zanzibar. Natepe wakati anajifikiria jinsi ya kwenda kumpongeza na kumuomba radhi kwa aliyomfanyia kabla ya kufikiria njia Mzee Mwinyi akaletwa bara mwaka 1985 kama Rais wa JMT.
Hapa sasa Natepe akajua kazi hana na atatimuliwa haraka iwezekanavyo tena na kutengwa na nyadhifa za JMT kwakuwa kuna mabaya ya wazi na ya sirini aliyomtendea Mzee Mwinyi.
Mzee Mwinyi baada tu ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT wakati anateua baraza la Mawaziri akamteua tena Natepe kuwa Waziri palepale Mambo ya Ndani.
Siku ya kumuapisha akamwambia Natepe sio kwamba nakupenda sana hapana ila napenda kazi yako unavyofanya endelea kufanya kazi.
Siku moja Mzee Mwinyi yupo Ikulu kapumzika akaona malori yanaingia na akaambiwa mzigo wako huu mh Rais akashtuka mbona sijaagiza kitu mie?
Ndipo akaambiwa umetoka kwa Natepe Mzee Mwinyi akacheka sana akawaambia wasaidizi wake shusheni mabati 150 na saruji 100 hizo ndio haki yangu zingine mrudishieni tu.
Natepe alipoingia tu ofisini alimtaka Waziri aliyemtangulia kutoka katika nyumba ya Waziri ili yeye aweze kukaa hapo kama Waziri.
Ilikuwa shida kidogo maana Waziri aliyeondoka bado alikuwa anatafuta makazi lakini alitakiwa haraka na Natepe kutoka.
Ikampasa Mzee Mwinyi kutoka kwa haraka na siku anatoka pale nyumbani alikuwa amenunua mabati 150 na mifuko ya saruji 100 ya kwake wala sio mali ya Serekali.
Natepe alimkatalia kuvichukua akidai ni mali ya Serekali kweli mzee Mwinyi akaviacha akaondoka.
Baada ya miezi kadhaa tu mzee mwinyi akateuliwa kuwa Rais Zanzibar. Natepe wakati anajifikiria jinsi ya kwenda kumpongeza na kumuomba radhi kwa aliyomfanyia kabla ya kufikiria njia Mzee Mwinyi akaletwa bara mwaka 1985 kama Rais wa JMT.
Hapa sasa Natepe akajua kazi hana na atatimuliwa haraka iwezekanavyo tena na kutengwa na nyadhifa za JMT kwakuwa kuna mabaya ya wazi na ya sirini aliyomtendea Mzee Mwinyi.
Mzee Mwinyi baada tu ya kuapishwa kuwa Rais wa JMT wakati anateua baraza la Mawaziri akamteua tena Natepe kuwa Waziri palepale Mambo ya Ndani.
Siku ya kumuapisha akamwambia Natepe sio kwamba nakupenda sana hapana ila napenda kazi yako unavyofanya endelea kufanya kazi.
Siku moja Mzee Mwinyi yupo Ikulu kapumzika akaona malori yanaingia na akaambiwa mzigo wako huu mh Rais akashtuka mbona sijaagiza kitu mie?
Ndipo akaambiwa umetoka kwa Natepe Mzee Mwinyi akacheka sana akawaambia wasaidizi wake shusheni mabati 150 na saruji 100 hizo ndio haki yangu zingine mrudishieni tu.