Jinsi muelekeo wa siasa zetu unavyoua uwezo wetu wa kufikiri na hatari iliyopo mbele yetu kama taifa

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,427
1618586093716.png
Kwa mujibu wa mfumo wetu, Wanasiasa ndio viongozi wa nchi ambapo kiongozi ndio hutoa muelekeo wa wapi pa kwenda au kutokwenda na ili iweje. Kwa mantiki hiyo, ili kupunguza ‘chances’ za kupotea, ni jambo la muhimu sana wanasiasa wetu wawe na uwezo mkubwa sana wa kufikiri.

Uwezo mkubwa wa kufikiri huchangiwa na mambo makubwa matatu. Changamoto, Ukosolewaji na kujifunza (Challenges, criticism and learning). Mtu yoyote mwenye akili timamu, akiyapitia hayo, lazima uwezo wake wa kufikiri uimarike.

Hata mtu akazaliwa akiwa na akili kiasi gani, asipokutana na changamoto za kutosha, mawazo yake kukoselewa sana na pia akajifunza sana, baada ya muda atakuwa ‘Very low’ na kinyume chake, sio kwa sababu ni mtu mbaya bali kwa sababu ya mazingira.

Sasa basi, kwa muelekeo wa siasa zetu, kuna kitu kinajengeka kwa kasi sana. Kutopenda kuwa ‘Challenged’ Kutopenda ‘kukosolewa’ na kupuuza ‘kujifunza’ (kusoma). Yaani mtu akipewa challenge anakasirika , akikosolewa anafanya uadui, akiona mtu amesoma, au anasoma utasikia ‘ kasoma lakini hana mchango kwa taifa’(maana yake tuna discourage wanasiasa/viongozi kujifunza).

Misuli ili ikue lazima kunyanyua vitu vizito, na kwa kadiri unavyonyanyua vitu vizito ndio misuli hukuwa zaidi na kinyume chake. Vile vile uwezo wa kufikiri; kwa kadiri unavyokumbana na ‘challenges’, ‘critiscims’ na kujifunza ndivyo uwezo wa kufikiri unavyokuwa na kinyume chake.

Nitoe mifano michache, Ukiwa na mtoto, kila anachotaka anapata bila kuhojiwa, unaandaa mtoto ambaye uwezo wake wa kufikiri utakuwa ‘very low’ na usipokuwepo atakuwa amekwisha. Kama Toyota kwa mfano wasingekuwa ‘challenged’ na Nissan n.k wasingekuja na uvumbuzi mpya kila siku. N.k.

Kwa hiyo hata binadamu hata awe mzuri vipi, asipokuwa ‘challenged & Criticized intensively’ atakuwa ‘very low’ hii ni kanuni tu ya kimaumbile. Hata wewe unayesoma hapa, kama vitu unavyofikiri, kusema na kufanya hakuna watu wanaoku ‘challenge’ na kuku ‘criticize seriously’, utakuwa ‘very low’ tu. Yaani kila unachosema watu ‘yes’ ukikohoa walioko karibu yako ‘wanasema umekohoa vizuri’ n.k lazima utaingia kwenye comfort zone na utapotea tu.

Wito wangu;
Ni muhimu sana kama taifa tukajenga mazingira ya kisiasa ambayo yatachochea kuongeza uwezo wa wanasiasa/viongozi kufikiri zaidi na zaidi. Mazingira hayo si mengine bali kujingea utamaduni wa kukubali kupewa changamoto, kuokosolewa, kujifunza/kutafuta elimu.

Kwa mantiki hiyo, sio tu kwamba tunapaswa kujijengea utamaduni wakukubali kukosolewa (japo kwa kujilazimisha kama mtu anavyojilazimisha kuamka asubuhi) bali pia tunatakiwa ku ‘promote’ utamaduni huo. Hiyo ndio njia pekee itakayotusaidia kuwa na wanasiasa na hatimaye viongozi wenye fikra madhubuti zaidi leo kuliko jana na kesho kuliko leo. Vinginevyo, tunatakuwa tumeemua kujielekeza shimoni wenyewe kwa hiyari yetu.

