nkasoukumu
JF-Expert Member
- Nov 27, 2010
- 888
- 408
A Letter from the President of Tanzania, Hon.
Benjamin Mkapa, in Response to Tanzanian
Muslims' Grievances
The President of the United The State House
Republic of Tanzania Dar es Salaam
17 Desemba 1999
Ndugu Saleh Al-Miskry,
Halmashauri Kuu ya Waislamu,
C/o Islamic Club,
S.L.P. 11392,
DAR ES SALAAM
Ndugu Al-Miskry,
Ninakiri kupokea, kwa shukrani, barua yako ya tarehe 26 Agosti 1999, pamoja na viambatisho
vyake. Imenichukua muda mrefu kukujibu kwa sababu mambo uliyoandika ni mazito, ya kitaifa, na
ilinibidi niyatafakari kwa kina, niyafanyie utafiti zaidi, na nishauriane na wenzangu Serikalini kabla ya
kuyajibu.
Leo ninakuandikia si kwa lengo la kujibu hoja moja baada ya nyengine, au kutoa jibu kwa kila
swali. Katiba ya Jamhuri yetu inanipa mimi, kama Rais, wasaidizi wengi. Ninaye Makamu wa Rais, na
ninaye Waziri Mkuu. Ninaye waziri kwa kila sekta, na ninao wakuu wa mikoa na wilaya kwa kila eneo la
nchi yetu. Nitakuwa siwatendei haki nikijibu maswali yanayowahusu wao. Ningeshauri, kama mlivyojenga
mahusiano mazuri nami, mjenge pia mahusiano mazuri na mawaziri, wakuu wa mikoa, na kadhalika, ili
kila jambo lisingoje mpaka lifikishwe kwa Rais.
Nina uhakika kwa mfano, kwamba Waziri wa Elimu ana uwezo wa madaraka ya kutosha
kushughulikia masuala ya elimu, ambayo kwangu ni muhimu sana. Akikwama atayaleta kwangu. Hiyo
itasaidia kufanya mawasiliano nami yawe yale yanayohusu mambo ya msingi, badala ya kujadili matukio.
Misingi hiyo itasaidia kuwaongoza watendaji wa Serikali na kuniwezesha mimi na nyinyi kuwa na vigezo
vya kupima tunafanikiwa kiasi gani katika kuhakikisha kila mwannvhi anapata haki zake za msingi bila
ubaguzi wowote kwa sababu za dini, dhehebu, kabila, jinsia, eneo analotoka, na kadhalika.
Msingi wa kwanza ni utawala wa sheria. Nchi yetu lazima iendelee kutawaliwa kwa msingi wa
sheria zilizowekwa kwa njia za demokrasia. Hivyo napata taabu kidogo raia wa nchi hii anapofikiri
matatizo aliyo nayo yanaweza kutatuliwa nje ya mfumo wa utawala wa sheria.
Kila mwenye kero
akichukua msimamo huo, nchi hii itakuwa haitawaliki tena; itakuwa vurugu tupu. Kazi ya msingi ya
Serikali yoyote ni kuhakikisha unakuwepo utawala wa sheri, ulinzi na usalama wa raia wote, wa aina na
imani zote. Uhalali wa raia kudai haki nje ya mfumo wa utawala wa sheria unaweza ukakubalika penye
utawala wa kikoloni, utawala wa ubaguzi wa rangi, au utawala wa kidikteta. Uhalali huo haupo hata kidog
katika nchi huru, inayoongozwa kwa misingi ya demokrasia kama ilivyo Tanzania.
Kwa sababu hiyo nimefadhaishwa sana na kauli za kuashiria shari za wale wanojiita "Shura ya
Maimau Dar es Salaam". Pamoja na mbmo mengine ya uchochezei wanasema, "Waislamu hatuna moyo
tena na Serikali ya nchi hii na vyombo vyake vyote likiwemo Bunge na Mahakama". Ninajua huu sio
msimamo wa Waislam walio wengi, lakini matamko yasiyokuwa na kiasi kama haya yasipokanushwa, na
wanaoyatoa wanapopewa fursa na majukwaa ya kuyasema, hiyo inawapa silaha wale wachache
wanojaribu kupakamatope heshima na picha nzuri ya Waislamu. Mimi na ninyi tuna kazi ya kuwashihisha
wenye hulka ya aina hiyo, lakini matamko kama haya yatafanya kazi hiyo iwe ngumu zaidi.
