Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Mhasibu wa halmashauri ya jiji la Arusha, Charles Jacob anasakwa na Mwajiri wake na ametakiwa kujisalimisha kituo cha polisi kabla ya kumpiga pingu kwa madai ya kutafuna kiasi cha sh,milioni 84 fedha za makusanyo ya kila mwezi kuanzia Machi, 2019 katika mizani wa mazao ya chakula.
Akiongea na vyombo vya habari mara baada ya kutembelea Mizani ya mazao iliyopo kwa Morombo ,jijini hapa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ,Dkt Maulid Madeni amesema tangu mizani hiyo ilipoanzishwa Machi, 2019 imekuwa ikiingiza Sh milioni 2.8 kwa siku lakini mhasibu hiyo amekuwa akiwasilisha kwenye akaunti ya halmashauri kiasi cha sh,110,000 tu kwa siku huku fedha zingine zikiishia mfukoni mwake.
Mhasibu huyo pamoja na wasimamizi wa mizani hiyo,Thobias Julius na Agness Loishiye ambao wanashikiliwa polisi ,wanadaiwa kusababisha upotevu huo wa fedha na kuisababishia hasara kubwa halmashauri hiyo.
Madeni amewakamata na kuwaweka ndani wafanyakazi hao na kuagiza Jacob ambaye hakuwepo kazini kujisalimisha mwenyewe kituo cha polisi na kwamba hadi sasa hapatikani nyumbani kwake hata Simu yake ya mkononi haipatikani.
Kwa mujibu wa dkt .Madeni kituo hicho cha kukusanya ushuru hakifanyi vyema na kusababisha fedha nyingi kuishia mikononi mwa wakusanyaji na mhasibu huyo.
“Nilifuatilia muda mrefu ukusanyaji wa mapato nikagundua kuna ulaji mkubwa wa fedha unaofanywa na mhasibu huyo ndio maana leo hajaja hapa.”
“Nitahakikisha wahasibu wote wenye tabia kama hii nawatia pingi siwezi kukubali fedha za rais Magufuli zichezewe hivi ni bora unichezee Mimi "Alibaimisha Dkt Madeni
Aliongeza kuwa wakati anaanza Kazi aliikuta halmashauri hiyo kama Shamba la bibi kila mtu anajichotea fedha anavyotaka.
" Kwa mfano masoko mbalimbali ya Jiji yalikuwa yakiingiza makusanyo ya shilingi milioni 10 kwa mwezi lakini sasa yanaingiza sh,milioni 60 kwa mwezi kwa kila soko" Amesema Madeni
Akiongea na vyombo vya habari mara baada ya kutembelea Mizani ya mazao iliyopo kwa Morombo ,jijini hapa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ,Dkt Maulid Madeni amesema tangu mizani hiyo ilipoanzishwa Machi, 2019 imekuwa ikiingiza Sh milioni 2.8 kwa siku lakini mhasibu hiyo amekuwa akiwasilisha kwenye akaunti ya halmashauri kiasi cha sh,110,000 tu kwa siku huku fedha zingine zikiishia mfukoni mwake.
Mhasibu huyo pamoja na wasimamizi wa mizani hiyo,Thobias Julius na Agness Loishiye ambao wanashikiliwa polisi ,wanadaiwa kusababisha upotevu huo wa fedha na kuisababishia hasara kubwa halmashauri hiyo.
Madeni amewakamata na kuwaweka ndani wafanyakazi hao na kuagiza Jacob ambaye hakuwepo kazini kujisalimisha mwenyewe kituo cha polisi na kwamba hadi sasa hapatikani nyumbani kwake hata Simu yake ya mkononi haipatikani.
Kwa mujibu wa dkt .Madeni kituo hicho cha kukusanya ushuru hakifanyi vyema na kusababisha fedha nyingi kuishia mikononi mwa wakusanyaji na mhasibu huyo.
“Nilifuatilia muda mrefu ukusanyaji wa mapato nikagundua kuna ulaji mkubwa wa fedha unaofanywa na mhasibu huyo ndio maana leo hajaja hapa.”
“Nitahakikisha wahasibu wote wenye tabia kama hii nawatia pingi siwezi kukubali fedha za rais Magufuli zichezewe hivi ni bora unichezee Mimi "Alibaimisha Dkt Madeni
Aliongeza kuwa wakati anaanza Kazi aliikuta halmashauri hiyo kama Shamba la bibi kila mtu anajichotea fedha anavyotaka.
" Kwa mfano masoko mbalimbali ya Jiji yalikuwa yakiingiza makusanyo ya shilingi milioni 10 kwa mwezi lakini sasa yanaingiza sh,milioni 60 kwa mwezi kwa kila soko" Amesema Madeni