Aidha, watu wanaotu challenge na kutukosoa au kutuelimisha; hatupaswi kuwachukulia kama maadui badi wadau wa maendeleo, kwani wanatuwezesha tufikiri zaidi na hivyo kufanya vyema zaidi na kuwa wabunifu.

Kupanga ni kuchagua, la muhimu ni kuchagua ukijua unachagua nini na ili iwe nini.
 
Kwa upande wangu binafsi kwa mfano, nishawahi kuchukia sana watu wanao ni 'challenge'. Niliowachukia zaidi walikuwa waalimu. Yaani unajibu maswali kwa namna ambayo ungetegemea upate 100% lakini unashangaa umepata 55% na ukiwauliza umekosea wapi hawakuelezi kitu cha maana. Nikaawa naamini wanaroho mbaya sana, wanoko wanoko na hawafai.

Baadae nikaja kugundua kuwa walikuwa na dhamira njema kabisa. Walichotaka ni kuni force nifikiri zaidi na nisije nikabweteka nikajiona najua sana mwishowe nikawa bonge la boya. Nilikuja kugundua jambo hili kwa kuchelewa sana.
 
Mkuu kwema? Mkuu una hoja nzuri sana lakini hujui namna ya kuwasilisha hoja kabisa. Uandishi wako haushawishi hata kidogo mkuu. You have to improve your communication skills.

Ahsante sana.
Sawa mkuu. Inawezekana na mimi nimeshaathiriwa na tatizo la msingi linalozungumziwa kwenyye hoja ya msingi maana limeshawaathiri wengi.

In summary, tunajenga aina ya siasa inayochochea utamaduni wa kutopenda kupewa changamoto, kutopenda kukosolewa au kujifunza. Matokeo yake mbele ya safari tutatukwa na kizazi cha wanasiasa (ambao kimsingi ndio viongozi) wasio na fikra madhubuti , na sio kwamba watapenda kuwa hivyo, bali itakuwa ni matokeo ya mazingira.

Ni vyema tukajisahihisha.
 
Kwa hiyo kwa kuzingatia mantiki ya hoja ya msingi, ni muhimu kukubali challenges na cricisms maana zinatujenga kiakili na hivyo ni faida kwetu kuliko kinyume chake.

Vile vile, inapotokea mtu akakupa wazo bora zaidi, bila kujali ni nani, busara ni mambo mawili; amma kulichukua, au kulazimisha akili yako kuja na wazo bora zaidi.

Ila kinyume chake lazima akili ziende kwenye 'confort zone' jamba ambalo ni hatari sana hasa zama hizi ambapo dunia huendeshwa kwa akili nyingi na nguvu kiduchu.
 
Sawa mkuu. Inawezekana na mimi nimeshaathiriwa na tatizo la msingi linalozungumziwa kwenyye hoja ya msingi maana limeshawaathiri wengi.

In summary, tunajenga aina ya siasa inayochochea utamaduni wa kutopenda kupewa changamoto, kutopenda kukosolewa au kujifunza. Matokeo yake mbele ya safari tutatukwa na kizazi cha wanasiasa (ambao kimsingi ndio viongozi) wasio na fikra madhubuti , na sio kwamba watapenda kuwa hivyo, bali itakuwa ni matokeo ya mazingira.

Ni vyema tukajisahihisha.
You are right brother. Also ,undoubtedly you're a decent man. Just wanted to see your reaction.
 
You are right brother. Also ,undoubtedly you're a decent man. Just wanted to see your reaction.
Nilifundishwa utulivu na mwalimu wangu mmoja. Kila ninachoaandika anasema 'Hamna kitu, nenda kaandike tena' nikimuuliza usahihi unapaswa kuwa vipi ananiambia 'nenda kafikiri zaidi uniletee majibu ya maana hapa' nikawa nakasirika weee lakini hatimaye nikagundua kuwa kweli kuna vitu vipya najifunza.