Utawala wa sheria chimbuko lake ni Katiba ya Jamhuri. Katiba yetu imepiga marufuku ubaguzi
wowote, kwa msingi wowote, ikiwemo dini, kabila, rangi, eneo analotoka mtu, na kadhalika. Katiba hiyo
pia imetoa uhuru kamili, ndani ya uwigo wa sheria, wa imani za dini kustawi katika uhuru wa ibada.
Isipokuwa kwa wale ambao hawan imani na vyombo vyote vya dola, mimi nina imani kuwa mahakama
zetu nina uwezo na uhusu kamili wa kumpa haki hizi za msingi yule ambaye atkauwa amenyimwa kwa
ubaguzi.
Narudia. Haki za msingi za kila raia zimo ndani ya Sheria Mama - Katiba - ya Jamhuri yetu.
Kama kweli upo uhsahidi kwamba baadhi ya taasisi za umma au viognozi wa umma, wamebuni mfumo
wao wa kuhakikisha Waislamu wananyimwa haki hizo, hao wala si wa kuchukuliwa hatua za nidhamu tu,
bali ni wa kushitakiwa mahakamani. Wasionewe haya. Tusaidianeni wahsitakiwe!
Siwezi kushangaa iwapo kuna mtu au kiongozi mahali ambaye ndani ya moyo wake ana chuku
dhidi ya Wakristo au dhidi ya Waislam; au ana chuki dhidi ya naume au wanawake; au ana chuku dhidi ya
wazramo au wahaya; au chuki dhidi ya watu warefu au wafupi. Ninachosema ni kuwa katika utafiti
niliofanya hakuna mahali popote katika Serikali hii ambapo mfumo rasmi wa kubagua au kumnyima haki
za msingi mtu yeyote kwa msingi wowote.
Kweli, zipo tofauti kati ya idadi ya Waislamu na wasio Waislamu katika shile, vyuo, sehemu
mbalimbli za kazi lakni huo si ushahidi wa mfumo wa ubaguzi. Sababu zake sote unazijua - ni za kihistoria
na za kijamii, kama ilivyo kwa tofauti kati ya idadi za watu wa kabila mbalimbali au jinsia. Ingekuwa
tofauti hizo peke yake zinatosha kuthibitisha mfumo rasmi wa Waislamu, kwa nini tusiseme pia kuwa upo
mfumo rasmi wa kubagua wanawake, au watu wa kabila fulani, au rangi fulani, au umbo fulani. Na ukweli
ni kuwa si kila mahali Waislamu ni wachache. Kwa mfano nimejaribu kuhesabu ni mabalozi wangapi, tena
kwenye zile Ofisi za ubalozi muhimu sana, ambao ni Waislamu. Naomba na ninyi mfanye hesabu hiyo.
Lakini turudi kwenye masuala ya msingi. Si jambo zuri sana kuanza kujena utamaduni wa
kuhesabu watu kwa misingi ya kabila zao, dini zao, rangi zao, jinsia zao, au maeneo wanayotoka. Tangu
uhuru tumejitahidi kujenga taifa ambapo haki na heshima ya mtu inatokana na utu wake, si dini yake,
kabila lake, jinsia yake, na kadhalika. Siko tayari kujenga mfumo wa utawala ambapo sifa ya mtu kupata
nafasi ya shule, au nafasi ya kazi, ni dini yake. Aidha, tukishaanza na dini tutawazuiaje wengine kudai nao
wafikiriwe kwa misingi ya dhehebu la dini, kabila, jinsia na kadhalika. Hapo tutakuwa tumefumua kabisa
misingi ya umoja, upendo, mshikamano na kuheshimiana waliyotuachia waasisi wa Taifa letu. Naomba
sana tusitafute dawa ya ugonjwa mdogo itakayozua magonjwa makubwa zaidi yasiyokuwa na tiba.
Vile vile kuanzisha taasisi mpya ya kupokea na kuchunguza ubaguzi wa kidini kutazidi kuvuruga
tu kwa vile ni kukiri kuwa kweli upo ubaguzi uliojengeka ndani ya mfumo wa utendaji Serikalini; jambo
ambalo si kweli. Aidha, kama nilivyosema, ukianzisha taasisi ya kushughulikia ubaguzi wa kidini, uwezi
kukataa wengine wakidai taasisi nyingine ya kushughulikia ubaguzi wa jinsia, ubaguzi wa kabila, rangi, na
kadhalika.