Kwa mantiki hiyo, tunatakiwa tujenge utamaduni wa siasa za kusikilizana na kujifunza.sio kuvumilia ukosoaji tu bali ku 'entertain challenges'. Ni kwa msingi huo pekee tunaweza kujenga nchi ya watu wanaofikiri ambayo ndio nguzo kuu ya uongozi bora na mafanikio katika zama hizi.

Kinyume chake tutakwisha, ni suala na muda tu.
 
Ni vema ungempa intro ya uandishi mzur na bora kuliko kulaumu na kukimbia
Ni changamoto mkuu, ila inaweza kuwa ni sehemu ya madhara ya yaliyoelezwa kwenye mada ya msingi. Ni muhimu kuwa na mkakati mpana wa kitaifa kujenga kizazi kinachofikiri 'Critical thinking generation' na tunaweza kufanya hivyo kwa kujenga utamaduni wa ku intertain challenges. Kinyume na hapo ni balaa ndugu yangu.
 
Kuna vitu vinavyochangia kushusha uwezo wa kufikiri kwa mtazamo wangu, aina za siasa, na wanasiasa wenyewe.

Siasa zetu hasa za mitandaoni kwetu mashabiki zimeegemea zaidi kwenye kujadili watu, na matukio, sio issues, tunapenda sana kumjadili Ndugai na mambo yake bungeni au Msukuma na mambo yake bungeni, lakini sio vile wanavyovizungumza watu hao, kwamba kama walishakosea mwanzo isiwe sababu ya kutojadili kile wanachokisema sasa kwa sababu ya rekodi zao zilizopita. Hapa napo kuna haja ya mashabiki kusoma vitabu inorder to stretch their brain muscles.

Pia, wanasiasa wenyewe, hawa nikichukulia mfano wa kule bungeni, wengi humezwa na tabia za wenzao na hivyo kujikuta automatically wanadumaza uwezo wao wa kufikiri, inafika mahala unaona mbunge hana sababu tena ya kusoma vitabu kama unavyosema kwasababu ameshazoea kama akiongea mpinzani atamzomea tu bila kujali ni kitu gani mpinzani ameongea, kama pangekuwepo na tabia ya kupingana kwa hoja kati yao kule bungeni naamini kabisa wengi wao wangekuwa ni watu wa kujisomea ili kuongeza uwezo wao wa kufikiri.

Cha ajabu zaidi, siku hizi bungeni kumezuka katabia cha kuwasifu wabunge wenye elimu ndogo kwa kusema ndio wenye point zaidi ya wale wenye elimu kubwa, hili ukiongeza na sifa ya mtu kuwa mbunge kwamba ajue kusoma na kuandika pekee ndio vitachangia zaidi kushusha uwezo wa wabunge kujiendeleza kielimu kwa sababu wale wenye elimu ndogo watajiona kumbe wako vizuri, na wale wengine watajiona walipofikia panatosha kwasababu wameshaonekana wanazidiwa kufikiri na "wadogo" zao.
 
Mkuu denooJ angalizo lako ni la msingi sana. Zaidi ya hapo ni kwamba kwa kawaida kama mtu hupati changamoto kwenye hoja unazotoa, kidogo kidogo una sees kufikiri. Ujue kufikiri ni kazi ngumu na inayosababisha disconfort, kwa hiyo bila push factors, hali hiyo lazima itokeee tu. Kwa hiyo muhimu ni kila mmoja wetu kujitahidi awezavyo kubalilia culture ya ku entertain challanges na kujifunza
 
Mkuu denooJ angalizo lako ni la msingi sana. Zaidi ya hapo ni kwamba kwa kawaida kama mtu hupati changamoto kwenye hoja unazotoa, kidogo kidogo una sees kufikiri. Ujue kufikiri ni kazi ngumu na inayosababisha disconfort, kwa hiyo bila push factors, hali hiyo lazima itokeee tu. Kwa hiyo muhimu ni kila mmoja wetu kujitahidi awezavyo kubalilia culture ya ku entertain challanges na kujifunza
Ni kweli unachosema, tatizo mlaji hula chakula anacholetewa mezani, wakileta hoja fikirishi zitajadiliwa, bahati mbaya mengi yanayoletwa mezani huwa hayahitaji akili kubwa kufikiria coz majibu yake huwa ni yale yale, unadhani kwanini thread nyingi unazoleta huwa zinakosa wachangiaji wengi? tatizo unawaletea chakula kigumu kutafuna wakati upande wa pili huwa kuna keki wanajua hata wakimumunya watameza tu.
 
Kwa mujibu wa mfumo wetu, Wanasiasa ndio viongozi wa nchi ambapo kiongozi ndio hutoa muelekeo wa wapi pa kwenda au kutokwenda na ili iweje. Kwa mantiki hiyo, ili kupunguza ‘chances’ za kupotea, ni jambo la muhimu sana wanasiasa wetu wawe na uwezo mkubwa sana wa kufikiri.

Uwezo mkubwa wa kufikiri huchangiwa na mambo makubwa matatu. Changamoto, Ukosolewaji na kujifunza (Challenges, criticism and learning). Mtu yoyote mwenye akili timamu, akiyapitia hayo, lazima uwezo wake wa kufikiri uimarike.

Hata mtu akazaliwa akiwa na akili kiasi gani, asipokutana na changamoto za kutosha, mawazo yake kukoselewa sana na pia akajifunza sana, baada ya muda atakuwa ‘Very low’ na kinyume chake, sio kwa sababu ni mtu mbaya bali kwa sababu ya mazingira.

Sasa basi, kwa muelekeo wa siasa zetu, kuna kitu kinajengeka kwa kasi sana. Kutopenda kuwa ‘Challenged’ Kutopenda ‘kukosolewa’ na kupuuza ‘kujifunza’ (kusoma). Yaani mtu akipewa challenge anakasirika , akikosolewa anafanya uadui, akiona mtu amesoma, au anasoma utasikia ‘ kasoma lakini hana mchango kwa taifa’(maana yake tuna discourage wanasiasa/viongozi kujifunza).

Misuli ili ikue lazima kunyanyua vitu vizito, na kwa kadiri unavyonyanyua vitu vizito ndio misuli hukuwa zaidi na kinyume chake. Vile vile uwezo wa kufikiri; kwa kadiri unavyokumbana na ‘challenges’, ‘critiscims’ na kujifunza ndivyo uwezo wa kufikiri unavyokuwa na kinyume chake.

Nitoe mifano michache, Ukiwa na mtoto, kila anachotaka anapata bila kuhojiwa, unaandaa mtoto ambaye uwezo wake wa kufikiri utakuwa ‘very low’ na usipokuwepo atakuwa amekwisha. Kama Toyota kwa mfano wasingekuwa ‘challenged’ na Nissan n.k wasingekuja na uvumbuzi mpya kila siku. N.k.

Kwa hiyo hata binadamu hata awe mzuri vipi, asipokuwa ‘challenged & Criticized intensively’ atakuwa ‘very low’ hii ni kanuni tu ya kimaumbile. Hata wewe unayesoma hapa, kama vitu unavyofikiri, kusema na kufanya hakuna watu wanaoku ‘challenge’ na kuku ‘criticize seriously’, utakuwa ‘very low’ tu. Yaani kila unachosema watu ‘yes’ ukikohoa walioko karibu yako ‘wanasema umekohoa vizuri’ n.k lazima utaingia kwenye comfort zone na utapotea tu.

Wito wangu;
Ni muhimu sana kama taifa tukajenga mazingira ya kisiasa ambayo yatachochea kuongeza uwezo wa wanasiasa/viongozi kufikiri zaidi na zaidi. Mazingira hayo si mengine bali kujingea utamaduni wa kukubali kupewa changamoto, kuokosolewa, kujifunza/kutafuta elimu.