Tusijitose sana katika zoezi la kuhesabu watu kwa misingi ya dini. Tukifanya hivyo tutaimarisha,
badala ya kujihisi kwanza kama Watanzania. Mimi nilifikiri kuwa Tanzania ilishavuka hatua hiyo.
Naomba usirudi nyuma kwenye kutukuza udini, ukabila, au maeneo tunayotoka. Tukishajitumbukiza huko
hatuwezi kutoka tena. Badala yake lengo letu liwe kuelekea mahali ambapo tutakuwa vipofu wa dini,
vipofu wa rangi, vipofu wa kabila, na kadhalika. Na pia tusisahau kuwa Tanzania yetu hii ina hata
Maaskofu wenye majina ya Ramadhani au Hussein, na wengine wengi ambao wana majina yasiyofichua
dini zao au kabila zao.
Jambo jingine la msingi ni kuhakikisha kuwa Tanzania kama Taifa, na kama Serikali au Chama
chochote cha siasa, inakuwa haina dini. Kwenye hili hakuna mjadala, maana ni hali hiyo ya kutinamia
upande wa dini yoyote ndiyo inayotupa nguvu ya kusimamia na kuhakikisha kila raia anapata haki zake za
imani za dini na uhuru wa ibada bila hofu au wasiwasi.
Kwa hili Serikali ni refa anayehakikisha kila upande una haki sawa, na uhuru sawa; na kuwa
uhuru wa kuabudu au kutangaza dini kwa upande mmoja hauathiri haki ya uhuru wa ibada na kutangaza
dini kwa upande wa pili.
Mimi ni Rais wa watu wa dini zote, na ni Rais pia wa wale wasiokuwa na dini; ni Rais wa kabila
zote na rangi zote, jinisa zote na hulka zote. Mimi ni Rais wa wanywa pombe na wasio wanywa pombe;
wala nguruwe na wasiokula nguruwe. Si kazi yangu kuhukumu nani kati yao ni mwema na nani si mwema.
Kunitaka nimkataze mmoja anachopenda ni kunitaka nifanye kazi ya kuhukumu juu ya imani za watu
ambayo si yangu; hiy mimi naamini ni kazi ya Mwenyezi Mungu mwenyewe.
Hiyo pia ndiyo inayonifanya nichelee kukubali haraka haraka hoja ya Tanzania kujiunga na
Shirika la Waislam (OIC). Nadhani si sahihi kuishinikiza Serikali ikubali hoja hiyo kwa vile tu zipo nchi
nyingine zilizojiunga. Kila nchi huangalia mazingira yake na sababu zake. Kwa vile ukijiunga unafanya
hivyo kama Taifa zima, si kama sehemu ya Taifa, siwezi kupuuza kabisa maoni ya wale ambao si
Waislamu. Hivyo huu si uamuzi ambao ninaweza kuufanya kwa wepesi; unahitaji mashauriano zaidi na
pande zote na kuelimishana ili Jamii yote ya Tanzania ielewane.
Kuhusu suala la Mwembe Chai mimi nlilifikiri tulishaelewana kuwa haitasidia sana kuunda Tume
ya Uchunguzi, maana unajua kulichotokea. Na tunajua kuwa zile fujo, ambazo hatimaye zilihitaji nguvu
kubwa ya dola kuzizima, hazikuwa na uhusiano na mambo ya dini kabisa. Ndio maana miongoni mwa
waliokamatwa walikuwapo wtu ambao wala si Waislamu. Bado haja na hoja ya kuunda Tume sijaiona.
Tulipokutana tarehe 7 Julai, mwaka huu, mojawapo ya mambo tuliyozungumzia ilikuwa umuhimu
wa kuwa na fursa ya mzungumzo ya kudumu baina ya waumini wa dini mbalimbali, (inter-faith dialogue),
ili mradi wahusika wawe watu waliokomaa kimawazo, wenye busara na nia njema. Hii itasaidia kujenga
maelewano baina ya waumini wa dini zote na hivyo kupunguza hisia za kibaguzi za kila upande, na
kujenga msingi bora zaidi wa kufurahia uhuru wa imani katika mazingira ya kupendana na kuheshimiana,
japo tuwe na imani tofauti za dini.
Benjamin Mkapa, in Response to Tanzanian
Muslims' Grievances
The President of the United The State House
Republic of Tanzania Dar es Salaam
17 Desemba 1999
Ndugu Saleh Al-Miskry,
Halmashauri Kuu ya Waislamu,
C/o Islamic Club,
S.L.P. 11392,
DAR ES SALAAM
Ndugu Al-Miskry,
Ninakiri kupokea, kwa shukrani, barua yako ya tarehe 26 Agosti 1999, pamoja na viambatisho
vyake. Imenichukua muda mrefu kukujibu kwa sababu mambo uliyoandika ni mazito, ya kitaifa, na
ilinibidi niyatafakari kwa kina, niyafanyie utafiti zaidi, na nishauriane na wenzangu Serikalini kabla ya
kuyajibu.
Leo ninakuandikia si kwa lengo la kujibu hoja moja baada ya nyengine, au kutoa jibu kwa kila
swali. Katiba ya Jamhuri yetu inanipa mimi, kama Rais, wasaidizi wengi. Ninaye Makamu wa Rais, na
ninaye Waziri Mkuu. Ninaye waziri kwa kila sekta, na ninao wakuu wa mikoa na wilaya kwa kila eneo la
nchi yetu. Nitakuwa siwatendei haki nikijibu maswali yanayowahusu wao. Ningeshauri, kama mlivyojenga
mahusiano mazuri nami, mjenge pia mahusiano mazuri na mawaziri, wakuu wa mikoa, na kadhalika, ili
kila jambo lisingoje mpaka lifikishwe kwa Rais.
Nina uhakika kwa mfano, kwamba Waziri wa Elimu ana uwezo wa madaraka ya kutosha
kushughulikia masuala ya elimu, ambayo kwangu ni muhimu sana. Akikwama atayaleta kwangu. Hiyo
itasaidia kufanya mawasiliano nami yawe yale yanayohusu mambo ya msingi, badala ya kujadili matukio.
Misingi hiyo itasaidia kuwaongoza watendaji wa Serikali na kuniwezesha mimi na nyinyi kuwa na vigezo
vya kupima tunafanikiwa kiasi gani katika kuhakikisha kila mwannvhi anapata haki zake za msingi bila
ubaguzi wowote kwa sababu za dini, dhehebu, kabila, jinsia, eneo analotoka, na kadhalika.
Msingi wa kwanza ni utawala wa sheria. Nchi yetu lazima iendelee kutawaliwa kwa msingi wa
sheria zilizowekwa kwa njia za demokrasia. Hivyo napata taabu kidogo raia wa nchi hii anapofikiri
matatizo aliyo nayo yanaweza kutatuliwa nje ya mfumo wa utawala wa sheria.
Kila mwenye kero
akichukua msimamo huo, nchi hii itakuwa haitawaliki tena; itakuwa vurugu tupu. Kazi ya msingi ya
Serikali yoyote ni kuhakikisha unakuwepo utawala wa sheri, ulinzi na usalama wa raia wote, wa aina na
imani zote. Uhalali wa raia kudai haki nje ya mfumo wa utawala wa sheria unaweza ukakubalika penye
utawala wa kikoloni, utawala wa ubaguzi wa rangi, au utawala wa kidikteta. Uhalali huo haupo hata kidog
katika nchi huru, inayoongozwa kwa misingi ya demokrasia kama ilivyo Tanzania.
Kwa sababu hiyo nimefadhaishwa sana na kauli za kuashiria shari za wale wanojiita "Shura ya
Maimau Dar es Salaam". Pamoja na mbmo mengine ya uchochezei wanasema, "Waislamu hatuna moyo
tena na Serikali ya nchi hii na vyombo vyake vyote likiwemo Bunge na Mahakama". Ninajua huu sio
msimamo wa Waislam walio wengi, lakini matamko yasiyokuwa na kiasi kama haya yasipokanushwa, na
wanaoyatoa wanapopewa fursa na majukwaa ya kuyasema, hiyo inawapa silaha wale wachache
wanojaribu kupakamatope heshima na picha nzuri ya Waislamu. Mimi na ninyi tuna kazi ya kuwashihisha
wenye hulka ya aina hiyo, lakini matamko kama haya yatafanya kazi hiyo iwe ngumu zaidi.
Utawala wa sheria chimbuko lake ni Katiba ya Jamhuri. Katiba yetu imepiga marufuku ubaguzi
wowote, kwa msingi wowote, ikiwemo dini, kabila, rangi, eneo analotoka mtu, na kadhalika. Katiba hiyo
pia imetoa uhuru kamili, ndani ya uwigo wa sheria, wa imani za dini kustawi katika uhuru wa ibada.
Isipokuwa kwa wale ambao hawan imani na vyombo vyote vya dola, mimi nina imani kuwa mahakama
zetu nina uwezo na uhusu kamili wa kumpa haki hizi za msingi yule ambaye atkauwa amenyimwa kwa
ubaguzi.
Narudia. Haki za msingi za kila raia zimo ndani ya Sheria Mama - Katiba - ya Jamhuri yetu.
Kama kweli upo uhsahidi kwamba baadhi ya taasisi za umma au viognozi wa umma, wamebuni mfumo
wao wa kuhakikisha Waislamu wananyimwa haki hizo, hao wala si wa kuchukuliwa hatua za nidhamu tu,
bali ni wa kushitakiwa mahakamani. Wasionewe haya. Tusaidianeni wahsitakiwe!
Siwezi kushangaa iwapo kuna mtu au kiongozi mahali ambaye ndani ya moyo wake ana chuku
dhidi ya Wakristo au dhidi ya Waislam; au ana chuki dhidi ya naume au wanawake; au ana chuku dhidi ya
wazramo au wahaya; au chuki dhidi ya watu warefu au wafupi. Ninachosema ni kuwa katika utafiti
niliofanya hakuna mahali popote katika Serikali hii ambapo mfumo rasmi wa kubagua au kumnyima haki
za msingi mtu yeyote kwa msingi wowote.
Kweli, zipo tofauti kati ya idadi ya Waislamu na wasio Waislamu katika shile, vyuo, sehemu
mbalimbli za kazi lakni huo si ushahidi wa mfumo wa ubaguzi. Sababu zake sote unazijua - ni za kihistoria
na za kijamii, kama ilivyo kwa tofauti kati ya idadi za watu wa kabila mbalimbali au jinsia. Ingekuwa
tofauti hizo peke yake zinatosha kuthibitisha mfumo rasmi wa Waislamu, kwa nini tusiseme pia kuwa upo
mfumo rasmi wa kubagua wanawake, au watu wa kabila fulani, au rangi fulani, au umbo fulani. Na ukweli
ni kuwa si kila mahali Waislamu ni wachache. Kwa mfano nimejaribu kuhesabu ni mabalozi wangapi, tena
kwenye zile Ofisi za ubalozi muhimu sana, ambao ni Waislamu. Naomba na ninyi mfanye hesabu hiyo.
Lakini turudi kwenye masuala ya msingi. Si jambo zuri sana kuanza kujena utamaduni wa
kuhesabu watu kwa misingi ya kabila zao, dini zao, rangi zao, jinsia zao, au maeneo wanayotoka. Tangu
uhuru tumejitahidi kujenga taifa ambapo haki na heshima ya mtu inatokana na utu wake, si dini yake,
kabila lake, jinsia yake, na kadhalika. Siko tayari kujenga mfumo wa utawala ambapo sifa ya mtu kupata
nafasi ya shule, au nafasi ya kazi, ni dini yake. Aidha, tukishaanza na dini tutawazuiaje wengine kudai nao
wafikiriwe kwa misingi ya dhehebu la dini, kabila, jinsia na kadhalika. Hapo tutakuwa tumefumua kabisa
misingi ya umoja, upendo, mshikamano na kuheshimiana waliyotuachia waasisi wa Taifa letu. Naomba
sana tusitafute dawa ya ugonjwa mdogo itakayozua magonjwa makubwa zaidi yasiyokuwa na tiba.
Vile vile kuanzisha taasisi mpya ya kupokea na kuchunguza ubaguzi wa kidini kutazidi kuvuruga
tu kwa vile ni kukiri kuwa kweli upo ubaguzi uliojengeka ndani ya mfumo wa utendaji Serikalini; jambo
ambalo si kweli. Aidha, kama nilivyosema, ukianzisha taasisi ya kushughulikia ubaguzi wa kidini, uwezi
kukataa wengine wakidai taasisi nyingine ya kushughulikia ubaguzi wa jinsia, ubaguzi wa kabila, rangi, na
kadhalika.
Tusijitose sana katika zoezi la kuhesabu watu kwa misingi ya dini. Tukifanya hivyo tutaimarisha,
badala ya kujihisi kwanza kama Watanzania. Mimi nilifikiri kuwa Tanzania ilishavuka hatua hiyo.
Naomba usirudi nyuma kwenye kutukuza udini, ukabila, au maeneo tunayotoka. Tukishajitumbukiza huko
hatuwezi kutoka tena. Badala yake lengo letu liwe kuelekea mahali ambapo tutakuwa vipofu wa dini,
vipofu wa rangi, vipofu wa kabila, na kadhalika. Na pia tusisahau kuwa Tanzania yetu hii ina hata
Maaskofu wenye majina ya Ramadhani au Hussein, na wengine wengi ambao wana majina yasiyofichua
dini zao au kabila zao.
Jambo jingine la msingi ni kuhakikisha kuwa Tanzania kama Taifa, na kama Serikali au Chama
chochote cha siasa, inakuwa haina dini. Kwenye hili hakuna mjadala, maana ni hali hiyo ya kutinamia
upande wa dini yoyote ndiyo inayotupa nguvu ya kusimamia na kuhakikisha kila raia anapata haki zake za
imani za dini na uhuru wa ibada bila hofu au wasiwasi.
Kwa hili Serikali ni refa anayehakikisha kila upande una haki sawa, na uhuru sawa; na kuwa
uhuru wa kuabudu au kutangaza dini kwa upande mmoja hauathiri haki ya uhuru wa ibada na kutangaza
dini kwa upande wa pili.
Mimi ni Rais wa watu wa dini zote, na ni Rais pia wa wale wasiokuwa na dini; ni Rais wa kabila
zote na rangi zote, jinisa zote na hulka zote. Mimi ni Rais wa wanywa pombe na wasio wanywa pombe;
wala nguruwe na wasiokula nguruwe. Si kazi yangu kuhukumu nani kati yao ni mwema na nani si mwema.
Kunitaka nimkataze mmoja anachopenda ni kunitaka nifanye kazi ya kuhukumu juu ya imani za watu
ambayo si yangu; hiy mimi naamini ni kazi ya Mwenyezi Mungu mwenyewe.
Hiyo pia ndiyo inayonifanya nichelee kukubali haraka haraka hoja ya Tanzania kujiunga na
Shirika la Waislam (OIC). Nadhani si sahihi kuishinikiza Serikali ikubali hoja hiyo kwa vile tu zipo nchi
nyingine zilizojiunga. Kila nchi huangalia mazingira yake na sababu zake. Kwa vile ukijiunga unafanya
hivyo kama Taifa zima, si kama sehemu ya Taifa, siwezi kupuuza kabisa maoni ya wale ambao si
Waislamu. Hivyo huu si uamuzi ambao ninaweza kuufanya kwa wepesi; unahitaji mashauriano zaidi na
pande zote na kuelimishana ili Jamii yote ya Tanzania ielewane.
Kuhusu suala la Mwembe Chai mimi nlilifikiri tulishaelewana kuwa haitasidia sana kuunda Tume
ya Uchunguzi, maana unajua kulichotokea. Na tunajua kuwa zile fujo, ambazo hatimaye zilihitaji nguvu
kubwa ya dola kuzizima, hazikuwa na uhusiano na mambo ya dini kabisa. Ndio maana miongoni mwa
waliokamatwa walikuwapo wtu ambao wala si Waislamu. Bado haja na hoja ya kuunda Tume sijaiona.
Tulipokutana tarehe 7 Julai, mwaka huu, mojawapo ya mambo tuliyozungumzia ilikuwa umuhimu
wa kuwa na fursa ya mzungumzo ya kudumu baina ya waumini wa dini mbalimbali, (inter-faith dialogue),
ili mradi wahusika wawe watu waliokomaa kimawazo, wenye busara na nia njema. Hii itasaidia kujenga
maelewano baina ya waumini wa dini zote na hivyo kupunguza hisia za kibaguzi za kila upande, na
kujenga msingi bora zaidi wa kufurahia uhuru wa imani katika mazingira ya kupendana na kuheshimiana,
japo tuwe na imani tofauti za dini.