Kwa mantiki hiyo, sio tu kwamba tunapaswa kujijengea utamaduni wakukubali kukosolewa (japo kwa kujilazimisha kama mtu anavyojilazimisha kuamka asubuhi) bali pia tunatakiwa ku ‘promote’ utamaduni huo. Hiyo ndio njia pekee itakayotusaidia kuwa na wanasiasa na hatimaye viongozi wenye fikra madhubuti zaidi leo kuliko jana na kesho kuliko leo. Vinginevyo, tunatakuwa tumeemua kujielekeza shimoni wenyewe kwa hiyari yetu.

Aidha, watu wanaotu challenge na kutukosoa au kutuelimisha; hatupaswi kuwachukulia kama maadui badi wadau wa maendeleo, kwani wanatuwezesha tufikiri zaidi na hivyo kufanya vyema zaidi na kuwa wabunifu.

Kupanga ni kuchagua, la muhimu ni kuchagua ukijua unachagua nini na ili iwe nini.
Very good, umejenga hoja yako vizuri sana
 
Azizi Mussa ,

Asante sana kwa hoja murua. Binafsi nami nimekuwa nikijiuliza sana, hivi tatizo la uwezo mdogo wa kufikiri ni tatizo la wanasiasa au ni tatizo la mfumo mzima wa jamii?

Unaweza kuwatazama wanasiasa kama ndiyo wenye nafasi na uwezo wa kuelekeza jamii yetu katika njia sahihi kwa maendeleo ya taifa letu. Hiyo ni njia moja ya kuangalia tatizo la ufikiri, na kwa mtazamo huo, ni dhahiri kuwa kuna mchango mkubwa wa viongozi wa kisiasa katika kuua/kudumaza uwezo wa kufikiri miongoni mwetu.

Lakini kwa upande mwingine, viongozi wa kisiasa kwa sehemu kubwa wanachaguliwa na sisi wananchi kupitia sanduku la kura. Hivyo ni sawa na kusema, hao viongozi ndiyo sisi tumewaona wanaweza kufikisha maono ya taifa mbele. Kwa maana nyingine, viongozi ni taswira ya jamiii iliyomchagua huyo kiongozi. Kuanzia wenyeviti wa serikali za mtaa, madiwani na wabunge ni taswira ya jamii wanazotoka. Ukitazama toka mlengo huu, utaona kuna tatizo kwenye jamii inayopeleka udhaifu mkubwa kwenye kufikiri.

Tukiona viongozi hawewezi kutusaidia na sera au mipango ya taifa kuinua uwezo wa kufikiri wa watu wake, basi tuanze mmoja mmoja na ndani ya familia na jumuiya zetu ndogo ndogo. Itachukua muda lakini kuna siku itafika sehemu kubwa ya jamii itakuwa imebadilika. Itakapofika wakati huo, jamii yenyewe itaona aina ya viongozi wanaofaa kuleta mabadiliko.

Miaka kama kumi hivi nyuma, kuna Daktari mmoja (PhD) , sikumbuki jina lake, aliliona tatizo la ufikiri duni, na akawa anaendesha semina/mafunzo ya critical thinking kwenye hotel moja Dar es Salaam, naamini kama yule daktari angeendelea na mafunzo yake, leo hii idadi ya wanufaika ingekuwa kubwa zaidi, na miaka ishirini ijayo kungeweza kuwa na mabadiliko.

Hata katika jamii zetu kuanzia ngazi ya familia, lazima tukubali kubadilika. Tujenge utamaduni wa kushindana kwa hoja, siyo kushinda kwa umri, jinsia, mamlaka au nafasi yetu katika jamii.
 
Mkuu Mzawa Halisi umeongea point za maana sana sana. Nimevutiwa sana na mchango wako.

Kimsingi hiyo ni tatizo la kijamii, lakini tatizo hilo ni zao la mifumo, na mifumo hiyo ni zao la siasa zetu kwa sababu siasa ndio huamua mifumo iweje. Kwa kiasi flani ni sawa na hadithi ya kuku na yai.

Nasema hivi nikiwa na uhakika kabisa. Kwa mfano watu hawa hawa wangehamishiwa china huko au marekani wakiwa watoto, wakiwa wakubwa wangekuwa na critical thinking bora zaidi. Hii ni kwa sababu ya mifumo ya mahali na mahali.

Mfano ulioutoa wa daktari aliyekuwa anafundisha critical thinking, na akaacha, aliacha kwa sababu solution ya tatizo hili inatakiwa kuanzia kwenye mifumo ya siasa juu, sio ufanye peke yako chini, mafanikio yatakuwa madogo sana.

Mfano, utashangaa ukitoa hoja ya maana hata anayejadili au kusoma hakuna sana sana unaweza kuwa clashed na kukatishwa tamaa. Sasa unakuwa na option useme kitu cha maana ujadili mwenyewe na usipate maslahi maana mfano hautoi maslahi kwa watu wa aina hiyo, au uwe unatoa makorokocho upate support ya kutosha na maslahi juu? You see the dilema?

Unakuta watu wanaoongea ujinga kwa mfano, ndio wanaotoka haraka kuliko wanaoongea mambo ya maana, sasa mtu anatakiwa kuchagua, mfano achafue wenzake atoke, au azungumze vitu critical apuuzwe.

Kwa hiyo ni suala compicated hivyo
 
Mkuu Mzawa Halisi nishawahi kusikia kuwa enzi za hitler kwa mfano, ilikuwa mtu akifanya kosa anapigwa jela, anapewa adhabu ya kuvumbua kitu kinachotatua tatizo flani la kijamii ndani ya muda flani, vinginevyo jamaa anakuua. Hii ikachochea sana critical thinking ujerumani.

Sasa fikiria tu mfano hapa kwetu tungejenga utamaduni kwamba mtu hapewi cheo chochote mpaka aje na wazo linalotatua changamoto fulani, kwa hiyo mchujo hufanyika kwa kuzingatia nani wanaongoza kwa mawazo bora, unadhani hii inge boost critical thinking kwa namna gani?

Ila kwa kipindi kirefu tumekuwa tukiona wanaosifia watu wengine na kuchafua wengine huwa ndio wanakuwa viongozi hapa na pale, sasa hii inaua critical thinking kwa kiasi gani?
 
Ni kweli unachosema, tatizo mlaji hula chakula anacholetewa mezani, wakileta hoja fikirishi zitajadiliwa, bahati mbaya mengi yanayoletwa mezani huwa hayahitaji akili kubwa kufikiria coz majibu yake huwa ni yale yale, unadhani kwanini thread nyingi unazoleta huwa zinakosa wachangiaji wengi? tatizo unawaletea chakula kigumu kutafuna wakati upande wa pili huwa kuna keki wanajua hata wakimumunya watameza tu.
Uko sahihi sana mkuu. Kuna suala pia la 'incentives'. Kama unajua ukiwa na mawaziri ya maana, ukisoma na kujielimisha na.k sio tu kwamba hutokubalika kulingana na mfumo uliopo bali pia hutopata ' incentives' lakini ukiwa mkurupukaji kwa mfano unachafu watu wengine, kwanza unapata support na pili unapata incentives, kwa vyovyote vile mazingira hayo yatawasukuma wengi kama sio wote kuchukua option ya pili. Ndio maana nasema ni mfumo fulani ambao pia unaweza kuwa kinyume chake
 
Thread za aina hii zingekuwa juu kule atleast watu wazione wajadili kuleta diversity ya mada, lakini umefichwa chini huku kwangu ninaetumia simu inakuwa shida kuuona wakati kule juu thread nyingi zinagusa mambo yale yale ya bungeni ya wakina Ndugai na wenzake, na teuzi za ikulu za kila siku.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom